VIPEPEO WEUSI
SEASON 2 - FROM ZURICH WITH RULES
EPISODE 23
Nilikuwa tena kwenye taxi kutokea mtaa wa Affolterntrasse ambako nilienda kutazama nyumba yenye anuani ambayo ilikuwa kwenye zile nyaraka nilizonazo. Kitu pekee ambacho niliondoka nacho kwenye ile nyumba ilikuwa ni ile picha ukutani. Picha ambayo inawaonyesha yule binti Erica muhudumu wa pape hotelini lakini kwenye nyaraka zangu picha yake imeandikwa jina la Ivanka, pamoja na Luke utotoni mwao wakiwa na mtu ambaye kwenye picha yuko kwenye picha nyingine nilizonazo.
Kuna wazo lilikuwa linanijia kichwani. Kuna taa ilianza kuwaka na kuanza
Niliitazama tena ile picha. Nikaitazama kwa makini kweli kweli. Yes! Huyu ni Erica akiwa mtoto, na huyu ni Luke akiwa mtoto. Na huyu mwanaume ndiye huyu ambaye yuko kwenye picha nyingine tatu nilizonazo. Moja akiwa na Rais Kafumu, ya pili akiwa mahala fulani mtaani na ya tatu akiwa na cheupe na baba yake. Mtu pekee ambaye sikumtambua kwenye ile picha alikuwa ni yule mwanamke. Kwa muktadha wa mantiki na mtindo wa upigaji huu picha ilionekana kabisa ilikuwa ni picha ya familia. Ikimaanisha kwamba Erica na Luke ni mtu na dada yake. Na yule jamaa ni baba yao. Na yule mwanamke ni mama yao.
Lakini kuna kitu ambacho kilikuwa kimenishangaza zaidi. Huyu mtu alikuwa anaonekana kana kwamba ni kijana mno kutosha kuwa mzazi wa kina Erica na Luke. Kwa sababu picha ambayo amepiga na Rais Kafumu inaonekana wazi kabisa kwamba imepigwa miaka ya hivi karibuni.
Nikaitazama tena picha kwa makini. Naam! Taa ilikuwa inawaka zaidi… nilianza kung'amua ile anuani ilikuwa na maana gani. Nilikuwa nahitaji tu kuhakikisha kama ninachokifikiria kilikuwa sahihi.
Nikiwa nimezama sana kwenye kutafakari ile picha mpaka sikujua kama tulikuwa tumefika tayari Haedstrasse mpaka pale dereva taxi aliponishtua na kunirejesha tena kwenye mawazo ya kawaida. Nikalipa na kushuka.
Nilikuwa natembea taratibu kuelekea kwenye uchochoro wa jengo ambao unaenda kwenye mlango wa nyuma ya jengo ambao nimekuwa nautumia mara zote. Nilikuwa natembea taratibu ili nisitoneshe kidonda pale tumboni. Nikakumbuka tena kwamba nahitaji daktari wa kukitazama hiki kidonda kabla hakijanipa madhara zaidi.
Nikakukumbuka tena kwamba napaswa pia kulitazama hili jengo zaidi, floor za juu kuna nini? Na pia The Board walilinunua kutoka kwa nani? Na walinunua kwa lengo lipi haswa?
Hili napaswa kulifanya asubuhi… kwa usiku huu napaswa kupumzika na kuchekecha akili kuhusu Erica, Luke na yule jamaa wa kwenye picha.
Nilipoufikia mlango niliukuta ukiwa umefunguliwa na kuegeshwa tu. Yaani kwamba ulionekana kuwa ulifunguliwa na kisha kurudishwa bila kufungwa tena tofauti na ambavyo niliuacha ukiwa umefungwa. Eidha kulikuwa na mtu ndani au mtu huyo aliingia na kutoka kwa haraka bila kufunga mlango.
Kama ambavyo nilijiapiza kwamba, safari hii sikimbii… nitapambana. Ndivyo ambacho nililifanya. Nilishinda woga wote ambao nilikuwa nausikia muda huu. Nikavuta pumzi ndefu ndani na kuishusha. Kisha nikafungua mlango na kuingia kwa tahadhali.
Pale koridoni kulikuwa na giza kama siku zote kwa hiyo nilitembea kwa kunyata taratibu mno ili nisimgutushe yeyote kama yuko humu ndani. Moyoni nilikuwa najilaumu sana kwa kutofanyia kazi mapema wazo la kuwa na silaha ambalo nilikuwa nalo tangu asubuhi.
"Damn! I really need a gun!"
Nilijilaumu moyoni huku nikinyata taratibu.
Nikiwa nanyata hivi taratibu pale pale koridoni nikaanza kusikia sauti. Sauti ya mtu akigugumia.
Mwanzoni nilihisi labda ni mtu yuko kwenye maumivu lakini niliposikiliza kwa makini niligundua kwamba alikuwa ni mtu analia, alikuwa analia kwa uchungu sana kiasi kwamba alikuwa inaifunda sauti ndani ili isitoke. Sauti iliashiria kwamba mtu huyo alikuwa analia kwa mida mrefu kiasi kwamba sauti ilianza kumkauka.
Nikatoa simu yangu mfukoni taratibu na kuwasha tochi. Hamad.!! Mbele yangu alikuwa Jimmy. Yule chokoraa ambaye juzi waliniokota yeye na Luke. Alikuwa amekaa chini amejikunyata kwa kuinamisha kichwa chake kwenye magoti ambayo alikuwa ameyakunja mpaka usawa wankifua.
Alipoona mwanga akainua kichwa chake kutazama. Usoni alikuwa amelowa machozi chapa chapa. Ule waupe wake wa kizungu ulikuwa umebadilika na kuwa mwekundu usoni kuashiria kwamba amekuwa akilia kwa muda mrefu sana.
"Jimmy!! What's wrong?" Nilitahamaki huku naenda haraka ukutani kuwasha taa.
"Get away from me.!!! Go away.!!" Jimmy alifoka huku analia.
Nilibaki nimepigwa butwaa tu. Jimmy alikuwa na nini? Au amepata habari juu ya kifo cha swahiba wake Luke?
"Look Jimmy, I am really so…"
"You are a jinxy! You are a jinxyyy.!! Jimmy alinikatisha na kufoka kwa hasira huku bado akiwa analia.
"Jimmy! I am sorry, I know Luke was your friend… I am really really sorry mate.!" Nilijitahidi kuongea kwa huzuni na kufariji kwa kadiri ambavyo niliweza.
Lakini nilishangaa Jimmy anainua uso na kunitolea macho kwa mshangao. Alitoa macho kana kwamba amesikia jambo kubwa asilolijua. Aliacha kulia ghafla. Aliinua uso na kunitazama kwa mshangao mkubwa. Mpaka nilianza kuogopa kutokana na mshangao wale usoni.
"What is it.!" Nilijitahidi kumuuliza.
"What did you just said?" Aliniuliza huku anaanza kuninuka.
Nilitafakari kama kwenye sentensi yangu nimeongea kitu chochote cha kukera au dhihaka? Lakini sikukiona… Jimmy alikuwa anainuka taratibu kana kwamba ni chui anajiandaa kurukia windo lake la siku.
"Chill out mate!" Nilijitahidi kumtuliza huku nimenyoosha mkono kuashiria awe mtulivu.
"No no no! What did you just say?"
"I said…I am sorry for Luke's death.!"
Mshangao usoni mwake ulikuwa mkubwa zaidi.
"Whaaaatt! When did this happen?"
"You dont know.?" Nilishangazwa. Ina maana hajui kwamba swahiba wake amefariki leo asubuhi? Kama hajui ni kitu gani kilikuwa kinamfanya alie kiasi hiki kama mtoto mdogo?
"When did this happen?" Aliniuliza tena kwa taharuki.
"Today morning… he was shot! Wait a minute… you dont know anything about this? Then why are you craying?"
Nikamuona anainamisha tena kichwa chini kwa uchungu. Nikaanza kusikia kwikwi. Mara moja akaanza tena kulia na kukaa tena chini sakafuni.
"You are jinxy mate! You are a jinxy!!" Jimmy alilalama huku analia pale sakafuni.
"Jimmy! Whats going on?"
Jimmy anasema kwamba alikuwa hajui kuhusu kifo cha Luke? Kwa nini analia? Na kwa nini kilio kimeongezeka zaidi baada ya kumuambia kuhusu kifo cha Luke?
"Jimmy! What's going on here?" Safari hii nilifoka.
Akainua kichwa na kunitazama cha uchungu.
"My sister died today! She shot.!!" Alinijibu kwa kifupi huku amenikazia macho.
Nikihisi kama jiwe zito limedondoshwa ndani ya nafsi yangu? Dada yake? Ina maana Jimmy huyu chokoraa naye ana dada? Na huyo dada naye ameuwawa leo? Tena naye kwa kupigwa risasi kama Luke?
Lazima kutakuwa na uhusiano.
"Your sister? Who is she… I mean am so sorry! When didi this happen?" Niljikuta napata kigugumizi nisijue ni kitu gani hasa niongee.
"I would rather show you!" Jimmy aliongea kwa hasira huku anainuka. "Lets go!"
"Where? To do what exactly?" Nilihamaki kwa mshangao.
Nini kimempata Jimmy? Nimemuuliza kuhusu dada yake aliyeuwawa badala yake ananieleza kwamba ni bora alinionyesha. Anataka kunionyesha nini?
"Do you want to know or what?" Aliniuliza bila kuniangalia akiwa amesimama kuelekea mlangoni.
"Ofcourse I want to know but…"
"Then lets go!"
Hakunisubiri nimjibu au chochote… tayari alishafika mlangoni na kuufungua kutoka nje.
Sikuwa na chaguo lingine zaidi ya kumfuata japo sikujua tunaenda wapi au anataka kunionyesha nini?
Tulifika barabarabi na kusimamisha taxi kwa mara nyingine tena.
"Freacht West!" Jimmy alimueleza dereva taxi baada ya sote kukwea ndani.
Moyo ulinipasuka. Huo ndio mtaa ambao iko hoteli ya Radisson Blu Hotel ambayo nilifikia siku nilipoingia hapa Zurich. Sikutaka kuonyesha mshangao wangu au kumuuliza Jimmy kitu chochote. Nikasubiri nione mwisho wa hii safari.
Kwenye taxi wote tulikuwa kimya. Kila mmoja akiwaza na kuwazua lakwake kichwani.
Nilikuwa najihisi kama vile niko kwenye "maze". Kana kwamba ni uwanda mpaka wenye mamia ya kuta na mamia ya kona kona na kukiwa na mlango mmoja tu wa kuingilia na kutokea. Ukiwa kwenye maze ukikata kona moja tu isiyo sahihi umekwisha. Utazunguka na kuzunguka ndani yake na kamwe hutouona mlango wa kutokea. Unapaswa kila kona ambayo unaipinda iwe sahihi.
Ndivyo ambavyo nilikuwa najihisi muda huu. Kulikuwa na kona kona nyingi mno za mafumbo na kama nitakosea hata suala moja tu nitajitumbukiza gizani zaidi kuzidi hata giza nililokuwepo kabla ya kufika hapa Zurich.
Tulienda kama mwendo wa dakika kumi na tano hivi tukiwa wote kimya kama mabubu. Taxi ilifika mpaka Freacht West. Tulikuwa kwenye 'blocks' zile zile ambazo ilipo Radisson Blu Hotel.
"Stop here!" Jimmy alimuamuru dereva taxi.
Gari ilipaki mkabala kabisa na Radisaon Blu Hote. Mahala pale pale ambako asubuhi ya leo nilikuja niliposikia kifo cha Luke.
Sasa nilielewa dada yake Jimmy ni nani. Sikuwa na hata haja ya kuuliza.
Safari hii Hoteli ilikuwa imefungwa kabisa. Pale mlangoni kulizungushiwa utepe wa njano wa polisi. Hii iliashiria kwamba mauaji hayo yalifanyika ndani ya Hoteli.
Niligeuka na kumtazama Jimmy kwa kumkazia macho. Kichwani mawazo kadhaa yalipita. Hivi huyu Jimmy ni chokoraa kweli au ni mtu tu amepandikizwa kwa kazi maalumu hapa Zurich?
"So Erica was your sister?" Nilimuuliza kwa hasira huku nahema.
Hasira nilizokuwa nazo ni kwa jinsi ambavyo Jimmy muda wote tangu siku ile wameniokota pale kwenye jengo Hardstrasse alikuwa anajifanya hajui chochote kuhusu mimi au kinachoendelea.
"Her name was Ivanka!" Jimmy alinijibu bila kuniangalia macho ameyalaza kuelekea mbele.
Jimmy alitaja jina la yule binti ambalo pia nililiona kwenye nyaraka zikiwa na picha yake.
Nikijikuta na hasira zaidi, kuchanganyikiwa zaidi lakini pia nikisikia hatia ndani yangu. Watu hawa wawili wameuwawa mara tu baada ya kukutana na mimi. Kwa namna fulani nilihisi kuna uhusiano wa vifo vyao na kukutana na mimi. Nilihisi ndio sababu ya Jimmy kung'aka akisema "you are a jinxy!"
"Jimmy!" Nilimuita kwa utulivu.
Hakugeuka. Aliendelea kukaza macho yake mbele.
"Jimmy! Do you know who I am? I mean before we met… did you know who I was?" Nilimuuliza tena kwa sauti ya utulivu.
"For two years she was obsessed with finding you… I knew this would bring bad luck. But she dint listen… she was too determined to find you!"
Jimmy alinijibu kwa uchungu huku bado akiwa amekaza macho mbele.
Kwa maneno mepesi alikuwa amekubali kuwa alikuwa ananijua kabla hata ya kuonana ile juzi pale kwenye jengo nilipopigwa risasi. Kwamba dada yake Erica, au Ivanka kwa usahihi zaidi… alikuwa na mshawasha na nadhiri ya kunipata. Kwa nini?
Mara ya kwanza baada ya kukuta ile picha kwenye nyumba ya Affolterntrasse nilidhani kwamba Luke na Erica ndio ndugu. Lakini Jimmy anasema Erica ni dada yake? Ina maana wote watatu ni ndugu? Haiwezekani, Jimmy ameguswa zaidi na kifo cha Erica kuzidi Luke.
Uzuri safari hii siko gizani tu peke yangu, bali niko hapa na mtu wa kunipa majibu yote haya ya maswali yangu, Jimmy.
"Jimmy! We need to talk. I need answers.. you hear me? we need to talk… hey take us back to Hardstrasse!"
Nilimuamuru dereva. Kuturudisha tena Hardstrasse. Jimmy hakukaidi. Nilihisi nae alikuwa amechoka kukaa na siri moyoni mwake. Alikuwa anataka hatimae atue mzigo huo alionao moyoni.
Dereva aligeuza gari na kuanza kurejea tulikotoka.
Tukiwa tunaondoka eneo hili. Nilitupa tena jicho pale nje ya hoteli palipozungushiwa utepe wa njano wa polisi. Inaonekana tukio lilikuwa limetokea si masaa mengi yaliyopita. Bado polisi walikuwa wanahoji watu hapa na pale. Na kulikuwa na wapita njia kadhaa kama kawaida wamesimama kushangaa na kupata 'umbea' wa kilichotokea.
Katika mkusanyiko huu wa wapita njia wachache waliosimama kutazama, nilimuona tena yule jamaa… yule jamaa wa asubuhi, mwenye kofia ya pama ya kijivu, koti refu lenye kufika usawa wa magoti, mkononi akiwa na gazeti, Jamaa yule yule ambaye juzi usiku alikuwa ameketi kwenye sofa za mapokezi ya hoteli akisoma gazeti nilipokuwa nabishana na Erica.
Inaonekana alikuwa anaangalia taxi yetu muda wote. Tulipoondoka nilimuona akitusindikiza kwa macho mpaka tulipopotea upeo wa macho yake.
Nikamgeukia Jimmy.
"Wewe mpumbavu leo una maswali mengi sana ya kunijibu!" Nilijikuta na hasira mpaka nimemsemesha kwa kiswahili nikijua kabisa hakuelewa chochote.
Nilitamani taxi ipae na kufika haraka nianze kupata majibu kutokakwa Jimmy.
Itaendelea…
Habibu B. Anga 'The Bold'
To Infinity and Beyond