Vincent Nyerere ampa Mkapa vidonge stahiki

.................,,, apson mwang'onda.............,,, dah..., hivi huyu chief wangu wa zamani yuko wapi skuizi?? mwenye taarifa jamani
 
Mkuu Mtanzania,

Hapo kwenye bold naomba kutofautiana na wewe kwenye hilo. Inategemeana ni case ya namna gani. Nilisoma kitabu cha mauaji ya Lumumba, more than 40 yrs later watu ndio wanakuja kukiri wazi wazi kwamba walienda na sumu DRC kwa malengo ya kummaliza Lumumba.

Kwa hawa wenzetu wazungu ukishaonekana ni mwiba kwenye maslahi yao, serikali zao ziko tayari kufanya lolote lile na hata kupindisha sheria ili wakumalize na biashara iishie hapo then maslahi yao yabaki salama. Tuseme ukweli, Nyerere alikuwa mwiba wa Globalization, hakuwa tayari kuona Tanzania inaingia kichwa kichwa bila ya maandalizi ya kutosha. Tumeingizwa kwenye globalization kichwa kichwa baada ya kuliwa ndo serikali inakuja kukiri kwamba hakukuwa na maandalizi ya kutosha na aliyetuingiza ni Mkapa huyu huyu.

Mkapa alikuwa Mwenyekiti Mwenza wa Globalization, akishirikiana na Tony Blair. Radar ilikuwa ni kashfa kubwa sana, lakini SFO wamekubali yaishe na kuimaliza kimya kimya. Sasa niambie kigezo cha SFO kufunika kombe ili mwana haramu apite [kulinda serikali yao] ndio madaktari watashindwa kufunika kombe?

Tuje na logic nyingine, lakini hizi za kusema wazungu/serikali za nchi za Magharibi hawawezi kufanya hiki au kile, hizo ni politics, wanacholinda na kutunza ni maslahi yao na si kingine. Ndo maana Charles Taylor amewaumbua wa-Marekani kwa kusema yeye [Taylor] alikuwa agent wa CIA na hivyo wakati anafanya yale madudu aliyoyafanya alikuwa na full support ya US. Siku zote US imekuwa ikikana kwamba hakuwahi. Majuzi hapa serikali imekiri na ikasema haiwezi kutoa more details on the subject. Ndio unakuja kushangaa kwamba Taylor alitoroka kwenye gereza ambalo lina maximum security hapa US, alichomokaje gerezani?


nakumbuka vizuri sana sumu ya lumumba ilikuja ikiwa imewekwa kwenye tube ya dawa ya meno bahati mbaya mpango haukufanikiwa akauawa kivingine.....huyu jamaa anawaamini waingereza labda kwa kuwa anaishi pale achana nae.....
 
Mkuu Mtanzania,

Hapo kwenye bold naomba kutofautiana na wewe kwenye hilo. Inategemeana ni case ya namna gani. Nilisoma kitabu cha mauaji ya Lumumba, more than 40 yrs later watu ndio wanakuja kukiri wazi wazi kwamba walienda na sumu DRC kwa malengo ya kummaliza Lumumba.

Kwa hawa wenzetu wazungu ukishaonekana ni mwiba kwenye maslahi yao, serikali zao ziko tayari kufanya lolote lile na hata kupindisha sheria ili wakumalize na biashara iishie hapo then maslahi yao yabaki salama. Tuseme ukweli, Nyerere alikuwa mwiba wa Globalization, hakuwa tayari kuona Tanzania inaingia kichwa kichwa bila ya maandalizi ya kutosha. Tumeingizwa kwenye globalization kichwa kichwa baada ya kuliwa ndo serikali inakuja kukiri kwamba hakukuwa na maandalizi ya kutosha na aliyetuingiza ni Mkapa huyu huyu.

Mkapa alikuwa Mwenyekiti Mwenza wa Globalization, akishirikiana na Tony Blair. Radar ilikuwa ni kashfa kubwa sana, lakini SFO wamekubali yaishe na kuimaliza kimya kimya. Sasa niambie kigezo cha SFO kufunika kombe ili mwana haramu apite [kulinda serikali yao] ndio madaktari watashindwa kufunika kombe?

Tuje na logic nyingine, lakini hizi za kusema wazungu/serikali za nchi za Magharibi hawawezi kufanya hiki au kile, hizo ni politics, wanacholinda na kutunza ni maslahi yao na si kingine. Ndo maana Charles Taylor amewaumbua wa-Marekani kwa kusema yeye [Taylor] alikuwa agent wa CIA na hivyo wakati anafanya yale madudu aliyoyafanya alikuwa na full support ya US. Siku zote US imekuwa ikikana kwamba hakuwahi. Majuzi hapa serikali imekiri na ikasema haiwezi kutoa more details on the subject. Ndio unakuja kushangaa kwamba Taylor alitoroka kwenye gereza ambalo lina maximum security hapa US, alichomokaje gerezani?


Mkuu,
Taratibu hiyo kashifa ya SFO ni serikali ya wapi iliyochunguza hilo, ama ni serikali gani ambayo imetuwekea wazi huu ufisadi?
 
Mkuu de'levis, please ningeku-PM ila natumia simu, naomba mwaga data za huyo jamaa jamvini maana nimekuwa nikiona comment zako kuhusu jamaa inaonekana una full data. Please JF is where we dare to talk!!
Huyu jamaa ni kweli yupo au pepele? Kama yupo, vp anaibuka lini Bongo? Na ameondoka kuelekea wapi?


kabla ya mwaka huu kuisha jogoo lazima awike......12.10.2012.....''he has a plan that he must follow''
 
Haya yote Mzee Mkapa kayataka mwenyewe kwa ukoo wa Nyerere kwani kwa kawaida mmbwa unapomfukuza siku zote atakimbia.

Lakini ukiendelea kumkabili zaidi na hata mbele yake kukatokea kuwa na ukuta bila ya sehemu nyingine zaidi pa kupita, basi hadi hapo ndipo mmbwa hugeuka mbogo na kumshambulia bila ajizi yule mbabe wake.

Tupeni majibu ya kifo cha Mwaalimu Nyerere. Wiki ile ya kuamua kwenda kujipima tu afya yake, Watanzania tulimuona akipalilia shamba lake la maharage Butiama.

Hata hivo msururu wa mambo mara baada ya mwaliko wa TUCTA na hotuba yake mwiba kwa watawala akiwa jijini Mbeya na ile ahadi kwamba akirudi kupima afya angeangusha BOMSHELL kwa sura ya UFISADI uliokithiri ndani ya CCM ...

... WaTanzania tunakutaka majibu Mzee Mkapa juu ya kifo cha Baba wa Taifa.

Kulikuwa hakuna polisi wa kumkamata vicent? Amepeleka ushahidi kwa manumba au bado?

Mlikuwa wapi kusema haya mpaka mkapa akaja arumeru? Nina uhakika vn angesema haya mapema bwm asingeenda ae.
 
Mkuu Rufiji,
Wapi Dr. Mwakyembe kasema amepewa sumu? Binafsi sijamsikia wala sijasoma popote pale aliposema amepewa sumu.

Akishasema mwenyewe basi wakati huo tutajadili zaidi. Hata kyela wananchi wake wanasubiri awaambie nini kinaendelea.

Mtanzania,

Ninaamini ya kuwa unaweza kusoma kati kati ya mstari , tafadhali soma hiyo taarifa hapo chini halafu unaimbie Mwakyembe alikuwa ana-imply ni nini haswa?

" Mwakyembe alisema, katika barua yake kwa IGP alieleza kuwa kundi hilo la mauaji lilikuwa limeelekezwa kumuua kwa kutumia sumu, taarifa ambayo kwa karibu mwaka mzima polisi hawakutaka kuifuatilia kwa sababu wanazozijua wao. Waziri huyo alieleza kushangazwa na msukumo mpya wa Jeshi la Polisi kutaka kujua kama alipewa sumu au la na kuamua kutoa tamko hata kabla ya kumchunguza alivyo.

Alisema polisi hawajawahi kumhoji yeye wala wasaidizi wake ofisini na hata kuongea na mabingwa wa Kihindi wanaomfanyia uchunguzi nchini India. Waziri huyo aliwashangaa polisi badala ya kumshukuru, Waziri Sitta kwa sababu amekuwa akiwapa tahadhari kuhusu afya yake ili suala hilo lichunguzwe kwa kina, badala yake sasa anaonekana adui wao. “Nimesoma darasa moja Kitivo cha Sheria Chuo Kikuu cha Dar es Salaam eneo la Mlimani na DCI Manumba."

Swali la kujiuliza Dr anamaanisha ni nini anaposema wamshukuru Sitta? Na je Sitta alisema nini kuhusu afya ya Mwakyembe.

Source:
Waraka wa Mwakyembe
 
Hebu jiulize kwa nini PM Tony Blair hakumaliza muda wake.

Hata aliyemuondoa madarakani Chancellor Helmut Kohl ni huyu huyu mama Angela Merkel na kibaya zaidi ni kuwa ni Kohl aliyemuingiza mama kwenye Siasa na kumpika. Inasemekana hadi kuna kipindi alimpa fedha akanunue nguo awe kama mwanamke maana alikuwa kakaa kama dumedume hivi.

Tony Blair alipotoka madarakani, ndiyo madudu yakaanza kufumuliwa. Au walifanya hivyo ili kupoza watu ili kuonyesha kuwa haya ndiyo mabaya ya Tony au kuna watu walikosana na wakaamua kumuanika.
Mkuu,
Taratibu hiyo kashifa ya SFO ni serikali ya wapi iliyochunguza hilo, ama ni serikali gani ambayo imetuwekea wazi huu ufisadi?
 
Watu msione WaTanzania karibu wote, na kwa ujinga wetu huo huo mnavyotuona siku zote, watu tukaamua kukiogopa CCM na viongozi wake kama ukoma na kuachana nacho kabisa mijini na vijijini; kifo cha Mwalimu Nyerere Tanzania One Theatre walikijulia wapi hata wakatunga nyimbo kwa mpangilio mkubwa, wasanii kibao na kufanya recording yenye ubora wa hali ya juu iliosambazwa kote nchini?

Kitu ambacho nashindwa kuelewa mpaka sasa hivi ni Kuwa, Mara tu yakutangaziwa kuwa baba aw Taifa kafariki, nakumbuka siku hiyohiyo nyimbo kibao ziliimbwa za maombelezo na bwana Komba, sasa nacho shangaa ni lini aliziandaa hizo nyimbo za mazishi!!!!! Je Komba alijuaje Nyerere angefariki ktk kipindi hicho
 
Keil,

Hizi habari zimenipita sana mwenzio kushoto. Nafikiri kwa sababu ya kukaa sana Sikonge tangu nilipomaliza JKT. Mengi yanayotokea Dar kwa kweli ni kusoma hapa JF, kwenye mitandao au nikiongea na Mtanzania.

Hii habari sijawahi kuisikia kabisa na kwa kweli imenishangaza mno. Nakumbuka kuangalia mazishi ya Nyerere kwenye BBC na CNN na kumuona hadi Mama Clinton akija Tanzania. Sikutegemea kuwa Mkapa atakuwa mkatili namna hiyo na mtu aliyeweka pesa mbele hadi kumtanguliza Mwalimu wake na mtu aliyemuweka madarakani.

Nakubaliana na wewe kuwa Dr. Slaa au Mbowe au Zitto, wampige STOP huyu V. Nyerere na hii habari asiiongelee tena. Kama sumu kashatema na mengine acha yaanze kushuka kwa gravitation force.

Ngoja nilale na asubuhi ntaamkia hapa kuifuatilia zaidi kama haitafutwa.

[Lali/dilagi mpola kwenuko ]

Hey Sikonge, siwezi kukulaumu kuhusu kutopata habari on time. Hata mimi naonekana kama nilipitwa na habari kwenye BBC or CNN wakionyesha Mama Clinton kwenye huo msiba. Mie nilidhani yule mama alikuwa Madeleine Albright aliyekuwa Waziri wa Mambo ya Nje wa US wakati huo!!
 
Wana JF leo katika viwanja vinne tofauti vya kampeni Mbunge wa Musoma Mjini ambae ndie Meneja Kampeni wa Arumeru Mashariki(Vincent Nyerere) amemjibu Mkapa kuwa.

Aache unafiki wa siasa kwani ana Siri nzito juu yake ambayo ni muda muafaka sasa kwa Watanzania kuijua,na kudai kuwa yeye si mtoto wa Julius Nyerere kama anavyopotosha Mkapa ila ni wa Josephat Nyerere

Josephat na Julius ni mtu na Mdogo wake(kama hataki ajinyonge) huku akishangiliwa na umati mkubwa Sana uliohudhuria katika viwanja vya mkuytano uliofanyika Sing'si alimtaka Mkapa ajibu na aweke wazi juu ya Kifo cha baba wa Taifa aliyeondoka Butiama akiwa Mzima aliyekwenda tu kupima Afya na kurudi Mfu,huku umati ukipiga Mayowe kwa kushangilia,alitaka aweke wazi kilichomuua baba wa Taifa huku akimwaga Hadharani tofauti zilizojitokeza na Ugomvi kati yake na Mwalimu kilichopelekea Mkapa kuamua na kulazmisha mwalimu apelekwe London kutibiwa(kuuwawa) huku Nyuma akimyamazisha Daktari wa Mwalimu kwa kumpa Uwaziri ili asiseme kilichotokea.

Na alisema ilikuwaje Mkapa ataje Ugonjwa wa mwalimu ili hali Daktari wake yupo?alihoji, amemwaga vitu vingi ambavyo kwa kweli vitaleta Maswali Mengi juu ya wananchi wa Tanzania na dunia kwa ujumlaa...

Nikiripoti kutoka Uwanja wa Mapambano wa Arumeru ni mimi Mgosi Mgeni wenu wa jamii Forums.


nimependa hapo penye red, Mkapa + CCM + WanaCCM wanahitaji kubuni biashara nyingine sasa, hii ya utawala imeshashindikana. Kinachofuatia ni aibu sasa!!!
 
sijaelewa hapo,......balali....???


siku ya kikao cha ccm sijui wanaita nec....lowasa aliposimama na kumnyooshea kidole kikwete na akasema ''kama mwenyekiti unabisha tumuite balali aje ili Mungu wa eliya na yakobo ajulikane, maana itachukua masaa 24 tu kwa babali kufika hapa''..unadhani lowasa alikuwa anatania? ni baada ya sentesi hiyo mkapa aliogonga meza na kumuomba mwenyekiti(kikwete) aahirishe hoja ya kuvuana gamba ......unadhani ni kwa nini mkapa aligonga meza?......ninayemzungumzia ni daudi balali na jana ameondoka hapa meryland....
 
Mkuu mimi naamini siasa hizi za maji taka zinaweza kuwa zinawasaidia CCM, sio bure kabisa, mkapa huyu huyu alifanya haya haya igunga na ccm ikapeta

Usisahau Igunga kulikuwa hakuna haya maneno mazito yaliyosemwa na Vincent Nyerere. Na huwezi kujua watu wengi watayachukuliaje? Assumptions hazina mahali kwa hili.
 
Mkuu,
Taratibu hiyo kashifa ya SFO ni serikali ya wapi iliyochunguza hilo, ama ni serikali gani ambayo imetuwekea wazi huu ufisadi?

SFO walifanya kazi yao kama kawaida, lakini serikali ya Uingereza ilipoona kwamba inaelekea kuzamishwa kwenye tope la kashfa ikaamua kusitisha zoezi hilo kwa makubaliano kwamba BAE warudishe change ya radar. Yale yale ya JK kusamehe wezi wa EPA kwa kigezo cha kurudisha walichoiba.

Serikali ya Tanzania isingeweza kufuatilia ufisadi huo kwa kuwa ni sawa na serikali yenyewe kujivua nguo mbele ya wananchi wake. Kama hizi nchi za Magharibi zinafuata sheria kikweli, basi serikali ya Uingereza ingewaacha SFO wafanye kazi yao mpaka mwisho na leo hii Chenge, Mkapa na wahindi waliopewa rushwa ya radar wagekuwa mahakamani. Ndio maana nasema kwamba serikali za Magharibi ziko kwa ajili ya maslahi yao na huwezi kusema kwamba kitu fulani HAKIWEZEKANI, never!
 
siku ya kikao cha ccm sijui wanaita nec....lowasa aliposimama na kumnyooshea kidole kikwete na akasema ''kama mwenyekiti unabisha tumuite balali aje ili Mungu wa eliya na yakobo ajulikane, maana itachukua masaa 24 tu kwa babali kufika hapa''..unadhani lowasa alikuwa anatania? ni baada ya sentesi hiyo mkapa aliogonga meza na kumuomba mwenyekiti(kikwete) aahirishe hoja ya kuvuana gamba ......unadhani ni kwa nini mkapa aligonga meza?......ninayemzungumzia ni daudi balali na jana ameondoka hapa meryland....


Nyerere angelikuwa Hai ...kuna watu ambao walilijuwa hili kuwa hawangepata wagawane huo Urais na Uwaziri Mkuu ...na laana na mikono yao iliyojaa damu..ndio zinawaandama wanashindwa kutawala nchi ,na hatuna uhakika kuwa wanafikaje 2015...na wengine wameutema uwaziri mkuu ndani ya mwaka mmoja...........
 
huyu ''mtanzania'' hawezi kuelewa lolote na nini kilikuwa nyuma ya kifo cha mwalimu...muache kama alivyo
Mkuu,
Huyu mtanzania ni mwanasiasa na aligombea Ubunge kule Kyela, nimemuuliza ana maoni gani kuhusu Afya ya Mwakyembe sijui alichojibu...

Nadhani ni mtu ambaye anajifanya kutokubali ukweli huenda kwa makusudi au vinginevyo, iwe Mkapa anahusika au ahusiki ila lazima tukiri kwamba wako watu uuawa kwa sababu za kibinadamu na vipo vifo vitokanavyo na mikono ya wanadamu, kuamini haya si lazima uwe mmoja wa watu walioenda Loliondo kwa Babu kunywa kikombe.

Na huenda Bw. Mtanzania anafurahia maradhi yaliyompata candidate mwenzake huko Kyela...
 
Dr. Mwakyusa naye anatakiwa kukaa mkao wa utayari all the times. Ninavyoamini hii issue ikishika kasi kwenye jamii, Mwakyusa ataanza kutafutwa kunyamazishwa kama yule dada aliyekwenda kumhudumia Dr. Mwakyembe pale wizarani. Alinyamazishwa within muda mfupi wakijua atamwaga ugali. Mwakyusa, be careful out there hii dhambi itawatafuna sana.
 
Back
Top Bottom