Habibu B. Anga
JF-Expert Member
- May 7, 2013
- 6,557
- 25,757
- Thread starter
- #241
VIPEPEO WEUSI
SEASON 1 – FROM ZURICH WITH RULES
Ilipoishia Episode 14…
“I think i have said enough… its your turn now! What happened to you? How did you get shot?” Akauliza huku anatoa tabasamu hafifu.
Nikakumbuka siku tatu zilizopita niliporejeshwa hotelini kwangu kutoka kule Wipkingen. Nikakumbuka kilichotokea masaa ishirini yaliyopita. Nikajiuliza kama ni sahihi kwangu kumuamini huyu mtu na kumueleza kila ambacho kilitokea. Nikakumbuka msemo wake wa fumbo kuwa “Kuna deni anataka kuwalipa Hudini”. Nikakumbuka alivyoeleza kuwa amekuwa akinitafuta kwa miaka kadhaa kwa kuwa aliamini akinipata mimi atawapata Hudini hasa kiongozi wao wa sasa, ambao alikuwa amekorofishana nao.
Nikakumbuka namna ambavyo hakunitambua mara ya kwanza na kutaka kuondoka. Nikakumbuka namna ambayo baada ya kumwambia mimi ni mmiliki wa hili jengo aliniita jina langu. Nikajiuliza kama alifahamu jina langu, na pia alifahamu mimi ni mtoto wa Charles kajuna, ameshindwaje kuijua sura yangu? Iweje anitafute miaka yote kama anavyosema na asiwahi kuona hata picha yangu?
Nikajiuliza tena kwa nini anieleza siri zote hizi. Kuanzia tatoo yake kifuani. Uanachama wake ndani ya Hudini. Shughuli za Hudini na hata ugomvi walio nao na juhudi zake za kuwapata ili “awalipe deni” kama anavyosema.
Nikajiuliza kama hakuna mtego hapa nimewekewa.
Nilikuwa nawaza haya huku nimejiinamia. Nikainua uso kumtazama. Alikuwa ananiangalia huku anatabasamu kama vile anaisoma akili yangu.
“What happened Ray? How did you get shot?” Akauliza tena huku anatabasamu.
Nikavuta pumzi ndefu na kuishusha. Isingelikuwa jeraha tumboni mwangu, ningeweza kuinuka na kutimua mbio.
Masaa 36 Yaliyopita…
Nilikuwa nimetoka usingizini baada ya kulala kwa masaa mengi tangu alfajiri ambapo nilirejeshwa na vijana wa Hudini.
Baada ya kuoga, kubadili nguo na kuonja kidogo chakula ambacho nilikuwa nimeletewa muda si mrefu na muhudumu wa hoteli nilikaa kitandani na kuanza kuchambua lundo la nyaraka ambazo nilipewa na Hudini siku ya Jana usiku kwenye like jumba lao linalonuka damu. Au niseme mzee ambaye kwa wakati huu nilikuwa nikiamini kwamba jina lake alikuwa ni Hudini.
Lilikuwa ni lundo la nyaraka pamoja na ile picha ya jamaa wa kizungu akiwa na Rais Albert Kafumu na picha nyingine akiwa na cheupe pamoja na baba yake.
Nikaziweka picha pembeni na kisha kuanza kupitia hizi nyaraka moja baada ya nyingine. Kwa namna fulani nyaraka hizi zilikuwa zinafanana na zile ambazo nilizikuta kwenye vault ndogo kule kwenye jengo ambalo nilisikiliza ujumbe wa marehemu baba yangu kwenye video.
Zilikuwa nyaraka ambazo ziliorodhesha umiliki wa mali ambazo nilikiwa sizijui, majengo, akaunti za benki. Pia kulikiwa na lundo la anuani za sehemu mbali mbali ambazo sikuelewa mara moja ni wa wapi na kulikuwa na maana gani.
Nilipitia nyaraka zote moja baada ya nyingine, lakini mpaka nilipofika karatasi ya mwisho bado nilikuwa naona maluelue tu. Ni kitu gani hasa ambacho nilikuwa natakiwa kukifanyia kazi kwenye nyaraka hizi? Niliona kila kitu orodha ya mali na majengo ambayo siyajui yalipo na wala sijawahi kuyaona. Niliona pia makumi ya namba za akaunti za benki! Napaswa kuchnguza moja baada ya nyingine? Niliona pia mamia ya anuani mbali mbali! Je napaswa pia kuchunguza kila anuani ambayo imeorodheshqa kwenye nyaraka hizi? Si itanibidi kukaa Zurich mwaka mzima?
“Fuuucckk.!!” Niling’aka peke yangu… huu ni zaidi ya uwendawazimu.
Nikainuka kutoka kitandani na kuanza kutembea kuelekea dirishani. Pembeni ya dirisha kulikuwa na kijimlango fulani hizi chembamba cha kioo ambacho nilikifungia na kutokezea kwenye ‘balcony’ ya chumba changu cha hoteli.
Nilisimama kwenye balcony na kuutazama mji wa Zurich. Namna mataa ambavyo yalikuwa yanang’ara usiku kama huu. Kulikuwa na manyunyu fulani ya mvua inayoanza. Kama ingelikuwa siku nyingine, nyakati nyingine ambayo haikuwa na maswali na mafumbo kichwani mwangu kama ilivyo sasa. Kama ingelikuwa siku nyingine Cheupe akiwa pembeni ya ubavu wangu, muonekano huu, kusimama hapa kwenye balcony na kutazama mataa ya Zurich usiku huu ingekuwa ni wasaa wa furaha tele. Lakini kwa muda huu kitu pekee ambacho kilikuwa kinauwezo wa kunipatia furaha na amani ndani ya moyo ni kufumba macho ya kuvuta kumbukumbu. Kumbukumbu ya enzi za utoto, nyumbani kwa shangazi yangu Mwembechai.
Nikafumba macho kukumbuka namna ambavyo siku ambazo zilikuwa na mvua kama hivi namna asubuhi yake kunavyokuwa kukimya. Namna ambacho jua linachomoza taratibu kujipenyeza dirishani na kumulika usoni kama vile linanijaza uhai wa siku hiyo. Naomna ambavyo asubuhi ya siku ya mvua pazia dirishani inakuwa tulivu kama vile imeninginizwa kwenye nyumba ambayo haina wakazi kwa miaka. Namna ambavyo masikio yanafurahi kusikia sauti hafifu za ndege wa asubuhi wakiimba kutokea mbali. Namna ambavyo bati linadondosha matone magodo ya maji taratibu kutokana manyunyu hafifu ya mvua inayokaribia kukoma.
Namna ambavyo nikitoka nje siku ya asubuhi ya mvua mtaa wote unakuwa kimya kabisa, mtaa wenye fujo lakini ukionekana kama hauna wakazi. Lakini japokuwa hakuna vingi vya kuviona, kuna vitu lukuki vya kuvihisi.
“There is much to be felt, and little to be seen.!” Nikatabasamu nikikumbuka msemo wangu huu wa utoto. “There is much to be felt, little to he seen.!” Nikaurudia tena na tena kichwani huku natabasamu.
Kadiri ambavyo nilikuwa naurudia kichwani ndivyo ambavyo kuna ‘taa’ ilikuwa inawaka kichwani mwangi. “There is much to be felt, little to be seen”. Kuna kitu nilihisi akili yangu imekihisi lakini sikujua ni kitu gani. Nikaurudia tena na tena ule msemo kichwani huku narudi ndani ya chumba cha hoteli. “There is much to be felt, and little to be seen.!”
Jicho langu lilitua juu ya lundo za nyaraka pale kitandani. ‘Taa’ ikawaka zaidi. Yes, ni hili lundo la nyaraka… nilikuwa nahangaika muda wote kutafuta kitu ndani yake chenye jibu la moja kwa moja kumbe labda ni ‘detail’ ndogo tu ndiyo nilikuwa natakiwa kuifahamu. Detail ambayo yawezekana akili yangu ilishaihisi. Jawabu halikiwa kwenye huu uwingi wa anuani na orodha za akaunti za benki. Bali suala fulani dogo tu. “There is much to be felt, and little to be seen.!” Nikaurudia tena msemo kichwani na kuanza kuzipekea tena kwa pupa.
Nilihisi kabisa kuna kitu hapa ambacho nilikidharau mwanzoni lakini ndicho ambacho kinaweza kuwa na majawabu ya kila kitu.
Nikapekua karibia dakika tatu nzima. Hatimaye nikakutana nacho. Au niseme kwa mujibu wangu nilihisi ndicho hicho.
Kulikuwa na karatasi moja tu ambayo ilikiwa maandishi ambayo uamefutwa kwa wino mweusi na katikati ilikuwa na kapicha kadogo cha ‘black and white’ ambacho kimechapwa kwenye karatasi. Yaani karatasi juu ilikuwa na ‘paragraph’ kadhaa ambazo zimefutwa kwa wino mweusi katika mtindo unaofanana kabisa na karatasi za mambo ya ujasusi na intelijensia huwa zinazibwa maandishi kwa wino mweusi ili kilichiandikwa kisisomwe.
Katikati kulikuwa na hicho kipicha cha ‘black and white” kisha chini yake kulikuwa na maelezo ambayo nayo yalifutwa kwa wino mweusi.
Nikaitazama hii picha kwa makini. Ni picha ya eneo. Sehemu ambayo naifahamu kabisa hapa Zurich. Ni ule mgahawa wa kichina ambao nilienda siku ya kwanza na kuchomwa kemikali nikapoteza fahamu. Nikaiangalia picha kwa makini zaidi. Nilikiwa sijakosea ni penyewe.
Maelezo ya hii picha yalikuwa yamezibwa kwa wino mweusi kama ilivyo kwa paragraph za juu yake. Lakini kwenye maelezo hayo yote yaliyofichwa kulikuwa na neno moja tu limeachwa na nina imani liliachwa kwa makusudi kabisa. Sikuelewa kwa nini liliachwa, na wala sikuelewa lilikuwa lina maanisha nini. Lakini kwenye karatasi hii kila kitu kilikuwa kimefutwa kwa ustadi kwa wino mweusi na kuachwa hii picha na neno moja tu;
“MELCHIZEDEK ”
Mvua nje ilikuwa imeshika kasi. Na safari hii nikaanza kuiskia radi ikipiga. Japokuwa mvua ilikuwa ni kubwa na radi lilipiga kwa nguvu lakini kitu nilikuwa nahisi ukimya wa ajabu ndani ya chumba cha hoteli. Kuna hisia mbaya nilianza kuisikia mpaka vinyweleo vilisisimaka. Ule ukimya. Sijui kama ulikuwa ukimya ndani ya chumba cha Hotel au ukimya kwenye nafsi yangu. Lakini nilihisi ukimya kiasi kwamba hata tone la maji linedondoka ningelisikia.
Kuna kitu hakikuwa sawa humu ndani ya hoteli.
Nikatazama ile karatasi na maandishi yake yaliyofutwa futwa kwa wino mweusi. Nikatazama ile picha ya mgahawa wa kichina katikati. Nikasoma tena yale maandishi yaliyoachwa.
” MELCHIZEDEK ”
Nilihisi nimepata wazo nianzie wapi kufumbua fumbo lililonileta hapa Zurich. Lakini bado nilipata hisia, kuna kitu hakikuwa sawa ndani ya hiki chumba cha hoteli. Ukimya ndani ya nafsi yangu ambao ulihamia mpaka kwenye chumba nilichomo ulikuwa ni ukimya wa kutisha.
Itaendelea…
THE BOLD
SEASON 1 – FROM ZURICH WITH RULES
Ilipoishia Episode 14…
“I think i have said enough… its your turn now! What happened to you? How did you get shot?” Akauliza huku anatoa tabasamu hafifu.
Nikakumbuka siku tatu zilizopita niliporejeshwa hotelini kwangu kutoka kule Wipkingen. Nikakumbuka kilichotokea masaa ishirini yaliyopita. Nikajiuliza kama ni sahihi kwangu kumuamini huyu mtu na kumueleza kila ambacho kilitokea. Nikakumbuka msemo wake wa fumbo kuwa “Kuna deni anataka kuwalipa Hudini”. Nikakumbuka alivyoeleza kuwa amekuwa akinitafuta kwa miaka kadhaa kwa kuwa aliamini akinipata mimi atawapata Hudini hasa kiongozi wao wa sasa, ambao alikuwa amekorofishana nao.
Nikakumbuka namna ambavyo hakunitambua mara ya kwanza na kutaka kuondoka. Nikakumbuka namna ambayo baada ya kumwambia mimi ni mmiliki wa hili jengo aliniita jina langu. Nikajiuliza kama alifahamu jina langu, na pia alifahamu mimi ni mtoto wa Charles kajuna, ameshindwaje kuijua sura yangu? Iweje anitafute miaka yote kama anavyosema na asiwahi kuona hata picha yangu?
Nikajiuliza tena kwa nini anieleza siri zote hizi. Kuanzia tatoo yake kifuani. Uanachama wake ndani ya Hudini. Shughuli za Hudini na hata ugomvi walio nao na juhudi zake za kuwapata ili “awalipe deni” kama anavyosema.
Nikajiuliza kama hakuna mtego hapa nimewekewa.
Nilikuwa nawaza haya huku nimejiinamia. Nikainua uso kumtazama. Alikuwa ananiangalia huku anatabasamu kama vile anaisoma akili yangu.
“What happened Ray? How did you get shot?” Akauliza tena huku anatabasamu.
Nikavuta pumzi ndefu na kuishusha. Isingelikuwa jeraha tumboni mwangu, ningeweza kuinuka na kutimua mbio.
Masaa 36 Yaliyopita…
Nilikuwa nimetoka usingizini baada ya kulala kwa masaa mengi tangu alfajiri ambapo nilirejeshwa na vijana wa Hudini.
Baada ya kuoga, kubadili nguo na kuonja kidogo chakula ambacho nilikuwa nimeletewa muda si mrefu na muhudumu wa hoteli nilikaa kitandani na kuanza kuchambua lundo la nyaraka ambazo nilipewa na Hudini siku ya Jana usiku kwenye like jumba lao linalonuka damu. Au niseme mzee ambaye kwa wakati huu nilikuwa nikiamini kwamba jina lake alikuwa ni Hudini.
Lilikuwa ni lundo la nyaraka pamoja na ile picha ya jamaa wa kizungu akiwa na Rais Albert Kafumu na picha nyingine akiwa na cheupe pamoja na baba yake.
Nikaziweka picha pembeni na kisha kuanza kupitia hizi nyaraka moja baada ya nyingine. Kwa namna fulani nyaraka hizi zilikuwa zinafanana na zile ambazo nilizikuta kwenye vault ndogo kule kwenye jengo ambalo nilisikiliza ujumbe wa marehemu baba yangu kwenye video.
Zilikuwa nyaraka ambazo ziliorodhesha umiliki wa mali ambazo nilikiwa sizijui, majengo, akaunti za benki. Pia kulikiwa na lundo la anuani za sehemu mbali mbali ambazo sikuelewa mara moja ni wa wapi na kulikuwa na maana gani.
Nilipitia nyaraka zote moja baada ya nyingine, lakini mpaka nilipofika karatasi ya mwisho bado nilikuwa naona maluelue tu. Ni kitu gani hasa ambacho nilikuwa natakiwa kukifanyia kazi kwenye nyaraka hizi? Niliona kila kitu orodha ya mali na majengo ambayo siyajui yalipo na wala sijawahi kuyaona. Niliona pia makumi ya namba za akaunti za benki! Napaswa kuchnguza moja baada ya nyingine? Niliona pia mamia ya anuani mbali mbali! Je napaswa pia kuchunguza kila anuani ambayo imeorodheshqa kwenye nyaraka hizi? Si itanibidi kukaa Zurich mwaka mzima?
“Fuuucckk.!!” Niling’aka peke yangu… huu ni zaidi ya uwendawazimu.
Nikainuka kutoka kitandani na kuanza kutembea kuelekea dirishani. Pembeni ya dirisha kulikuwa na kijimlango fulani hizi chembamba cha kioo ambacho nilikifungia na kutokezea kwenye ‘balcony’ ya chumba changu cha hoteli.
Nilisimama kwenye balcony na kuutazama mji wa Zurich. Namna mataa ambavyo yalikuwa yanang’ara usiku kama huu. Kulikuwa na manyunyu fulani ya mvua inayoanza. Kama ingelikuwa siku nyingine, nyakati nyingine ambayo haikuwa na maswali na mafumbo kichwani mwangu kama ilivyo sasa. Kama ingelikuwa siku nyingine Cheupe akiwa pembeni ya ubavu wangu, muonekano huu, kusimama hapa kwenye balcony na kutazama mataa ya Zurich usiku huu ingekuwa ni wasaa wa furaha tele. Lakini kwa muda huu kitu pekee ambacho kilikuwa kinauwezo wa kunipatia furaha na amani ndani ya moyo ni kufumba macho ya kuvuta kumbukumbu. Kumbukumbu ya enzi za utoto, nyumbani kwa shangazi yangu Mwembechai.
Nikafumba macho kukumbuka namna ambavyo siku ambazo zilikuwa na mvua kama hivi namna asubuhi yake kunavyokuwa kukimya. Namna ambacho jua linachomoza taratibu kujipenyeza dirishani na kumulika usoni kama vile linanijaza uhai wa siku hiyo. Naomna ambavyo asubuhi ya siku ya mvua pazia dirishani inakuwa tulivu kama vile imeninginizwa kwenye nyumba ambayo haina wakazi kwa miaka. Namna ambavyo masikio yanafurahi kusikia sauti hafifu za ndege wa asubuhi wakiimba kutokea mbali. Namna ambavyo bati linadondosha matone magodo ya maji taratibu kutokana manyunyu hafifu ya mvua inayokaribia kukoma.
Namna ambavyo nikitoka nje siku ya asubuhi ya mvua mtaa wote unakuwa kimya kabisa, mtaa wenye fujo lakini ukionekana kama hauna wakazi. Lakini japokuwa hakuna vingi vya kuviona, kuna vitu lukuki vya kuvihisi.
“There is much to be felt, and little to be seen.!” Nikatabasamu nikikumbuka msemo wangu huu wa utoto. “There is much to be felt, little to he seen.!” Nikaurudia tena na tena kichwani huku natabasamu.
Kadiri ambavyo nilikuwa naurudia kichwani ndivyo ambavyo kuna ‘taa’ ilikuwa inawaka kichwani mwangi. “There is much to be felt, little to be seen”. Kuna kitu nilihisi akili yangu imekihisi lakini sikujua ni kitu gani. Nikaurudia tena na tena ule msemo kichwani huku narudi ndani ya chumba cha hoteli. “There is much to be felt, and little to be seen.!”
Jicho langu lilitua juu ya lundo za nyaraka pale kitandani. ‘Taa’ ikawaka zaidi. Yes, ni hili lundo la nyaraka… nilikuwa nahangaika muda wote kutafuta kitu ndani yake chenye jibu la moja kwa moja kumbe labda ni ‘detail’ ndogo tu ndiyo nilikuwa natakiwa kuifahamu. Detail ambayo yawezekana akili yangu ilishaihisi. Jawabu halikiwa kwenye huu uwingi wa anuani na orodha za akaunti za benki. Bali suala fulani dogo tu. “There is much to be felt, and little to be seen.!” Nikaurudia tena msemo kichwani na kuanza kuzipekea tena kwa pupa.
Nilihisi kabisa kuna kitu hapa ambacho nilikidharau mwanzoni lakini ndicho ambacho kinaweza kuwa na majawabu ya kila kitu.
Nikapekua karibia dakika tatu nzima. Hatimaye nikakutana nacho. Au niseme kwa mujibu wangu nilihisi ndicho hicho.
Kulikuwa na karatasi moja tu ambayo ilikiwa maandishi ambayo uamefutwa kwa wino mweusi na katikati ilikuwa na kapicha kadogo cha ‘black and white’ ambacho kimechapwa kwenye karatasi. Yaani karatasi juu ilikuwa na ‘paragraph’ kadhaa ambazo zimefutwa kwa wino mweusi katika mtindo unaofanana kabisa na karatasi za mambo ya ujasusi na intelijensia huwa zinazibwa maandishi kwa wino mweusi ili kilichiandikwa kisisomwe.
Katikati kulikuwa na hicho kipicha cha ‘black and white” kisha chini yake kulikuwa na maelezo ambayo nayo yalifutwa kwa wino mweusi.
Nikaitazama hii picha kwa makini. Ni picha ya eneo. Sehemu ambayo naifahamu kabisa hapa Zurich. Ni ule mgahawa wa kichina ambao nilienda siku ya kwanza na kuchomwa kemikali nikapoteza fahamu. Nikaiangalia picha kwa makini zaidi. Nilikiwa sijakosea ni penyewe.
Maelezo ya hii picha yalikuwa yamezibwa kwa wino mweusi kama ilivyo kwa paragraph za juu yake. Lakini kwenye maelezo hayo yote yaliyofichwa kulikuwa na neno moja tu limeachwa na nina imani liliachwa kwa makusudi kabisa. Sikuelewa kwa nini liliachwa, na wala sikuelewa lilikuwa lina maanisha nini. Lakini kwenye karatasi hii kila kitu kilikuwa kimefutwa kwa ustadi kwa wino mweusi na kuachwa hii picha na neno moja tu;
“MELCHIZEDEK ”
Mvua nje ilikuwa imeshika kasi. Na safari hii nikaanza kuiskia radi ikipiga. Japokuwa mvua ilikuwa ni kubwa na radi lilipiga kwa nguvu lakini kitu nilikuwa nahisi ukimya wa ajabu ndani ya chumba cha hoteli. Kuna hisia mbaya nilianza kuisikia mpaka vinyweleo vilisisimaka. Ule ukimya. Sijui kama ulikuwa ukimya ndani ya chumba cha Hotel au ukimya kwenye nafsi yangu. Lakini nilihisi ukimya kiasi kwamba hata tone la maji linedondoka ningelisikia.
Kuna kitu hakikuwa sawa humu ndani ya hoteli.
Nikatazama ile karatasi na maandishi yake yaliyofutwa futwa kwa wino mweusi. Nikatazama ile picha ya mgahawa wa kichina katikati. Nikasoma tena yale maandishi yaliyoachwa.
” MELCHIZEDEK ”
Nilihisi nimepata wazo nianzie wapi kufumbua fumbo lililonileta hapa Zurich. Lakini bado nilipata hisia, kuna kitu hakikuwa sawa ndani ya hiki chumba cha hoteli. Ukimya ndani ya nafsi yangu ambao ulihamia mpaka kwenye chumba nilichomo ulikuwa ni ukimya wa kutisha.
Itaendelea…
THE BOLD