Vincent Laswai wa Kibo Palace na Trust Bureau de changes yuko matatani?

Vincent Laswai wa Kibo Palace na Trust Bureau de changes yuko matatani?

simwonei huruma haya majizi kupitia kwa wakuu, hizo bureau zilikuwa za kutakatisha pesa, sasa nchi imerudi kwenye misingi sahihi, Big up Pombe tajiri mwizi lazima aishi kama shetani
 
hakuna sababu yoyote ya msingi japo zaidi ya uonevu,kujihami na kutokujiamini kwa huyu bichwa baya a.k.a jiwe.
Ukiondolea mbali jeshi la polisi,tiss na baadhi ya watumishi wa umma, hakuna CCM..

Sure,bila hizi apparatus na state machinery hakuna CCM!

Na siku mpaka waje wagundue wanayoyafanya ni kwa ajili ya short time benefits watakua washachelewa aisee!
 
Laswai anachunguzwa kwa makosa ya kutakatisha fedha,hizo Bureau De Change zake zimefungwa kwa sababu zilikuwa zinatumika kupitisha fedha chafu kwa hiyo mnaoendekeza ukabila endeleeni tu maana akili zenu zinasoma mwisho mita 20
 
Wanajamvi,
Vincent Laswai ni mfanyabiashara maarufu sana pale Moshi. Ndiye mwenye ile Kibo Palace Arusha, mwenye Bureau de changes Moshi na Arusha ambazo zilivamiwa na jeshi kipindi kile, na hadi sasa zimefungwa. Pia ana biashara za jumla kuagiza sukari na bidhaa nyingine kama batteries nk kutoka nje.

Kuna waliokuwa wakisema hiyo Kibo Palace wako na Uhuru Kenyatta. Hoteli hiyo ni maarufu sana. Viongozi wakubwa hufikia hapo. Kuanzia kina Kenyatta, Kikwete, na hata Bernard Membe, ambaye naye inasemekana ni rafiki mkubwa wa ndugu Laswai!

Sasa mida hii ninayozungumza, maafisa usalama pamoja na askari wamezunguka biashara zake na inasemekana anatafutwa. Nadhani tayari alikuwa amesha surrender passport yake, ila kama kachomoka, pengine alikuwa na zaidi ya moja.

Kuna wanaodai kuwa kuna mipango inayoendelea dhidi ya wafanyabiashara flani, wengine wanasema ni ukaribu wake na Bernard Membe ndiyo umemponza! Amekuwa monitored na hakuwa akiweza kuongea hata kwa simu bila kufuatiliwa.

Bado nasubiria kusikia nini hatma yake. Sijui kama ni issue ya utakatishaji fedha au ni kitu gani!

Pia wamebeba computers nk, kama kuna wenye info ya kinachoendelea watueleze. Hapo chini akiwa na JKView attachment 1032828
Huyu Jamaa namkumbuka alikuja kwenye msiba wa bana yangu. Huko kaskazini kazi mnayo
 
Mfanyabiashara maarufu mjini Moshi achunguzwa

THURSDAY FEBRUARY 28 2019




swai+pic.jpg


Mfanyabiashara maarufu mjini Moshi achunguzwa
 
Huyu Jamaa namkumbuka alikuja kwenye msiba wa bana yangu. Huko kaskazini kazi mnayo
Msiba ulikuwa wapi? Ana dereva wake mmoja mnene, jamaa yeye mwembamba tu, basi wakisimama mahali, watu wanamfuata dereva wakidhani yeye ndo bosi kisa unene!😀

Ila ni kweli hii zamu ya wachagga kuishi kama mashetani!
 
Laswai anachunguzwa kwa makosa ya kutakatisha fedha,hizo Bureau De Change zake zimefungwa kwa sababu zilikuwa zinatumika kupitisha fedha chafu kwa hiyo mnaoendekeza ukabila endeleeni tu maana akili zenu zinasoma mwisho mita 20
Leo naona wamefanya na Dar ili kukwepa lawama za ukabila. Lakini kule bandarini mmeanzisha TACS kwa misingi gani?
 
Kama ndio hivyo itakuwa ni mmoja ya aliyesababisha bureau de change kufungiwa Arusha, alijipanga
Sasa naskia za Dar nazo zimefungwa na pesa wamechukuwa! Hapo unasemaje?

Mi nadhani issue ya koro show! Pesa za kigeni zimekosekana pale. Na shida ni kwamba tunaagiza almost kila kitu kutoka nje ya nchi! Hivyo dola hakuna, na kwa mwelekeo huu, tunaweza wasili Zimbabwe faster!
 
Back
Top Bottom