Mpaka auze nakala za kutosha ndiyo atarudi.Hivi hii kitu inaendelea au ndio bye bye hapo ilipoishia polisi wa Zurich wakigonga mlango??
AhahahahahaHuyu jamaa bado yupo hai???
Isiwe amesha kufa sisi bado tunasubiri mwendelezo tu
Sio shabiki maandazi ila Dogo (fundi) unaweza...VIPEPEO WEUSI
SEASON 2 - FROM ZURICH WITH RULES
EPISODE 21
Nilisikia wale watu ambao walikuwa wamejitambulisha kama polisi wakigonga tena.
Wasiwasi wangu wa kwanza ulikuwa ni kidonda tumboni kwangu, nilikuwa nawaza hawa polisi wakiniuliza kidonda hicho ni cha nini nitajibu vipi? Lakini pia wasiwasi wangu wa pili ulikuwa ni kitu gani hasa polisi hao kimewaleta haswa mahala hapa.
Sikutaka wagonge sana mlango kwani wangeweza kuingiwa na wasiwasi. Nikijikaza kiume kwa nguvu zangu zote na ujasiri wangu wote niweze kutembea sawasawa bila kuchechemea.
"…good morning Sir.!"
"…morning. How can I help you?"
Niliwasalimia lakini hawakunijibu haraka walibakia kunitumbulia macho tu kisha wakaangaliana. Walikuwa mwanaume mmoja na mwingine alikuwa ni mwanadada. Wote wawili walikuwa wamevalia suti. Nilielewa wazi kabisa walikuwa ni askari wapelelezi
"Do you live here?" Yule mwanadada aliniuliza huku bado amenitumbulia macho.
"No, why? Is there a problem?" Nikamuuliza.
"I am detective Corol Lawrence and this detective Noah Johnson. We would like to ask you a few questions… can we come in?" Yule dada aliongea huku ananionyesha kitambulisho chake cha upolisi.
"Yes, ofcourse!"
Niliwakaribisha ndani na haraka nikaenda kuketi kwenye sofa. Sikutaka kujibaraguza kwa kufanya ukarimu wa kuwapa kahawa au kinywaji kama ilivyo desturi ya wazungu. Niliketi haraka ili maumivu tumboni yasinizidie na wakagundua kuwa nina kidonda tumboni yakaanza maswali ya jeraha hilo kimelipataje.
"How do you know Luke Madison?" Yule mwanaume aliniuliza swali.
"Ahn! We are friends!" Nilitoa jibu la haraka haraka.
"Friends like how? You guys live together or….!"
"Im am sorry detective, you are asking me all these questions but i dont why? What is happening? Why am i being interrogated?" Nikawauliza nikiwa na uso serious. Tayari nilijua kuwa kuna kitu kilikuwa hakiko sawa kwa hiyo kabla sijasema maneno mengine yoyote ambayo yangeweza kunitia matatani.
"Well, its not an interrogation. Just some routine questions!" Yule dada aliongea huku analazimisha tabasamu.
"There is nothing 'routine' about this. You guys have come here for a reasons! I want to know why before I answer any more questiins!"
Niliwaona wanaangaliana na kupeana ishara fulani hivi. Kisha yule mpelelezi mwanamke akaongea.
"Luke is dead!"
Nilihisi kama sijasikia vizuri au labda sikumuelewa.
"What? What did you just say?" Niliongea kwa mshituko mkubwa usoni.
"Luke is dead?"
Mpelelezi mwanamke, Carol alinijibu tena. Nilitamani kama vile wawe wananitania tu. Inawezekana vipi? Luke ameondoka hapa kama nusu saa tu iliyopita.
"How? What happened?" Niliuliza nikiwa bado kwenye mshituko.
"He was shot few minutes ago!" Akanijibu tena huku amenikazia macho nahisi akitaka kuona mwitikio wangu usoni.
Nilijiinamia uso viganjani kwa sekunde kadhaa. Wao walidhani labda nilikuwa nasikitika kwa taarifa hii ya msiba, lakini kichwani mwangu kulikuwa na kitu kingine kabisa kinapita. Nilikuwa nawaza kama kuna uwezekano wa aliyenipiga risasi juzi usiku, Erica… kuwa ndiye huyo huyo ambaye alikuwa amempiga risasi Luke. Kuna upande fulani wa akili yangu ulikuwa unataka niwaambie maaskari hawa kuhusu tukio ambalo lilinitokea, lakini moyo wangu ulikuwa unasita kabisa kuwapa taarifa hii.
"Where did this happen?" Nikawauliza kwa sauti ya unyonge.
"Freacht West Street…!"
Wakanitajia mtaa ule ule ambao kuna hotel ya Radisson Blu ambayo nilifikia nilipoingia hapa Zurich. Luke pia alipoondoka hapa tulikubaliana aende hotelini pale ili kupata taarifa juu ya yule binti muhudumu Erica ambaye alinipiga risasi.
"Sir, if there is any information that can help us we will be happy to hear it!"
Kichwani nikajiuliza ni kitu gani hasa niwaambie? Niwaeleze ukweli? Je, sitaingia matatizoni kwa kuwaeleza ukweli na lengo langu la kuja hapa Zurich kuvurugika? Hapana siwezi kuwaambia ukweli…
Ilibidi nitunge uongo usio na kichwa wala miguu lakini wenye kuweza kuaminika.
Kwanza niliwadanganya jina langu3… niliwaelezankuwa naitwa "Jimmy Adekela", asili yangu ni Nigeria lakini naishi hapa Zurich kwa mwaka wa pili sasa. Kwa hiyo sikuwaeleza ukweli kwamba mimi ni Mtanzania ambaye nimeingia hapa Zurich siku chache tu zilizopita.
Nilijua kwa ujio wao huu wa haraka haraka hawawezi kunibana sana kwa maswali labda waseme wananikamata na kunipeleka kituoni, lakinj uzuri hawakuwa na sababu ya kunikamata. Japokuwa kama nikiwaeleza uongo na baadae wakigundua kuwa nimewadanganya lazima wanisake ili kunikamata na kunihoji ili kufahamu najua nini kuhusiana na kifo hicho cha Luke.
Nilikata shauri kichwani mwangu niwadanganye, siwezi kuwaeleza ukweli… nikawaeleza kwamba Luke ni rafiki yangu wa muda mrefu tu na mimi nilikuwa nimekuja hapa kumtembelea jana usiku na ndio maana ilinibidi kulala hapa. Asubuhi ya leo aliniaga kwamba anatoka kwa muda mfupi tu na atarudi baada ya dakika chache lakini badala yake ni wao wamekuja kunipa taarifa kwamba amepigwa risasi.
"…can you think of anyone who might want to kill him? Anyone… an enemy or someone who may be had a fight with a few days ago… anyone?"
Yule mpelelezi wa kiume, Noah aliniuliza.
"No.! I dont think if there is anyone who would want to kill Luke… he was a very good guy!" Nikadanganya tena.
"Ok sir, we would like to talk to you again later, but thats it for now… thank you sir!"
"No problem.!"
"If you remember anything, please give us a call… this is my number..!"
"Thank you!"
Walinipatia 'business card' nikaipokea na kuiweka mfukoni. Wakafungua mlango na kuondoka.
Nilivuta pumzi ndefu ndani na kuishusha. Sikuamini kama hatimaye wameondoka. Lakini huu haukuwa mwisho… hawa wanaonekana ni wapelelezi wazoefu, lazima watakuwa wamegundua kwamba kuna jambo nilikuwa naficha. Wameamua kuondoka kana kwamba hawanitilii mashala ili 'nirelax'. Hawataki niingiwe na wasiwasi kisha nikakimbia. Lazima wanaenda kuhakiki taarifa nilizowapa kabla hawajaja kunikamata rasmi wakigundua uongo niliowaeleza. Huu ulikuwa ni muda wa kufanya maamuzi ya haraka kabla sijachelewa.
Nikafunua shati nililovaa kutazama kidonda changu ambacho kimefungwa bandeji. Kilikuwa kiko sawia.
Nikaelekea mpaka karibu na kitanda ambako kulikuwa na mabegi yangu. Nikaanza kuyaburuza na kuondoka.
Sikutaka kupitia mlango rasmi wa mbele ya jengo au kutumia lifti. Nikihofia ningeweza kukutana na askari wale ambao wameondoka muda huu. Au labda wameacha mtu nje kunichunguza nyendo zangu.
Nikaburuza begi langu na kushuka ngazi taratibu kuelekea mlango wa nyuma wa dharura. Kutokana na kuhofia kutonesha kidonda tumboni ilinibidi kutembea taratibu sana na kwa tahadhari. Ilinichukua karibia dakika kumi nzima mpaka kutokea kwenye mlango wa nyuma wa dharura. Nikasogea mpaka barabarani na kuita Taxi.
"Freacht West Street… Radisson Blu Hotel!" Nilimuelekeza dereva taxi kisha aling'oa gari na kuondoka.
Katika ambao nilitakiwa kuwa makini kupitiliza basi ulikuwa ni huu. Nilikuwa kwenye nchi ya kigeni na tayari kulikuwa na kila dalili ya kuingia kwenye matatizo makubwa na vyombo vya usalama. Hiki kilikuwa ni kitu cha mwisho ambacho nilikuwa sitaki kitokee. Tayari nina adui asiyejulikana ambaye alikuwa ananiwinda. Sihitaji tena kuingia kwenye uadui na vyombo vya usalama.
Pia kila nilipokuwa nafikiria hii taarifa juu ya Luke kupigwa risasi nilikuwa siishi kujiuliza kama ni yule mwanadada Erica ndiye anayehusika. Nilijikuta tu natamani kufika pale hotelini ili kujionea walau kwa macho yangu ni nini hasa ambacho kilikuwa kinaendelea.
Kama dakika saba baadae tulikuwa tumeingia mtaa wa Freacht West. Nilimuelekeza dereva apaki gari upande wa pili wa barabara mkabala na Radisson Blu Hotel. Nilikuwa nataka kuona kile ambacho kilikuwa kinaendelea pale hotelini lakini sikutaka kufika kuhofia kutambulika na pengine kuingia kwenye matatizo zaidi. Hapa tulipopaki upande wa pili wa barabara nilikuwa naweza kuona vyema kabisa kile ambacho kilikuwa kinaendelea.
Nje ya hoteli pembeni karibu na mlangoni, kulikuwa kumefungwa utepe wa njano wa polisi kuashiria kwamba hiyo ndiyo 'crime scene'. Ndipo mahala ambapo Luke alipigwa risasi.
Kulikuwa na kama polisi watano hivi wenye sare ambao walikuwa eneo hili. Pia kulikuwa na watu wawili ambao walionekana ni watu wa 'forensic' mmoja akiwa anapiga picha lile eneo sakafuni na mwingine akiwa kama anapima vitu fulani hivi pale chini.
Pembeni nje ya ule utepe kulikuwa na raia kadhaa wasiozidi kumi na tano wamesimama wakishangaa. Nilimuona moja ya askari akiwa anachukua maelezo ya meneja wa Hoteli, yule jamaa ambaye juzi alinikuta mapokezi nabishana na Erica na kunitaka niondoke.
Nikapepesa macho yangu kutazama watu walioko pale wakishangaa. Moyo wangu ulipasuka ghafla nilipomuona moja ya watu ambao walikuwa eneo hili. Katika lile kundi la raia ambao walikuwa wamesimama wakishangaa alikuwepo yule jamaa anayevaa kofia ya 'pama'. Yule jamaa mweusi ambaye juzi hapa hotelini alikuwa ameketi kwenye moja ya sofa za pale mapokezi anasoma gazeti. Jamaa ambaye Erica alikuwa anaongea na mimi huku anamwangalia kwa kuibia ibia kana kwamba anamuhofia hivi. Ni yule jamaa alikuwepo tena mahala hapa kwenye kundi la raia wanaoshangaa.
Tangu juzi sikuweza kumuona sura yake kutokana na kofia lake la pama. Na hata leo hii muda huu pia sikuweza kuona sura yake. Lakini nilikuwa na hakika kwa asilimia mia moja kwamba alikuwa ni yeye. Kofia yake ile ile ya pama kubwa kiasi ya rangi ya kijivu. Koti lake jeusi refu lenye kufika mpaka usawa wa magoti na kuvuka chini kidogo. Mkononi ameshikilia gazeti. Hakika sikuwa nakosea. Alikuwa ni yeye. Alikuwa anatazama kinachoendelea pale kama vile watazamaji wengine.
"Ni nani huyu mtu?" Nilijiuliza mwenyewe kichwani.
Nikiwa najiuliza hivu maswali kichwani… ghafla! yule jamaa akageuka na kutazima upande wetu, hapa taxi ilikopaki. Ubaya ni kwamba nilikuwa nimeshusha dirisha chini kidogo ili niweze kuona kwa usawia. Nilijikuta macho yangu na yake yanagongana. Kijasho kilianza kunitoka huku nahema kwa nguvu. Tulikaziana macho kwa takribani sekunde thelathini nzima. Sasa ndio nilipata wasaa wa kumuona vyema. Upande wa kushoto usoni alikuwa na kovu kubwa kana kwamba aliwahi kupata jeraha kubwa la kukatwa na kitu.
"Namjua huyu jamaa.!!"
Ndilo wazo la kwanza ambalo lilikatisha akilini mwangu. Nilikuwa na hakika kwa asilimia mia moja kwamba huyu mtu namfahamu. Nimeshawahi kumuona hapo kabla siku za nyuma kabla ya hapa hotelini. Kovu lake hili ndilo haswa lilinipa uhakika kwamba namfahamu huyu mtu. Lakini sikuweza kukumbuka ni wapi. Akili ilikiwa inashindwa kutambua ni wapi haswa niliwahi kumuona. Lakini kwa hakika kabisa kumbukumbu yangu iliniambia huyu mtu namfahamu.
Nilimkazia macho. Sikupepesa hata kidogo japo nilikuwa nimekumbwa na woga wa ghafla moyoni mpaka jasho linanitoka.
Taratibu nikamuona anageuka na kuendelea kushangaa kule kwenye eneo la tukio.
Nikamuamuru dereva tuondoke.
"Hardstrasse.!" Nikamuelekeza kwa kuelekea.
Ndio. Hardstrasse. Ndio mahala pekee ambako kwa sasa nilihisi palikuwa sahihi kwangu kwenda. Siwezi kukaaa tena hotelini. Itakuwaje kama Polisi wakinishuku kuwa nimehusika na mauaji ya Luke na picha yangu kusambazwa? Nimewadanganya kila taarifa ambayo nimewapa. Wakigundua uongo huo wana kila sababu ya kunishuku kuhusika na mauaji hayo. Kwa hiyo nahitaji kukaa mbali na maeneo ya umma.
Lakini huku Hardstrasse ambako tunaelekea kwenye lile jumba ndipo ambako nimepigwa risasi juzi na kuokotwa na kina Luke. Lakini uziri wake polisi walikuwa hawaifahamu hii sehemu. Kwa hiyo hata wanitafute vipi hawaezi kujua ni wapi watanipata.
"This time I fight back.!'
Nilijipa moyo. Kwamba ikitokea nikishambuliwa tena safari hii nitapambana.
Huu si muda wa kujiuliza maswali tena. Nimejiuliza maswali ambayo kila muda yaninipa maswali na vitendawili vingine. Huu ni muda wa kutafuta majibu.
Sihitaji tena kujificha mbali na adui ambaye ananiwinda. Huu ni muda wa kupambana. Kupambana mpaka nipate jawabu la kile kilichonileta hapa Zurich.
Nilikuwa nahema kwa nguvu kana kwamba nimepandwa na maruhani. Maruhani ya ushari na kupambana. Nilijikuta hofu yote imeniondoka. Kitu pekee ambacho kilikuwa kimeujza moyo wangu sasa hivi ilikuwa ni hasira.
"I need a gun!" Niliwaza moyoni huku bado nahema kwa nguvu.
Nilidhamiria kupambana sasa. Nilidhamiria kupata majibu.
Itaendelea….
Habibu B. Anga 'The Bold'
To Infinity and BeyondView attachment 776942
Mkuu asante kwa madini mazuri haya usisahau na other half umepotea sana kuleVIPEPEO WEUSI
SEASON 2 - FROM ZURICH WITH RULES
EPISODE 21
Nilisikia wale watu ambao walikuwa wamejitambulisha kama polisi wakigonga tena.
Wasiwasi wangu wa kwanza ulikuwa ni kidonda tumboni kwangu, nilikuwa nawaza hawa polisi wakiniuliza kidonda hicho ni cha nini nitajibu vipi? Lakini pia wasiwasi wangu wa pili ulikuwa ni kitu gani hasa polisi hao kimewaleta haswa mahala hapa.
Sikutaka wagonge sana mlango kwani wangeweza kuingiwa na wasiwasi. Nikijikaza kiume kwa nguvu zangu zote na ujasiri wangu wote niweze kutembea sawasawa bila kuchechemea.
"…good morning Sir.!"
"…morning. How can I help you?"
Niliwasalimia lakini hawakunijibu haraka walibakia kunitumbulia macho tu kisha wakaangaliana. Walikuwa mwanaume mmoja na mwingine alikuwa ni mwanadada. Wote wawili walikuwa wamevalia suti. Nilielewa wazi kabisa walikuwa ni askari wapelelezi
"Do you live here?" Yule mwanadada aliniuliza huku bado amenitumbulia macho.
"No, why? Is there a problem?" Nikamuuliza.
"I am detective Corol Lawrence and this detective Noah Johnson. We would like to ask you a few questions… can we come in?" Yule dada aliongea huku ananionyesha kitambulisho chake cha upolisi.
"Yes, ofcourse!"
Niliwakaribisha ndani na haraka nikaenda kuketi kwenye sofa. Sikutaka kujibaraguza kwa kufanya ukarimu wa kuwapa kahawa au kinywaji kama ilivyo desturi ya wazungu. Niliketi haraka ili maumivu tumboni yasinizidie na wakagundua kuwa nina kidonda tumboni yakaanza maswali ya jeraha hilo kimelipataje.
"How do you know Luke Madison?" Yule mwanaume aliniuliza swali.
"Ahn! We are friends!" Nilitoa jibu la haraka haraka.
"Friends like how? You guys live together or….!"
"Im am sorry detective, you are asking me all these questions but i dont why? What is happening? Why am i being interrogated?" Nikawauliza nikiwa na uso serious. Tayari nilijua kuwa kuna kitu kilikuwa hakiko sawa kwa hiyo kabla sijasema maneno mengine yoyote ambayo yangeweza kunitia matatani.
"Well, its not an interrogation. Just some routine questions!" Yule dada aliongea huku analazimisha tabasamu.
"There is nothing 'routine' about this. You guys have come here for a reasons! I want to know why before I answer any more questiins!"
Niliwaona wanaangaliana na kupeana ishara fulani hivi. Kisha yule mpelelezi mwanamke akaongea.
"Luke is dead!"
Nilihisi kama sijasikia vizuri au labda sikumuelewa.
"What? What did you just say?" Niliongea kwa mshituko mkubwa usoni.
"Luke is dead?"
Mpelelezi mwanamke, Carol alinijibu tena. Nilitamani kama vile wawe wananitania tu. Inawezekana vipi? Luke ameondoka hapa kama nusu saa tu iliyopita.
"How? What happened?" Niliuliza nikiwa bado kwenye mshituko.
"He was shot few minutes ago!" Akanijibu tena huku amenikazia macho nahisi akitaka kuona mwitikio wangu usoni.
Nilijiinamia uso viganjani kwa sekunde kadhaa. Wao walidhani labda nilikuwa nasikitika kwa taarifa hii ya msiba, lakini kichwani mwangu kulikuwa na kitu kingine kabisa kinapita. Nilikuwa nawaza kama kuna uwezekano wa aliyenipiga risasi juzi usiku, Erica… kuwa ndiye huyo huyo ambaye alikuwa amempiga risasi Luke. Kuna upande fulani wa akili yangu ulikuwa unataka niwaambie maaskari hawa kuhusu tukio ambalo lilinitokea, lakini moyo wangu ulikuwa unasita kabisa kuwapa taarifa hii.
"Where did this happen?" Nikawauliza kwa sauti ya unyonge.
"Freacht West Street…!"
Wakanitajia mtaa ule ule ambao kuna hotel ya Radisson Blu ambayo nilifikia nilipoingia hapa Zurich. Luke pia alipoondoka hapa tulikubaliana aende hotelini pale ili kupata taarifa juu ya yule binti muhudumu Erica ambaye alinipiga risasi.
"Sir, if there is any information that can help us we will be happy to hear it!"
Kichwani nikajiuliza ni kitu gani hasa niwaambie? Niwaeleze ukweli? Je, sitaingia matatizoni kwa kuwaeleza ukweli na lengo langu la kuja hapa Zurich kuvurugika? Hapana siwezi kuwaambia ukweli…
Ilibidi nitunge uongo usio na kichwa wala miguu lakini wenye kuweza kuaminika.
Kwanza niliwadanganya jina langu3… niliwaelezankuwa naitwa "Jimmy Adekela", asili yangu ni Nigeria lakini naishi hapa Zurich kwa mwaka wa pili sasa. Kwa hiyo sikuwaeleza ukweli kwamba mimi ni Mtanzania ambaye nimeingia hapa Zurich siku chache tu zilizopita.
Nilijua kwa ujio wao huu wa haraka haraka hawawezi kunibana sana kwa maswali labda waseme wananikamata na kunipeleka kituoni, lakinj uzuri hawakuwa na sababu ya kunikamata. Japokuwa kama nikiwaeleza uongo na baadae wakigundua kuwa nimewadanganya lazima wanisake ili kunikamata na kunihoji ili kufahamu najua nini kuhusiana na kifo hicho cha Luke.
Nilikata shauri kichwani mwangu niwadanganye, siwezi kuwaeleza ukweli… nikawaeleza kwamba Luke ni rafiki yangu wa muda mrefu tu na mimi nilikuwa nimekuja hapa kumtembelea jana usiku na ndio maana ilinibidi kulala hapa. Asubuhi ya leo aliniaga kwamba anatoka kwa muda mfupi tu na atarudi baada ya dakika chache lakini badala yake ni wao wamekuja kunipa taarifa kwamba amepigwa risasi.
"…can you think of anyone who might want to kill him? Anyone… an enemy or someone who may be had a fight with a few days ago… anyone?"
Yule mpelelezi wa kiume, Noah aliniuliza.
"No.! I dont think if there is anyone who would want to kill Luke… he was a very good guy!" Nikadanganya tena.
"Ok sir, we would like to talk to you again later, but thats it for now… thank you sir!"
"No problem.!"
"If you remember anything, please give us a call… this is my number..!"
"Thank you!"
Walinipatia 'business card' nikaipokea na kuiweka mfukoni. Wakafungua mlango na kuondoka.
Nilivuta pumzi ndefu ndani na kuishusha. Sikuamini kama hatimaye wameondoka. Lakini huu haukuwa mwisho… hawa wanaonekana ni wapelelezi wazoefu, lazima watakuwa wamegundua kwamba kuna jambo nilikuwa naficha. Wameamua kuondoka kana kwamba hawanitilii mashala ili 'nirelax'. Hawataki niingiwe na wasiwasi kisha nikakimbia. Lazima wanaenda kuhakiki taarifa nilizowapa kabla hawajaja kunikamata rasmi wakigundua uongo niliowaeleza. Huu ulikuwa ni muda wa kufanya maamuzi ya haraka kabla sijachelewa.
Nikafunua shati nililovaa kutazama kidonda changu ambacho kimefungwa bandeji. Kilikuwa kiko sawia.
Nikaelekea mpaka karibu na kitanda ambako kulikuwa na mabegi yangu. Nikaanza kuyaburuza na kuondoka.
Sikutaka kupitia mlango rasmi wa mbele ya jengo au kutumia lifti. Nikihofia ningeweza kukutana na askari wale ambao wameondoka muda huu. Au labda wameacha mtu nje kunichunguza nyendo zangu.
Nikaburuza begi langu na kushuka ngazi taratibu kuelekea mlango wa nyuma wa dharura. Kutokana na kuhofia kutonesha kidonda tumboni ilinibidi kutembea taratibu sana na kwa tahadhari. Ilinichukua karibia dakika kumi nzima mpaka kutokea kwenye mlango wa nyuma wa dharura. Nikasogea mpaka barabarani na kuita Taxi.
"Freacht West Street… Radisson Blu Hotel!" Nilimuelekeza dereva taxi kisha aling'oa gari na kuondoka.
Katika ambao nilitakiwa kuwa makini kupitiliza basi ulikuwa ni huu. Nilikuwa kwenye nchi ya kigeni na tayari kulikuwa na kila dalili ya kuingia kwenye matatizo makubwa na vyombo vya usalama. Hiki kilikuwa ni kitu cha mwisho ambacho nilikuwa sitaki kitokee. Tayari nina adui asiyejulikana ambaye alikuwa ananiwinda. Sihitaji tena kuingia kwenye uadui na vyombo vya usalama.
Pia kila nilipokuwa nafikiria hii taarifa juu ya Luke kupigwa risasi nilikuwa siishi kujiuliza kama ni yule mwanadada Erica ndiye anayehusika. Nilijikuta tu natamani kufika pale hotelini ili kujionea walau kwa macho yangu ni nini hasa ambacho kilikuwa kinaendelea.
Kama dakika saba baadae tulikuwa tumeingia mtaa wa Freacht West. Nilimuelekeza dereva apaki gari upande wa pili wa barabara mkabala na Radisson Blu Hotel. Nilikuwa nataka kuona kile ambacho kilikuwa kinaendelea pale hotelini lakini sikutaka kufika kuhofia kutambulika na pengine kuingia kwenye matatizo zaidi. Hapa tulipopaki upande wa pili wa barabara nilikuwa naweza kuona vyema kabisa kile ambacho kilikuwa kinaendelea.
Nje ya hoteli pembeni karibu na mlangoni, kulikuwa kumefungwa utepe wa njano wa polisi kuashiria kwamba hiyo ndiyo 'crime scene'. Ndipo mahala ambapo Luke alipigwa risasi.
Kulikuwa na kama polisi watano hivi wenye sare ambao walikuwa eneo hili. Pia kulikuwa na watu wawili ambao walionekana ni watu wa 'forensic' mmoja akiwa anapiga picha lile eneo sakafuni na mwingine akiwa kama anapima vitu fulani hivi pale chini.
Pembeni nje ya ule utepe kulikuwa na raia kadhaa wasiozidi kumi na tano wamesimama wakishangaa. Nilimuona moja ya askari akiwa anachukua maelezo ya meneja wa Hoteli, yule jamaa ambaye juzi alinikuta mapokezi nabishana na Erica na kunitaka niondoke.
Nikapepesa macho yangu kutazama watu walioko pale wakishangaa. Moyo wangu ulipasuka ghafla nilipomuona moja ya watu ambao walikuwa eneo hili. Katika lile kundi la raia ambao walikuwa wamesimama wakishangaa alikuwepo yule jamaa anayevaa kofia ya 'pama'. Yule jamaa mweusi ambaye juzi hapa hotelini alikuwa ameketi kwenye moja ya sofa za pale mapokezi anasoma gazeti. Jamaa ambaye Erica alikuwa anaongea na mimi huku anamwangalia kwa kuibia ibia kana kwamba anamuhofia hivi. Ni yule jamaa alikuwepo tena mahala hapa kwenye kundi la raia wanaoshangaa.
Tangu juzi sikuweza kumuona sura yake kutokana na kofia lake la pama. Na hata leo hii muda huu pia sikuweza kuona sura yake. Lakini nilikuwa na hakika kwa asilimia mia moja kwamba alikuwa ni yeye. Kofia yake ile ile ya pama kubwa kiasi ya rangi ya kijivu. Koti lake jeusi refu lenye kufika mpaka usawa wa magoti na kuvuka chini kidogo. Mkononi ameshikilia gazeti. Hakika sikuwa nakosea. Alikuwa ni yeye. Alikuwa anatazama kinachoendelea pale kama vile watazamaji wengine.
"Ni nani huyu mtu?" Nilijiuliza mwenyewe kichwani.
Nikiwa najiuliza hivu maswali kichwani… ghafla! yule jamaa akageuka na kutazima upande wetu, hapa taxi ilikopaki. Ubaya ni kwamba nilikuwa nimeshusha dirisha chini kidogo ili niweze kuona kwa usawia. Nilijikuta macho yangu na yake yanagongana. Kijasho kilianza kunitoka huku nahema kwa nguvu. Tulikaziana macho kwa takribani sekunde thelathini nzima. Sasa ndio nilipata wasaa wa kumuona vyema. Upande wa kushoto usoni alikuwa na kovu kubwa kana kwamba aliwahi kupata jeraha kubwa la kukatwa na kitu.
"Namjua huyu jamaa.!!"
Ndilo wazo la kwanza ambalo lilikatisha akilini mwangu. Nilikuwa na hakika kwa asilimia mia moja kwamba huyu mtu namfahamu. Nimeshawahi kumuona hapo kabla siku za nyuma kabla ya hapa hotelini. Kovu lake hili ndilo haswa lilinipa uhakika kwamba namfahamu huyu mtu. Lakini sikuweza kukumbuka ni wapi. Akili ilikiwa inashindwa kutambua ni wapi haswa niliwahi kumuona. Lakini kwa hakika kabisa kumbukumbu yangu iliniambia huyu mtu namfahamu.
Nilimkazia macho. Sikupepesa hata kidogo japo nilikuwa nimekumbwa na woga wa ghafla moyoni mpaka jasho linanitoka.
Taratibu nikamuona anageuka na kuendelea kushangaa kule kwenye eneo la tukio.
Nikamuamuru dereva tuondoke.
"Hardstrasse.!" Nikamuelekeza kwa kuelekea.
Ndio. Hardstrasse. Ndio mahala pekee ambako kwa sasa nilihisi palikuwa sahihi kwangu kwenda. Siwezi kukaaa tena hotelini. Itakuwaje kama Polisi wakinishuku kuwa nimehusika na mauaji ya Luke na picha yangu kusambazwa? Nimewadanganya kila taarifa ambayo nimewapa. Wakigundua uongo huo wana kila sababu ya kunishuku kuhusika na mauaji hayo. Kwa hiyo nahitaji kukaa mbali na maeneo ya umma.
Lakini huku Hardstrasse ambako tunaelekea kwenye lile jumba ndipo ambako nimepigwa risasi juzi na kuokotwa na kina Luke. Lakini uziri wake polisi walikuwa hawaifahamu hii sehemu. Kwa hiyo hata wanitafute vipi hawaezi kujua ni wapi watanipata.
"This time I fight back.!'
Nilijipa moyo. Kwamba ikitokea nikishambuliwa tena safari hii nitapambana.
Huu si muda wa kujiuliza maswali tena. Nimejiuliza maswali ambayo kila muda yaninipa maswali na vitendawili vingine. Huu ni muda wa kutafuta majibu.
Sihitaji tena kujificha mbali na adui ambaye ananiwinda. Huu ni muda wa kupambana. Kupambana mpaka nipate jawabu la kile kilichonileta hapa Zurich.
Nilikuwa nahema kwa nguvu kana kwamba nimepandwa na maruhani. Maruhani ya ushari na kupambana. Nilijikuta hofu yote imeniondoka. Kitu pekee ambacho kilikuwa kimeujza moyo wangu sasa hivi ilikuwa ni hasira.
"I need a gun!" Niliwaza moyoni huku bado nahema kwa nguvu.
Nilidhamiria kupambana sasa. Nilidhamiria kupata majibu.
Itaendelea….
Habibu B. Anga 'The Bold'
To Infinity and BeyondView attachment 776942
Shukrani chiefSio shabiki maandazi ila Dogo (fundi) unaweza...
Naweka TOH muda si mrefu leo hiiMkuu asante kwa madini mazuri haya usisahau na other half umepotea sana kule
Ni kweli mkuu, nitajitajidi kuweka episode mfululizo.Mkuu usipotee mazima bhana uwe unatupia hata kwa wiki mara 2.salaam kwa nipha naona kazira kabisaaa
Dah! So sorry, now najitahidi iwe jiwe kuu ya jiweThe Bold jamani mpaka tumesahau shukrani sana
Sawa kaka tupo tunasubiriaDah! So sorry, now najitahidi iwe jiwe kuu ya jiwe
Mkuu hii ahadi umeshaisahau au saumu?Dah! So sorry, now najitahidi iwe jiwe kuu ya jiwe
Kumbe Shunie ni bingwa wa kuzoea arostos🙁🙂😉The Bold jamani mpaka tumesahau shukrani sana
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23] Nimeshajizoelea mie na arosto zanguKumbe Shunie ni bingwa wa kuzoea arostos🙁🙂😉