Mkuu
Kiranga nimekufuatilia tangu mchango wa kwanza ktk hili bandiko. Una maantiki ktk hoja zako,lkn mimi nataka nikusaidie hapa ulipohoji kwa nn Mungu mwenye upendo wote kaumba ulimwengu ambao mabaya yanawezekana na wakati alikuwa na uwezo wa kuumba ulimwengu ambao mabaya hayawezekani..!? Ukweli Mungu hakuumba ulimwengu ambao mabaya yanawezekana,Mungu alimuumba mwanadamu kwa sura na mfano wake. Hilo ndo jambo kubwa sana alilofanya,Mungu aliweka kila kitu ktk uwezo wa mwanadamu wa kuchagua namna ya kuishi bila msaada wake. Mabaya yanayotokea ni uamzi wa mwanadamu wala si wa shetani wala Mungu km wengine wanavyosingizia.
Kila unachotenda hapo ulipo ni kwa msaada wa akili yako. Kwa mfano: ukiona kitu kimeandikwa hii ni sumu usiinywe,lkn wewe unasema nainywa Mungu yupo ataniponya,hapo unamfanya Mungu awe kibarua wako na ndo hasa ulichomaanisha ktk maswali yako. Hebu me nikuulize hivi kwa mfano wanadamu wote kwa pamoja tukiamua kuishi kwa kutenda mema 100% hilo swali lako litakuwa na maana kweli!!? Ntarudi..
Hujaelewa swali.
Swali ni kwamba, kabla ya mtu kuumbwa, kwa mujibu wa mapokeo yenu, mungu aliumba ulimwengu.
Alivyokuwa anaumba ulimwengu huu, alikuwa na uwezo wa kuuumba ulimwengu uwe vyovyote anavyotaka.
Akachagua kuumba ulimwengu ambao mabaya yanawezekana.
Wakati alikuwa anaweza kuumba ulimwengu ambao mabaya hayawezekani.
Kwa nini?
Ukianza kusema habari za binadamu kaumbwa kwa mfano wa mungu unaonyesha hujaelewa swali.
Swali linauliza kabla mtu hajaumbwa.
Mungu alikuwa na uwezo wa kuumba ulimwengu ambao mabaya hayawezekani.
Kwa nini hakuumba ulimwengu huo?
Unaposema mabaya ni uamuzi wa mwanadamu, mabaya hayo yamewezekanaje bila mungu kuyaruhusu?
Na kwa nini karuhusu yawepo?
Alishindwa kuumba ulimwengu ambao maamuzi ya binadamu yatakuwa kati ya mazuri na mazuri zaidi tu?
Kama alishindwa, je ni kweli anaweza yote?
Ama aliweza kuumba ulimwengu usio na mabaya, ila hakutaka tu?
Kama aliweza ila hakutaka tu, kwa nini katubania kwa makusudi? Ni kweli ana upendo wote?
Huyu mungu yupo kweli au ni hadithi tu?