Kweli maisha ya sasa, ndoa inatafutwa kwa lazima

Equation x

JF-Expert Member
Sep 3, 2017
29,429
40,418
Kutokana na changamoto za kiuchumi pamoja na uhaba wa wanaume wenye sifa za uoaji kupungua; mabinti wakileo wameanzisha utaratibu wa kujisogeza kwa mwanaume na kuanza naye maisha, bila kufuata taratibu za ndoa.

Kuna binti mmoja amemaliza chuo, na kukaa mwaka mmoja nyumbani bila kazi, akaona haya maisha hayaeleweki, akabeba nguo zake akajisogeza kwa baharia (mchumba wake), sasa hivi wanaishi nyumba moja, pika nipakue.

Wengine wako chuo wanasema, kazi nikose, na mume pia nikose? Kwa hiyo wanahitimu chuo, na baada ya hapo wanajisogeza kwa wachumba zao na kuanza kuishi pamoja kama mke na mume.

Wengine wako mtaani, wakiona wapenzi wao wana muelekeo fulani wa kimaisha, wanahisi wanaweza kuja kutelekezwa; kinachofanyika ni mabinti kubeba vitu vyao na kuamia kwa wapenzi wao bila utaratibu ule wa zamani wa kusubiri ndoa.

Ama kweli si mwanamke wala si mwanaume; nyakati hizi wote ni mabaharia.

Kweli maisha ya sasa, ndoa inatafutwa kwa lazima.​
 
Kutokana na changamoto za kiuchumi pamoja na uhaba wa wanaume wenye sifa za uoaji kupungua; mabinti wakileo wameanzisha utaratibu wa kujisogeza kwa mwanaume na kuanza naye maisha, bila kufuata taratibu za ndoa.

Kuna binti mmoja amemaliza chuo, na kukaa mwaka mmoja nyumbani bila kazi, akaona haya maisha hayaeleweki, akabeba nguo zake akajisogeza kwa baharia (mchumba wake), sasa hivi wanaishi nyumba moja, pika nipakue.

Wengine wako chuo wanasema, kazi nikose, na mume pia nikose? Kwa hiyo wanahitimu chuo, na baada ya hapo wanajisogeza kwa wachumba zao na kuanza kuishi pamoja kama mke na mume.

Wengine wako mtaani, wakiona wapenzi wao wana muelekeo fulani wa kimaisha, wanahisi wanaweza kuja kutelekezwa; kinachofanyika ni mabinti kubeba vitu vyao na kuamia kwa wapenzi wao bila utaratibu ule wa zamani wa kusubiri ndoa.

Ama kweli si mwanamke wala si mwanaume; nyakati hizi wote ni mabaharia.

Kweli maisha ya sasa, ndoa inatafutwa kwa lazima.​
😆😆😆
 
Back
Top Bottom