Vipepeo weusi season 2: From Zurich with rules

Vipepeo weusi season 2: From Zurich with rules

Hivi hii kitu inaendelea au ndio bye bye hapo ilipoishia polisi wa Zurich wakigonga mlango??
 
Huyu jamaa bado yupo hai???
Isiwe amesha kufa sisi bado tunasubiri mwendelezo tu
 
VIPEPEO WEUSI



SEASON 2 - FROM ZURICH WITH RULES




EPISODE 21


Nilisikia wale watu ambao walikuwa wamejitambulisha kama polisi wakigonga tena.
Wasiwasi wangu wa kwanza ulikuwa ni kidonda tumboni kwangu, nilikuwa nawaza hawa polisi wakiniuliza kidonda hicho ni cha nini nitajibu vipi? Lakini pia wasiwasi wangu wa pili ulikuwa ni kitu gani hasa polisi hao kimewaleta haswa mahala hapa.

Sikutaka wagonge sana mlango kwani wangeweza kuingiwa na wasiwasi. Nikijikaza kiume kwa nguvu zangu zote na ujasiri wangu wote niweze kutembea sawasawa bila kuchechemea.

"…good morning Sir.!"

"…morning. How can I help you?"

Niliwasalimia lakini hawakunijibu haraka walibakia kunitumbulia macho tu kisha wakaangaliana. Walikuwa mwanaume mmoja na mwingine alikuwa ni mwanadada. Wote wawili walikuwa wamevalia suti. Nilielewa wazi kabisa walikuwa ni askari wapelelezi

"Do you live here?" Yule mwanadada aliniuliza huku bado amenitumbulia macho.

"No, why? Is there a problem?" Nikamuuliza.

"I am detective Corol Lawrence and this detective Noah Johnson. We would like to ask you a few questions… can we come in?" Yule dada aliongea huku ananionyesha kitambulisho chake cha upolisi.

"Yes, ofcourse!"

Niliwakaribisha ndani na haraka nikaenda kuketi kwenye sofa. Sikutaka kujibaraguza kwa kufanya ukarimu wa kuwapa kahawa au kinywaji kama ilivyo desturi ya wazungu. Niliketi haraka ili maumivu tumboni yasinizidie na wakagundua kuwa nina kidonda tumboni yakaanza maswali ya jeraha hilo kimelipataje.

"How do you know Luke Madison?" Yule mwanaume aliniuliza swali.

"Ahn! We are friends!" Nilitoa jibu la haraka haraka.

"Friends like how? You guys live together or….!"

"Im am sorry detective, you are asking me all these questions but i dont why? What is happening? Why am i being interrogated?" Nikawauliza nikiwa na uso serious. Tayari nilijua kuwa kuna kitu kilikuwa hakiko sawa kwa hiyo kabla sijasema maneno mengine yoyote ambayo yangeweza kunitia matatani.

"Well, its not an interrogation. Just some routine questions!" Yule dada aliongea huku analazimisha tabasamu.

"There is nothing 'routine' about this. You guys have come here for a reasons! I want to know why before I answer any more questiins!"

Niliwaona wanaangaliana na kupeana ishara fulani hivi. Kisha yule mpelelezi mwanamke akaongea.

"Luke is dead!"

Nilihisi kama sijasikia vizuri au labda sikumuelewa.

"What? What did you just say?" Niliongea kwa mshituko mkubwa usoni.

"Luke is dead?"

Mpelelezi mwanamke, Carol alinijibu tena. Nilitamani kama vile wawe wananitania tu. Inawezekana vipi? Luke ameondoka hapa kama nusu saa tu iliyopita.

"How? What happened?" Niliuliza nikiwa bado kwenye mshituko.

"He was shot few minutes ago!" Akanijibu tena huku amenikazia macho nahisi akitaka kuona mwitikio wangu usoni.

Nilijiinamia uso viganjani kwa sekunde kadhaa. Wao walidhani labda nilikuwa nasikitika kwa taarifa hii ya msiba, lakini kichwani mwangu kulikuwa na kitu kingine kabisa kinapita. Nilikuwa nawaza kama kuna uwezekano wa aliyenipiga risasi juzi usiku, Erica… kuwa ndiye huyo huyo ambaye alikuwa amempiga risasi Luke. Kuna upande fulani wa akili yangu ulikuwa unataka niwaambie maaskari hawa kuhusu tukio ambalo lilinitokea, lakini moyo wangu ulikuwa unasita kabisa kuwapa taarifa hii.

"Where did this happen?" Nikawauliza kwa sauti ya unyonge.

"Freacht West Street…!"

Wakanitajia mtaa ule ule ambao kuna hotel ya Radisson Blu ambayo nilifikia nilipoingia hapa Zurich. Luke pia alipoondoka hapa tulikubaliana aende hotelini pale ili kupata taarifa juu ya yule binti muhudumu Erica ambaye alinipiga risasi.

"Sir, if there is any information that can help us we will be happy to hear it!"

Kichwani nikajiuliza ni kitu gani hasa niwaambie? Niwaeleze ukweli? Je, sitaingia matatizoni kwa kuwaeleza ukweli na lengo langu la kuja hapa Zurich kuvurugika? Hapana siwezi kuwaambia ukweli…

Ilibidi nitunge uongo usio na kichwa wala miguu lakini wenye kuweza kuaminika.
Kwanza niliwadanganya jina langu3… niliwaelezankuwa naitwa "Jimmy Adekela", asili yangu ni Nigeria lakini naishi hapa Zurich kwa mwaka wa pili sasa. Kwa hiyo sikuwaeleza ukweli kwamba mimi ni Mtanzania ambaye nimeingia hapa Zurich siku chache tu zilizopita.
Nilijua kwa ujio wao huu wa haraka haraka hawawezi kunibana sana kwa maswali labda waseme wananikamata na kunipeleka kituoni, lakinj uzuri hawakuwa na sababu ya kunikamata. Japokuwa kama nikiwaeleza uongo na baadae wakigundua kuwa nimewadanganya lazima wanisake ili kunikamata na kunihoji ili kufahamu najua nini kuhusiana na kifo hicho cha Luke.

Nilikata shauri kichwani mwangu niwadanganye, siwezi kuwaeleza ukweli… nikawaeleza kwamba Luke ni rafiki yangu wa muda mrefu tu na mimi nilikuwa nimekuja hapa kumtembelea jana usiku na ndio maana ilinibidi kulala hapa. Asubuhi ya leo aliniaga kwamba anatoka kwa muda mfupi tu na atarudi baada ya dakika chache lakini badala yake ni wao wamekuja kunipa taarifa kwamba amepigwa risasi.

"…can you think of anyone who might want to kill him? Anyone… an enemy or someone who may be had a fight with a few days ago… anyone?"

Yule mpelelezi wa kiume, Noah aliniuliza.

"No.! I dont think if there is anyone who would want to kill Luke… he was a very good guy!" Nikadanganya tena.

"Ok sir, we would like to talk to you again later, but thats it for now… thank you sir!"

"No problem.!"

"If you remember anything, please give us a call… this is my number..!"

"Thank you!"

Walinipatia 'business card' nikaipokea na kuiweka mfukoni. Wakafungua mlango na kuondoka.

Nilivuta pumzi ndefu ndani na kuishusha. Sikuamini kama hatimaye wameondoka. Lakini huu haukuwa mwisho… hawa wanaonekana ni wapelelezi wazoefu, lazima watakuwa wamegundua kwamba kuna jambo nilikuwa naficha. Wameamua kuondoka kana kwamba hawanitilii mashala ili 'nirelax'. Hawataki niingiwe na wasiwasi kisha nikakimbia. Lazima wanaenda kuhakiki taarifa nilizowapa kabla hawajaja kunikamata rasmi wakigundua uongo niliowaeleza. Huu ulikuwa ni muda wa kufanya maamuzi ya haraka kabla sijachelewa.

Nikafunua shati nililovaa kutazama kidonda changu ambacho kimefungwa bandeji. Kilikuwa kiko sawia.

Nikaelekea mpaka karibu na kitanda ambako kulikuwa na mabegi yangu. Nikaanza kuyaburuza na kuondoka.

Sikutaka kupitia mlango rasmi wa mbele ya jengo au kutumia lifti. Nikihofia ningeweza kukutana na askari wale ambao wameondoka muda huu. Au labda wameacha mtu nje kunichunguza nyendo zangu.
Nikaburuza begi langu na kushuka ngazi taratibu kuelekea mlango wa nyuma wa dharura. Kutokana na kuhofia kutonesha kidonda tumboni ilinibidi kutembea taratibu sana na kwa tahadhari. Ilinichukua karibia dakika kumi nzima mpaka kutokea kwenye mlango wa nyuma wa dharura. Nikasogea mpaka barabarani na kuita Taxi.

"Freacht West Street… Radisson Blu Hotel!" Nilimuelekeza dereva taxi kisha aling'oa gari na kuondoka.

Katika ambao nilitakiwa kuwa makini kupitiliza basi ulikuwa ni huu. Nilikuwa kwenye nchi ya kigeni na tayari kulikuwa na kila dalili ya kuingia kwenye matatizo makubwa na vyombo vya usalama. Hiki kilikuwa ni kitu cha mwisho ambacho nilikuwa sitaki kitokee. Tayari nina adui asiyejulikana ambaye alikuwa ananiwinda. Sihitaji tena kuingia kwenye uadui na vyombo vya usalama.
Pia kila nilipokuwa nafikiria hii taarifa juu ya Luke kupigwa risasi nilikuwa siishi kujiuliza kama ni yule mwanadada Erica ndiye anayehusika. Nilijikuta tu natamani kufika pale hotelini ili kujionea walau kwa macho yangu ni nini hasa ambacho kilikuwa kinaendelea.

Kama dakika saba baadae tulikuwa tumeingia mtaa wa Freacht West. Nilimuelekeza dereva apaki gari upande wa pili wa barabara mkabala na Radisson Blu Hotel. Nilikuwa nataka kuona kile ambacho kilikuwa kinaendelea pale hotelini lakini sikutaka kufika kuhofia kutambulika na pengine kuingia kwenye matatizo zaidi. Hapa tulipopaki upande wa pili wa barabara nilikuwa naweza kuona vyema kabisa kile ambacho kilikuwa kinaendelea.

Nje ya hoteli pembeni karibu na mlangoni, kulikuwa kumefungwa utepe wa njano wa polisi kuashiria kwamba hiyo ndiyo 'crime scene'. Ndipo mahala ambapo Luke alipigwa risasi.
Kulikuwa na kama polisi watano hivi wenye sare ambao walikuwa eneo hili. Pia kulikuwa na watu wawili ambao walionekana ni watu wa 'forensic' mmoja akiwa anapiga picha lile eneo sakafuni na mwingine akiwa kama anapima vitu fulani hivi pale chini.

Pembeni nje ya ule utepe kulikuwa na raia kadhaa wasiozidi kumi na tano wamesimama wakishangaa. Nilimuona moja ya askari akiwa anachukua maelezo ya meneja wa Hoteli, yule jamaa ambaye juzi alinikuta mapokezi nabishana na Erica na kunitaka niondoke.
Nikapepesa macho yangu kutazama watu walioko pale wakishangaa. Moyo wangu ulipasuka ghafla nilipomuona moja ya watu ambao walikuwa eneo hili. Katika lile kundi la raia ambao walikuwa wamesimama wakishangaa alikuwepo yule jamaa anayevaa kofia ya 'pama'. Yule jamaa mweusi ambaye juzi hapa hotelini alikuwa ameketi kwenye moja ya sofa za pale mapokezi anasoma gazeti. Jamaa ambaye Erica alikuwa anaongea na mimi huku anamwangalia kwa kuibia ibia kana kwamba anamuhofia hivi. Ni yule jamaa alikuwepo tena mahala hapa kwenye kundi la raia wanaoshangaa.

Tangu juzi sikuweza kumuona sura yake kutokana na kofia lake la pama. Na hata leo hii muda huu pia sikuweza kuona sura yake. Lakini nilikuwa na hakika kwa asilimia mia moja kwamba alikuwa ni yeye. Kofia yake ile ile ya pama kubwa kiasi ya rangi ya kijivu. Koti lake jeusi refu lenye kufika mpaka usawa wa magoti na kuvuka chini kidogo. Mkononi ameshikilia gazeti. Hakika sikuwa nakosea. Alikuwa ni yeye. Alikuwa anatazama kinachoendelea pale kama vile watazamaji wengine.

"Ni nani huyu mtu?" Nilijiuliza mwenyewe kichwani.

Nikiwa najiuliza hivu maswali kichwani… ghafla! yule jamaa akageuka na kutazima upande wetu, hapa taxi ilikopaki. Ubaya ni kwamba nilikuwa nimeshusha dirisha chini kidogo ili niweze kuona kwa usawia. Nilijikuta macho yangu na yake yanagongana. Kijasho kilianza kunitoka huku nahema kwa nguvu. Tulikaziana macho kwa takribani sekunde thelathini nzima. Sasa ndio nilipata wasaa wa kumuona vyema. Upande wa kushoto usoni alikuwa na kovu kubwa kana kwamba aliwahi kupata jeraha kubwa la kukatwa na kitu.

"Namjua huyu jamaa.!!"

Ndilo wazo la kwanza ambalo lilikatisha akilini mwangu. Nilikuwa na hakika kwa asilimia mia moja kwamba huyu mtu namfahamu. Nimeshawahi kumuona hapo kabla siku za nyuma kabla ya hapa hotelini. Kovu lake hili ndilo haswa lilinipa uhakika kwamba namfahamu huyu mtu. Lakini sikuweza kukumbuka ni wapi. Akili ilikiwa inashindwa kutambua ni wapi haswa niliwahi kumuona. Lakini kwa hakika kabisa kumbukumbu yangu iliniambia huyu mtu namfahamu.

Nilimkazia macho. Sikupepesa hata kidogo japo nilikuwa nimekumbwa na woga wa ghafla moyoni mpaka jasho linanitoka.
Taratibu nikamuona anageuka na kuendelea kushangaa kule kwenye eneo la tukio.

Nikamuamuru dereva tuondoke.

"Hardstrasse.!" Nikamuelekeza kwa kuelekea.

Ndio. Hardstrasse. Ndio mahala pekee ambako kwa sasa nilihisi palikuwa sahihi kwangu kwenda. Siwezi kukaaa tena hotelini. Itakuwaje kama Polisi wakinishuku kuwa nimehusika na mauaji ya Luke na picha yangu kusambazwa? Nimewadanganya kila taarifa ambayo nimewapa. Wakigundua uongo huo wana kila sababu ya kunishuku kuhusika na mauaji hayo. Kwa hiyo nahitaji kukaa mbali na maeneo ya umma.
Lakini huku Hardstrasse ambako tunaelekea kwenye lile jumba ndipo ambako nimepigwa risasi juzi na kuokotwa na kina Luke. Lakini uziri wake polisi walikuwa hawaifahamu hii sehemu. Kwa hiyo hata wanitafute vipi hawaezi kujua ni wapi watanipata.

"This time I fight back.!'

Nilijipa moyo. Kwamba ikitokea nikishambuliwa tena safari hii nitapambana.
Huu si muda wa kujiuliza maswali tena. Nimejiuliza maswali ambayo kila muda yaninipa maswali na vitendawili vingine. Huu ni muda wa kutafuta majibu.
Sihitaji tena kujificha mbali na adui ambaye ananiwinda. Huu ni muda wa kupambana. Kupambana mpaka nipate jawabu la kile kilichonileta hapa Zurich.

Nilikuwa nahema kwa nguvu kana kwamba nimepandwa na maruhani. Maruhani ya ushari na kupambana. Nilijikuta hofu yote imeniondoka. Kitu pekee ambacho kilikuwa kimeujza moyo wangu sasa hivi ilikuwa ni hasira.

"I need a gun!" Niliwaza moyoni huku bado nahema kwa nguvu.

Nilidhamiria kupambana sasa. Nilidhamiria kupata majibu.




Itaendelea….



Habibu B. Anga 'The Bold'
To Infinity and Beyond
tapatalk_1519472923336.jpeg
 
VIPEPEO WEUSI



SEASON 2 - FROM ZURICH WITH RULES




EPISODE 21


Nilisikia wale watu ambao walikuwa wamejitambulisha kama polisi wakigonga tena.
Wasiwasi wangu wa kwanza ulikuwa ni kidonda tumboni kwangu, nilikuwa nawaza hawa polisi wakiniuliza kidonda hicho ni cha nini nitajibu vipi? Lakini pia wasiwasi wangu wa pili ulikuwa ni kitu gani hasa polisi hao kimewaleta haswa mahala hapa.

Sikutaka wagonge sana mlango kwani wangeweza kuingiwa na wasiwasi. Nikijikaza kiume kwa nguvu zangu zote na ujasiri wangu wote niweze kutembea sawasawa bila kuchechemea.

"…good morning Sir.!"

"…morning. How can I help you?"

Niliwasalimia lakini hawakunijibu haraka walibakia kunitumbulia macho tu kisha wakaangaliana. Walikuwa mwanaume mmoja na mwingine alikuwa ni mwanadada. Wote wawili walikuwa wamevalia suti. Nilielewa wazi kabisa walikuwa ni askari wapelelezi

"Do you live here?" Yule mwanadada aliniuliza huku bado amenitumbulia macho.

"No, why? Is there a problem?" Nikamuuliza.

"I am detective Corol Lawrence and this detective Noah Johnson. We would like to ask you a few questions… can we come in?" Yule dada aliongea huku ananionyesha kitambulisho chake cha upolisi.

"Yes, ofcourse!"

Niliwakaribisha ndani na haraka nikaenda kuketi kwenye sofa. Sikutaka kujibaraguza kwa kufanya ukarimu wa kuwapa kahawa au kinywaji kama ilivyo desturi ya wazungu. Niliketi haraka ili maumivu tumboni yasinizidie na wakagundua kuwa nina kidonda tumboni yakaanza maswali ya jeraha hilo kimelipataje.

"How do you know Luke Madison?" Yule mwanaume aliniuliza swali.

"Ahn! We are friends!" Nilitoa jibu la haraka haraka.

"Friends like how? You guys live together or….!"

"Im am sorry detective, you are asking me all these questions but i dont why? What is happening? Why am i being interrogated?" Nikawauliza nikiwa na uso serious. Tayari nilijua kuwa kuna kitu kilikuwa hakiko sawa kwa hiyo kabla sijasema maneno mengine yoyote ambayo yangeweza kunitia matatani.

"Well, its not an interrogation. Just some routine questions!" Yule dada aliongea huku analazimisha tabasamu.

"There is nothing 'routine' about this. You guys have come here for a reasons! I want to know why before I answer any more questiins!"

Niliwaona wanaangaliana na kupeana ishara fulani hivi. Kisha yule mpelelezi mwanamke akaongea.

"Luke is dead!"

Nilihisi kama sijasikia vizuri au labda sikumuelewa.

"What? What did you just say?" Niliongea kwa mshituko mkubwa usoni.

"Luke is dead?"

Mpelelezi mwanamke, Carol alinijibu tena. Nilitamani kama vile wawe wananitania tu. Inawezekana vipi? Luke ameondoka hapa kama nusu saa tu iliyopita.

"How? What happened?" Niliuliza nikiwa bado kwenye mshituko.

"He was shot few minutes ago!" Akanijibu tena huku amenikazia macho nahisi akitaka kuona mwitikio wangu usoni.

Nilijiinamia uso viganjani kwa sekunde kadhaa. Wao walidhani labda nilikuwa nasikitika kwa taarifa hii ya msiba, lakini kichwani mwangu kulikuwa na kitu kingine kabisa kinapita. Nilikuwa nawaza kama kuna uwezekano wa aliyenipiga risasi juzi usiku, Erica… kuwa ndiye huyo huyo ambaye alikuwa amempiga risasi Luke. Kuna upande fulani wa akili yangu ulikuwa unataka niwaambie maaskari hawa kuhusu tukio ambalo lilinitokea, lakini moyo wangu ulikuwa unasita kabisa kuwapa taarifa hii.

"Where did this happen?" Nikawauliza kwa sauti ya unyonge.

"Freacht West Street…!"

Wakanitajia mtaa ule ule ambao kuna hotel ya Radisson Blu ambayo nilifikia nilipoingia hapa Zurich. Luke pia alipoondoka hapa tulikubaliana aende hotelini pale ili kupata taarifa juu ya yule binti muhudumu Erica ambaye alinipiga risasi.

"Sir, if there is any information that can help us we will be happy to hear it!"

Kichwani nikajiuliza ni kitu gani hasa niwaambie? Niwaeleze ukweli? Je, sitaingia matatizoni kwa kuwaeleza ukweli na lengo langu la kuja hapa Zurich kuvurugika? Hapana siwezi kuwaambia ukweli…

Ilibidi nitunge uongo usio na kichwa wala miguu lakini wenye kuweza kuaminika.
Kwanza niliwadanganya jina langu3… niliwaelezankuwa naitwa "Jimmy Adekela", asili yangu ni Nigeria lakini naishi hapa Zurich kwa mwaka wa pili sasa. Kwa hiyo sikuwaeleza ukweli kwamba mimi ni Mtanzania ambaye nimeingia hapa Zurich siku chache tu zilizopita.
Nilijua kwa ujio wao huu wa haraka haraka hawawezi kunibana sana kwa maswali labda waseme wananikamata na kunipeleka kituoni, lakinj uzuri hawakuwa na sababu ya kunikamata. Japokuwa kama nikiwaeleza uongo na baadae wakigundua kuwa nimewadanganya lazima wanisake ili kunikamata na kunihoji ili kufahamu najua nini kuhusiana na kifo hicho cha Luke.

Nilikata shauri kichwani mwangu niwadanganye, siwezi kuwaeleza ukweli… nikawaeleza kwamba Luke ni rafiki yangu wa muda mrefu tu na mimi nilikuwa nimekuja hapa kumtembelea jana usiku na ndio maana ilinibidi kulala hapa. Asubuhi ya leo aliniaga kwamba anatoka kwa muda mfupi tu na atarudi baada ya dakika chache lakini badala yake ni wao wamekuja kunipa taarifa kwamba amepigwa risasi.

"…can you think of anyone who might want to kill him? Anyone… an enemy or someone who may be had a fight with a few days ago… anyone?"

Yule mpelelezi wa kiume, Noah aliniuliza.

"No.! I dont think if there is anyone who would want to kill Luke… he was a very good guy!" Nikadanganya tena.

"Ok sir, we would like to talk to you again later, but thats it for now… thank you sir!"

"No problem.!"

"If you remember anything, please give us a call… this is my number..!"

"Thank you!"

Walinipatia 'business card' nikaipokea na kuiweka mfukoni. Wakafungua mlango na kuondoka.

Nilivuta pumzi ndefu ndani na kuishusha. Sikuamini kama hatimaye wameondoka. Lakini huu haukuwa mwisho… hawa wanaonekana ni wapelelezi wazoefu, lazima watakuwa wamegundua kwamba kuna jambo nilikuwa naficha. Wameamua kuondoka kana kwamba hawanitilii mashala ili 'nirelax'. Hawataki niingiwe na wasiwasi kisha nikakimbia. Lazima wanaenda kuhakiki taarifa nilizowapa kabla hawajaja kunikamata rasmi wakigundua uongo niliowaeleza. Huu ulikuwa ni muda wa kufanya maamuzi ya haraka kabla sijachelewa.

Nikafunua shati nililovaa kutazama kidonda changu ambacho kimefungwa bandeji. Kilikuwa kiko sawia.

Nikaelekea mpaka karibu na kitanda ambako kulikuwa na mabegi yangu. Nikaanza kuyaburuza na kuondoka.

Sikutaka kupitia mlango rasmi wa mbele ya jengo au kutumia lifti. Nikihofia ningeweza kukutana na askari wale ambao wameondoka muda huu. Au labda wameacha mtu nje kunichunguza nyendo zangu.
Nikaburuza begi langu na kushuka ngazi taratibu kuelekea mlango wa nyuma wa dharura. Kutokana na kuhofia kutonesha kidonda tumboni ilinibidi kutembea taratibu sana na kwa tahadhari. Ilinichukua karibia dakika kumi nzima mpaka kutokea kwenye mlango wa nyuma wa dharura. Nikasogea mpaka barabarani na kuita Taxi.

"Freacht West Street… Radisson Blu Hotel!" Nilimuelekeza dereva taxi kisha aling'oa gari na kuondoka.

Katika ambao nilitakiwa kuwa makini kupitiliza basi ulikuwa ni huu. Nilikuwa kwenye nchi ya kigeni na tayari kulikuwa na kila dalili ya kuingia kwenye matatizo makubwa na vyombo vya usalama. Hiki kilikuwa ni kitu cha mwisho ambacho nilikuwa sitaki kitokee. Tayari nina adui asiyejulikana ambaye alikuwa ananiwinda. Sihitaji tena kuingia kwenye uadui na vyombo vya usalama.
Pia kila nilipokuwa nafikiria hii taarifa juu ya Luke kupigwa risasi nilikuwa siishi kujiuliza kama ni yule mwanadada Erica ndiye anayehusika. Nilijikuta tu natamani kufika pale hotelini ili kujionea walau kwa macho yangu ni nini hasa ambacho kilikuwa kinaendelea.

Kama dakika saba baadae tulikuwa tumeingia mtaa wa Freacht West. Nilimuelekeza dereva apaki gari upande wa pili wa barabara mkabala na Radisson Blu Hotel. Nilikuwa nataka kuona kile ambacho kilikuwa kinaendelea pale hotelini lakini sikutaka kufika kuhofia kutambulika na pengine kuingia kwenye matatizo zaidi. Hapa tulipopaki upande wa pili wa barabara nilikuwa naweza kuona vyema kabisa kile ambacho kilikuwa kinaendelea.

Nje ya hoteli pembeni karibu na mlangoni, kulikuwa kumefungwa utepe wa njano wa polisi kuashiria kwamba hiyo ndiyo 'crime scene'. Ndipo mahala ambapo Luke alipigwa risasi.
Kulikuwa na kama polisi watano hivi wenye sare ambao walikuwa eneo hili. Pia kulikuwa na watu wawili ambao walionekana ni watu wa 'forensic' mmoja akiwa anapiga picha lile eneo sakafuni na mwingine akiwa kama anapima vitu fulani hivi pale chini.

Pembeni nje ya ule utepe kulikuwa na raia kadhaa wasiozidi kumi na tano wamesimama wakishangaa. Nilimuona moja ya askari akiwa anachukua maelezo ya meneja wa Hoteli, yule jamaa ambaye juzi alinikuta mapokezi nabishana na Erica na kunitaka niondoke.
Nikapepesa macho yangu kutazama watu walioko pale wakishangaa. Moyo wangu ulipasuka ghafla nilipomuona moja ya watu ambao walikuwa eneo hili. Katika lile kundi la raia ambao walikuwa wamesimama wakishangaa alikuwepo yule jamaa anayevaa kofia ya 'pama'. Yule jamaa mweusi ambaye juzi hapa hotelini alikuwa ameketi kwenye moja ya sofa za pale mapokezi anasoma gazeti. Jamaa ambaye Erica alikuwa anaongea na mimi huku anamwangalia kwa kuibia ibia kana kwamba anamuhofia hivi. Ni yule jamaa alikuwepo tena mahala hapa kwenye kundi la raia wanaoshangaa.

Tangu juzi sikuweza kumuona sura yake kutokana na kofia lake la pama. Na hata leo hii muda huu pia sikuweza kuona sura yake. Lakini nilikuwa na hakika kwa asilimia mia moja kwamba alikuwa ni yeye. Kofia yake ile ile ya pama kubwa kiasi ya rangi ya kijivu. Koti lake jeusi refu lenye kufika mpaka usawa wa magoti na kuvuka chini kidogo. Mkononi ameshikilia gazeti. Hakika sikuwa nakosea. Alikuwa ni yeye. Alikuwa anatazama kinachoendelea pale kama vile watazamaji wengine.

"Ni nani huyu mtu?" Nilijiuliza mwenyewe kichwani.

Nikiwa najiuliza hivu maswali kichwani… ghafla! yule jamaa akageuka na kutazima upande wetu, hapa taxi ilikopaki. Ubaya ni kwamba nilikuwa nimeshusha dirisha chini kidogo ili niweze kuona kwa usawia. Nilijikuta macho yangu na yake yanagongana. Kijasho kilianza kunitoka huku nahema kwa nguvu. Tulikaziana macho kwa takribani sekunde thelathini nzima. Sasa ndio nilipata wasaa wa kumuona vyema. Upande wa kushoto usoni alikuwa na kovu kubwa kana kwamba aliwahi kupata jeraha kubwa la kukatwa na kitu.

"Namjua huyu jamaa.!!"

Ndilo wazo la kwanza ambalo lilikatisha akilini mwangu. Nilikuwa na hakika kwa asilimia mia moja kwamba huyu mtu namfahamu. Nimeshawahi kumuona hapo kabla siku za nyuma kabla ya hapa hotelini. Kovu lake hili ndilo haswa lilinipa uhakika kwamba namfahamu huyu mtu. Lakini sikuweza kukumbuka ni wapi. Akili ilikiwa inashindwa kutambua ni wapi haswa niliwahi kumuona. Lakini kwa hakika kabisa kumbukumbu yangu iliniambia huyu mtu namfahamu.

Nilimkazia macho. Sikupepesa hata kidogo japo nilikuwa nimekumbwa na woga wa ghafla moyoni mpaka jasho linanitoka.
Taratibu nikamuona anageuka na kuendelea kushangaa kule kwenye eneo la tukio.

Nikamuamuru dereva tuondoke.

"Hardstrasse.!" Nikamuelekeza kwa kuelekea.

Ndio. Hardstrasse. Ndio mahala pekee ambako kwa sasa nilihisi palikuwa sahihi kwangu kwenda. Siwezi kukaaa tena hotelini. Itakuwaje kama Polisi wakinishuku kuwa nimehusika na mauaji ya Luke na picha yangu kusambazwa? Nimewadanganya kila taarifa ambayo nimewapa. Wakigundua uongo huo wana kila sababu ya kunishuku kuhusika na mauaji hayo. Kwa hiyo nahitaji kukaa mbali na maeneo ya umma.
Lakini huku Hardstrasse ambako tunaelekea kwenye lile jumba ndipo ambako nimepigwa risasi juzi na kuokotwa na kina Luke. Lakini uziri wake polisi walikuwa hawaifahamu hii sehemu. Kwa hiyo hata wanitafute vipi hawaezi kujua ni wapi watanipata.

"This time I fight back.!'

Nilijipa moyo. Kwamba ikitokea nikishambuliwa tena safari hii nitapambana.
Huu si muda wa kujiuliza maswali tena. Nimejiuliza maswali ambayo kila muda yaninipa maswali na vitendawili vingine. Huu ni muda wa kutafuta majibu.
Sihitaji tena kujificha mbali na adui ambaye ananiwinda. Huu ni muda wa kupambana. Kupambana mpaka nipate jawabu la kile kilichonileta hapa Zurich.

Nilikuwa nahema kwa nguvu kana kwamba nimepandwa na maruhani. Maruhani ya ushari na kupambana. Nilijikuta hofu yote imeniondoka. Kitu pekee ambacho kilikuwa kimeujza moyo wangu sasa hivi ilikuwa ni hasira.

"I need a gun!" Niliwaza moyoni huku bado nahema kwa nguvu.

Nilidhamiria kupambana sasa. Nilidhamiria kupata majibu.




Itaendelea….



Habibu B. Anga 'The Bold'
To Infinity and BeyondView attachment 776942
Sio shabiki maandazi ila Dogo (fundi) unaweza...
 
VIPEPEO WEUSI



SEASON 2 - FROM ZURICH WITH RULES




EPISODE 21


Nilisikia wale watu ambao walikuwa wamejitambulisha kama polisi wakigonga tena.
Wasiwasi wangu wa kwanza ulikuwa ni kidonda tumboni kwangu, nilikuwa nawaza hawa polisi wakiniuliza kidonda hicho ni cha nini nitajibu vipi? Lakini pia wasiwasi wangu wa pili ulikuwa ni kitu gani hasa polisi hao kimewaleta haswa mahala hapa.

Sikutaka wagonge sana mlango kwani wangeweza kuingiwa na wasiwasi. Nikijikaza kiume kwa nguvu zangu zote na ujasiri wangu wote niweze kutembea sawasawa bila kuchechemea.

"…good morning Sir.!"

"…morning. How can I help you?"

Niliwasalimia lakini hawakunijibu haraka walibakia kunitumbulia macho tu kisha wakaangaliana. Walikuwa mwanaume mmoja na mwingine alikuwa ni mwanadada. Wote wawili walikuwa wamevalia suti. Nilielewa wazi kabisa walikuwa ni askari wapelelezi

"Do you live here?" Yule mwanadada aliniuliza huku bado amenitumbulia macho.

"No, why? Is there a problem?" Nikamuuliza.

"I am detective Corol Lawrence and this detective Noah Johnson. We would like to ask you a few questions… can we come in?" Yule dada aliongea huku ananionyesha kitambulisho chake cha upolisi.

"Yes, ofcourse!"

Niliwakaribisha ndani na haraka nikaenda kuketi kwenye sofa. Sikutaka kujibaraguza kwa kufanya ukarimu wa kuwapa kahawa au kinywaji kama ilivyo desturi ya wazungu. Niliketi haraka ili maumivu tumboni yasinizidie na wakagundua kuwa nina kidonda tumboni yakaanza maswali ya jeraha hilo kimelipataje.

"How do you know Luke Madison?" Yule mwanaume aliniuliza swali.

"Ahn! We are friends!" Nilitoa jibu la haraka haraka.

"Friends like how? You guys live together or….!"

"Im am sorry detective, you are asking me all these questions but i dont why? What is happening? Why am i being interrogated?" Nikawauliza nikiwa na uso serious. Tayari nilijua kuwa kuna kitu kilikuwa hakiko sawa kwa hiyo kabla sijasema maneno mengine yoyote ambayo yangeweza kunitia matatani.

"Well, its not an interrogation. Just some routine questions!" Yule dada aliongea huku analazimisha tabasamu.

"There is nothing 'routine' about this. You guys have come here for a reasons! I want to know why before I answer any more questiins!"

Niliwaona wanaangaliana na kupeana ishara fulani hivi. Kisha yule mpelelezi mwanamke akaongea.

"Luke is dead!"

Nilihisi kama sijasikia vizuri au labda sikumuelewa.

"What? What did you just say?" Niliongea kwa mshituko mkubwa usoni.

"Luke is dead?"

Mpelelezi mwanamke, Carol alinijibu tena. Nilitamani kama vile wawe wananitania tu. Inawezekana vipi? Luke ameondoka hapa kama nusu saa tu iliyopita.

"How? What happened?" Niliuliza nikiwa bado kwenye mshituko.

"He was shot few minutes ago!" Akanijibu tena huku amenikazia macho nahisi akitaka kuona mwitikio wangu usoni.

Nilijiinamia uso viganjani kwa sekunde kadhaa. Wao walidhani labda nilikuwa nasikitika kwa taarifa hii ya msiba, lakini kichwani mwangu kulikuwa na kitu kingine kabisa kinapita. Nilikuwa nawaza kama kuna uwezekano wa aliyenipiga risasi juzi usiku, Erica… kuwa ndiye huyo huyo ambaye alikuwa amempiga risasi Luke. Kuna upande fulani wa akili yangu ulikuwa unataka niwaambie maaskari hawa kuhusu tukio ambalo lilinitokea, lakini moyo wangu ulikuwa unasita kabisa kuwapa taarifa hii.

"Where did this happen?" Nikawauliza kwa sauti ya unyonge.

"Freacht West Street…!"

Wakanitajia mtaa ule ule ambao kuna hotel ya Radisson Blu ambayo nilifikia nilipoingia hapa Zurich. Luke pia alipoondoka hapa tulikubaliana aende hotelini pale ili kupata taarifa juu ya yule binti muhudumu Erica ambaye alinipiga risasi.

"Sir, if there is any information that can help us we will be happy to hear it!"

Kichwani nikajiuliza ni kitu gani hasa niwaambie? Niwaeleze ukweli? Je, sitaingia matatizoni kwa kuwaeleza ukweli na lengo langu la kuja hapa Zurich kuvurugika? Hapana siwezi kuwaambia ukweli…

Ilibidi nitunge uongo usio na kichwa wala miguu lakini wenye kuweza kuaminika.
Kwanza niliwadanganya jina langu3… niliwaelezankuwa naitwa "Jimmy Adekela", asili yangu ni Nigeria lakini naishi hapa Zurich kwa mwaka wa pili sasa. Kwa hiyo sikuwaeleza ukweli kwamba mimi ni Mtanzania ambaye nimeingia hapa Zurich siku chache tu zilizopita.
Nilijua kwa ujio wao huu wa haraka haraka hawawezi kunibana sana kwa maswali labda waseme wananikamata na kunipeleka kituoni, lakinj uzuri hawakuwa na sababu ya kunikamata. Japokuwa kama nikiwaeleza uongo na baadae wakigundua kuwa nimewadanganya lazima wanisake ili kunikamata na kunihoji ili kufahamu najua nini kuhusiana na kifo hicho cha Luke.

Nilikata shauri kichwani mwangu niwadanganye, siwezi kuwaeleza ukweli… nikawaeleza kwamba Luke ni rafiki yangu wa muda mrefu tu na mimi nilikuwa nimekuja hapa kumtembelea jana usiku na ndio maana ilinibidi kulala hapa. Asubuhi ya leo aliniaga kwamba anatoka kwa muda mfupi tu na atarudi baada ya dakika chache lakini badala yake ni wao wamekuja kunipa taarifa kwamba amepigwa risasi.

"…can you think of anyone who might want to kill him? Anyone… an enemy or someone who may be had a fight with a few days ago… anyone?"

Yule mpelelezi wa kiume, Noah aliniuliza.

"No.! I dont think if there is anyone who would want to kill Luke… he was a very good guy!" Nikadanganya tena.

"Ok sir, we would like to talk to you again later, but thats it for now… thank you sir!"

"No problem.!"

"If you remember anything, please give us a call… this is my number..!"

"Thank you!"

Walinipatia 'business card' nikaipokea na kuiweka mfukoni. Wakafungua mlango na kuondoka.

Nilivuta pumzi ndefu ndani na kuishusha. Sikuamini kama hatimaye wameondoka. Lakini huu haukuwa mwisho… hawa wanaonekana ni wapelelezi wazoefu, lazima watakuwa wamegundua kwamba kuna jambo nilikuwa naficha. Wameamua kuondoka kana kwamba hawanitilii mashala ili 'nirelax'. Hawataki niingiwe na wasiwasi kisha nikakimbia. Lazima wanaenda kuhakiki taarifa nilizowapa kabla hawajaja kunikamata rasmi wakigundua uongo niliowaeleza. Huu ulikuwa ni muda wa kufanya maamuzi ya haraka kabla sijachelewa.

Nikafunua shati nililovaa kutazama kidonda changu ambacho kimefungwa bandeji. Kilikuwa kiko sawia.

Nikaelekea mpaka karibu na kitanda ambako kulikuwa na mabegi yangu. Nikaanza kuyaburuza na kuondoka.

Sikutaka kupitia mlango rasmi wa mbele ya jengo au kutumia lifti. Nikihofia ningeweza kukutana na askari wale ambao wameondoka muda huu. Au labda wameacha mtu nje kunichunguza nyendo zangu.
Nikaburuza begi langu na kushuka ngazi taratibu kuelekea mlango wa nyuma wa dharura. Kutokana na kuhofia kutonesha kidonda tumboni ilinibidi kutembea taratibu sana na kwa tahadhari. Ilinichukua karibia dakika kumi nzima mpaka kutokea kwenye mlango wa nyuma wa dharura. Nikasogea mpaka barabarani na kuita Taxi.

"Freacht West Street… Radisson Blu Hotel!" Nilimuelekeza dereva taxi kisha aling'oa gari na kuondoka.

Katika ambao nilitakiwa kuwa makini kupitiliza basi ulikuwa ni huu. Nilikuwa kwenye nchi ya kigeni na tayari kulikuwa na kila dalili ya kuingia kwenye matatizo makubwa na vyombo vya usalama. Hiki kilikuwa ni kitu cha mwisho ambacho nilikuwa sitaki kitokee. Tayari nina adui asiyejulikana ambaye alikuwa ananiwinda. Sihitaji tena kuingia kwenye uadui na vyombo vya usalama.
Pia kila nilipokuwa nafikiria hii taarifa juu ya Luke kupigwa risasi nilikuwa siishi kujiuliza kama ni yule mwanadada Erica ndiye anayehusika. Nilijikuta tu natamani kufika pale hotelini ili kujionea walau kwa macho yangu ni nini hasa ambacho kilikuwa kinaendelea.

Kama dakika saba baadae tulikuwa tumeingia mtaa wa Freacht West. Nilimuelekeza dereva apaki gari upande wa pili wa barabara mkabala na Radisson Blu Hotel. Nilikuwa nataka kuona kile ambacho kilikuwa kinaendelea pale hotelini lakini sikutaka kufika kuhofia kutambulika na pengine kuingia kwenye matatizo zaidi. Hapa tulipopaki upande wa pili wa barabara nilikuwa naweza kuona vyema kabisa kile ambacho kilikuwa kinaendelea.

Nje ya hoteli pembeni karibu na mlangoni, kulikuwa kumefungwa utepe wa njano wa polisi kuashiria kwamba hiyo ndiyo 'crime scene'. Ndipo mahala ambapo Luke alipigwa risasi.
Kulikuwa na kama polisi watano hivi wenye sare ambao walikuwa eneo hili. Pia kulikuwa na watu wawili ambao walionekana ni watu wa 'forensic' mmoja akiwa anapiga picha lile eneo sakafuni na mwingine akiwa kama anapima vitu fulani hivi pale chini.

Pembeni nje ya ule utepe kulikuwa na raia kadhaa wasiozidi kumi na tano wamesimama wakishangaa. Nilimuona moja ya askari akiwa anachukua maelezo ya meneja wa Hoteli, yule jamaa ambaye juzi alinikuta mapokezi nabishana na Erica na kunitaka niondoke.
Nikapepesa macho yangu kutazama watu walioko pale wakishangaa. Moyo wangu ulipasuka ghafla nilipomuona moja ya watu ambao walikuwa eneo hili. Katika lile kundi la raia ambao walikuwa wamesimama wakishangaa alikuwepo yule jamaa anayevaa kofia ya 'pama'. Yule jamaa mweusi ambaye juzi hapa hotelini alikuwa ameketi kwenye moja ya sofa za pale mapokezi anasoma gazeti. Jamaa ambaye Erica alikuwa anaongea na mimi huku anamwangalia kwa kuibia ibia kana kwamba anamuhofia hivi. Ni yule jamaa alikuwepo tena mahala hapa kwenye kundi la raia wanaoshangaa.

Tangu juzi sikuweza kumuona sura yake kutokana na kofia lake la pama. Na hata leo hii muda huu pia sikuweza kuona sura yake. Lakini nilikuwa na hakika kwa asilimia mia moja kwamba alikuwa ni yeye. Kofia yake ile ile ya pama kubwa kiasi ya rangi ya kijivu. Koti lake jeusi refu lenye kufika mpaka usawa wa magoti na kuvuka chini kidogo. Mkononi ameshikilia gazeti. Hakika sikuwa nakosea. Alikuwa ni yeye. Alikuwa anatazama kinachoendelea pale kama vile watazamaji wengine.

"Ni nani huyu mtu?" Nilijiuliza mwenyewe kichwani.

Nikiwa najiuliza hivu maswali kichwani… ghafla! yule jamaa akageuka na kutazima upande wetu, hapa taxi ilikopaki. Ubaya ni kwamba nilikuwa nimeshusha dirisha chini kidogo ili niweze kuona kwa usawia. Nilijikuta macho yangu na yake yanagongana. Kijasho kilianza kunitoka huku nahema kwa nguvu. Tulikaziana macho kwa takribani sekunde thelathini nzima. Sasa ndio nilipata wasaa wa kumuona vyema. Upande wa kushoto usoni alikuwa na kovu kubwa kana kwamba aliwahi kupata jeraha kubwa la kukatwa na kitu.

"Namjua huyu jamaa.!!"

Ndilo wazo la kwanza ambalo lilikatisha akilini mwangu. Nilikuwa na hakika kwa asilimia mia moja kwamba huyu mtu namfahamu. Nimeshawahi kumuona hapo kabla siku za nyuma kabla ya hapa hotelini. Kovu lake hili ndilo haswa lilinipa uhakika kwamba namfahamu huyu mtu. Lakini sikuweza kukumbuka ni wapi. Akili ilikiwa inashindwa kutambua ni wapi haswa niliwahi kumuona. Lakini kwa hakika kabisa kumbukumbu yangu iliniambia huyu mtu namfahamu.

Nilimkazia macho. Sikupepesa hata kidogo japo nilikuwa nimekumbwa na woga wa ghafla moyoni mpaka jasho linanitoka.
Taratibu nikamuona anageuka na kuendelea kushangaa kule kwenye eneo la tukio.

Nikamuamuru dereva tuondoke.

"Hardstrasse.!" Nikamuelekeza kwa kuelekea.

Ndio. Hardstrasse. Ndio mahala pekee ambako kwa sasa nilihisi palikuwa sahihi kwangu kwenda. Siwezi kukaaa tena hotelini. Itakuwaje kama Polisi wakinishuku kuwa nimehusika na mauaji ya Luke na picha yangu kusambazwa? Nimewadanganya kila taarifa ambayo nimewapa. Wakigundua uongo huo wana kila sababu ya kunishuku kuhusika na mauaji hayo. Kwa hiyo nahitaji kukaa mbali na maeneo ya umma.
Lakini huku Hardstrasse ambako tunaelekea kwenye lile jumba ndipo ambako nimepigwa risasi juzi na kuokotwa na kina Luke. Lakini uziri wake polisi walikuwa hawaifahamu hii sehemu. Kwa hiyo hata wanitafute vipi hawaezi kujua ni wapi watanipata.

"This time I fight back.!'

Nilijipa moyo. Kwamba ikitokea nikishambuliwa tena safari hii nitapambana.
Huu si muda wa kujiuliza maswali tena. Nimejiuliza maswali ambayo kila muda yaninipa maswali na vitendawili vingine. Huu ni muda wa kutafuta majibu.
Sihitaji tena kujificha mbali na adui ambaye ananiwinda. Huu ni muda wa kupambana. Kupambana mpaka nipate jawabu la kile kilichonileta hapa Zurich.

Nilikuwa nahema kwa nguvu kana kwamba nimepandwa na maruhani. Maruhani ya ushari na kupambana. Nilijikuta hofu yote imeniondoka. Kitu pekee ambacho kilikuwa kimeujza moyo wangu sasa hivi ilikuwa ni hasira.

"I need a gun!" Niliwaza moyoni huku bado nahema kwa nguvu.

Nilidhamiria kupambana sasa. Nilidhamiria kupata majibu.




Itaendelea….



Habibu B. Anga 'The Bold'
To Infinity and BeyondView attachment 776942
Mkuu asante kwa madini mazuri haya usisahau na other half umepotea sana kule
 
tapatalk_1519472923336.jpeg



VIPEPO WEUSI



SEASON 2 - FROM ZURICH WITH RULES




EPISODE 22



Nilikiwa nimefika kwenye lile jumba mtaa wa Hardstrasse karibia masaa manne yaliyopita. Muda wote huu nilikuwa nachambua lundo la nyaraka nilizonazo. Kuanzia zile ambazo nilizipata kwenye bahasha aliyoniachia mzee wangu mpaka zile ambazo nilizipata kutoka kwa Hudini.

Kama mara zote zilizopita, nyaraka hizi zilikuwa hazieleweki kabisa. Zilikuwa na mfululizo wa anauani pamoja na majina ya watu na namba za akaunti za benki pamoja na kumbukumbu za miamala. Wingi wa nyaraka hizi ulikuwa unanifanya nishindwe hata kuweka kipaumbele nianze kufuatilia anuani ipi, au jina lipi au anuani ipi kwanza kabla ya nyingine. Walau ingekuwa orodha yenye vitu vichache ningeweza kusema nifuatilie kitu kimoja baada ya kingine mpaka nipate jawabu. Lakini lundo hili la nyaraka na orodha ndefu namna hii ilikuwa inanifanya nishindwe kufanya maamuzi ya wapi hasa nianzie.

Lakini nikiwa katika mkanganyiko huu kuna jambo moja ambalo nilihisi lilikuwa dhahiri mbele yangu ambalo walau nilikuwa naweza kuanza kuanzia. Ilikuwa ni ile anuani. Anuani ambayo niliikuta kwenye bahasha ambayo nilipewa na mzee wangu ikiwa na jina la Hudini lakini pia anuani hiyo hiyo nilikuja kuikuta kwenye nyaraka nikizopewa hapa Zurich ikiwa na jina picha ya Erica lakini jina tofauti la kike.

IVANKA WYCLIFFE
AFFOLTERNSTRASSE 44
CITYPORT
POSTFACH 8131
8050
ZURICH

Anuani hii ilikuwa inarandana kabisa na ile ambayo nilikuta ndani ya bahasha niliyopewa na mzee wangu.


HUDINI
AFFOLTERNSTRASSE 44
CITYPORT
POSTFACH 8131
8050
ZURICH
SWITZERLAND.

Tofauti ikiwa jina la kwanza tu.


Nikakata shauri kichwani mwangu kwamba hii ndio anuani ambayo natakiwa kuanza nayo kwa sababu katika lundo la nyaraka hizi na orodha ya majina, akaunti, miamala na anuani zote zilizopo hapa, ni anuani hii tu ambayo mara moja iliamsha udadisi ndani yangu. Nyingine zote sikuzielewa.

Nikachukua simu yangu na kufungua upande wa utafutaji wa ramani. Nikachagua mji wa Zurich. Nikatafuta mtaa wa Affolterntrasse 44. Nikaupata. Nikatazama umbali ulipo kutoka hapa mtaa wa Hardstrasse. Nikaona ni mwendo wa kama dakika kumi na tano hivi kwa gari.

Nikatazama saa kwenye simu. Ilikuwa saa tisa kasoro mchana.

Huu haukuwa muda mzuri kwangu kuzurura mitaani. Bado sijajua kama wale wapelelezi kama wameshang'amua taarifa za uongo ambazo niliwapa. Kwa hiyo sikutaka kujiweka kwenye matata kirahisi rahisi. Ni vyema nisubiri. Ndio, ni vyema nisubiri giza liingie kisha nianze kuchanja mbuga kufuatilia hii anuani.

Nikainua shati kutazama kidonda tumboni. Bado kilikuwa kwenye hali nzuri, lakini nahitaji baada ya muda fulani kubadili bandeji kwenye hiki kidonda. Ubaya ni kwamba siwezi kwenda hospitali. Hivyo nahitaji kuchakata akili haraka nifanye nini kuhusu huduma ya kidaktari juu ya hili jeraha.

Nilikuwa na karibia siku mbili sijapata usingizi wa uhakika. Nikakata shauri muda huu ambao nasubiria giza liingie ni vyema niutumie kupunguza lundo la usingizi nilionao kichwani.

Nilijisogeza mpaka pembezoni mwa ukuta. Nikafungua begi langu na kutoa nguo kadhaa. Nikazikunja vyema na kuziweka sakafuni na kisha kulalia kama mto.

Nililala chali macho nikitazama juu. Mawazo kadha wa kadha yalikuwa yanapita kichwani.
Sikuwa salama nje mitaani kwa kuwa naweza kukumbuna na polisi ambao nilikuwa na hakika kabisa kwamba walikuwa wananitafuta muda huu. Lakini pia siko salama mahala hapa kwa kuwa ni siku mbili tu zilizopita nilipigwa risasi humu humu ndani ya hili jengo.


Nahitaji kujilinda. Nahitaji kupambana kama nitakabiliana na hatari kwa mara nyingine. "I need a gun.!"

Nikiwa bado nimejilaza vile nikaanza kutafakari kuhusu jengo hili. Kuna nini kwenye floor za juu? Nimekuwa nikifika hapa kwa mara kadhaa sasa lakini bado sikuwahi kupandisha floor za juu. Kuna kitu gani hasa huko juu?
Kwa nini pia mzee Rweyemamu alinunua hili jengo? Alilinunua kutoka kwa nani? Lazima kutakuwa na sababu mahususi ya yeye au wao kununua jengo hili. Nahitaji kufahamu kwa nini.

Nikiwa kwenye huku kuwaza na kuwazua na kujiuliza maswali usingizi ukanipitia.


******

Sikuwasikia wakiingia au mlango kufunguliwa. Nilishangaa tu ghafla walikuwa mbele yangu au tuseme juu yangu kwa ufasaha zaidi.

Nilikuwa bado nimejilaza sakafuni, wao walikuwa wamesimama wakinitazama. Walikuwa ni yule mzee wa Hudini, Erica na Luke.
Nilijihisi kama nimeona jini nilipomuona Luke akiwa hai, mzima na salama bin salmin ananitazama.

"Luke? You are alive?" Nikatahamaki.

Hakujibu chochote. Alitabasamu tu. Lilikuwa ni tabasamu la kifedhuli ambalo halikuashiria kheri mbele yangu.
Nikamuona yule mzee wa Hudini akimgeukia Erica na kumpa ishara fulani hivi kwa kumkonyeza.
Nikamshuhudia Erica akiingiza mkono kwenye mkoba wake wa mokononi na kutoa bastola na kuninyooshea. Aliielekea usawa wa kichwa.

Naamini alikuwa anaona uso wangu wa woga na wasiwasi na ilikuwa inampa furaha nafsini mwake. Alitabasamu huku yule mzee wa Hudini na Luke wakitoa vicheko vya kifedhuli.

"Goodbye Ray!" Aliongea kwa sauti kali ya kunong'ona ikiashiria ukatili ulioko nafsini mwake.
Akafyatua risasi. "BAAAANNNGGG.!!"


"Nooooooo.!!"

Nilishituka kutoka usingizini jasho likinitiririka kama nimemwagiwa maji. Nilikuwa nahema kwa nguvu nikitazma huku na huko. Ilikuwa ni ndoto tu lakini ilinifanya nisikie hofu kana kwamba nilichokiona kilikuwa ni kitu halisi kinanitokea.

Nikachukua simu na kutazama muda. Ilikuwa ni saa mbili na dakika tano usiku. Nilikuwa nimelala kwa zaidi ya masaa manne.

Nikainuka na kuanza kukushanya makaratasi yangu vyema pale safuni ambayo nilikuwa nayafanyia uchunguiz awali na kuyarejesha kwenye begi. Nikazikunja vyema zile nguo nilizozilalia na pia nazo kuzirejesha kwenye begi.

Nikainuka na kuanza kuondoka. Ulikuwa ni muda sasa kufuatilia ile anuani mtaa wa Affolterntrasse.

Sikujua ni kwa nini lakini kidonda tumboni kilikuwa kinaanza kuniuma. Nilikuwa nahitaji daktari wa kukitazama haraka lakini sikujua ni nini hasa napaswa kukifanya. Nikajikaza kiume na kutembea mpaka nje ya jengo mpaka barabarani.

"Affolterntrasse 44."

Nilimuambia dereva taxi baada ya kusimama na kukwea ndani.
Ilituchukua karibia nusu saa nzima kufika mtaa wa Affolterntrasse tofauti na ambavyo nilikuwa nimekadiria awali.

"Keep change.!"

Nilimlipa dereva taxi na kushuka.

Nilishuka upande wa pili wa barabara mkabala na nyumba yenye anuania ambayo ilikuwa imeandika kwenye zile nyaraka zangu.

Nyumba hii ilikuwa kwenye moja ya mitaa iliyoko pembezoni kidogo mwa jiji hili la Zurich. Ni mitaa ambayo kwa umombo wanaita "suburbs". Mitaa yenye kuishi watu wenye kipato cha kati. Sio mitaa ya kitajiri sana lakini wanaishi watu wenye haueni kubwa ya kimaisha. Nyumba zake zote zilikuwa za kufanana. Zilikuwa nyumba kubwa nzuri zenye mandhari ya kuvutia.

Zilikuwa nyumba za rangi nyeupe ambazo zilikuwa na ghorofa moja juu kila myumba. Nyumba zote zilikuwa na ukoka wa kijani kibichi ambao ulionekana kutunzwa vizuri na kukatwa kimaridadi. Kwa mbele kila nyumba ilikuwa na uzio wa mbao za urefu wa kama mita moja ambazo zilikatwa nadhifu na kupakwa rangi nyeupe yenye kurandana na rangi ya nyumba hizi.


Jambo la haraka ambalo nililing'amua mara moja ni kwamba nyumba ambayo ilikuwa na anuani ya kwenye nyaraka yangu ndio pekee ambayo haikuwa inawaka taa ndani yake. Yaani kwamba nyumba zote nyingine zilionekana taa ndani na nje zikiwaka huku nikisikia vicheko na sauti hafifu za maongezi ya hapa na pale kuonyesha nyumba hizo wenyewe walikuwepo wakipiga soga. Lakini nyumba hii ya anuani yangu haikuwa inawaka taa wala kuonyesha dalili ya uwepo wa watu ndani yake.

Sikutaka kupoteza muda kujiuliza maswali. Nikavuka barabara na kutembea mpaka mlangoni mwa ile nyumba.

"Hallowwwww.!!"

Nilibisha hodi.

"Hallowwww… anybody home?"

Nilibisha tena hodi bila majibu. Nikabisha tena hodi na tena na tena lakini palikuwa kimya. Hakuna mtu ambaye alijibu. Ilithibitisha nilichokuwa nakiwaza. Hakukuwa na mtu ndani ya nyumba hii?
Nilianza kuwaza nifanye nini? Niondoke? Hapana… siwezi kuja mpaka hapa nakugeuza tu. Nifanyeje sasa?

Uzuri au ubaya wa mitaa hii ya "suburbs" duniani kote ni namna ambavyo majirani wanavyoishi. Kila mtu anajali maisha yake. "Everyone minds his own business." Hakuna ambaye anajali nini kinaendelea kwa jirani. Hakuna kuombana 'chumvi' kama mitaa ya uswahilini. Iwe ni Masaki, Dar es Salaam au Saratoga, California au Affolterntrasse, hapa Zurich au sehemu yoyote ile yenye suburbs duniani. Ukiishi hapo tegemea maisha ya upweke kana kwamba hauna majirani.

Siku pekee ambayo utajua una jirani ni msimu wa sikukuu jirani akikuletea 'pie' aliyoipika kwake au bakshishi nyingine kama pipi na vikolombwezo vidogo vidogo kukutakia heri ya sikukuu.

Hii ilikuwa ni faida kwangu. Niliamini kabisa hakuna jirani ambaye alikuwa anafuatilia nyendo zangu au hata kujua kama niko hapo. Nikazunguka nyuma ya nyumba. Nikapekua pekua mpaka kupata kipande cha waya mgumu kama pini hivi. Japokuwa sikuwa hodari sana lakini nilikuwa najua namna la 'ku-pick lock' za vitasa. Nilikuwa najua nini cha kufanya.

Nikahangaika na kitasa karibia dakika kumi nzima mpaka nilipokisikia kimefyatuka. Nikaingia ndani bila kupoteza muda. Sikutaka kuwasha taa ili nisije kuwashitua watu kama kuna yeyote ambaye alikuwa anafuatilia. Niliamua kutumia tochi ya simu yangu.

Kwa muonekano wa haraka tu, ndani humu kulikuwa ni nadhifu mno. Vitu vikiwa vimepangika sawia. Lakini kulikuwa kunatoa taswira mbili zenye kukinzana.
Moja kulionekana kuna watu wanaishi kwa kuwa hakukuwa na vumbi na vitu vilipangwa sawa sawa. Lakini taswira ya pili palikuwa panaonyesha dalili kinzani kwamba hakukuwa na watu wanaishi hapo. Kwa sabahu vitu vilikuwa vimepangwa kwa usahihi mno wa kupitiliza. Nyumba ambayo watu wanaishi lazima uone rapsha za hapa na pale. Labda sofa limebonyea au kuvurugika fulani… hiki kiko pale ambako hakitakiwi kuwa na kadhalika. Kuna dalili fulani hivi unaiona mahala ambako kuna binadamu anaishi. Lakini hapa palikuwa pamepangiliwa kuwa ufasaha mno.

Nilikuwa sebuleni mwa nyumba hii nikimulika huku na huko. Sikuona kitu chochote cha kushitua au kuvutia kukidadisi. Ni mpaka mwanga wa tochi yangu ya simu ulipotua ukutani ndipo ambapo mapigo yangu ya moyo yalianza kwenda mbio.

Nikasogea karibu kutazama.

Ukutani kulikuwa kumewekwa picha kadhaa zikiwa kwenye 'fremu' nadhifu. Lakini katika picha hizi ni picha moja ambayo ilinifanya moyo kwenda mbio. Ilikuwa ni picha ikionekana ya familia. Kulikuwa na baba, mama na watoto watatu. Watoto wawili wa kiume na mmoja wa kike.

Mwanamama sikumtambua lakini yule ambaye alikuwa anaonekana kama baba alikuwa ni jamaa yule yule mzungu ambaye yuko kwenye picha ambayo niliikuta kwenye bahasha niliyopewa na mzee wangu imeandikwa '"Strike #1" ambayo yuko mahala fulani kama bandarini kwenye makontena yeye na Rais Albert Kafumu na watu wengine. Ni mtu huyu huyu ambaye pia yuko kwenye picha ile nyingine iliyoandikwa "Strike #5" ambayo kama imepigwa mahala fulani mtaani maeneo ya ulaya au Marekani. Lakini pia ni mtu huyu huyu ambaye yuko kwenye picha niliyopewa na Hudini akiwa kwenye picha ya pamoja na baba yake Cheupe na Chuepe mwenyewe akiwa mtoto.

Lakini kilichonishitua zaidi ni wale watoto walioko kwenye picha hii. Hasa watoto wawili… yule wa kiume mmoja na yule wa kike. Sura zao hazikuwa ngeni kwangu. Nilikuwa nzifahamu… walikuwa ni Luke aliyeniokoa siku niliyopigwa risasi na ambaye leo asubuhi ameuwawa na yule mtoto wa kike alikuwa ni Erica yule binti muhudumu wa hoteli na ambaye alinipiga risasi juzi usiku.

Nilihisi labda macho yangu hayaoni sawa sawa. Nikayafikicha na kisha kumulika tochi yangu kwa karibu zaidi.

Sikukosea… alikuwa ni Luke na Erica wakiwa watoto.


Kichwani taa ikianza kuwaka. Nikaanza kung'amua hii anuani ina maana gani hasa.




Itaendelea…


Habibu B. Anga 'The Bold'
To Infinity and Beyond
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom