Viongozi mliohudhuria mkutano wa UN rudini nyumbani na mikakati, msirudi na suti

kavulata

JF-Expert Member
Aug 2, 2012
12,307
12,602
Kuona ni kuamini, think globally and act locally. Tunaomba viongozi wetu wa bara la Afrika tuliowasafirisha kwenda New York kwa kodi zetu kuhudhuria mkutano mkuu wa Baraza la Dunia, UN mrudi nyumbani na mipango mkakati ya kuboresha maisha ya watu wenu.

Sina shaka kila kiongozi aliyekwenda New York aliona na kusikia mambo mengi huko yakiwemo maduka makubwa (Malls) yaliyosheheni bidhaa zenye ubora, lakini sisi wananchi wenu tungependa mrudi na yafuatayo:

1. Usafi wa mitaa na majengo ya New York unafanyukaje. Je wana takataka zilizozagaa barabarani wala vibanda vya wasiokuwa na ajira kwenye njia za waenda kwa miguu?.
2. Mkutane na marais waliopatikana kwa njia za kidemokrasia, muwaulize wao wanafanye?
3. Mkutane na wenyeviti wa vyama vya siasa mjue vinavyoendeshwa
4. Uchumi wao unavyoendeshwa na kusimamiwa.
5. Namna ya mikataba ya kimataifa inavyofungwa na mambo ya kuzingatia wakati wa kuingia mikataba
6. Namna bidhaa zetu zinavyoweza kupenya kwenye masoko yao kwa wepesi
7. Mpate na mrudi na elimu ya namna mifuko ya jamii inavyojiendesha na kusimamiwa
8. Ulizeni uhusiano uliopo kati ya kulipa mishahara mikubwa watumishi na ukuaji wa sekta nyingine kama viwanda, kilimo, biashara, afya na elimu.
9. Ulizeni kuhusu adhabu wanazopewa wakwepa kodi na wanaoiba mali za umma.
10. Waulizeni namna wanavyodhibiti ubora wa bidhaa na huduma zinazozalishwa, kutolewa na kuingia kwenye masoko yao.
11. Kilimo chao wanalima vipi na wakulima wanawezeshwa vipi ili kulima kwa tija.

Ni matumaini yetu kuwa muda wa kujifunza haya mambo 11 mnao huko, tafadhalini sana msirudi nyumbani na mabegi mapya makubwa ya nguo kutoka huko na kuja kuendelea na business as usual.

Ni aibu kubwa kuyaacha mazuri yote hukohuko na kubeba suti zake na za uwapendao.
 
Wwnzako wanafikilia jinsi ya kufungua accoynt Uswiss,,na jinsi ya kupata mikopo ila watanue zaidi kwa kutumia jasho la wananchi wao amabo wengi ni wanyonhe wa kiuchumi
 
Tunataka matendo. Maneno mengi tumeshayasikia. Tunataka maendeleo. Sio ubabaishaji usioisha
 
Tunataka matendo. Maneno mengi tumeshayasikia. Tunataka maendeleo. Sio ubabaishaji usioisha
Value for money ya kodi yetu ya kuwapeleka New York,

Mfano, safari moja ya aina hii imegarimu vituo vingapi vya afya? na je safari kama hii italeta vituo vingapi vya afya? Hesabu zetu lazima tusipige kwa aina hii, ili tuone faida na hasara. Jamani wazungu hawana kitu cha bure nyie!!!
 
Wanajua kabisa na wale jamaa hawanaga rafiki wa kudumu.......eti mama ndo kaekwa kwene mabango barabarani nchini MAREKANI!!!!
 
Wanataka resources. Rare earth metal, cobalt, nickel, lithium, iron, gold, graphite etc.

Tusipoipenda na kuipambania nchi yetu ipate maendeleo, nani mwingine atafanya hivyo? Tunataka wawekezaji wa ukweli ili wao na sisi tunufaike
 
huko bwashe wameenda kutalii tu hakuna lolote.mbona tangu tupate uhuru misele ya huko ilikuwa inaendelea tu lkn hakuna lilobadilika.Labda the late JPM naona atleast alikuwa na maono ya kuipeleka nchi mbele.
 
Mtu anayekwenda mahali kujifunza huenda kwa nauli yake, lakini hao wote wameenda kwa kodi za umma, na imprest juu. Je unategemea wajifunze lolote la maana zaidi ya kuwa na picha zikionyesha waliwahi kufika US?
ni kuamini, think globally and act locally. Tunaomba viongozi wetu wa bara la Afrika tuliowasafirisha kwenda New York kwa kodi zetu kuhudhuria mkutano mkuu wa Baraza la Dunia, UN mrudi nyumbani na mipango mkakati ya kuboresha maisha ya watu wenu.

Sina shaka kila kiongozi aliyekwenda New York aliona na kusikia mambo mengi huko yakiwemo maduka makubwa (Malls) yaliyosheheni bidhaa zenye ubora, lakini sisi wananchi wenu tungependa mrudi na yafuatayo:

1. Usafi wa mitaa na majengo ya New York unafanyukaje. Je wana takataka zilizozagaa barabarani wala vibanda vya wasiokuwa na ajira kwenye njia za waenda kwa miguu?.
2. Mkutane na marais waliopatikana kwa njia za kidemokrasia, muwaulize wao wanafanye?
3. Mkutane na wenyeviti wa vyama vya siasa mjue vinavyoendeshwa
4. Uchumi wao unavyoendeshwa na kusimamiwa.
5. Namna ya mikataba ya kimataifa inavyofungwa na mambo ya kuzingatia wakati wa kuingia mikataba
6. Namna bidhaa zetu zinavyoweza kupenya kwenye masoko yao kwa wepesi
7. Mpate na mrudi na elimu ya namna mifuko ya jamii inavyojiendesha na kusimamiwa
8. Ulizeni uhusiano uliopo kati ya kulipa mishahara mikubwa watumishi na ukuaji wa sekta nyingine kama viwanda, kilimo, biashara, afya na elimu.
9. Ulizeni kuhusu adhabu wanazopewa wakwepa kodi na wanaoiba mali za umma.
10. Waulizeni namna wanavyodhibiti ubora wa bidhaa na huduma zinazozalishwa, kutolewa na kuingia kwenye masoko yao.
11. Kilimo chao wanalima vipi na wakulima wanawezeshwa vipi ili kulima kwa tija.

Ni matumaini yetu kuwa muda wa kujifunza haya mambo 11 mnao huko, tafadhalini sana msirudi nyumbani na mabegi mapya makubwa ya nguo kutoka huko na kuja kuendelea na business as usual.

Ni aibu kubwa kuyaacha mazuri yote hukohuko na kubeba suti zake na za uwapendao.
 
Wanataka resources. Rare earth metal, cobalt, nickel, lithium, iron, gold, graphite etc.

Tusipoipenda na kuipambania nchi yetu ipate maendeleo, nani mwingine atafanya hivyo? Tunataka wawekezaji wa ukweli ili wao na sisi tunufaike
wakezaji wa ukweli atawaleta nani?, wakija tutawafahamuje? nani ataingia makubaliano nao? wenyenyewe tunataka ngapi? ni maswali tu mwanzo mwisho
 
huko bwashe wameenda kutalii tu hakuna lolote.mbona tangu tupate uhuru misele ya huko ilikuwa inaendelea tu lkn hakuna lilobadilika.Labda the late JPM naona atleast alikuwa na maono ya kuipeleka nchi mbele.
Hata JPM kuna stage angewafuata mwenyewe tu waliko. Mabeberu ni kama chatu, mbwa anajipeleka mwenyewe tu.
 
Back
Top Bottom