Kwa mabinti wote na wamama mliopo humu. Happy Mother's Day jamani. Hakuna upendo kama wa mama hapa duniani. Hakuna !!!
Na kwenu ambao bado mama zenu wako hai. Wapendeni sana. Msimalize wiki bila kuwajulia hali. Na vizawadi vidogo vidogo (na vikubwa) kwa mama viwe ni kawaida...Wakija kuondoka maumivu na majuto yake huwa havielezeki. Na pengo lao huwa halizibiki...
Miaka mitatu nyuma mama yangu aliitwa. Kitinda mimba wake mimi nikaachwa mpweke. Mpaka leo simu yake bado ipo...na kuna siku mambo yakinizidia huwa napiga tu namba ile kama nilivyokuwa nimezoea...lakini sauti ile ya upendo na kicheko kile chenye kuondoa hofu vimenyamaza kimya. Happy Mother's Day Mom. Happy Mother's Day to you all


View attachment 1778739View attachment 1778746