Eti kwa vile huko nyuma ulikuwa umezoea kuiba bila kukamatwa leo umeiba ukakutana na za mwizi arobaini ukakamatwa ndo uanze kulalamika kuwa mbona huko nyuma nilikuwa naiba lakini sikamatwi?. Kha !!!
Tujaribuni kujenga jamii inayofuata sheria, haki na usawa - hasa katika utawala huu wa mama. Tabia ya kupindisha pindisha sheria na kanuni tulizojiwekea sisi wenyewe kwa visingizio hivi na vile siyo nzuri. Kama sheria au kanuni fulani hatuipendi basi tuibadilishe kwa kufuata utaratibu tuliojiwekea. Binafsi Yanga wamenikosha sana !!!