Vitambulisho vya Taifa (NIDA) havitambuliwi na BOT

Vitambulisho vya Taifa (NIDA) havitambuliwi na BOT

Hakuna asiyejua kuwa hako kachip kana hizo taarifa,issue hapa is it relevant kwa mazingira yetu? kwa hiyo unawaambiaje watu wa bank wanotaka kutmia hizo Id lakini wanashindwa kutokana na hizo Id kukosa sifa stahiki?Na ingepunguza nini kuifanya iwe analogically acceptable na kukawa kuna hizo taarifa kweye chip? Au unafikiri hizo Ids ni kwa Dar tu ndugu yangu? BoT wameshatoa tamko hizo Ids kukosa sifa kwa matumizi ya kibank kwa hiyo unafikiri hao pia hawajui kinachoendelea "nchi za wenzetu"? Nimeanza kutumia hicho kinachoitwa smart card nikiwa UDSM 2002 kwa hiyo hakuna kipya unachodhani unafahamu
Kama kuna shida ni kiasi cha kurekebisha ili mikoa mingine waweze kutoa vikiwa na taarifa za msingi maana wao wamefanya kadi ya NSSF ambayo inatumika kwa kazi maalumu, yaani hata driving license ina zile information za msingi za awali, vingine vyote vikae kwenye chip lakini kuna tarehe ya kuzaliwa, signature, picha na permanent address sio P.O box angalau inaonyesha Sumbawanga maana kwa mazingira yetu hatujafika level ya kuwa digitali everywhere kuna maeneo mtu anatakiwa akiangalie alafu analinganisha na sura alafu anakwambia embu piga na mkwaju wako tuone
 
Kile kitambulisho ndani kina smart chip ambayo inakua nantaarifa zote ulizojaza muombaji, na kama umeenda kuchukua chako utakua umekumbana na shughuli za kuhakiki taarifa zako za kibiologia yena, kama alama za vidole, na hio date off issued inajazwa kwenye taarifa zako zilizo ndani ya hio chip ndo maana zoezi linaitwa Insueance, swali mjiulize je hao BOT wana machine tambuzi?? Ambazo unaweza ku swap kadi ikadisplay information?? Ni muda tubadilike ki analogy, kitambulisho kwa juu hakiwezi kubeba maandishi yote

Ok,nimekuelewa hapo kwenye red. Kwa hiyo unafikiri isingewezekana kuwa na sahihi na tarehe ya kuzaliwa na hizo alama nyingine za kibaolojia zikawa kwenye chip au siyo?
 
Mtoa thread tunaomba aweke huo muhtasari wa BoT humu jamvini kwa sababu taarifa yake ni dhahiri kwamba ni ya kupika na hana lengo zuri na Vitabulisho vya Taifa ambavyo vimeleta maendeleo makubwa ya uchumi na kuimarisha usalama kwenye nchi zenye Vitambulisho. Huu ni upotoshaji.

CCM wameifanya Tanzania kuwa ni nchi isiyo rasmi; hakuna mipango miji, hakuna mfumo wa maji salama unaoeleweka, hakuna uhakika wa umeme, health system imefail, barabara mbovu mpaka juzi zimeua basi zima na hakuna anayewajibika, wizi wa pesa za uma bila kuwajibika, mauaji ya albino kila kona.

Lazima waliingia maagano na shetani kuiongoza nchi hii maana huu ni ushetani per se, wanacopy na kupaste wanayoyaona kuzimu wakienda kwenye vikao na shetani.
 
Kama kuna shida ni kiasi cha kurekebisha ili mikoa mingine waweze kutoa vikiwa na taarifa za msingi maana wao wamefanya kadi ya NSSF ambayo inatumika kwa kazi maalumu, yaani hata driving license ina zile information za msingi za awali, vingine vyote vikae kwenye chip lakini kuna tarehe ya kuzaliwa, signature, picha na permanent address sio P.O box angalau inaonyesha Sumbawanga maana kwa mazingira yetu hatujafika level ya kuwa digitali everywhere kuna maeneo mtu anatakiwa akiangalie alafu analinganisha na sura alafu anakwambia embu piga na mkwaju wako tuone

Upo sahihi kabisa mkuu. Kuna watu hawaoni kitu rahisi kama hicho wanakomaa tu kuna chip sijui blah blah,ninachoona hapa ni kwamba hawa vijana waliozaliwa na kuishi Dar maisha yao yote wanafikiri Tanzania yote ipo kama Dar!
 
Hivi, NIDA kuna wasomi kweli! Hawa wahitimu wa vyuo vikuu hapa nchini wanaajiriwa wapi! Nahisi ndo matunda ya ubovu wa elimu nchini. Mtu anashindwa kutambua umuhimu wa hivyo vipengele muhimu kabisa katika kitambulisho. 11. USIWE CCM.
 
kitambulisho cha taifa...

ipo tarehe ya kuzaliwa ambayo inaonyesha mwanzo wa utaifa wa mwenye kitambulisho.

Angalia pasport ilivyo details zake... Tz ilitakiwa kila mzazi/mlezi anapoprocess birth certificate apewe na pasport ya mtoto... Ingekuwa safi sana.
 
Niliwahi kuuliza hapa ni kwa nini hivyo vitambulisho vya taifa (nafikiri tungekuwa tunaviita vitambulisho vya utaifa sio taifa) kwa nini vina expiry date? Ina maana inafika uraia wa mtanzania utakuwa unakoma? Nimeviona vitambulisho vya jirani zetu hapo Kenya, havina expiry date. Na ukipoteza kitambulisho chako, hakitolewi kipya, you can only get a duplicate of your original ID. Sasa hivi vya kwetu eti vinaisha muda wake.

No wonder muandikishaji wa vitambulisho kwenye eneo langu alikataa kuitambua passport yangu kama utambulisho kamili akataka nilete barua ya balozi. Niliamua kuachana na hivyo vitambulisho, na leo eti taasisi za serikali hazivitambui. Hiki ni kichekesho.

Tiba

hata Mimi nashindwa kuekewa why expire date..Ina maana muda ukiisha Mimi sio RAIA tena?
ngoja waje wataalam watuhabarishe .
 
Usajili na Utoaji wa Vitambulisho vya Taifa ninavyofahamu unakwenda kwa awamu, wamegawa IDs Zanzibar yote, Dar na Pwani. Pia nasikia wamesajili zaidi ya mikoa sita, tuvute subira watakamilisha nchi nzima na matunda yake tutayaona kama vile kurahisisha kupata mitaji kwenye taasisi za fedha, kuongeza mawanda ya mapato ya Serikali, kupunguza wafanyakazi hewa......

The way ulivyo-respond awali you sounded like tayari maendeleao makubwa yalishaletwa na upatikanaji wa hivyo vitambulisho. Kumbe hizo ni prospects tu. Anyway, still wanaweza kusahisha hayo makosa yaliyojitokeza.
 
Serikali ya CCM katika hali ya ubora wake uliotia fora!!
 
Niliwahi kuuliza hapa ni kwa nini hivyo vitambulisho vya taifa (nafikiri tungekuwa tunaviita vitambulisho vya utaifa sio taifa) kwa nini vina expiry date? Ina maana inafika uraia wa mtanzania utakuwa unakoma? Nimeviona vitambulisho vya jirani zetu hapo Kenya, havina expiry date. Na ukipoteza kitambulisho chako, hakitolewi kipya, you can only get a duplicate of your original ID. Sasa hivi vya kwetu eti vinaisha muda wake.

No wonder muandikishaji wa vitambulisho kwenye eneo langu alikataa kuitambua passport yangu kama utambulisho kamili akataka nilete barua ya balozi. Niliamua kuachana na hivyo vitambulisho, na leo eti taasisi za serikali hazivitambui. Hiki ni kichekesho.

Tiba
Tiba,
Hakuna ID isiyokuwa na tarehe ya mwisho wa matumizi. Ni kama passport. Hiyo tarehe ya mwisho wa matumizi haimaanishi utaifa wako umekoma. Inakuwepo ili ku-update vitu vingi eg sura ya picha yako na hata kuondoa vya walifariki, kubadilsha utaifa, nk. Tena ID na passport za nchi nyingi zilizoendela zinakuwa na umri wa miaka mitano tu na sio kumi kama huku kwetu.
 
Tiba,
Hakuna ID isiyokuwa na tarehe ya mwisho wa matumizi. Ni kama passport. Hiyo tarehe ya mwisho wa matumizi haimaanishi utaifa wako umekoma. Inakuwepo ili ku-update vitu vingi eg sura ya picha yako na hata kuondoa vya walifariki, kubadilsha utaifa, nk. Tena ID na passport za nchi nyingi zilizoendela zinakuwa na umri wa miaka mitano tu na sio kumi kama huku kwetu.

Si kweli kwamba hakuna ID isiyo kuwa na mwisho wa matumizi kama unavyojaribu kuhaminisha. Hiki ni kitambulisho cha uraia sasa kwa nini kiwe na mwisho wa kutumika? Usilinganishe kitambulisho hiki na kitambulisho cha kazi au benki. Nimekupa mfano wa majirani zetu Kenya national ID hazina expiry date.

Lakini pia nafikiri tunge tofautisha ID ya uraia na passport. Passport kwisha muda ni sawa kwani pamoja na kwamba ni chanzo kimojawapo cha mapato ya serikali lakini pia sura ya mtu inabadilika pia kwa ajili ya kuzeeka. Kitambulisho cha uraia inabidi kiwe cha kudumu na wala hakipashwi kuwa na mwisho wa kutumika. Wenzetu Italy wana vyeti vya uraia wanaviita codice fiscale, hivi ukiishapewa basi tena hakibadilishwi tena na wenzetu hawaweki picha ya mtu.

Anyway hata mkiamua kiishe muda wake ni sawa tu kwani hakiko linked na kitu kingine chochote. Viongozi wetu wangekua smart vitambulisho hivi vingepashwa kuwa linked na TIN ya TRA na driving licence.

We still have a long way to go.

Tiba
 
Si kweli kwamba hakuna ID isiyo kuwa na mwisho wa matumizi kama unavyojaribu kuhaminisha. Hiki ni kitambulisho cha uraia sasa kwa nini kiwe na mwisho wa kutumika? Usilinganishe kitambulisho hiki na kitambulisho cha kazi au benki. Nimekupa mfano wa majirani zetu Kenya national ID hazina expiry date.

Lakini pia nafikiri tunge tofautisha ID ya uraia na passport. Passport kwisha muda ni sawa kwani pamoja na kwamba ni chanzo kimojawapo cha mapato ya serikali lakini pia sura ya mtu inabadilika pia kwa ajili ya kuzeeka. Kitambulisho cha uraia inabidi kiwe cha kudumu na wala hakipashwi kuwa na mwisho wa kutumika. Wenzetu Italy wana vyeti vya uraia wanaviita codice fiscale, hivi ukiishapewa basi tena hakibadilishwi tena na wenzetu hawaweki picha ya mtu.

Anyway hata mkiamua kiishe muda wake ni sawa tu kwani hakiko linked na kitu kingine chochote. Viongozi wetu wangekua smart vitambulisho hivi vingepashwa kuwa linked na TIN ya TRA na driving licence.

We still have a long way to go.

Tiba

Asante sana. Kwenye maandishi niliyoweka mekundu yamemaliza kila kitu. (Je hizo ID zina picha kama passport? 🙂) Halafu cheti cha uraia ni tofauti na kitambulisho cha uraia. Mimi nilichoshangaa ni pale wanaposema havina 'date issued' na ''signature''. Hivi ni vitu muhimu wameacha (hata kama viko ki-digital kama wanavyodai wengine) kwani hivi vitambulisho vinatumika sehemu nyingi ambazo hazina card reader. Halafu hivi wanajua maana na signature kweli? Hivi wanajua mtu mtu mwenye credit card huwezi kuitumia kama haina signature yako? Wanajua maana yake?
HALAFU: mimi nafikiria hii kuita ''vitambulisho vya uraia'' inachanganya watu. Hizi mbwembwe tu za wanasiasa.
 
Benki kuu ya Tanzania imetoa muhtasari wa kutokutambua vitambulisho vya taifa kwa kuwa vina mapungufu makubwa kama kutokuwa na date of issue , signature of the ID holder, Place of issue etc etc.... na hivyo kutkufaa kwenye matumizi yeyote ya kibenk ikiwemo kufungua account na kufanya transaction zozote zile za kibenk.
Taarifa zaidi zitawajia..

Huu ni mwendelezo tu wa namna tunavyokurupuka kama taifa kufanya maamuzi ya zima moto kweye mambo ya msingi...... naangalia namna tunavyoandaa vitambulisho vya kuipiga kura, katiba mpya , Bara bara za lami, shule za kata, umeme nk.....

Mkuu na mabilioni yote hayo! Kwa maana hiyo fedha za wadanganyika zimeliwa tena.
 
12.gif
ID%20cards.jpg
images
142376_max.jpg
images
9k=
9k=
president.png

Tunapojadili hili tuangalie kwa ulinganifu na vitambulisho vya kitaifa vya mataifa mengine barani Afrika na mabara mengine duniani.
  • Nini kinakosekana ambacho katika vitambulisho vya matafa mengine wanavyo?
  • Draft ya vitambulisho haikufanyiwa uhakiki kulinganisha na vitambulisho vinavyotumiwa na mataifa mengine?

Ninavyojua mimi kitambulisho cha kitaifa ni short form ya passport, hivyo mfumo ni ule unaoonekana kwenye passport unatakiwa uwekwe wazi kwenye kitambulisho. Haiwezekani imformation zibaki kwenye data base wakati zinahitajika wakati anapojitambulisha kwa njia yo yote.

CC,
mfianchi
 
Hakuna hata umuhimu wa kuvifuatilia manake unapoteza muda na takataka usikuja itumia milele

Hapana mimi bado sijaona kosa la hivyo vitambulisho,vitambulisho hivyo vina siku,mwezi,na mwaka wa kuzaliwa na saini imewekwa kwenye kumbukumbu ya data base ya NIDA,mimisijawahi kuona eti kitambulisho cha taifa kina kuwa na tarehe ya ukomo wake kama ilivyo passport,halafu nadhani umefika wakati wa aserikali kuingilia kati,haiwezekani kwa serikali hiyohiyo ianze kuvikataa tena,na hizi benki zinafanya uhuni tu,mbona Benki ya Posta wanavitambua.
Ngoja tupeleke malalamiko yetu NIDA ili tuone hawa wanaotusumbua watachukuliwa hatua gani.
 
mkiambiwa nyie watu hamko organized mnajaa mapovu bure tu.
just imagine taasisi kubwa Kama BOT na mabenki mengi wanazikataa national IDs,kisa hawana vifaa vya kusomea hizo chip za kwenye National IDs,this is a lough of the day.
some people somewhere are not doing their jobs properly,siku zote communication ni muhimu Sana,kitu ambacho NIDA angefanya mapema ni kuagiza mabenki yote yawe na hicho kifaa cha kusomea IDs from HQ to the furthest branch in this country.
let's say Leo Mimi naenda kwetu wilayani muleba,with means ntakosa huduma muhimu kwa sababu za uzambe wa watu flani.
nimebahatika kutembekea nchi tatu jirani,National Ids zako hazina hizo chip mnazosema,kwanza upatikanaji wa ID inaanzia kwa balozi wako ,then mwenyekiti wa mtaa,then form yako inapelekwa kwa karibu tarafa,from there to the district level then finally national level.
Leo hapa kwetu waliojiandikisha mwaka Jana tena hapa hapa Dar hadi Leo hawajapata vitambulisho vyao,na waliotumiwa SMS na NIDA walienda kuchukua wengine wakikosa,hata hao waliochukua vilikusanywa tena due to kasoro mbali mbali,what a shame.
complications hizi zote zinatokana na watu kupiga deal,yaani tunaingia kwenye mambo makubwa wakati hatujajiandaa vizuri technologically .
swala la national IDs linaitaji umakini wa hali ya huu Sana,kazi kubwa inafanyika grass root level huku ndio anapotambulika muombaji,yeye ni Mtoto wa nani na mjukuu wa nani,its not a mater ya u hire few staffs Kama vile wanao andikisha wapiga kura.
kwanza kazi hii ilikuwa inatakiwa ifanywe na wazawa wa eneo husika,Kama nilivyo ainisha hapo juu.

Mkuu hapa penye maandishi mekundu natofautiana na wewe,je pale tunapoambiwa tuwe na passport/kitambulisho cha kupigia kura/NSSF/Leseni je kuna mitambo inayo soma hizo chip kwenye hayo mabenki?jibu ni kuwa hakuna,unachofanya ni kutoa photocopy ambayo karani anabaki nayo na anaangali hicho kitambulisho/passport basi mchezo umekwisha.Kwahiyo mimikwa hilo baado sijaona sababu za National ID kukataliwa ,kwanza National ID nibora kuliko hizo IDs zingine,kwani zina hadi kijiji.mtaa uliozaliwa wakati hivi vingine vinaeleza tu wilaya uliyozaliwa.
 
Si kweli kwamba hakuna ID isiyo kuwa na mwisho wa matumizi kama unavyojaribu kuhaminisha. Hiki ni kitambulisho cha uraia sasa kwa nini kiwe na mwisho wa kutumika? Usilinganishe kitambulisho hiki na kitambulisho cha kazi au benki. Nimekupa mfano wa majirani zetu Kenya national ID hazina expiry date.

Lakini pia nafikiri tunge tofautisha ID ya uraia na passport. Passport kwisha muda ni sawa kwani pamoja na kwamba ni chanzo kimojawapo cha mapato ya serikali lakini pia sura ya mtu inabadilika pia kwa ajili ya kuzeeka. Kitambulisho cha uraia inabidi kiwe cha kudumu na wala hakipashwi kuwa na mwisho wa kutumika. Wenzetu Italy wana vyeti vya uraia wanaviita codice fiscale, hivi ukiishapewa basi tena hakibadilishwi tena na wenzetu hawaweki picha ya mtu.

Anyway hata mkiamua kiishe muda wake ni sawa tu kwani hakiko linked na kitu kingine chochote. Viongozi wetu wangekua smart vitambulisho hivi vingepashwa kuwa linked na TIN ya TRA na driving licence.

We still have a long way to go.

Tiba

Pole kwa kutotambua hilo kuhusu mwisho wa matumizi.
Kitambulisho cha kitaifa ni short form ya passport. Tarehe ya kuzaliwa, mahali ulipozaliwa, majina yote matatu kirefu, tarehe ya kutolewa na mahali ilipotolewa, mwisho wa matumizi ingawa haina maana kutotolewa tena ila inamaanisha renewal, TIN number, mahali na address unapoishi, namba ya kadi, bila kusahau picha na sahihi ya mwenye kitambulisho. Kuna viashiria vya siri pia ndani ya kitambuliso kwa ajili ya kuhakiki utapeli.

Kitambulisho cho chote cha kumtambulisha mtu iwe kitaifa au kimataifa mwisho wa matumizi yake ni miaka kumi, kwa vile binadamu anazaliwa, anakua, anazeeka na mwisho hufa, hivyo sura na umbo hubadilikabadilika, hali kadhalika makazi pia, ndio maana lazima vitu hivyo vyote muhimu viwemo na kwamba kila baada ya miaka kumi abadilishe kupata kitambulisho kipya.

Soma bandiko langu katika mada hii #97 ambalo nimeambatanisha taswira za vitambulisho vya kitaifa Tanzania na mataifa mengine, kisha linganisha mapungufu tajwa katika kitambulisho chetu kwa ulinganifu na vitambulisho vya mataifa mengine.

CC;
mfianchi
 
Back
Top Bottom