Vipepeo weusi season 2: From Zurich with rules

Vipepeo weusi season 2: From Zurich with rules

Na nyie mmezidi kuwa wazuri sana
Nafsi ni shida sana inatamani kila kitu
Ukipata mweupe unataka mweusi ukipata mnene utataka mwembamba Mara mwenye chura Mara nini sijui yaani
Wanaume tumeumbwa Mateso Mateso kuhangaika [emoji443] [emoji444] [emoji442] [emoji442] [emoji443] [emoji444] [emoji445]
Mtamaliza mabucha nyama ni ileile
 
Mtamaliza mabucha nyama ni ileile
Aaah, mabucha mengine nyama ya juzi, mengine kachinjwa ng'ombe mzee.

Watu wanataka fresh meat!

[emoji39] [emoji39] [emoji39] [emoji39] [emoji39]
 
Sawa endeleeni
Aaah, mabucha mengine nyama ya juzi, mengine kachinjwa ng'ombe mzee.

Watu wanataka fresh meat!

[emoji39] [emoji39] [emoji39] [emoji39] [emoji39]
 
Wakuu vipi imeisha hii simulizi au bado??
Maana naogopa alosto
 
VIPEPEO WEUSI


SEASON 2 – FROM ZURICH WITH RULES


EPISODE 16


Mara nyingi sana katika maisha kadiri ambavyo utakuwa unahangaika kutoka kwenye jambo ndivyo ambavyo unakuwa unapalilia kina cha kuzama. Ni kama vile kuzama kwenye bwawa lililojaa tope tupu, kadiri ambavyo utahangaika kujiokoa ndivyo ambavyo unazama zaidi na zaidi.

Ndivyo namna ambavyo maisha yanakupa kitendawili mara nyingi, kitendawili ambacho jawabu lake ni fumbo na kadiri ambavyo utaling’amua hilo fumbo ndivyo unaingia kwenye sintofahamu ya fumbo kubwa zaidi.

Unapozama kwenye bawa lenye tope tupu, busara ni ipi? Utulie tu na kushuhudia nafsi yako ikiondokewa na uhai au uhangaike na kuzama zaidi ndani ya tope?

Ni ajabu kwa kiasi gani maisha yanaweza kugeuka na kuwa uwanja wa mahangaiko… kadiri tunavyohangaika kuboresha maisha yetu ndivyo kadiri ambavyo tunazidisha msongo vichwani.
Ni ajabu namna gani ambavyo kadiri tunavyojitahidi kujifunza na kufahamu ndivyo ambavyo maswali mengi zaidi yanaibuka vichwani.
Ni ajabu ni namna gani ambavyo tunapenda ndivyo ambavyo tunazidi kuumiza mioyo yetu.

Ni ajabu ni namna gani tumezaliwa na kupewa aina ya maisha ambayo hatukuiomba. Maisha ambayo yanahitaji mapambano kuyajaza fahari. Mapambano ambayo muda mwingine yanaweza kuchukua miaka yetu yote ambayo tutaishi hapa duniani.

Ni ajabu kwa nini tumetengewa maisha ambayo tunayo.!


Japo tayari zilikuwa zimepita karibia dakika tano tangu nifike nje ya mgahawa huu wa kichina lakini bado nilikiwa nashindwa kufanya uamuzi wa nini hasa cha kufanya.

Mlango wa mgahawa ulikuwa umefungwa na kibao kilichosomeka “CLOSED” kilikuwa kinaning’inia mlangoni. Japokuwa mgahawa huu mbele ulikuwa na vioo tupu lakini sikuweza kuona ndani kutokana na giza na taa zake kuzimwa. Kuna hisia fulani nilikuwa naipata kwamba kulikuwa na uwezekano mgahawa huu ulikuwa haujafunguliwa kwa siku kadhaa, labda pengine tangu siku ile nilipofika hapa. Haikuwa sawa sawa kwa mgahawa hapa Zurich kufungwa muda huu kwa sababu hata saa tatu usiku ilikuwa haijafika bado.

Mvua bado ilikiwa inanyesha na nilikiwa naloa nikiwa nimesimama hapa nje ya mgahawa najiuliza ni nini hasa natakiwa kufanya ingawa hata nilikuwa sijui ni kwa nini hasa nilikuwa hapa. Mfukoni mwangu nilikiwa na kijipande cha karatasi nilichokitoa kwenye lile lundo la makabrasha nililoacha hotelini. Nilichukua kipande hiki tu cha karatasi ambacho kilikuwa na maandishi yaliyofutwa futwa yote yakiacha neno moja tu “MELCHIZEDEK”, pamoja na Picha ya mgahawa huu.

Kwa hiyo sababu pekee ambayo ilikuwa imenileta hapa ilikuwa ni kwa sababu picha yake mgahawa huu ilikuwa kwenye makabrasha ambayo nilikabidhiwa na Hudini. Sikujua ni nini hasa nilikuwa nakitafuta lakini niliamini tu kwamba ingeweza kunifumbua macho juu ya lengo langu la kuwa hapa Zurich.

Katika muda kama huu ndivyo ambavyo nilijikuta kwa kiwango fulani nilikuwa najuta kwa nini nilikuja hapa Zurich? Nafsi yangu mara kadhaa nilijikuta kama kuna sauti inaniuliza, kwa nini uko hapa?

Yote kwa ajili ya kukonga kiu yangu ya kutaka kujua. Yote kwa sababu ya kukonga kiu yangu ya fumbo ambalo marehemu baba yangu alinifumba siku ambayo alijitoa uhai wake mbele yangu.
” Au labda kuna lingine la zaidi akilini mwangu ambalo naogopa kulikiri hata kwa nafsi yangu mimi mwenyewe?” Nilijikuta najiuliza moyoni mwangu. Kwamba labda kuna jambo la zaidi kuhusu The Board ambalo nafsi yangu ilikuwa imeshawishika lakini nilikuwa nashindwa kukiri ndani ya nafsi yangu.

Nikaliondoa hilo wazo haraka kichwani mwangu. Nikarejesha akili yangu kwenye lililo mbele yangu, mgahawa huu wa kichina.

Mvua bado ilikuwa inanyesha kwa fujo, ikimiminika mwilini mwangu kama vile wingu lilikuwa juu ya kichwa changu.

Kama ilivyo kwa mgahawa mingine yote niliamini kabisa kwamba pia hata mgahawa huu wa kichina lazima nao utakuwa na mlango wa nyuma. Mlango ambao unaenda moja kwa moja jikoni kama ilivyo ada kwenye mgahawa mingine yote.

Sikuwa na hakika sana mlango huu nilikiwa nauhitaji kwa sababu gani lakini hulka yangu ya kutorudi nyuma ilikuwa inanisukuma kufanya hivyo. Baada ya kufika hapa tu mgahawani japokuwa nimeukuta umefungwa lakini kwa namna nilivyo si jambo ambalo linawezekana kwangu kugeuza na kurudi hotelini kwangu bila kufanya chochote kile.

Mgahawa huu ulikuwa kwenye Jengo lenye kama ghorofa tano juu ambalo sikujua kama juu lilikuwa linatumika kama makazi ya watu au maofisi. Pembezoni kwa jengo kulikuwa na uchochoro unaoingia na kufanya kama unazunguka nyuma ya jengo. Niliamini kabisa kama kulikuwa na mlango wa nyuma wa kuingia jikoni basi mlango huo utakuwa kwenye uchochoro huu.

Sikutaka kupoteza muda, nikaanza kutembea kuufuata huu uchochoro.

Mvua bado ili kuwa inaendelea kunyesha na nilikuwa naendelea kuloa.

Sauti ya ngurumo ilivyokuwa inapiga, radi ikimetata meta kila baada ya dakika kadhaa, matone yenyewe ya mvua mfululizo, kila kitu kilikuwa kinafanya nafsi yangu kujipa tathimini. Kila tone la mvua ambalo nilikuwa nalisikia likitiririka kutoka kichwani, shavuni na kisha mwilini, yalinikumbusha machozi yote ambayo nimewahi kuyasababisha kwa watu kutokana na maamuzi ambayo nimewagi kuyanfanya na nilijikuta najiuliza kwa hiki ninachokifanya sasa hapa Zurich huko mbeleni nitasababisha machozi kwa watu wangapi?

Na kila ambapo sauti ya ngurumo ikilia ilinifanya nijisikie hasira. Hasira juu ya nafsi yangu mwenyewe, hasira juu ya maamuzi ninayoyafanya kila siku ambayo yanaweza kuleta vidonda visivyo pona nafsini. Lakini kila baada ya dakika kadhaa radi ilipiga. Japokuwa mwanga wake uliangaza kwa kasi kuweza macho yangu kuufaidi nuru yake, lakini kila muda mwanga wa radi ulipooiga nilijikuta moyoni najipa moyo, najifariji kwamba labda iko nuru mbele, liko tumaini. Kwamba maumivu yote haya yanastahili ilo kufikia nuru hiyo.

Nikaendelea kuufuata ule uchochoro. Kulikuwa na malundo kadhaa ya mifuko mikubwa ya plastiki, meusi ambayo ilikuwa imejaa taka za vyakula. Moyoni nikajipongeza kuwa nilikuwa sahihi, uchochoro huu ulikuwa unaelekea moja kwa moja kwenye mlango wa nyuma wa mgahawa kuingia jikoni.

Nikatembea hatua kadhaa kupita ile mifuko ya plastiki ya kuwekea taka. Nilipoipita na kutembea kama hatua tano tu nikakutana na mlango. Mlango wa chuma kama geti dogo tu la kawaida la rangi nyeusi. Nilipoufikia tu mlango bila kujiuliza mara mbili au kufikiri sana nilinyoosha mkono na kuujaribu kufungua. Mlango ulifunguka.

Nilishangaa. Ilimaanisha kwamba mlango ulikuwa umeegeshwa tu bila kufungwa na funguo. Kwa hiyo ilikuwa na maana kwamba kulikuwa na watu huku ndani jikoni japokuwa mgahawa ulikuwa umefungwa kule mbele.

Nilipiga hatua na kuanza kuingia ndani kwa tahadhari kubwa sana. Nilihakikisha kuwa kila hatua ambayo nilikuwa nakanyaga chini haikuwa inasikika. Nikaingia ndani na kuufunga mlango kama ambavyo nilikuwa nimeukuta. Ndani taa zilikuwa hazijawashwa hivyo kulikuwa na kiza kikubwa. Nilitamani ninyoonye mkono ukutani kupapasa kutafuta swichi ili niwashe taa, lakini sikutaka kufanya chochote kile tofauti na namna ambavyo nilipakuta hapa ndani kwa kuwa nilihofu uwepo wa watu wengine humu.

Nilisimama ka karibia dakika mbili kuyapa macho yangu muda wa kuzoea kiasi hali hii ya giza ili niweze kung’amua vitu japo kwa uchache.

Nikaanza kuona japo kwa mbali sana na kwa uhafifu. Nilikuwa kwenye korido ambayo kama hauta saba kutoka nilipo kulikuwa na mlango unaoingia kulia ambako niliamini kwamba huko ndiko kwenye jiko. Hatua kama tano hivi kutoka mlango huo kulikuwa na mlango mwingine ambao nao ulikuwa mkono wa kulia ambao nao nilihisi kwamba ulikuwa unaelekea mgahawani kule mbele ambako hukaa wateja.


Mkono wa kushoto kulikuwa na mlango mmoja tu ambao sikujua hasa ulikuwa ni mlango wa nini.

Nikaanza tena kutembea kwa kunyata nikihakikisha hakuna hata hatua yangu moja ambayo ilikuwa inasikika nikikanyaga hapa sakafuni.

Nikatembea haraka haraka lakini kwa tahadhari kubwa sana na kisha nikakunja kulia kwenye mlango wa kwanza ambao niliamini kuwa ulikuwa ni mlango wa jikoni. Kutokana na kuukuta ule mlango wa nje uko wazi nilikuwa na imani kubwa sana kuwa japokuwa humu kulikuwa na giza lakini sikuwa peke yangu. Kuna sababu kwa nini mlango ule umeachwa wazi.

Kutokana na kitete changu cha kutembea haraka haraka, nikajikuta nimekanyaga kitu sakafuni… sijui ilikuwa ni sufuria, sijui ni sahani lakini ninachokumbuka ni kwamba kilitoa mlio mkubwa. Moyo ulipasuka na kutulia kimya kabisa kusikilizia kama nitasikia mtu yeyote anakuja.

Sikusikia mtu akiwa anakuja, wala sikusikia purukushani yoyote ile, nilishituka tu taa ikiwa imewashwa na kijana wa kichina aliyevalia suti nyeusi na bastola mkononi akiwa amesimama mbele yangu.

“…#####%%&&&&&&&#…”

Sikuelewa alichokuwa anakiongea. Alikuwa anaongea kichina kwa jazba huku ameinua bastola na kuninyooshea.
Nilibakia nimetumbua macho na kuinua mikono huku natetemeka.

“Don’t shoot. Don’t shoot.!” Niliongea huku nimeinua mikono juu natetemeka.

“…#&#$&$&#&$…!”

Aliongea tena kwa jazba bado bastola ikiwa imeelekea upande wangu.

“Melchizedek.!! I’m looking for Melchizedek.!” Nilijikuta naropoka bila hata kuelewa kama nilikuwa sahihi au ni kwa namna gani kutaja jina hilo la Melchizedek kungenisaidia mchina huyu aliyepandwa na mori asinitandike risasi.

Lakini nilipotaja tu jina la Melchizedek niligundua kwamba alipatwa na mshituko ghafla usoni.

“..&$%*##&$##..!” Aliongea kitu fulani hivi kwa kichina lakini alikiongea kwa taratibu huku amenikazia mamcho. Nilihisi alisema “Umesemaje?”

“Melchizedek.! I’m looking for Melchizedek.!” Nikarudia tena kujibu.

Hakunisemesha kitu chochote kile. Alinifuata haraka pale nilipo na kunikunja shati kifuani na kuanza kunivuta kutoka mule jikoni.

Alinivuta huku anatembea haraka mpaka tukafika koridoni. Kote huku nako taa zilikuwa zimewashwa. Aliendelea kunivuta tukauvuka ule mlango unaopinda kulia kwenda mgahawani kwenyewe, alinivuta mpaka kwenye mlango ambao ulikuwa upande wa kushoto. Hakukuwa na chumba bali kulikuwa na ngazi kuelekea ghorofa ya juu.

Tulipanda ngazi haraka haraka huku akiendelea kunivuta shati kwa nguvu mpaka tukatokezea juu ghorofani ambako mbele yetu kulikuwa na mlango. Akagonga mlango kwa haraka kama kulikuwa na dharura fulani hivi. Mlango ukafunguliwa na akanitutusa na kunitupia ndani.

Kulikuwa na lijichumba likubwa mno. Karibia nusu ya ‘floor’ yote ilikuwa ni lichumba hili au ‘hall’ naweza kusema.

Kulikuwa na makorokoro mengi sana lakini mengi yakiwa ni maboksi yaliyotengenezwa kwa mbao ambayo sikujua mara moja yalikuwa na nini hasa ndani yake.

Upande mmoja kulikuwa na meza na kiti kama ofisi na juu ya kiti alikuwa ameketi yule mzee wa kichina. Ni mzeebyule yule ambaye alinichoma sindano ya kemikali siku ya kwanza nilipokuja hapa na nikazimia na kuja kuzinduka nikiwa kwenye jengo kule mtaa wa Hardstrasse. Pamoja na yeye kulikuwa na vijana wengine wenye asili ya kichina kama kumi hivi.


“….##&&$&##%#&##&…Melchizedeck…!”

Yule jamaa ambaye alinikwida na kunileta hapa msobesobe alizungumza kichina na nilifanikiwa kung’amua neno “Melchizedek” kwenye sentensi zake.

Wote mle ndani akiwemo yule mzee wa kichina niliwaona wameshituka ghafla baada ya yule mwenzao kutamka jina la “Melchizedek”.

Yule mzee wa kichina aligeuka na kunikazia macho kwa karibia dakika tatu bila kusema neno lolote lile. Alikuwa kama anatathimini kitu fulani hivi. Nadhani uwepo wangu hapo na kile ambacho mwenzake alikuwa amemueleza.


“Is it true?” Aliniuliza bado akiwa amenikazia macho.

“What? I didn’t understand what he said!” Nikamjibu huku nikijitahidi nionyeshe taswira ya kujiamini.

“Is it true that Melchizedek sent you here?” Hakupepesa macho hata kwa sekunde. Aliniuliza huku ananiangalia moja kwa moja akiwa amekaza macho.

Sikuwa na muda wa kufikiri au kutafakari nitoe jibu gani. Kwa jinsi ambavyo alikuwa amenikazia macho kama ningethubutu kutafakari japo kwa sekunde tu basi angehisi nilikuwa nadanganya. Na kwa kuwa hakutaka nidanganye basi nikachukua uamuzi wa kumdanganya. Bila kufikiria sana nikajikuta tu nimeropoka,

“Yes! Melchizedek sent me here..!!”

Niliona mshituko wake usoni. Mara moja alisimama kutoka pale kwenye kiti ambako alikuwa ameketi. Sikujua kama ilikuwa ni hasira au alikuwa kwenye mshangao. Nakumbuka tu aliinuka haraka na kwa taharuki na kuanza kutembea kwa haraka kunifuata pale nilipo.

Nilianza kutamani labda nisingesema uongo. Lakini kwa kuwa tayari nimeshaanza na uongo niliousema basi napaswa kusimamia uongo huo. Lakini mtihani niliokuwa nao ni kwamba hata huyo Melchizedek sikumjua ni nani au anafanya nini au ilikuwa na maana gani.

Japokuwa mzee huyu anajifanya kufanya biashara ya mgahawa uliopo hapo chini lakini kwa hakika kabisa biashara yake halisi ilikuwa ni suala fulani la hatari au uhalifu kutokana na hawa vijana alionao ambao kwa mtindo ambao walikuwa wamevaa makoti yao ya suti nilikuwa na hakika kabisa kila mmoja wao alikuwa na silaha ya moto kiunoni.

Mzee alitembea mpaka mbele yangu kabisa tukawa tunaangaliana uso kwa uso.

“Where is the package?” Aliniuliza huku amenikazia macho na anapumua kwa hasira.

Nilitamani nimuulize “mzigo gani?” Lakini nikajua kuwa ndio nitaharibu kabisa. Nahitaji kutoka jibu la maana kabla hawajajua nadanganya na hata kile nilichotumaini kukipata hapa ili kinisaidie kwenye hizi harakati zangu nikakikosa.!!


Itaendelea…


THE BOLD
humorous episode😀
 
sasa ntaenda na ninyi sambamba ndio namaliza epispde ya mwisho kuwekwa hapa nimeanzia huko season 1 na sasa nipo hapa.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom