Viongozi wasio waadilifu wapuuzwe

Bams

JF-Expert Member
Oct 19, 2010
16,555
41,066
Siyo kila kiongozi ana akili. Siyo kila kiongozi ana busara. Siyo kila kiongozi ni mwadilifu.

Kiongozi anaweza kuwa mwenye akili, hekima na mwadilifu. Pia mnaweza kuwa na kiongozi mwongo, hana busara, fisadi, mnafiki na mropokaji.

Kwa sasa tuna viongozi wengi wanafiki, waongo, na sifa nyingi mbaya. Kutokana na uwezo wao wa uongozi kuwa mdogo, kwa sababu wanajuu hawana uwezo, wanachokifanya, wakati wote ni kumpa Mh. Rais rushwa ya sifa, wakijua kwa kufanya hivyo watampumbaza asiyaone mapungufu yao.

Viongozi hao, wapo tayari kutoa hata sifa za kejeli kwa Rais. Unapompa mtu sifa ambayo unajua kabisa ni ya uwongo, hiyo ni kumkejeli huyo unayemsifia na unamfanya hana akili ya kutambua kuwa hiyo sifa unayompa ni ya uwongo.

Wengi wenye akili na wanaotamani nchi hii iongozwe na watu wenye akili timamu, walionyoka kwa kauli na matendo, walio wakweli wa nafsi na wenye dhamira njema kwa Taifa lao, mara nyingi wamesikika wakiilalamikia hii tabia ya hovyo, ya kumsifia Rais hata kwa mambo ambayo wala hayafanyiki kwa sababu Rais. Kuna wakati ni jitihada tu wahusika, mapenzi ya Mungu, kodi na kujitoa kwa wananchi wenyewe.

Kuthibitisha tuna viongozi wengi wa hovyo, hivi karibuni mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam, amewajibu wanaohoji tabia ya hovyo ya uchawa ya baadhi ya viongozi, eti yeye hawezi kumsifia Mbowe, atamsifia Rais! Hakika huyu ni miongoni mwa viongozi wanaodhihirisha kuwa ni wa hovyo, na aliyekosa hata ile akili ya kawaida ambayo kiongozi anastahili kuwa nayo.

Hivi kuna mtu yeyote ambaye yeye Chalamila anaweza kumtaja kwa ushabidi kuwa alisema Rais asisifiwe kwa mambo ambayo ni kejeli, na kwa hayo mambo asifiwe Mbowe au mtu mwingine yeyote?

Hii nchi, kwa aina ya viongozi wa namna hii, tunaua matumaini na ndoto za wananchi wa Taifa hili. Siku zote kiongozi ambaye anaonekana hovyo kwa machache tunayoyajua, uwezekano mkubwa atakuwa hovyo hata kwa mengi tusiyoyajua.

Siku zote kazi ya kiongozi ni kuwa mbele, na anaowaongoza wanatakiwa kuwa nyuma yake, na yeye akiwaongoza kuwapeleka kwenye maono sahihi. Viongozi hawa wanafiki, wanawaongoza wananchi kuelekea kwenye unafiki, na hivyo kulijenga Taifa la watu wanafiki, waongo, wapiga porojo na mafisadi, kama walivyo wao viongozi.

Kiongozi apongezwe kwa kufanya vema, aonywe na kukosolewa anapotenda hovyo, aondolewe na afurushwe anapoonekana amedhamiria kulipotosha Taifa au jamii.
 
Kila kitokacho mdomoni kwa Chalamilia huwa sikiamini.

Huyu bwana ni kama ana mkataba wa kudumu na Uropokaji. Sijawahi kumsikia hata mara moja akitoa kauli inayoashiria ni kiongozi mwenye hekima.
 
Chanzo Cha haya yote ni mfumo mbovu wa elimu.elimu yetu imetuletea viongozi wakujipendekeza.tuige elimu ya Kenya au Uganda maana Kule huwezi kumuona kiongozi anajipendekeza Kwa rais ili apate uteuzi.kule kama rais amekosea anaambiwa ukweli umekosea lakini hapa kwetu hata Cha kupuuzi kabisa kinasifiwa tu
 
Hii dunia, tunastaabishwa na ya mussa.

iu

Picture:NYTimes
 
Mfano makondakta yaani hata marekani wanajua na hawataki hata kumuona!!
Shangaa kunamtu anampeenda na anamchagua kutoa mafunzo na itikadi... Alafu uniambie eti kuna Foo Ara
 
Mfano makondakta yaani hata marekani wanajua na hawataki hata kumuona!!
Shangaa kunamtu anampeenda na anamchagua kutoa mafunzo na itikadi... Alafu uniambie eti kuna Foo Ara

Yaani inakuwa ni kama vile nchi imeamua kuwa ya uovu, hivyo waliobobea kwenye uovu wanapewa uongozi ili wawafundishe jinsi ya kuwa waovu. Fikiria wauaji wanapewa nafasi ya kuongoza chama. Je, CCM imeamua kuwa chama cha wauaji kiasi cha kuhitaji wenye uzoevu wa kuua kuwa viongozi wake?
 
Chanzo Cha haya yote ni mfumo mbovu wa elimu.elimu yetu imetuletea viongozi wakujipendekeza.tuige elimu ya Kenya au Uganda maana Kule huwezi kumuona kiongozi anajipendekeza Kwa rais ili apate uteuzi.kule kama rais amekosea anaambiwa ukweli umekosea lakini hapa kwetu hata Cha kupuuzi kabisa kinasifiwa tu
Tanzania "kujipendekeza" yanafundishwa? Shuleni?

Na hiyo mifumo unayopiga vita ya elimu, ni mifumo gani haswa?

Elimu ya Darasani-Walileta Wazungu ama nakosea?

Elimu ya kurithi? Isiyo rasmi kwenye vitabu...Folklore etc...


Sasa unachokataa ni nini Utamaduni au Elimu ya kuiga?
 
Mfano makondakta yaani hata marekani wanajua na hawataki hata kumuona!!
Shangaa kunamtu anampeenda na anamchagua kutoa mafunzo na itikadi... Alafu uniambie eti kuna Foo Ara
Sio kweli Marekani hawataki kumuona Kondakta-Unapotosha.

Tangia waanzishe mashine za kukusanya hela ,makampuni mengi ya mabasi yaliona hapakuwa na sababu ya kuwalipa mishahara makondakta-Yaani kupunguza head cost na sio kwamba-hawakupenda
 
Hao viongozi wanajua tabia za mkuu wao, anapenda sifa, ndio maana nao wanampa hata sifa za uongo nae anazipokea.

Uchawa unampa kiongozi usalama mahali pake pa kazi, ndio maana sidhani kama utaisha hivi karibuni.
 
Sio kweli Marekani hawataki kumuona Kondakta-Unapotosha.

Tangia waanzishe mashine za kukusanya hela ,makampuni mengi ya mabasi yaliona hapakuwa na sababu ya kuwalipa mishahara makondakta-Yaani kupunguza head cost na sio kwamba-hawakupenda
Jiongeze kidogo tumia brain
 
Kwa sasa tuna viongozi wengi wanafiki, waongo, na sifa nyingi mbaya. Kutokana na uwezo wao wa uongozi kuwa mdogo, kwa sababu wanajuu hawana uwezo, wanachokifanya, wakati wote ni kumpa Mh. Rais rushwa ya sifa, wakijua kwa kufanya hivyo watampumbaza asiyaone mapungufu yao.
Baba pokea maua yako 💪 🥀🌹🌹🎋🍄
 
Back
Top Bottom