Rev. Kishoka
JF-Expert Member
- Mar 7, 2006
- 4,526
- 1,529
Wakati tunagombania ulaji wa Vitambulisho vya Taifa, ni lazima tuwe wakweli tujiulize huu uharaka wa kukamilisha hili zoezi, huku ukweli ni kuwa ni asilimia 25 (25%) au juu kidogo ndio watakuwa na manufaa na kufanikisha zoezi hili.
Asilimia hii ndogo ni ya wale walioko mijini, wenye akaunti benki na kuajiriwa.
Mimi najiuliza, kwa nini tusibadilishe mwondoko huu wa Vitambulisho kwa kuufanyia kazi kwa makini na kuleta matunda ya manufaa?
Kama ni gharama, tupende tusipende, lazima tutaingia gharama. Je kufanya zoezi hilo leo ni muhimu kuliko kesho au jana? Jibu ni kuwa hakuna lililobora pamoja na kilio cha kusema tusitumie hizo pesa kutengeneza vitambulish, bali tununulie mahindi na dawa za malaria.
Mimi nina mawazo tofauti na kwa Ukihiyo wangu, naonelea kuwa zoezi hili lina walakini si kwa ajili ya harufu ya uhujumu au ufisadi, bali limekosa umakini unaohitajika ambao unelipa zoezi zima la vitambulisho vya Taifa maana.
1. Tunafanyaje zoezi huku hatuna mfumo bora wa kufuatilia vifo na uzazi? Je kule Dongobesh anapozaliwa Mmang'ati anapewa cheti cha kuzaliwa na nani? siku akifa ni nani anatoa hati ya kifo?
2. Yule mmaonde wa Beira aliyehamia Tanzania na watoto wake wakakulia Newala, na kakaa vizuri na mwenyekiti wa kaya, tutahakikishaje yeye huyu mmakode au wale watusi na wacongo wa mipakani hawatajifanya ni Watanzania kwa kuidhinishwa uhalali wao na mwenyekiti wa kata na si cheti cha kuzaliwa ambacho watadai hawana kama yule Mmang'ati?
Je sisi wengine wakimbizi wakazi wa nje ya nchi tutapewa vitambulisho hivi?
Je suala la uraia wa nchi mbili likoje kwenye suala hili nyeti la vitambulishi vya Taifa?
Sasa ukishayasoma maswali haya mawili, Mchungaji anasema badala ya kuleta vitambulisho, uanze zoezi la kuboresha takwimu na kumbukumbu kupitia sensa.
Ndiyo nimesema Sensa ambayo tulishindwa kuifanya hivi karibuni kwa ukosefu wa fedha.
Ushauri wangu ni huu: tujiandae kikamilifu kufanya zoezi la sensa ambalo:
Suali linakuja, jee tutapeleka teknolojia kwa kila kona ya nchi? je tutaruhusu hospitali na zahanati kutoa vyeti vya kuzaliwa na kifo na kuhakikisha kuwa vinasajiliwa na kuhifadhiwa katika mkongo wa Taifa wa kumbukumbu (database)?
Je leo hii tunapojenga mtambo wa fibreoptic kwenye bahari, hatuwezi kuupitisha kwa kila mkoa na wilaya ili tuwezekujenga mtandao mzuri wa teknolojia amba utaweka kumukumbu hizi za watu, leseni za magari, leseni za biashara, kufuatilia kodi, kadi ya kupiga kura, kutoa pasipoti na vitu vingine ambavyo ni muhimu na tunataka kuvipatia ufumbuzi kwa kutumia vitambulisho vya Taifa?
Hofu yangu ni kuingia gharama mara kumi, kwa kitu ambacho tungeweza kukifanya kwa umakini na mapana na hivyo kutoa suluhisho la matatizo yote.
Ikiwa Uhamiaji, BRELA na Usalama wa Barabara na Tume za uchaguzi bado wanatumia madaftari na uthibitisho wa mwenyekiti wa kaya na tarafa, je tunategemeaje kuwa tukitoa vitambulisho vya Utaifa tutaleta hatua za kiteknolojia?
Asilimia hii ndogo ni ya wale walioko mijini, wenye akaunti benki na kuajiriwa.
Mimi najiuliza, kwa nini tusibadilishe mwondoko huu wa Vitambulisho kwa kuufanyia kazi kwa makini na kuleta matunda ya manufaa?
Kama ni gharama, tupende tusipende, lazima tutaingia gharama. Je kufanya zoezi hilo leo ni muhimu kuliko kesho au jana? Jibu ni kuwa hakuna lililobora pamoja na kilio cha kusema tusitumie hizo pesa kutengeneza vitambulish, bali tununulie mahindi na dawa za malaria.
Mimi nina mawazo tofauti na kwa Ukihiyo wangu, naonelea kuwa zoezi hili lina walakini si kwa ajili ya harufu ya uhujumu au ufisadi, bali limekosa umakini unaohitajika ambao unelipa zoezi zima la vitambulisho vya Taifa maana.
1. Tunafanyaje zoezi huku hatuna mfumo bora wa kufuatilia vifo na uzazi? Je kule Dongobesh anapozaliwa Mmang'ati anapewa cheti cha kuzaliwa na nani? siku akifa ni nani anatoa hati ya kifo?
2. Yule mmaonde wa Beira aliyehamia Tanzania na watoto wake wakakulia Newala, na kakaa vizuri na mwenyekiti wa kaya, tutahakikishaje yeye huyu mmakode au wale watusi na wacongo wa mipakani hawatajifanya ni Watanzania kwa kuidhinishwa uhalali wao na mwenyekiti wa kata na si cheti cha kuzaliwa ambacho watadai hawana kama yule Mmang'ati?
Je sisi wengine wakimbizi wakazi wa nje ya nchi tutapewa vitambulisho hivi?
Je suala la uraia wa nchi mbili likoje kwenye suala hili nyeti la vitambulishi vya Taifa?
Sasa ukishayasoma maswali haya mawili, Mchungaji anasema badala ya kuleta vitambulisho, uanze zoezi la kuboresha takwimu na kumbukumbu kupitia sensa.
Ndiyo nimesema Sensa ambayo tulishindwa kuifanya hivi karibuni kwa ukosefu wa fedha.
Ushauri wangu ni huu: tujiandae kikamilifu kufanya zoezi la sensa ambalo:
- kwanza litatupa idadi kamili ya Watanzania,
- pili tuhakikishe kuwa katika zoezi hili, tunathibitisha Utaifa ama kwa watu kutoa vyeti vya kuzaliwa au kithibitisho kingine kile kinachokubalikakuwa huyu ni Mtanzania
- tatu, wakati wa zoezi hili, namba za Taifa zitolewe kwa wananchi an zirekodiwe kwa teknolojia bora
- nne, sensa, ibainishe yafuatayo, jinsi, umri, elimu, kipato, dini na ajira
Suali linakuja, jee tutapeleka teknolojia kwa kila kona ya nchi? je tutaruhusu hospitali na zahanati kutoa vyeti vya kuzaliwa na kifo na kuhakikisha kuwa vinasajiliwa na kuhifadhiwa katika mkongo wa Taifa wa kumbukumbu (database)?
Je leo hii tunapojenga mtambo wa fibreoptic kwenye bahari, hatuwezi kuupitisha kwa kila mkoa na wilaya ili tuwezekujenga mtandao mzuri wa teknolojia amba utaweka kumukumbu hizi za watu, leseni za magari, leseni za biashara, kufuatilia kodi, kadi ya kupiga kura, kutoa pasipoti na vitu vingine ambavyo ni muhimu na tunataka kuvipatia ufumbuzi kwa kutumia vitambulisho vya Taifa?
Hofu yangu ni kuingia gharama mara kumi, kwa kitu ambacho tungeweza kukifanya kwa umakini na mapana na hivyo kutoa suluhisho la matatizo yote.
Ikiwa Uhamiaji, BRELA na Usalama wa Barabara na Tume za uchaguzi bado wanatumia madaftari na uthibitisho wa mwenyekiti wa kaya na tarafa, je tunategemeaje kuwa tukitoa vitambulisho vya Utaifa tutaleta hatua za kiteknolojia?