Viongozi, wanasiasa na wafanyabiashara wazaliwa wa SINGIDA, Manyara na Kagera ni chanzo kikubwa cha umaskini kwenye mikoa yao

Resilience

JF-Expert Member
Jan 4, 2023
876
4,101
Kila ukipita Singida unaona hali ni ileile miaka nenda rudi same applies to Manyara. Na hapa tunapita mjini hata maji ya kunywa shida, ukienda huko wilayani kisha vijijini hali ni mbaya zaidi.

Mkoa wa Kagera ni moja ya mikoa maskini nchini kwa sasa. Pamoja na hali ya hewa nzuri na kuzalisha watu wengi wasomi lakini hakuna maendeleo. Sababu kubwa ni wenyeji kupakataa kwao lakini cha pili ni Serikali kutopeleka miradi ya kimkakati.

Wakati uwanja wa ndege wa Chato unajengwa niliamini watu wa Kagera wangetumia vyema rasilimali hii kufanya biashara na Kongo, Uganda, Rwanda na Burundi lakini matokeo yake viongozi wa kanda ile walichokifanya sasa hivi nikwenda Dodoma kudhibiti hata maono ya JPM ya kupata mkoa mpya yasifikiwe. Unajiuliza mkoa mpya unawanyima kuishi masaki? Mkoa mpya wa Chato ungeweza kuwanyima wananchi chakula au ungeleta chakula zaidi?

Haya ni baadhi ya mambo ambayo ninapotafakari umaskini wa mikao hii natamani sana kujua kama ipo mikakati ya kuwakomboa wananchi wanaoteseka.

Mfano maji ya ziwa Victoria kwanini yasifike wilaya zote za Singida na Manyara kisha yakasambaa vijijini hata kwa kukopa trilions? Wananchi wakipata maji watazalisha na muda mfupi trilioni tuliyokopa itarejeshwa.

Kwanini tusifungue masoko makubwa ya mafuta na viwanda Singida? Mafuta yakzalishwa na kufungwa tayari kwa kuuza? Kwanini tusifungue mashamba ya kilimo makubwa ya umwagiliaji? Viongozi wote wazaliwa wa Singida na Manyara wanaishi Dar es Salaam lini watafikiria kurudisha nyumbani?
 
Una hoja. Lakini hili la kuanzisha mkoa wa Chato HAPANA
 
Upo sahihi lakini kwani ni lazima maji ya ziwa Victoria yafike Singida? Singida kuna maeneo Yana maji mengi sana yanayofaa kwa matumizi ya binadamu changamoto ni kuwa Serikali haitaki wananchi wake wapate maisha mazuri.

Gharama iliyotumika kununua Ndege zinazoendeshwa kwa hasara ilitosha kabisa kuweka miundombinu ya kuchima visima na kuwawezesha wananchi kulima kwa ufasahaa.

Unanunua ndege then unaiendesha kwa hasara alafu unaona wananchi wako wanakunywa maji machafu na kulala kwenye nyumba za Tembe huku watoto wakipata udumavu wa akili....then unajitapa kuwa unawaletea wananchi maendeleo.
 
Embu leta takwimu rasmi na jadidi ikionesha kuwa Manyara ni maskini kama Singida na Kagera??!!!
 
Upo sahihi lakini kwani ni lazima maji ya ziwa Victoria yafike Singida? Singida kuna maeneo Yana maji mengi sana yanayofaa kwa matumizi ya binadamu changamoto ni kuwa Serikali haitaki wananchi wake wapate maisha mazuri.

Gharama iliyotumika kununua Ndege zinazoendeshwa kwa hasara ilitosha kabisa kuweka miundombinu ya kuchima visima na kuwawezesha wananchi kulima kwa ufasahaa.

Unanunua ndege then unaiendesha kwa hasara alafu unaona wananchi wako wanakunywa maji machafu na kulala kwenye nyumba za Tembe huku watoto wakipata udumavu wa akili....then unajitapa kuwa unawaletea wananchi maendeleo.
Maeneo gani hayo ya singida wewe umeona kuna maji mengi?
 
Back
Top Bottom