Chachu Ombara
JF-Expert Member
- Dec 11, 2012
- 5,897
- 10,358
Hawa viongozi ni wala rushwa wakubwa wanasababisha wakazi wa eneo lile tuteseke kwa harufu kali sana wakati wa usiku inayotokana na mabaki ya kuku.
Iko hivi...
Nyuma ya kituo cha daladala cha 'Kwa Ndevu', Tegeta kama unaelekea Bunju kuna mtaro mkubwa unaopeleka maji kwenye mto ulio katikati ya Kituo Kipya na Kwa Ndevu. Nyuma ya Kituo cha kwa Ndevu kuna machinjio ya kuku. Hivyo inapofika usiku kuanzia saa nane, kuna bomba linaelekezwa kwenye huo mtaro halafu yanafunguliwa maji yanayotoka machinjioni.
Yale maji yananuka sana sijapata kusikia harufu ya vile tokea nizaliwe. Nilikuwa nimekaa na bodaboda na bajaji ikabidi tukimbie. Nilipohoji nikaambiwa ile ni kawaida, viongozi wa mtaa huo walishaambiwa ila wakapozwa kidogo. Polisi nao walishakuja ila nao wakapozwa hivyo hakuna ufuatiliaji kabisa, tunabaki kuumia tunaotumia huduma za pale maana kuna soko kubwa tu na wengi mahitaji tunapata pale.
Mamlaka zichukue hadhari kabla ya maafa makubwa hayajatokea.
PICHA: Mabomba ya kimkakati yanayoletwa usiku wa manane kufanya uchafuzi wa mazingira. Mchana ukipita pale huyakuti. Mnaweza kuona aina ya uchafu unaotoka kwenye mabomba hayo.
Iko hivi...
Nyuma ya kituo cha daladala cha 'Kwa Ndevu', Tegeta kama unaelekea Bunju kuna mtaro mkubwa unaopeleka maji kwenye mto ulio katikati ya Kituo Kipya na Kwa Ndevu. Nyuma ya Kituo cha kwa Ndevu kuna machinjio ya kuku. Hivyo inapofika usiku kuanzia saa nane, kuna bomba linaelekezwa kwenye huo mtaro halafu yanafunguliwa maji yanayotoka machinjioni.
Yale maji yananuka sana sijapata kusikia harufu ya vile tokea nizaliwe. Nilikuwa nimekaa na bodaboda na bajaji ikabidi tukimbie. Nilipohoji nikaambiwa ile ni kawaida, viongozi wa mtaa huo walishaambiwa ila wakapozwa kidogo. Polisi nao walishakuja ila nao wakapozwa hivyo hakuna ufuatiliaji kabisa, tunabaki kuumia tunaotumia huduma za pale maana kuna soko kubwa tu na wengi mahitaji tunapata pale.
Mamlaka zichukue hadhari kabla ya maafa makubwa hayajatokea.
PICHA: Mabomba ya kimkakati yanayoletwa usiku wa manane kufanya uchafuzi wa mazingira. Mchana ukipita pale huyakuti. Mnaweza kuona aina ya uchafu unaotoka kwenye mabomba hayo.