Viongozi kuweni makini na Watanzania, wengi wao ni Wanafiki

Burkinabe

JF-Expert Member
Feb 12, 2023
1,892
3,196
Asalaam Aleykum.

Bila shaka wote mko vizuri na mnaendelea na kazi za ujenzi wa Taifa letu.

Leo ninao wosia kwa viongozi wa nchi yetu kuwa makini na raia wao, maana ni ukweli usiopingika kwamba Watanzania wengi ni wanafiki. Mnafiki ni mtu anayejifanya vile asivyo. Kwa maneno mengine, mnafiki ni mtu kigeu-geu.

Hili linaweza kuthibitishwa na mtizamo wa Watanzania kwa sakata la mkataba kati ya Serikali na DP World. Watanzania wanaohudhuria mikutano ya upinzani wote wanaonekana kuupinga mkataba huo ilihali wale wanaohudhuria mikutano ya chama tawala huonekana kuunga mkono 100%!

Nimekaa nikatafakari kwamba, siyo kweli kwamba wote huwa wanakubaliana na aidha viongozi wa chama tawala au upinzani, bali wengi huwa wanataka kuwaridhisha tu viongozi wao wanaoendesha mikutano hiyo.

Kwa kawaida huwezi kutenganisha uoga na unafiki. Hivyo, kwa sababu Watanzania wengi ni waoga, basi hujikuta wanakuwa wanafiki automatically kwa sababu tu ya kuonekana kuwa tofauti na viongozi wao hasa hasa wa chama tawala.

Hivyo, kwa kuhitimisha, nawaomba viongozi wa serikali wawe makini sana na hawa Watanzania hasa wanaoonekana kukubaliana na mkataba kati ya DP World na serikali pamoja na mapungufu yake.

Muda ukifika, wanaweza kujikuta wanashangaa kuona wamegeukwa na raia hasa baada ya kutoka madarakani.

Mungu wabariki viongozi wetu wafanye maamuzi bora kwa ajili ya ustawi wa raia wote wa nchi hii. Pia naomba uwasaidie raia wa nchi hii kuondokana na uoga pamoja na unafiki. Wawaambie viongozi wao ukweli. Wawasifu viongozi wao pale wanapotenda vyema, wawakosoe pia pale wanapokosea; maana hata wao ni binadamu pia.

AMIN.
 
Huu ndio ukweli Mchungu,Watanzania wengi ni Wanafiki sana.Enzi za JPM walikuwa wanamsema vibaya sana Kwa jinsi alivyokuwa anaongoza.Leo hii amekuja Mhe.Rais Samia na kaja na style yake ya Uongozi ya Kipekee yenye Kujali Utu, maendeleo bila kubaguana,na Huku akiruhusu Uhuru wa kutoa maoni na amani Kwa watu wote,ila Bado watu wanaanza kumsema vibaya Mama yetu na bila woga wanaleta dharau kila akifanyacho.
Nitatoa mfano wa mambo kadhaa Leo...

1.Masuala ya Ajira

Miaka kadhaa Watanzania walilalamika Serikali kutoajiri,Leo hii Mhe.Samia kaajiri Ajira Kibao Kwa Vijana,kuanzia Walimu,Afya,Majeshi yote na Ajira nyinginezo Kwenye Mashirika Na Taasisi zote za Umma ambapo hivyo Vibali vyote Kasaini yeye.Siku hizi Suala la Ajira sio Inshu Tena kwenye Serikali ya Mhe.Samia kwani Ajira zipo Nje nje, zinaendelea kutangazwa na watu wanaitwa Kazini kila Siku.
Watanzania Ingieni Hapa Mjionee

2.Suala La Bandari na Uwekezaji Kwa Ujumla.
Miaka kadhaa Watanzania wengi mlikuwa mnalalamika ya kuwa Bandari yetu haifanyi vizuri,na nyie wenyewe mlitoa mawazo ya kuwa atafutwe mwekezaji mwingine ya Kuwa aliyepo Hatoshi,Leo hii Serikali imetafuta mwekezaji Mpya lakini Bado mnapinga..
Sasa serikali Ifanye lipi Tena????
Ndio shida ya Watanzania Hata ufanye zuri lipi watajifanya Wajuaji wanajua kila kitu kuliko Serikali.

Mimi Kwa Leo naomba niishie hapa ila nataka kusema ya kuwa nimekaa na Kujifunza Mengi sana kuhusu Sisi Watanzania,ki ukweli Watanzania wengi Ujuaji na kutokuwa na hulka ya kusema Asante Kwa mambo mazuri tunayofanyiwa ndio kinachoendelea Sasa.
Mhe.Rais Mimi na ombi kwako najua una Nia Njema sana na sisi Watanzania Hata kauli zako unajua Watanzania tunataka Nini,Wewe mama yetu chapa Kazi,Sisi tunaona Nchi hii Toka umechukua imetulia na kazi zinafanyika.Hawa Wajuaji na wapinga maendeleo Kesho tutakuwa pamoja,endelea kuijenga Tanzania mpya chini yako.
 
Back
Top Bottom