Vituko vya Mwananyamala: Mtaa kwa mtaa (special thread)

Vituko vya Mwananyamala: Mtaa kwa mtaa (special thread)

Nimepitia comments nyingi zinaonyesha m'nyamala ilikuwa pasua kichwa enzi hizo. Mliokuwepo enzi hizo hebu mtutoe tongotongo je m'nyamala ilikuwa sehemu balaa zaidi kuliko maeneo kama magomeni, keko au ubungo?

Maana nimewahi kusikia maeneo haya (magomeni, keko na ubungo) yalikuwa na balaa nyingi zikifanywa huko.
 
Bila kumsahau mtuma salamu maarufu na mshiriki wa kipindi cha chemsha bongo...Mohamed Kiyaiyai..mzee wa niambrieeeee...kutoka KomaKoma .
Huyu alikuwa anazinguana sana na Misanya Bingi...yaani akipiga simu anaanza kutaja washikaji walioko pembeni yake kama kumi hivi halafu ndio aanze kuwatumia salamu watu watatu...yaani ndani ya sekunde 60 anakuwa keshatuma salamu kwa watu zaidi ya 15 hivi....Misanya Bingi alimshtukia akawa anamgongea kipusa na kumkata hewani.
Halafu misanya alikuwa anamkomesha kwa kugonga kipusa kama dakika moja hivi...yaani ukitafsiri ni kama vile alikuwa anamporomoshea mitusi kwake na kwa ndugu na masela wake.

Yaani huu utundu wa wabongo ungekuwa ni wa kutengeneza vyombo vya anga mwezini tungekuwa tushahamia.
[emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23]
 
mshana juzi tulivyokuwa kibaha tulimuongelea huyu hatukujua km kashavuta kumbe
gari yake anaipiga service mwenyewe kaipaki kibaraxani kwake anaipiga jeki na ovaroli anazamchini
ana mikogo balaa

shunie kumbe mtoto wa mwananyama enzi ya NDEKA nakupa list lazima hawa maticha lazima uwafahamu
NDAGO la kwanza darasa lake lipo juu mlango unaangalia unaangalia geti la shure chumba cha kwanza njia ya kwenda assemble upande wa msikitini Huyu ticha kawafundisha wadangaji na wezi wote wa mwananyamala

MWAMBOLA akiwa zamu ukinunua askrimu anakuachia upite ila anagonga fimbo balaa

MANYANGA kazi yake kutongoza wanafunzi

MWANACHIA anapiga balaa

MBOGOLO mguu mbovu huyu ticha hakuna muhuni wa mwananyamala asomjua


getini enzi tunasoma alikuwa mlizi wa kimasai LAZARO mwalimu mkuu mwakatobe

enzi niliosoma MWANANYAMALA B choo kilibomoka tukawa tunarudi saa nne mpk kilipojengwa choo kingine bila kumsahauTicha MALIPURA wa la SABA kujinadi anao mtihani na majibu ya mtihani wa la saba taifa


vipi la saba la Ticha MADANDI ulikuwepo mkali wa MATH kipindi hicho tunapiga tuiton kwa Ticha maiko Ujiji Tumegawanywa kwa DALASA la A ndo wenye AKILI ukiwa F au E we kilaza wa kutupwa


itakuwa umekula sana miogo ya MZEE MSIBA na ndizi za MAMA ABDALAH canteen pale ha ha ha [emoji1] [emoji1] [emoji1] [emoji1] [emoji1]
Umenikumbusha mbali kinoma
We utakuwa umemaliza na kina Ally mtasha...sadat...kizibo
 
Umenikumbusha mbali kinoma
We utakuwa umemaliza na kina Ally mtasha...sadat...kizibo
ha ha ha KIZIBO namkumbuka ila alitupita darasa moja wao walianza kumaliza mwaka mmoja mbele class yetu sisi ilikuwa na kina jafar santo fatum kawale ally loko na kina abd ljoh
 
Pale shule ya msingi kinondoni
Kulikuwa na Walimu wanaitwa
Mwl. Simbani Na Mwl. Shuma..
Ikitokea wametoa adhabu kwa wanafunzi wanaotokea Mitaa ya Msisiri B
Maeneo Ya One Nil Area Nondo na Jerusa.. au Around Mwananyamala Hospitali..
Walimu walikuwa wanabadili njia kurudi makwao..
Shuma alikuwa anakaa Mitaa ya Ujiji
Simbani Tandale
Walikuwa hawakatizi njia ya msisiri B kupitia Kamanyola..
Maana walikuwa wanaogopa kufanyiziwa...
 
Back
Top Bottom