Mshana Jr
Platinum Member
- Aug 19, 2012
- 269,634
- 697,928
Hayati mwendazake aliifahamu vema nguvu ya uma, kuchokwa kwa chama chake na kutopendwa kwa viongozi wa chama chake ndio maana aliamua kibabe sana kukataza mikutano ya kisiasa na mijadala huru ya wananchi...
NGUVU ya uma ni kitu chenye nguvu sana maana ni muunganiko wa roho nyingi zenye nishati inayowaza jambo moja kwa pamoja, tofauti kabisa na nguvu ya kiongozi anayewaza jambo moja kwa msaada wa vyombo vya ulinzi vinavyopokea ujira na kumtumikia mtawala!
Chama tawala kimechokwa na hata wanachama wake! Hili si jambo la kushangaza hasa kutokana na ukongwe wake.. Wananchi wa Mtwara wanaojulikana kwa misimamo na utata wiki iliyopita baada ya kuchoshwa na ujinga wa viongozi wao wakaamua kwenye mkutano wa hadhara kurudisha kadi za CCM kufikisha ujumbe kunakohusika.
Watawala ama kwa kukurupuka ama kwa kutafuta huruma ya jamii ama kwa kutowaza kwa weledi wakaamua kwa haraka kuwatumbua viongozi wa kisiasa waliosababisha tatizo! Haikuwa hatua mbaya walifanya vema kusimama na wananchi. Lakini kwakuwa mambo ni mengi na muda ni mchache wakadhani hilo limeisha.
Jana kwenye mkutano wa hadhara huko wilayani Lushoto moja ya ngome kongwe za CCM wananchi wa kijiji cha View Point kwenye mkutano wa hadhara nao wakarudisha kadi za ccm kuonesha kutoridhishwa kwao na viongozi wao wa kisiasa
Mbegu iliyopandwa Mtwara imechipukia Milimani lushoto mamia ya kilometa. Moto uliowashwa Mtwara umeruka hadi Lushoto mwendo wa masaa si chini ya 20 kwa mwendo wa gari.
Tafsiri yake ninini hapa? Wananchi wamechoka na uoga hatimaye umewatoka! Hawaogopi tena! Ni ngumu kutabiri kituo kifuatacho kitakuwa wapi.. Kama kikiwa kanda ya ziwa hiyo ni habari ya kutisha sana...
Swali la kujiuliza je na DC wa Lushoto naye atatumbuliwa kwa kuzembea mpaka wananchi wakarudisha kadi za chama?
Je, asipotumbuliwa itakuwaje kwa aliyetumbuliwa? Maana makosa yanafanana.
Na je hili vuguvugu la kurudisha kadi za ccm tena kwenye mikutano isiyokuwa ya wapinzani likishika kasi. Watatumbuliwa wangapi!? Au wangapi hawatatumbuliwa?
NGUVU ya uma ni kitu chenye nguvu sana maana ni muunganiko wa roho nyingi zenye nishati inayowaza jambo moja kwa pamoja, tofauti kabisa na nguvu ya kiongozi anayewaza jambo moja kwa msaada wa vyombo vya ulinzi vinavyopokea ujira na kumtumikia mtawala!
Chama tawala kimechokwa na hata wanachama wake! Hili si jambo la kushangaza hasa kutokana na ukongwe wake.. Wananchi wa Mtwara wanaojulikana kwa misimamo na utata wiki iliyopita baada ya kuchoshwa na ujinga wa viongozi wao wakaamua kwenye mkutano wa hadhara kurudisha kadi za CCM kufikisha ujumbe kunakohusika.
Watawala ama kwa kukurupuka ama kwa kutafuta huruma ya jamii ama kwa kutowaza kwa weledi wakaamua kwa haraka kuwatumbua viongozi wa kisiasa waliosababisha tatizo! Haikuwa hatua mbaya walifanya vema kusimama na wananchi. Lakini kwakuwa mambo ni mengi na muda ni mchache wakadhani hilo limeisha.
Jana kwenye mkutano wa hadhara huko wilayani Lushoto moja ya ngome kongwe za CCM wananchi wa kijiji cha View Point kwenye mkutano wa hadhara nao wakarudisha kadi za ccm kuonesha kutoridhishwa kwao na viongozi wao wa kisiasa
Mbegu iliyopandwa Mtwara imechipukia Milimani lushoto mamia ya kilometa. Moto uliowashwa Mtwara umeruka hadi Lushoto mwendo wa masaa si chini ya 20 kwa mwendo wa gari.
Tafsiri yake ninini hapa? Wananchi wamechoka na uoga hatimaye umewatoka! Hawaogopi tena! Ni ngumu kutabiri kituo kifuatacho kitakuwa wapi.. Kama kikiwa kanda ya ziwa hiyo ni habari ya kutisha sana...
Swali la kujiuliza je na DC wa Lushoto naye atatumbuliwa kwa kuzembea mpaka wananchi wakarudisha kadi za chama?
Je, asipotumbuliwa itakuwaje kwa aliyetumbuliwa? Maana makosa yanafanana.
Na je hili vuguvugu la kurudisha kadi za ccm tena kwenye mikutano isiyokuwa ya wapinzani likishika kasi. Watatumbuliwa wangapi!? Au wangapi hawatatumbuliwa?