VIPEPEO WEUSI: MKAKATI NAMBA 0034
EPISODE 16
Wote wawili, Issack na Cheupe wakabaki wamenikodolea macho kwa mshangao.
"Una maana gani kuwa umeshajua Veronica feki ni nani!" Issack akaniuliza kwa mshangao.
"Mnakumbuka nilivyo waambia nilipochukuliwa na Maafisa wa Usalama wa Taifa na kunipeleka maeneo ya Mbezi walikuwa maafisa wanne na mmoja ni mwanamke??" Nikawauliza.
"Yeah nakumbuka" wote wakaitikia kwa pamoja.
"Sasa yule mwanamke alikuwa ni Mnyaruanda. Hata kiswahili hajui kukiongea ingawa anakielewa, na nikawa najiuliza sana kwanini Maafisa Usalama wa Tanzania washirikiane na Mnyaruanda na Rwanda wana maslahi gani mpaka watume mtu huku?? Sasa kidogo nimeanza kuelewa!"
"Well, na umeelewa nini" Issack akauliza.
Nikasogea karibu na nyavu na kuongea kama nawanong'oneza.
"Nina hakika kuwa kuna kitu nchi ya Rwanda inachunguza kwenye mtandao wa The Board. Kwahiyo ninachokihisi ni kwamba Veronica ni mwanausalama wa nchi ya Rwanda na akatatumia mbinu kuanzisha uhusiano na Eric Kaburu ili aweze kupepeleza na kupata hiyo taarifa wanayohitaji. Ndio maana Rwanda mpaka leo hii wako interested na hii ishu ya The Board"
"Wow! Ina make sense kabisa. Nadhani ndio sababu kwanini Kaburu akamuua, itakuwa alikuja kubaini Veronica ni Afisa Usalama" Issack aongezea.
"No sidhani kama alimuua." Nikamjibu.
"Kwanini unasema hivyo" akauliza kwa mshangao.
"Nimekaa hii karibia siku ya sita gereza moja na Kaburu, nimeongea nae ana kwa ana na kumsoma ni mtu wa aina gani. Trust me, Kaburu sio dizaini ya mtu mwenye uwezo wa kuua! So nina uhakika kabisa hakumuua Veronica." Nikamfafanulia.
"But Kaburu mwenyewe alikiri kuwa amemuua!"
"Whaaaat??" Nikajikuta nauliza kwa mshangao.
"Yes kipindi kesi inasikilizwa mwanzoni kabisa mwa kesi, Kaburu akakiri kutenda hilo tukio! Ndio sababu kwanini kesi iliisha haraka haraka"
Nikashikwa na butwaa. Nikahisi hapa kuna jambo zito limejificha. Inawezekanaje mtu akiri kuua alafu ahukumiwe adhabu ya kuua bila kukusudia na apewe miaka saba pekee jela. Nikawa na uhakika kabisa kuna jambo limejificha hapa.
"Veronica alikuafaje?" Nikamuuliza Issack, licha ya kesi hii kuandikwa sana lakini nilikuwa nimesahau matukio mengi kuhusu kesi hii.
"Walikuwa Nyumbani kwa Kaburu, wakaanza kugombana na baadae Kaburu akaanza kumpiga! Inaelezwa kuwa akampiga mpaka akapoteza fahamu kisha akamchoma moto.. Na kwa mujibu ya magazeti yalivyoandika kipindi kile... Wanaeleza kuwa kisa ni wivu wa mapenzi" Issack akanifafanulia.
Taa ikazidi kuwaka kichwani mwangu. Nikahisi naanza sasa kuungajisha dots na kupata picha kamili.
"Wow! Ok ok, wow" nikajikuta naongea huku natikisa kichwa baada ya dots kuanza kuungana.
"What is it!" Cheupe akauliza kwa shauku.
"They fell in love" nikamjibu huku nawaangalia kwa tabasamu kwa furaha.
"Who fell in love?" Cheupe akauliza tena.
"Kaburu na Veronica! They fell in love!" Nikawajibu huku bado natabasamu.
"How? Kaburu amekiri kuwa alimuua?" Issack akauliza kwa mshangao.
"No hakumuua! Hicho ndicho Kaburu anachotaka watu wa amini.. Na amefanikiwa kuwaaminisha watu.. But the truth is hakumuua.. They fell in love"
Nikaongea huku natabasamu lakini niko serious.
"Oyaaaaa! Muda wenu ushaisha.. Tokeni huko" nikasikia sauti ya askari inaitilia nje ya chumba.
"Leo nitaongea na Kaburu na najua nimbane vipi ili aongee na mimi kwa hizi taarifa mlizonipa.. Nahitaji kesho mje tena hapa kuna maagizo tupene tena nina hakika nikiongea naye lazima nitapata kitu amabcho nitahitaji mkakifanyoe kazi huko nje"
Nikaongea huku tunainuka kwenye viti kwenye kile chumba cha kuongea na wageni.
* * * * * *
Nilikuwa nimeketi mbele ya Kaburu kwenye upande wa gereza ambao kuna kisehemu cha wagonjwa kupumzika.
Kaburu alikuwa amekaa hapa ametandikiwa godoro amepumzika baada ya kutoka zahanati ya magereza kutokana na kipigo kizito cha virungu juzi.
"I'm impressed! Sikudhani kama unaweza kufanya kama kitu ulichokifanya juzi" aliongea akikumbushia tukio la juzi. Ni dhahiri alikuwa amegundua kuwa mimi ndiye niliyeufanya ule mchezo wote.
"Na hapo haujaona hata nusu ya kile ninachoweza kukifanya my friend" nikamjibu seriously nikimkazia macho.
"Ni nini unachoweza kukifanya?" Akaniuliza kwa dharau.
"Nina uwezo wa kukufanya uongee na mimi na unambie ninachokitaka kwa hiari yako au kwa kukulazimisha ufanye hivyo" nikajibu kwa kiburi.
"Hahahahaha!! Wooow, i'm really scared!" Akaongea huku anacheka kwa dhihaka.
"Unajua kipindi nasoma advance Sekondari ya Tambaza!! Kulikuwa na jamaa mmoja hivi ambaye alikuwa na tabia za kishenzi sana.. Kutukana watu, kupigana, uonevu wa kijinga jinga.. Sasa kuna siku akajichanganya akanitukana mbele ya darasa zima!! Unajua nilianyaje" nikamuuliza huku nimemkazia macho.
"Ulifanyaje" akaniuliza.
"Nikamfuata faragha akiwa peke yake, nikamwambia nampa siku tatu aniombe msamaha mbele ya darasa zima na asipofanya hivyo atajuta kwa kitakachomkuta"
"Alikuomba msamaha?"
"Hapana! Alinitukana tena hapo hapo.. Lakini unajua nini kilifuata?" Nikamuuliza.
"Ukampiga ngumi?"
"No! Wiki moja baadae akafukuzwa shule kwa kosa la kusambaza picha za uchi za demu wake" nikamueleza huku nimemkazia macho na kumsogelea.
"Wow! Kumbe hii michezo ya kuwafanya watu waonekane wamefanya vitu ambavyo hawajavifanya umeianza zamani sana kijana" akaongea huku anang'ata midomo kwa hasira.
"Ninachojaribu kukwambia ni kwamba, I always get what i want.. Nikitaka kitu kitokee akili yangu itapata namna ya kufanya ili nipate hicho kitu"
"And unahitaji nini kutoka kwangu?" Akaniuliza huku amenikazia macho.
"Nahitaji unieleze kila unachokijua kuhusi The Board" nikamjibu huku pia nimemkazia macho.
"Hahahahaha! Unaota kijana.. Kirahisi tu hivyo?? Hahahaha, endelea kuota" akajibu huku anacheka kwa dharau.
"Well, sio kirahisi rahisi tu... Itabidi unieleze ninachohitaji ili nikae kimya nisiwaeleze watu wa Usalama kwamba Veronica bado yuko hai" nikaongea kwa kusogelea karibu kabisa nikitoa sauti kama nanong'ona.
Nikauona mshtuko wake kwenye macho yake. Nilikuwa nimegusa 'ikulu'.
"Umeanza kuchanganyikiwa Dogo" akanijibu kwa sauti ya woga huku anajigeuza kwenye gorodo na kuangalia pembeni.
"Really?? Nimechanganyikiwa? Una hakika?" Nikaongea huku nazunguka godoro kwenda upande ule aliogeukia. Nilikuwa nataka niongee naye huku namuangalia usoni ili maneno yangu yawe na effect niliyoitaka.
"Sikiliza Kaburu" nikaanza kuongea mara bada ya kuwa upande ule mwingine tunaangaliana. "Nafahamu kuwa Veronica Nyaulingo sio jina la mpenzi wako ambaye watu wanaamini amekufa. Amechukua jina la mtu ambaye mpaka sasa najiuliza amepoteaje huyo mtu. Ninachokiwaza ni kwamba wewe na wenzako The Board, kuna kitu mlikuwa mnakifanya nchini Rwanda na serikali ya Rwanda ikaja kugundua. Baada ya kugundua ndipo wakampandikiza afisa usalama wao ambaye alichukua 'identity' ya Veronica Nyaulingo ma kujiweka karibu na wewe na matokeo yake mkawa wapenzi. Naamini kuwa baada ya muda ingawa hii kwake kuwa na wewe kimapenzi ilikuwa ni assignment lakini akajikuta amekupenda kikweli kweli na wewe ukampenda. Na kama watoto wa sekondari vile mkajikuta mpo kwenye mapenzi mazito. Sasa lazima ikafika kipindi The Board wakagundua kuwa Veronica ni 'spy' na amepandikizwa kwenye maisha yako ili akupeleleze. Nina hakika kuwa kuna siri nyingi tayari alikuwa amezijua kuhusu wewe na The Board, kwahiyo The Board lazima wakafikia uamuzi kuwa inabidi auwawe. My guess is, wewe Kaburu ukawaambia wenzako kuwa wakuachie wewe hiyo kazi ya kumuua Veronica." Nikanyamaza kidogo na kumuangalia usoni. Nikaona jinsi haya maneno yanavyomgusa moyoni. Niakaendelea.
"Najiuliza sana mwili ulioichoma moto uliutoa wapi. Na ni mwili wa nani, lakini nafahamu na nina uhakika kabisa sio Veronica Nyaulingo. Mpenzi wako Veronica kwa kutumia uzoefu wake wa ushushushu ukaenda kumficha mahali salama kabisa ambako anaishi mpaka leo hii, lakini huku nyuma ulimwengu mzima ukaamini kuwa wivu wa mapenzi umekufanya umempiga mpenzi wako na kumchoma moto!! Sasa wanasema kuwa 'you can fool some people for some time but can't fool all the people all the time'! Nina hakika kuwa watu wa usalama kutoka Rwanda wakaja kugundua mchezo ulioufanya wewe na mpenzi wako, na si wao tu peke yao bali pia The Board nao wakagundua kitu ulichokifanya. Ndio hapo sekeseke lilipoanzia. Watu wa usalama wa Rwanda wanahitaji afisa wao wampate lakini pia nina hakika kuna taarifa muhimu wanaamini anayo ambayo wanahitaji waipate. Lakini pia The Board wamegundua kuna taarifa muhimu mno wanaamini utakuwa nayo na ni taarifa 'vital' mno kwao na hii ndio sababu mpaka leo hii upo hai hawajakuua.!"
Nikanyamaza tena kumuangalia. Alikuwa amenikodolea macho haamini ni namna gani nimeweza kuchekecha akili na kung'amua haya ninayomueleza. Sikutaka kumchelewesha, nikaendekea.
"Sasa basi, kama wanavyosema watu.. Mapenzi ni upofu, mapenzi yanatia ukichaa ndicho hicho ninachokiona kati yenu wewe na Veronica! Veronica akaamua kuwasaliti wanausalama wenzake ili awe na wewe, na wewe ukawasaliti wenzako The Board ili uishi maisha ya furaha na Veronica. Ndio sababu kwanini ulikiri mahakamani kuwa umemuua. Ulikuwa unaogopa kuwa mtaani baada ya tukio lile kutokea. Nina hakika The Board walimuhonga Jaji ili asikutie hatiani uachiliwe urudi uraiani ambapo wenyewe wanajua ni namna gani wataipata hiyo taatifa uliyo nayo. Kwahiyo kabla kesi haijaenda mbali sana ukaamua ukiri kuwa ulimuua ili kumnyima nafasi Jaji asikuachie huru mwisho wa kesi. Kwa hiyo Jaji ambaye nina hakika labda alikuwa anatumiwa na The Board licha ya kutamani kukuachia huru urudi uraiani ambapo The Board wanakusubiri wakudhibiti, ikabidi akupe kifungo chepesi cha miaka saba tu kwa hukumu ya kuua bila kukusudia"
Nikanyamaza tena na kumkazia macho.
"Umeongea maneno mengi bado haujaniambia point ni nini dogo?" Akaniuliza kwa hasira.
"My point is. Kwa hii hukumu yako ya miaka saba gerezani, tukiondoa 'remission' ya magereza maana yake unatumikia kama miaka minne na nusu pekee, na ukizingatia umeshakaa karibia miaka miwili na nusu that means umebakisha miaka miwili pekee urudi uraiani. Najua wewe ni mtu makini lazima umeshaweka mipango ni namna gani utawaepuka The Board ukiachiwa baada ya miaka miwili. Sasa unaonaje nikifanya figisu ushtakiwe upya kwa kosa la ule mwili uliouchoma moto safari hii iwe kesi halisi kabisa ya kuua na ulimwengu mzima ujue udanganyifu mlioufanya wewe na Veronica wako? Na amini mahakama safari hii itakusweka humu miaka mingi uozee humu humu maisha yako yote huyo veronica uwe unamuona kwenye ndoto pekee badala ya miaka miwili kutoka sasa?"
Kama kawaida nikanyamaza ili nione reaction yake. Alikuwa ameng'ata midomo kwa hasira. Maneno yangu yalikuwa yanamgusa penyewe kabisa. Sikumchelewesha tena, nikaendelea.
"Kama hiyo haitoshi, unaonaje nikiwamegea siri Usala wa Taifa au The Board kuhusu mahali Veronica alipojificha? Naomba nikuhakikishie kuwa kama unavyoona nywele zako zilivvyo karibu karibu ndivyo nilivyo close kufahamu Veronica alipo" nikampiga mkwara.
"Wenzako watu wa Usalama na The Board, mwaka wa pili wanakimbiza kivuli tu hawajui Veronica yuko wapi" akaongea kwa hasira.
"Well, mimi sio Usalama au The Board, mimi ni Rweyemamu Charles Kajuna!! Na kama nilovyomuonya yule jamaa niliyekwambia shuleni Tambaza, nakuambia na wewe na wala sikupi wiki au siku tatu, nakupa chance sasa hivi! Nieleze ninachokubembeleza siku zote hizi.. La sivyo help me God, usinilaumu kwa nitakacho kifanya" nikaongea kwa hasira nimemkazia macho huku nimemsogelea karibi pua zigusane.
Kaburu akashusha pumzi na kisha kuanza kuongea.
"He was right you know!"
"Who was right?" Nikamuuliza kwa kukereka.
"Dr. Shirima! He was right!" Akaongea.
"Right about what??" Nikamuuliza kwa hasira nikiona kama anataka kuhamisha magoli.
"Miaka mitatu kama na nusu hivi iliyopita nilikuwepo kwenye kikao ambacho alipendekeza kuwa tumuingize kwenye michakato yetu mwanafunzi wake anayeitwa Rweyemamu Charles Kajuna. Nakumbuka namna ambavyo alikuwa anasifia. Kuwa ni kijana genius na persistent! Kwamba unapontential hata tunaweza kukutengeneza ukawa kiongozi mzito huko mbeleni. Nilipokuja kupewa file lako na kulisoma nilikuwa impressed sana na ni moja ya watu ambao waliunga mkono pendekezo la Dr. Shirima kuwa tukuingize kwenye michakato yetu! Kijana genius ma persistent!"
Kaburu akaongea huku kwa kiasi fulani akiwa ana maanisha anachokisema na kuna kiasi Fulani alikuwa ananiinjoi.
"Thank you for your vote of confidence" nikamjibu kwa kumuinjoi pia.
"Except for one thing kijana! Kuwa king'ang'anizi kwenye maisha ni asset na pia ni liability.! Ni asset pale tu unapokuwa king'ang'anizi kwenye jambo sahihi na ni liability pale unapokuwa king'ang'anizi kwenye jambo lisilo sahihi. Na kwenye hili hauko sahihi kijana.. No one can take down The Board! No one"
Akaongea huku amenikazia macho.
"Don't worry about that! I will take my chances.. Hilo halikuhusu kabisa! Just tell what I want to know" nikamjibu kwa hasira nimiona kama anazunguka mbuyu tu.
"Ok! Nahitaji unisaidie kutoroka humu gerezani!" Akaongea akinikazia macho.
"What?" Nikamuuliza kwa mshangao.
"Nahitaji unisaidie kutoroka gerezani! Nataka uchekeche hizo akili zako kama unavyojigamba."
"Ok! Na unaweza kuniambia kwanini unataka kutoroka" nikamuukiza tena kwa mshangao.
"Humu sio mahali Salama tena kwangu, umeshaharibu kila kitu. Huo utaratibu tu aliouweka Mkuu wa gereza kuwa kuanzia jumatatu nianze kwenda shamba mi hatari kwa usalama wangu.. Na si hivyo tu! The Board wanajua uwezo wako wa kupanga mipango na ulivyo king'ang'anizi, wakihisi tu kuwa naweza kukupa taarifa muhimu nakuapia kwa Mungu watatumaliza wote wawili ili waondoe udhia once and for all"
Kaburu akaongea huku nikihisi hofu iliyokuwa kwenye sauti yake.
"Ok! Nitafikiria hilo but first things first.. Naomba info ninazozitaka kwanza" nikamkazia macho.
"Ok! Unapaswa kufahamu kuwa ndani ya The Board ni watu wawili pekee wanaojua kila kitu kinagaubaga. Hao wawili ndio wanaojua akaunti zote za siri, majina yote ya vibaraka wao serialini, kwenye vyombo vya usalama, majina ya wanachama wote walio hai na waliokufa, na mikakati yote kuanzia wa kwanza mpaka mkakati wa sasa wa 34!!"
Akaongea huku anafumba macho. Nilihisi kuwa alikuwa anajijutia kwa haya mambo anayonieleza.
"Ok! Ni nani hao wawili" nikauliza kwa shauku kubwa.
"Ni chairman na kuna mtu tunamuita The Book Keeper! Chairman huwezi kumpata na wala siwezi kukuambia lakini The Book Keeper una mfahamu vizuri sana" akaongea huku anafumbua macho baada ya kuyafunga alipokuwa anaongea.
Moyo ukaanza kunienda mbio.
"Ni nani?" Nikaukiza kwa shuku kubwa.
"Vincent Mallya" akaongea kwa kifupi huku akifumba tena macho.
"Whaaaaatt!" Nikapigwa na mshangao.
"Yes, Vincent Mallya" akaongea kwa kifupi tu huku bado amefunga macho.
"Vincent Mallya Mkurugenzi Mkuu wa Benki ya CRBB??" Nikamuuliza kwa mshangao.
"Yeah! That's him, ndiye The Book Keeper wa The Board.! Yeye ndiye anatunza kumbukumbu zote za The Board ambazo nimekueleza. Na kumbukumbu hizi haziwekwi kwenye vifaa vya digitali kama computer kuogopa watu kudukua.. Taarifa zote zinahifadhiwa kwenye karatasi na mafaili na yapo mahali yamehifadhiwa ambapo naweza kukuelekeza ukaenda kuyachukua kama unaokota dodo kwenye mwembe, but first inabidi unitoroshe humu gerezani." akaongea akiwa amenikazia macho kweli kweli.
Moyo ulienda kasi kweli kweli. Nikatafakari karibu vitu mia kwa wakati mmoja. Mbele yangu nimebakiza hatua moja tu nitimize lengo langu la kunileta humu. Lakini hatua yenyewe ni dhahiri ilikuwa ni impossible.
Nini kitafuata??
ITAENDELEA JUMATANO…