Vita Dhidi ya Madawa ya Kulevya: JamiiForums na wanachama wake wanaongoza!. Lets Be More Proactive!

Pascal Mayalla

Platinum Member
Sep 22, 2008
50,582
113,776
Wanabodi,
Kwenye hii vita ya madawa ya kulevya iliyopamba moto baada ya kupata chachu mpya toka kwa Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda , nimepata fursa kupitia mabandiko ya wana JF wengi.

Kama serikali ingekuwa inatoa tuzo kwa taasisi mbalimbali zilizo mstari wa mbele katika vita hii, ni pamoja na Mtandao huu wa JamiiForums, umeweka thread maalum kupiga vita madawa ya kulevya, na kuifanya sticky.

JamiiForums most of the times JF tumekuwa very active as a passive whistle Blower, sasa tuwe more proactive kwa wana JF kujitokeza kumsaidia Makonda, Mwigulu na Jeshi letu la Polisi kusaidia any info we have kupitia michango ya wana JF humu. I don't know how we can achieve this, bali tusiishie kusema tuu, kama tunaweza kutenda, pia tutende no matter how little it might be, but let's do something.

Mfano hata tuki print tuu mabandiko kuhusu Madawa ya kulevya na kutoa Hard Copy 10 tuu, it's not nothing, it is something.

Hizo Copy 10 za kwanza zitue Kwenye meza za hawa wafuatao
1.Rais wa JMT
2.VP
3.PM
4.Waziri wa Mambo ya Ndani.
5.IGP
6.Director wa TISS
7.Director wa Immigration
8.Director wa PCCB
9.Director wa Tume ya Madawa
10. Paul Makonda.

Hongera sana, Mike, Max na wana JF wengine wote mnaochangia vita hii, let's keep fighting hata kama mchango wetu hauonekani, ila tunajiwekea akiba nzuri sana ya good karma ambayo ina thamani kubwa kuliko tuzo yoyote.

Nawatakia Jumapili Njema.
Paskali.

NB: Usisahau kupitia hii thread=>Madawa ya Kulevya na aibu ya Tanzania - Yatosha sasa!

Pascal Mayalla Said;
Nikiwa mwandishi wa newsroom wakati huo nikiishi Ilala, nikapangwa kusafiri na Mkapa Sweden, US na UK, three days kabla ya safari majira ya saa 3:00 nikatembelewa na ugeni wa jamaa wawili, mwanamke na mwanaume. Wakajitambulisha na kunieleza nía ya ugeni wao.

Kiukweli nilishangaa jinsi walivyojua niko kwenye msafara, ndipo wakanijulisha mizigo yetu yote inapelekwa Ikulu siku moja kabla ya safari na haikaguliwi inasafirishwa under a diplomatic bag. Wakaniomba niwabebe parcel yao, kuwa ndiyo the safest way na kila siku ndio zao! . Fungu nililotajiwa sikuamini. Kiukweli roho ilinidunda, bulungutu limetolewa na kuwekwa mezani ni mshahara wa zaidi ya miaka 10 ya kiwango changu!.

Kiukweli niliogopa, what if itajulikana?!. Wakanihakikishia its never na wengine wote wanabeba! . Kiukweli niliogopa nikawaambia siwezi! . Jamaa walinishawishi sana mwisho wakakasirika na kuondoka kwa hasira huku wakinilaani nitakufa masikini!. Pia walinionya nikisema popote hata kwa mke wangu, wao watajua na kitakachonifika sitaweza kusimulia! .

Nikasafiri na msafara na kweli a day kabla ya safari mizigo ni Ikulu na siku ya kurudi inakabidhiwa hotelini unakuja kuipokelea Ikulu a day baada ya kurudi.

Kiukweli tukiwa huko majuu ndipo nikashangaa wenzetu wanavyofanya mi shopping ya nguvu, umasikini wa Tanzania unajulikana, mishahara ya serikali ya enzi hizo inatilisha huruma, lakini maofisa wadogo wadogo tuu wana má jumbo suitcases mawili matatu yamejaa vitu vya thamani, nikahisi usikute ni kweli! ,hivyo kuna umasikini wa baadhi yetu ni umasikini wa kujitakia. Safari zilizofuata nikataka kushawishika, roho ikakataa, bora kuwa masikini wa kutupwa with peace of mind luliko kuwa tajiri mwenye mashaka.

That was then, sijui how the situation is of now, ndio maana kulipoibuka tuhuma hii kuhusu China, niliuliza swali hili.
Membe amejuaje Contents za 'Diplomatic Bag'? Uwezo kukanusha kaupata wapi? - Tusidanganyane!
Paskali

 
JamiiForums Ipo juu sana kwa kila jambo.

Cha ajabu na hovyo kabisa serikali hii ya ccm haitaki whistleblowers.

Badala source hizi serikali izitumie kufikia malengo MUJARABU wao nikutisha nakufunga midomo

Bwana mkubwa aachie watu waseme yeye afanyie kazi taarifa sio kutufunga na kututishia.

Mwigulu....mzigo huo hapo juu....natimu yako fanyia kazi acha kufungafunga Cdm na Cuf ....nikujipotezea weledi.
 
Mkuu Pasikali una ushauri mzuri sana huenda ukifanyika unaweza kusaidia lolote. Ila nikuulize, hivi unadhani hao uliopendekeza hawajui? Huenda wao hawana muda au si wasomaji wa mitandao ya kijamii hususani jf. Je hata wapambe wao hawaoni? Mbona mtu akitukana mara moja wanawaambia na hatua zinachukuliwa?
 
Mkuu Pasikali una ushauri mzuri sana huenda ukifanyika unaweza kusaidia lolote. Ila nikuulize, hivi unadhani hao uliopendekeza hawajui? Huenda wao hawana muda au si wasomaji wa mitandao ya kijamii hususani jf. Je hata wapambe wao hawaoni? Mbona mtu akitukana mara moja wanawaambia na hatua zinachukuliwa?
Mkuu Tindo
Kwanza kuna tofauti kubwa kati ya impact ya kusoma soft copy online
na hard copy mezani kwako.

Pili matukio mengi yametokea zamani, sii rahisi mtu kupata muda wote kupitia threads zote ziko very scattered lakini ukimfanyia compilation na kumtupia mezani ni tofauti.

Tatu mengi yalitokea nyakati zile za thamani ya mtu ni pesa zake, hivyo kama unapesa hadi ikulu inanunuliwa. Huu sasa ni wakati mwingine, thamani ya mtu ni utu wake na sio pesa zake.

Mfano tuhuma hii

https://www.google.com/url?sa=t&sou...x28jtvfnGP_UlkifA&sig2=wvvbiqcj0JbWWioIQKqt7g
Watu wametajwa hadi majina, na viwango vya fedha walizopokea na the Don mwenyewe pia anajulikana ila hakutajwa kwa sababu huyu mlalamikaji anakijua kitakacho mkuta yoyote atakaye mtaja jina the Don.

Paskali
 
Hii vita mh. Makonda anastahili pongezi kwa uthubutu. Ameonyesha ujasiri wa hali ya juu.
Its high time apewe uwaziri wa mambo ya ndani ili amalize changamoto nyingi zinazolikabili taifa letu
Naunga mkono hoja.
Paskali
 
Tangu nyuzi hizi ziwekwe hapa hadi sasa kwa kias gani wenye mamlaka wamezitumia?Leo hii RC ndo anamuibua IGP.Kwa Kino hakuna raia asomjua Swai na Makufuli,leo hii askar 12 wanatiwa nyavuni kwa unga,hata ukipeleka taarifa polisi bado kuna masalia,hilo jeshi walisafishe
 
Kuna uzi mmoja niliandika comment nilisema usalama wa taifa na polisi wanahusika na kuuza na kusafirisha madawa, kuna lijamaa lilinikomalia na kusema nitaishia segerea kwa kuwasingizia. Juzi Makonda kawataja polisi 12 pia kuna muuza ngada mmoja anamtumia mpaka mkubwa mmoja wa polisi na kumwambia kijana wako flani mpeleke sehemu flani anifanyie kazi yangu vizuri. Yupo rafiki yangu kaishia south afrika alikamatwa na yule dada mwenye makalio makubwa, Na yule aliekamatwa China (Jack) nilijua ataisha tu nilipomuona na kuna rafiki yangu mmoja muuza ngada mkubwa na lina mahela hatareee.
 
Mimi naamini hii vita ina baraka za JPM, mimi naamini combination ya JPM, Mwigulu na Makonda mbona kitaeleweka tu!!

Madawa ya Kulevya yanawafanya watumiaji wawe kama mazombi!. hapana aisee, hayakubariki hata kidogo, lazima hii vita ipiganwe!!!

Napendekeza sheria itungwe, mtumiaji na msambazaji wote wapigwe risasi, hiyo itapunguza sana!!
 
Mkuu Pasikali una ushauri mzuri sana huenda ukifanyika unaweza kusaidia lolote. Ila nikuulize, hivi unadhani hao uliopendekeza hawajui? Huenda wao hawana muda au si wasomaji wa mitandao ya kijamii hususani jf. Je hata wapambe wao hawaoni? Mbona mtu akitukana mara moja wanawaambia na hatua zinachukuliwa?
Akiwakosoa tu wao hukimbilia kusema wametukanwa/mchochezi/anahatarisha amani ya nchi.

Yaani hawa watu kama hawana akili timamu siwaelewi hata.
 
Back
Top Bottom