Vituko mitandaoni. Tupia chako

Vituko mitandaoni. Tupia chako

Speedo
IMG_20220919_191241_861.jpg
 

Mwanaume kupatwa...​

Marafiki wawili (Jose na Ben) walikuwa wanatembea mtaani akatokea mwanamke akarusha busu kwa mmojawapo kupitia dirishani katika jengo la ghorofa tatu.

Wakaanza kujadiliana kama ifuatavyo:

Ben: Muone yule mrembo amenirushia busu

Jose: tafadhali achana na huyo mwanamke, usimjali..

(baadae yule mwanamke akamuashiria aende)

Ben: yule mwanamke ameniita!

Jose: Rafiki yangu, usiende tafadhali

Ben: Kwa nini unaniambia nisiende wakati mrembo kama yule ananiita? Huu wivu sasa.

Jose: Ben, Nakwambia, tafadhali usiende

(Ben alienda. Ghafla wakiwa wanataka kuanza mambo, wakasikia mlio wa gari getini)..

Lady: (akiangalia kupitia dirishani)
Oooh dear! Yule ni mume wangu karudi!!

Ben: Mama yangu nafwaaa!
Tufanyeje sasa?

Lady: Usiwe na khofu, jifanye we Dobi na anza kupiga pasi hizo nguo hapo

(akimuonyesha lundo kubwa sana la nguo)

(Ben alitumia masaa matano kukamilisha kazi ya kunyoosha zile nguo kwa sababu yule mume hakutoka tena siku ile)

(Siku iliyofuatia Ben alikwenda kwa Rafiki yake)

Ben:
Kaka, unaweza kuamini Jana nimepiga pasi nguo kwa masaa matano pale kwa yule mrembo??!!!

Jose: Lakini nilikwambia usiende ukakaidi..
Amini usiamini, nguo zote hizo ulizonyoosha, Nilizifua Mimi Juzi🙄

When an experienced person speaks, you better listen!
 
View attachment 2362065

Afrika ingekuwa na mipango kama ya wazungu hivi leo kusingekuwa na Mafoleni ya kusubiri viongozi wapite .

Hebu angalieni jinsi wanavyotusumbua huku na Jinsi walivyokusanywa huko Ulaya
Kiukweli viongozi wa Kiafrika ni majanga. Sasa kama inawezekana kubana matumizi, kwa nini wanatutesa wananchi wao kwa misafara yao mirefu isiyo na tija, na matumizi ya magari ya kifahari!!
 
Back
Top Bottom