Ngonepi
JF-Expert Member
- Jun 2, 2013
- 1,872
- 1,212
Rais anongoza Taifa kwa matamko ya kukurupuka!Mkuu tatizo la serikali yetu ni kuongozwa na viongozi waliogubikwa na nidhamu ya woga.Binafsi sikuona mantiki ya kila waziri kujinasibu kwenye vyombo vya habari huku wakitoa matamko yenye kila rangi juu ya adhima ya kuhamia Dodoma.Rais kutamka kuwa atahakikisha ametimiza ahadi iliyoahidiwa kwa muda mrefu kuhamia dodoma ndani ya miaka hii iliyosalia alijua kuwa bado anahitaji kudunduliza vijisenti katika bajeti zilizobaki kabla ya kuhitimisha muhula wake wa uongozi.
Tatizo ni kutoelewa kusudio la mkuu wa nchi kuwa hakusema waanze kuhama wala kufurahisha hadhira kupitia matamko yao.Kusema akihama tu waandamizi wake inabidi wafanye hima.Mkuu sasa wameumbuka maana kuna waliosema mwisho wa wiki hizi zilizopita eti watakuwa wametimiza agizo la mkuu kumbe hawakudhani kuwa isingewezekana kwani si kuhama wao tu bali waandamizi wote.Daima kesheni mkiomba utajiri wa FIKRA na uwezo wa kutafakari kabla ya kutenda.Samahani wakuu nimewaza kwa sauti.
Na tatizo letu viongozi wetu hawajiamini kabisa na hili ni tatizo la miaka mingi kidogo, yaani kitu akizungumza Rais hata kiwe cha kipuuzi hakuna kiongozi hata mmoja anayejipa muda kukitafakari!!
Wao kwa kutaka kumfurahisha wanacheza ngoma yoyote apigayo!!