Vituko mitandaoni. Tupia chako

Vituko mitandaoni. Tupia chako

67777506_2324633224271488_8649082682577256448_n.jpg
 
Sheria ni sheria na unapaswa kuheshimu hata wakichoma nchi yote ibaki majivu ila sheria itabaki pale pale, yeye ana mahela ya kutosha ya kuajiri jopo la mawakili wampambanie, hivyo haipaswi makajamba wote waingie barabarani na kupora, huu upumbavu hata hapa Kenya huwa tunakua nawo mara moja moja eti tukihisi kiongozi fulani kadhulumiwa tunaanza uporaji, huyo unayempora mtaji wake na kumrudisha zero kisa ujinga wako wa kuabudu mungu mtu.
Salute Kiongozi.
Fikiria mathalani, Katiba ile ya Kenya ilipatikana kwa machozi, jasho na damu, halafu kinajitokeza kijitu kinakuja kudharau muhimili wa mahakama kwa kiburi tu.
Baadaye anachukuliwa hatua kuna wananchi waje waandamane!!

Nakuunga mkono.

Wapigwe tu.
Watu wameuana kupata Katiba, halafu mnaitekeleza mnaanza kuuana tena.
Ni ujuha.
 

MARTIN MAYANJA MASESE.

na kunao watu wamemfollow taahira kama huyu😂😂😂😂😂

Anataka atapike kisa mafanikio ya mwingine😂😂😂😂😂😂

USHAURI WANGU KWAKE.

anywe maji mengi sana kwa sababu badala ya kutolea mapovu mafanikio ya wengine atakua bize tuu kukojoa chooni.

Muda huo atakosa kabisa😂😂😂😂😂😂

Matackle kabisa😈😈
 
Siyo kweli japo hoja yako ina mashiko kuhusu uamilifu wa sheria kama msumeno unaopaswa kukereza kote kote bila kujali hadhi ya anayekerezwa. Katika uhalisia wake hata hivyo mambo hayako hivyo. Na ishu ya Afrika Kusini kidogo ni tata kulingana na historia yao ngumu waliyopitia hasa hawa weusi. Ati; Angekuwa ni De Klerk au P.W. Botha ndiyo kafanya kosa alilofanya Zuma (ana sababu nzuri tu); ni kweli angefungwa?

Ni vizuri kuangalia historia ya watu kwa uangalifu ili kuyaweka na kuyatafsiri matendo yao katika muktadha sahihi. Nina marafiki wako huko na wanaeleza mkanganyiko uliopo katika vurugu zinazoendelea na wanasema kuwa ni hisia za ubaguzi pamoja na migongano ya kitabaka; na umasikini sugu kwa hawa weusi. Ukimsikiliza Mh. Malema naye pia anagusia mkanganyiko huu na kumlaumu jaji aliyegoma kujitoa kwenye shauri hili; na Zuma kwa kuwa kichwa ngumu huku akijua hali na fikra za watu zilivyo.

Hata kwenu huko sidhani kama ni kuabudu mtu (Odinga?). Ukichimbua kidogo utakuta kuna sababu zingine za kijamii na hata kiuchumi na kihistoria. Ukabila!
Kama Katiba na sheria zao nyingiene zimekaa kwenye mfumo wa kibaguzi basi wazifumue.
Haiwezekani nchi moja iwe na sheria kwa watu tofauti.
Lakini hili ni jambo lingine, kikubwa sheria iliyopo imetekelezwa.
Kuhusu Jaji au hakimu kujiondoa kwenye shauri lako ni jambo la kisheria.

Mathalani kwa sheria za Tanzania mshitakiwa anaruhusiwa kuomba hakimu abadirishwe, lakini huyo hakimu au Jaji ana hiyari, kujiondoa au kutojiondoa.
 
Back
Top Bottom