Vituko mitandaoni. Tupia chako

Vituko mitandaoni. Tupia chako

Screenshot_20210714-194740_Instagram.jpg
 
Fisadi wako ni shujaa wa mwingine (and vaisi vesa). Usifikiri wote walioingia (hawajapelekwa) barabarani ni wajinga!

Na Zuma wala hajahukumiwa kwa ufisadi. Amehukumiwa kwa kuidharau mahakama baada ya kutokwenda kusikiliza shauri lake. Na ana sababu za msingi zana kutokwenda. Kuna jaji ambaye ni adui yake na alitaka huyo jaji aondolewe katika jopo la majaji waliokuwa wamepangwa kusikiliza kesi yake. Na hii ni haki ya mshitakiwa. Jaji alikataa kujitoa naye Zuma akasema nami siendi kwa sababu hakutakuwa na haki. Kwa hivyo wengi wanaona Zuma kaonewa na haki zake za kikatiba zimevunjwa kwa vile tu ni mweusi. Angekuwa ni mzungu asingefungwa kwa sababu kimsingi hana kosa.

Kilichompeleka gerezani hakihusiani na ufisadi !!!

Sheria ni sheria na unapaswa kuheshimu hata wakichoma nchi yote ibaki majivu ila sheria itabaki pale pale, yeye ana mahela ya kutosha ya kuajiri jopo la mawakili wampambanie, hivyo haipaswi makajamba wote waingie barabarani na kupora, huu upumbavu hata hapa Kenya huwa tunakua nawo mara moja moja eti tukihisi kiongozi fulani kadhulumiwa tunaanza uporaji, huyo unayempora mtaji wake na kumrudisha zero kisa ujinga wako wa kuabudu mungu mtu.
 
Sheria ni sheria na unapaswa kuheshimu hata wakichoma nchi yote ibaki majivu ila sheria itabaki pale pale, yeye ana mahela ya kutosha ya kuajiri jopo la mawakili wampambanie, hivyo haipaswi makajamba wote waingie barabarani na kupora, huu upumbavu hata hapa Kenya huwa tunakua nawo mara moja moja eti tukihisi kiongozi fulani kadhulumiwa tunaanza uporaji, huyo unayempora mtaji wake na kumrudisha zero kisa ujinga wako wa kuabudu mungu mtu.
Siyo kweli japo hoja yako ina mashiko kuhusu uamilifu wa sheria kama msumeno unaopaswa kukereza kote kote bila kujali hadhi ya anayekerezwa. Katika uhalisia wake hata hivyo mambo hayako hivyo. Na ishu ya Afrika Kusini kidogo ni tata kulingana na historia yao ngumu waliyopitia hasa hawa weusi. Ati; Angekuwa ni De Klerk au P.W. Botha ndiyo kafanya kosa alilofanya Zuma (ana sababu nzuri tu); ni kweli angefungwa?

Ni vizuri kuangalia historia ya watu kwa uangalifu ili kuyaweka na kuyatafsiri matendo yao katika muktadha sahihi. Nina marafiki wako huko na wanaeleza mkanganyiko uliopo katika vurugu zinazoendelea na wanasema kuwa ni hisia za ubaguzi pamoja na migongano ya kitabaka; na umasikini sugu kwa hawa weusi. Ukimsikiliza Mh. Malema naye pia anagusia mkanganyiko huu na kumlaumu jaji aliyegoma kujitoa kwenye shauri hili; na Zuma kwa kuwa kichwa ngumu huku akijua hali na fikra za watu zilivyo.

Hata kwenu huko sidhani kama ni kuabudu mtu (Odinga?). Ukichimbua kidogo utakuta kuna sababu zingine za kijamii na hata kiuchumi na kihistoria. Ukabila!
 
Back
Top Bottom