Vituko vya Mwananyamala: Mtaa kwa mtaa (special thread)

Vituko vya Mwananyamala: Mtaa kwa mtaa (special thread)

....umejitia uwakili kwa vitu usivyovijua;kukusaidia tu,matukio yote ya Ngomero hayakusemwa kwenye ule uzi ila bottom line ni kuwa ulikuwa ni uzi wa 'kumtukuza' muuaji!
...swali rahisi:akili yako imekutuma kabisa kuamini yeye kuniwazia mimi ni 'mpuuzi' ni sawa,ila mimi kumuwazia yeye ni 'jinga kabisa' ni sivyo alivyo;
....dah,we mkewe??
Mkuu mbona unapenda utata kausha bhana
 
Mkuu mbona unapenda utata kausha bhana
Mkuu njoo PM bhana nimekucheck tuyajenge...then hao watu wengine achana nao awana madhara wana stress zao tu Topic ya ngomero ipo sehem nyingne...pia hakauna sehem ata moja mtu yoyote aliyesema amemkuta james anaua zaid ni tetesi na maneno yake akishalewa hizo issue za kuchimba makaburi zipo na anafanya kweli issue ya kuifadhi maiti za vichanga kinyume na taratibu kwel alifanya na pia polis alipelekwa sie sio mahakama wala atujui kwanini yupo uraiani mpka leo..hakuna mwenye evidence kuwa alikuwa anakula nyama ya mtu, anachinja watu n.k
 
Kombe la Dunia Mwaka 199O
Mwananyamala nzima..
TV tulikuwa tunaangalia kwa Mzee Tabu Jumanne Mangala..
alikuwa Mkuu wa Jeshi la Magereza...
Lazima Uoge ndo uingie ukacheki Game ndani
Tena TV ilikuwa inawekwa nje uani.....
[emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23]
 
nimekaa sana Manjunju kwa mjeda mmoja, pia nimekaa Ujiji pale mahakama ya simu, rafiki yangu aliwahi kuishi kisiwani hapo Muigizaji TEA nae alikuwa anakaa pande hizo kwa mama mmoja Mkinga aliyemgeuza mumewe Ndondocha wanadai alikuwa mchafu sana huyo TEA haipiti wiki Mama mwenye nyumba hawajakwaruzana nae, Pale Kisiwani Bangi inavutwa hadharani, Pande za Ujiji madirisha karibu yote lazima ukute yamekatwa watu wanaweza vutia bangi dirishani kwako na huwezi wafanya chochote, kwa wale wapenda urahisi soko la mwananyamala ndio lina bei chee ya mchele, maharage na mahitaji mengine ya kunyumba
 
Nikiwa maeneo fulani nikaitwa baa kufika nikaagiza soda baada ya muda washkaji wakajua natokea mwananyamala, wakaniambia umeishi Mwananyamala halafu haunywi pombe?

Nikajibu ndiyo.

Wala hauvuti sigara wala bangi?

Nikajibu ndiyo.

Mshkaji akamalizia 'Ms.nge unajifanyisha siyo kweli'

Mkuu nafuatilia sana comment zako [emoji24], nacheka kishenzi, unaonekana mtoto wa kihuni wa Mwananyamala uliyestaarabika ambae unaijua kiundani.
 
Nimepitia comments nyingi zinaonyesha m'nyamala ilikuwa pasua kichwa enzi hizo. Mliokuwepo enzi hizo hebu mtutoe tongotongo je m'nyamala ilikuwa sehemu balaa zaidi kuliko maeneo kama magomeni, keko au ubungo?

Maana nimewahi kusikia maeneo haya (magomeni, keko na ubungo) yalikuwa na balaa nyingi zikifanywa huko.
Keko kuna balaa toka enzi na enzi mpaka kesho ,keko usiende kuishi kila aina ya usela uko huko ,mchana kweupe unakabwa na watu wanaendelea na shughuli zao ,kijana wa miaka 16 anakushikia panga mchana,keko pasua kichwa watoto na watu wa huko wameshindikana ....keko kuna story tamu hope Uzi wake utafunguliwa

Magomeni pako poa sio kihivyo ,magomeni kagera mpaka Argentina hupenda sana michezo ya ngumi na vijana wengi wameingia huko ndio kwakina Thomas mashali huko kila mtu anajifanyia bondia

Mwembechai,mikumi,mapipa palikuwa hot lkn sio kama keko,mwananyamala,kigogo nk ..binafsi ni mzoefu wa magomeni mapipa mitaa ya suna huku ukitaka druglords ,watengeneza hela feki utawapata ,matapeli ,watoto wa mjini utawapata mpaka watoto waliosumbua miaka ya 2014,2015 kwa jina la panya road utawapata wakazi wa kinondoni wanawafahamu sana hawa


Ila kigogo,keko,Tandale ndio yanashabihiana na mwananyamala ..magomeni utundu upo ila maisha ya huku yapo medium kati kwa kati ndio maana kuna utofauti na mitaa tajwa hapo juu hivyo usela sio sana kama huko ila pachangamfu


Nimepitia comments nyingi zinaonyesha m'nyamala ilikuwa pasua kichwa enzi hizo. Mliokuwepo enzi hizo hebu mtutoe tongotongo je m'nyamala ilikuwa sehemu balaa zaidi kuliko maeneo kama magomeni, keko au ubungo?

Maana nimewahi kusikia maeneo haya (magomeni, keko na ubungo) yalikuwa na balaa nyingi zikifanywa huko.
 
Back
Top Bottom