VIPEPEOWEUSI
FROM ZURICHWITH RULES
EPISODE 26
Yule binti kwa kiasi fulani alikuwa 'amerelax' tofauti na zile hasira zake za mwanzo alivyoshuka kwenye gari na kuja kutugongea kwenye kioo.
Alikuwa amenitambulisha jina lake kwamba anaitwa Winnie Akoh. Alikuwa ni mwanafunzi kutoka nchini Senegal na yuko hapa Zurich kama mwanafunzi akisomea "Banking and Finance" katika chuo kikuu cha Zurich.
"What are doing in that house?" Nakumbuka nilimuuliza.
Winnie alinieleza kwamba miaka miwili iliyopita alipowasili hapa Zurich kwa ajili ya masomo kama ilivyo kawaida ya wanafunzi wengi ughaibuni ilimlazimu kutafuta kibarua ambacho atakuwa akifanya katika muda wake wa ziada ili aweze kuingiza kipato cha kumuwezesha kujikimu.
Winnie alinieleza, kwamba aliomba kazi kadhaa mtandaoni… kuanzia uhudumu kwenye mgahawa, uhudumu kwenye kituo cha kutunza wazee, kuwa mtu wa mauzo wa kampuzi za vipodozi na kadhalika na kadhalika. Alinieleza kwamba aliomba kazi nyingi sana na kusubiri aone ipi ambayo atapata majibu. Katika mlolongo wa huo wa kuomba kazi mtandaoni aliona tangazo lenye maelezo mafupi tu likisema "Earn $ 3000/month cleaning a house".
Winnie alinieleza kwamba mwanzoni alihisi labda ni utani au tangazo la uongo kama ambavyo yamejaa huko mitandaoni. Lakini akaamua kutuma tu maombi aone kama ni kweli au la.
Anasema kwamba siku tatu baadae alipigiwa simu na mtu aliyejitambulisha kuwa ni muwakilishi wa kampuni walioweka tangazo lile ambalo yeye aliomba kazi.
"Did he tell you the company's name?" Nilimuuliza.
"Yes! REMODO HOLDINGS." Winnie alinijibu.
"Can I have their adress?" Nilimuuliza.
"I might still have their business card in my car…!" Winnie alinijibu.
Kisha akaendelea kunieleza kwamba mtu huyo alimuhoji maswali kadhaa kuhusu taarifa zake na kisha akamtaka waonane baada ya siku moja.
"Did you meet him?" Nakumbuka nilimuuliza.
"Yes! We did meet two days after the phone call."
"Where did you guys meet?"
"Freacht West Street… there is a fancy chinese restaurant there."
"Chinese restaurant??"
Nilishtuka sana aliponitajia kwanza Freacht West Street. Huu ndio mtaa ambao kuna Radison Blu Hotel ambayo nilifikia nilipoingia hapa Zurich na ndio mahala ambako siku mbili zilizopita yamefanyika mauaji ya Luke na Ivanka. Lakini nilishtuka zaidi aliponitajia mgahawa wa kichina… kwa sababu niliamini kabisa alikuwa anaongelea mgahawa ule ambao niliwahi kufika siku ya kwanza na kuchomwa sindano ya kemikali na kupoteza fahamu na baadae kujikuta nimeamka kwenye lile jengo mtaa wa Hardstrasse.
"Is everything ok?" Winnie aliniuliza baada kuona mshtuko wangu.
"Everything is ok! I was just thinking about that meeting place… it seems like an odd choice." Nilijitahidi kumzuga. Sikutaka ajue chochote kile ambacho nakifahamu kuhusu sehemu hizo.
"Why is that?" Aliniuliza
"No! Nothing… what happened next?"
Akaendelea kunieleza kwamba, mtu huyo alichukua nakala zake za hati ya kusafiria, kitambulisho cha uanafunzi chuoni pamoja na namba yake ya akaunti ya benki. Kisha akamlipa dola elfu moja tasilimu papo hapo na kumwambia kuwa anatakiwa kuanza kazi kesho yake.
"What was the job about… what where you suppose to do?" Nilimuuliza.
Alinijibu kwamba, alikuwa anatakiwa kufika kwenye ile nyumba ya mtaa wa Affolterntrassemara mbili kila wiki kwa ajili ya kufanya usafi na kupokea barua zozote ambazo zitatumwa kwenye anuani ya nyumba hiyo. Hiyo ndio ilikuwa kazi yake.
"Thats it?" Nilimuuliza.
"Yap! Thats it.." alinijibu huku anatabasamu.