Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 33,476
- 39,995
Baada ya furaha za mwanzo za maisha ya pamoja kuna baadhi ya wanaume huanza kunyemelea nyumba zao wenyewe. Mtu toka anatoka kazini anapiga mahesabu ya jinsi gani ataingia nyumbani bila kusababisha mfarakano. Wengine huja na giza za 'uchovu' wengine huja na giza 'kukasirishwa' na mtu huko na wengine huja na hata gia za 'unyonge'. Lengo la gia hizo zote na nyingine nyingi ni kutuliza hasira za mwenza wake pale nyumbani. Lakini wakati mwingine, mwanamme anaingia nyumbani kwa kunyemelea kwa sababu ya hofu ya kile atakachokikuta nyumbani siku hiyo.
Ni vitu gani hasa vinaweza kumfanya mwanamme apaone nyumbani pake pa chungu na hivyo kutafuta kila sababu ya kuchelewa au hata kukwepa kulala nyumbani siku fulani fulani?
Ni vitu gani hasa vinaweza kumfanya mwanamme apaone nyumbani pake pa chungu na hivyo kutafuta kila sababu ya kuchelewa au hata kukwepa kulala nyumbani siku fulani fulani?