Viktor Orban Ashindwa Uchaguzi huko Hungary

Viktor Orban Ashindwa Uchaguzi huko Hungary

Somo kwetu kutokana na uchaguzi huu ni kuwa:
1. Hauwezi kulazumisha upendezwe siku zote. Iko siku utatoka. Huyu jamaa alibadili Katiba ili iwe vigumu chama chake kushindwa. Ametawala kibabe lakini wananchi walipomchoka wakamtema.
2. Hauwezi kuung'oa utawala uliokuwepo kwa amani kwa kususia uchaguzi. Hapa kwetu ACT wanalijua hilo lakini Chadema waliamini inawezekana. Wapinzani Hungary waliingia katika uchaguzi huku wakijua thika kwamba mazingira ya uchaguzi si rafiki. Na kuwa mpinzani wao anapendwa anapendwa na watawala wa Marekani na Urusi. Yote hayo hayakusaidia kitu. Tuliona hilo pia Zambia.
3. Lilikuwa kosa kubwa kwa Chadema kutoshiriki uchaguzi. Wangeshiriki wangekuwa katika nafasi nzuri sana kwa ajili ya chaguzi za 2029 na 2030. Wote tunajua kuwa wabunge wachache wa Chadema wanatosha sana kuwapeleka puta wabunge wa chama tawala.
4. Utawala mpya wa Hungary sasa unaweza kurekebisha uchafu wote wa utawala uliopita kwa sababu wameshika mpini. Hapa kwetu hiyo nafasi haipo.

Amandla...
 
Obran amekubali kushindwa na kuwa mpinzani.

CCM na wao wajifunze

Kwapamoja wanisiasa wanatakiwa kujifunza kushindwa!!! Kuwa mpinzani na kugombea hakuna maana ya kuwa lazima Ushinde !!!

ukishindwa nongwa unataka kuleta fujo!!!
 
Somo kwetu kutokana na uchaguzi huu ni kuwa:
1. Hauwezi kulazumisha upendezwe siku zote. Iko siku utatoka. Huyu jamaa alibadili Katiba ili iwe vigumu chama chake kushindwa. Ametawala kibabe lakini wananchi walipomchoka wakamtema.
2. Hauwezi kuung'oa utawala uliokuwepo kwa amani kwa kususia uchaguzi. Hapa kwetu ACT wanalijua hilo lakini Chadema waliamini inawezekana. Wapinzani Hungary waliingia katika uchaguzi huku wakijua thika kwamba mazingira ya uchaguzi si rafiki. Na kuwa mpinzani wao anapendwa anapendwa na watawala wa Marekani na Urusi. Yote hayo hayakusaidia kitu. Tuliona hilo pia Zambia.
3. Lilikuwa kosa kubwa kwa Chadema kutoshiriki uchaguzi. Wangeshiriki wangekuwa katika nafasi nzuri sana kwa ajili ya chaguzi za 2029 na 2030. Wote tunajua kuwa wabunge wachache wa Chadema wanatosha sana kuwapeleka puta wabunge wa chama tawala.
4. Utawala mpya wa Hungary sasa unaweza kurekebisha uchafu wote wa utawala uliopita kwa sababu wameshika mpini. Hapa kwetu hiyo nafasi haipo.

Amandla...
Kuna kitu naona huelewi hapo.

Huyo Vikter Orban ameshindwa tu kwa sababu ni mzungu ila angekuwa ni mswahili ndio amekaa madarakani kwa miaka 16 kamwe asingeshindwa na mifano ipo mingi tu.

Pili, Hungary wana tume huru ya ukweli ambayo haina machawa wa chama tawala tofauti kabisa na Tanzania ambapo kuwa mjumbe wa tume sifa kuu ni kuwa mkereketwa wa ccm au usalama wa taifa.

Tatu, nchini Hungary vyombo vyote vya ulinzi na usalama vinatumikia nchi chini ya kiapo wakati Tanzania vyombo kama hivyo ni vitiifu kwa rais na chama chake.

Kwa mantiki hiyo huwezi kabisa kulinganisha nchi za Ulaya na nchi kama Tanzania, tofauti ni kama usiku na mchana.
 
Kuna kitu naona huelewi hapo.
Nielimishe.
Huyo Vikter Orban ameshindwa tu kwa sababu ni mzungu ila angekuwa ni mswahili ndio amekaa madarakani kwa miaka 16 kamwe asingeshindwa na mifano ipo mingi tu.
Hiyo ni inferiority complex. Nchi nyingi za kiafrika zimewatoa viongozi na/au vyama vilivyotawala kwa miaka mingi. Kenya kulikuwa na KANU, Zambia UNIP n.k. Chama tawala cha Botswana cha UDC kilitokana na baadhi ya vyama vya upinzani kuungana. Chama tawala cha wakati ule cha BDP kilikuwa kimetawala toka Botswana ipate uhuru 1966 hadi kiliposhindwa 2024. Aliyeshindwa alikubali matokeo. Hao wote ni waafrika.
Rais Alexander Lukashenko wa Belarus alishinda uchaguzi kwa mara ya kwanza 1994. Hajashindwa tena uchaguzi. Na watu wengi tu wameuawa katika chaguzi za Belarus. Lukashenko ni mzungu.
Pili, Hungary wana tume huru ya ukweli ambayo haina machawa wa chama tawala tofauti kabisa na Tanzania ambapo kuwa mjumbe wa tume sifa kuu ni kuwa mkereketwa wa ccm au usalama wa taifa.
Orbàn alibadilisha sheria za uchaguzi kupendelea chama chake. Aliminya media ili nazo zipendelee chama chake. Pamekuwa na ukiukwaji wa taratibu za uchaguzi. Kilichomshinda na kumzuia kufanya upuuzi wowote ni mwamko wa raia, ambapo zaidi ya 80% walijitokeza kupiga kura. Hapakuwa na nafasi ya kuchakachua matokeo.
Tatu, nchini Hungary vyombo vyote vya ulinzi na usalama vinatumikia nchi chini ya kiapo wakati Tanzania vyombo kama hivyo ni vitiifu kwa rais na chama chake.
Viapo havijawahi kuzuia watu kufanya ubaladhuli. Mfano ni mambo yanayo endelea Marekani. Ingawa Katiba ya Marekani haimpi mamlaka Rais kutangaza vita, Trump ameiingiza nchi yake katika vita bila kibali cha Congress. Na kama rais Trump alikula kiapo kuilinda Katiba.
i
Kwa mantiki hiyo huwezi kabisa kulinganisha nchi za Ulaya na nchi kama Tanzania, tofauti ni kama usiku na mchana.
Nadhani hauzijui nchi za Ulaya. Rais wa Marekani aliposhindwa alijaribu kupora ushindi kwa hila ( alimuomba Secretary of State wa Georgia amtafutie kura ambazo zingempa ushindi) na nguvu ( aliwahimiza wafuasi wake wavamie jumba la Congress ili kuzuia kutangazwa mshindi wa uchaguzi). Na muhula huu amejaza watu ambao loyalty yao ni kwake na sio Katiba. Na kuna kitu kinaitwa gerrymandering kinaendekea ili hata kama kitapigiwa kura chache kishinde uchaguzu. Ingawa Trump ana rangi ya orange bado ni mzungu.

Ninachokisema mimi ni kuwa kuondoa utawala uliodumu kwa miaka mingi kuna hitaji uvumilivu, ushirikiano na strategy. Bahati mbaya, Chadema ya sasa haina vyote hivyo.

Naamini Chadema au chama kingine kikijipanga vizuri (na kikishirikiana na vyama vingine thabiti vya upinzani )kitaweza kuleta mabadiliko nchini.

Amandla...
 
Nielimishe.

Hiyo ni inferiority complex. Nchi nyingi za kiafrika zimewatoa viongozi na/au vyama vilivyotawala kwa miaka mingi. Kenya kulikuwa na KANU, Zambia UNIP n.k. Chama tawala cha Botswana cha UDC kilitokana na baadhi ya vyama vya upinzani kuungana. Chama tawala cha wakati ule cha BDP kilikuwa kimetawala toka Botswana ipate uhuru 1966 hadi kiliposhindwa 2024. Aliyeshindwa alikubali matokeo. Hao wote ni waafrika.
Rais Alexander Lukashenko wa Belarus alishinda uchaguzi kwa mara ya kwanza 1994. Hajashindwa tena uchaguzi. Na watu wengi tu wameuawa katika chaguzi za Belarus. Lukashenko ni mzungu.

Orbàn alibadilisha sheria za uchaguzi kupendelea chama chake. Aliminya media ili nazo zipendelee chama chake. Pamekuwa na ukiukwaji wa taratibu za uchaguzi. Kilichomshinda na kumzuia kufanya upuuzi wowote ni mwamko wa raia, ambapo zaidi ya 80% walijitokeza kupiga kura. Hapakuwa na nafasi ya kuchakachua matokeo.

Viapo havijawahi kuzuia watu kufanya ubaladhuli. Mfano ni mambo yanayo endelea Marekani. Ingawa Katiba ya Marekani haimpi mamlaka Rais kutangaza vita, Trump ameiingiza nchi yake katika vita bila kibali cha Congress. Na kama rais Trump alikula kiapo kuilinda Katiba.

Nadhani hauzijui nchi za Ulaya. Rais wa Marekani aliposhindwa alijaribu kupora ushindi kwa hila ( alimuomba Secretary of State wa Georgia amtafutie kura ambazo zingempa ushindi) na nguvu ( aliwahimiza wafuasi wake wavamie jumba la Congress ili kuzuia kutangazwa mshindi wa uchaguzi). Na muhula huu amejaza watu ambao loyalty yao ni kwake na sio Katiba. Na kuna kitu kinaitwa gerrymandering kinaendekea ili hata kama kitapigiwa kura chache kishinde uchaguzu. Ingawa Trump ana rangi ya orange bado ni mzungu.

Ninachokisema mimi ni kuwa kuondoa utawala uliodumu kwa miaka mingi kuna hitaji uvumilivu, ushirikiano na strategy. Bahati mbaya, Chadema ya sasa haina vyote hivyo.

Naamini Chadema au chama kingine kikijipanga vizuri (na kikishirikiana na vyama vingine thabiti vya upinzani )kitaweza kuleta mabadiliko nchini.

Amandla...
Una point za msingi ila kuhusu uchaguzi wa Tanzania ni maigizo matupu. Ni mtu anapanga matokeo kabla ya game.

Kwa aina ya uchaguzi wetu hata upigiwe kura namna gani huwezi kushinda.
1.Matokeo hayapingwi popote
2. Wakala anazuiwa kutoka na copy ya matokeo kwa ajili ya uhakiki.

Kama utakuwa na akili timamu na ukawaza unaweza kushinda uchaguzi wa namna hii basi una tatizo kichwani.
 
Una point za msingi ila kuhusu uchaguzi wa Tanzania ni maigizo matupu. Ni mtu anapanga matokeo kabla ya game.

Kwa aina ya uchaguzi wetu hata upigiwe kura namna gani huwezi kushinda.
1.Matokeo hayapingwi popote
2. Wakala anazuiwa kutoka na copy ya matokeo kwa ajili ya uhakiki.

Kama utakuwa na akili timamu na ukawaza unaweza kushinda uchaguzi wa namna hii basi una tatizo kichwani.
Unadhania hiyo ni unique kwa Tanzania peke yake? Unadhani walioshinda walishinda chini ya Tume Huru ya uchaguzi? Shida yetu ni kupenda visingizio na vitu vya dezo! Kwa mawazo kama hayo, CCM itaendelea kutawala milele.

Amandla...
 
Idadi ya watu Hungary ni sawa na idadi ya watu katika mikoa ya dar es Salaam na pwani tu
 
Nielimishe.

Hiyo ni inferiority complex. Nchi nyingi za kiafrika zimewatoa viongozi na/au vyama vilivyotawala kwa miaka mingi. Kenya kulikuwa na KANU, Zambia UNIP n.k. Chama tawala cha Botswana cha UDC kilitokana na baadhi ya vyama vya upinzani kuungana. Chama tawala cha wakati ule cha BDP kilikuwa kimetawala toka Botswana ipate uhuru 1966 hadi kiliposhindwa 2024. Aliyeshindwa alikubali matokeo. Hao wote ni waafrika.
Rais Alexander Lukashenko wa Belarus alishinda uchaguzi kwa mara ya kwanza 1994. Hajashindwa tena uchaguzi. Na watu wengi tu wameuawa katika chaguzi za Belarus. Lukashenko ni mzungu.

Orbàn alibadilisha sheria za uchaguzi kupendelea chama chake. Aliminya media ili nazo zipendelee chama chake. Pamekuwa na ukiukwaji wa taratibu za uchaguzi. Kilichomshinda na kumzuia kufanya upuuzi wowote ni mwamko wa raia, ambapo zaidi ya 80% walijitokeza kupiga kura. Hapakuwa na nafasi ya kuchakachua matokeo.

Viapo havijawahi kuzuia watu kufanya ubaladhuli. Mfano ni mambo yanayo endelea Marekani. Ingawa Katiba ya Marekani haimpi mamlaka Rais kutangaza vita, Trump ameiingiza nchi yake katika vita bila kibali cha Congress. Na kama rais Trump alikula kiapo kuilinda Katiba.

Nadhani hauzijui nchi za Ulaya. Rais wa Marekani aliposhindwa alijaribu kupora ushindi kwa hila ( alimuomba Secretary of State wa Georgia amtafutie kura ambazo zingempa ushindi) na nguvu ( aliwahimiza wafuasi wake wavamie jumba la Congress ili kuzuia kutangazwa mshindi wa uchaguzi). Na muhula huu amejaza watu ambao loyalty yao ni kwake na sio Katiba. Na kuna kitu kinaitwa gerrymandering kinaendekea ili hata kama kitapigiwa kura chache kishinde uchaguzu. Ingawa Trump ana rangi ya orange bado ni mzungu.

Ninachokisema mimi ni kuwa kuondoa utawala uliodumu kwa miaka mingi kuna hitaji uvumilivu, ushirikiano na strategy. Bahati mbaya, Chadema ya sasa haina vyote hivyo.

Naamini Chadema au chama kingine kikijipanga vizuri (na kikishirikiana na vyama vingine thabiti vya upinzani )kitaweza kuleta mabadiliko nchini.

Amandla...
Kwa mazingira ya Tanzania ambapo uchaguzi ni suala la kufa na kupona ili ccm iondoke madarakani lazima iwepo something close to a civil war kwa sababu ni watu ambao wako tayari kufanya mauaji ya halaiki ili tu wabakie mamlakani.

Ni kweli kwamba wenyewe kabla hata ya huo wanaouita uchaguzi kufanyika tayari wanakuwa wana matokeo nchi nzima na uchaguzi unakuwa ni kutimiza mradi tu.

Kumbuka wanaamua wawe na madiwani wangapi na wabunge wangapi na pia rais wampatie asilimia ngapi za kura na ikiwapendezea wanaamua vyama machawa wawape nini na ni hivyo hivyo kwa vitongoji, vijiji na mitaa.

So without something close to a civil war this party will continue to remain in power for foreseeable future.
 
View attachment 3571650

Uchaguzi wa Hungary umekwisha na aliyekuwa Waziri Mkuu kwa miaka 16, Viktor Orban, kipenzi cha Trump na Putin, na mwiba mkali kwa European Union na Ukraine amepigwa chini vibaya sana.

Kwenye bunge lenye viti 199, chama cha mpinzani wake, Péter Magyar, kimejizolea zaidi ya viti 135 ambayo ni zaidi ya theluthi mbili itakayowapa mandate ya kufanya mabadiliko ya katiba bila kuzuiliwa.

Kwenye uchaguzi wa mwaka 2010, chama cha Viktor Orban kilipata hiyo super majority na kubadili katiba iliyofanya awe anashinda viti hata kama anapata kura chache ikiwamo pamoja na kupunguza viti kwenye miji mikubwa ambako alikuwa na ushindani na kuongeza viti kwenye maeneo ya vijijini ambako alikuwa anawarubuni kirahisi ingawa majimbo hayo yana watu wachache kulinganisha na mjini.

Kufuatia mabadiliko hayo aliendelea kushinda mara tatu zaidi na hivyo kukaa madarakani miaka 16.

Utawala wake ulijaa rushwa na upendeleo sana huku hali ya uchumi wa nchi ikiwa inazidi kuwa mbaya siku hadi siku.

Sijui kama hilo linaweza kufanyika Tanzania.

======

Waziri Mkuu wa Hungary, Viktor Orbán, amekubali kushindwa katika uchaguzi uliofanyika Jumapili, Aprili 12, 2026, na hivyo kuhitimisha utawala wake wa miaka 16. Orbán amekiri kuwa matokeo hayo yana "maumivu" lakini yako wazi, na amesema yeye pamoja na chama chake cha Fidesz sasa watalitumikia taifa wakiwa upande wa upinzani.

Uchaguzi huo umeshindwa na chama cha Tisza, kinachoongozwa na Péter Magyar. Kwa wasiomfahamu, Magyar alikuwa mshirika wa karibu wa zamani wa Orbán kabla ya kugeuka na kuwa mkosoaji wake namba moja.

Dondoo Muhimu za Uchaguzi Huu:

Mshindi: Chama cha Tisza cha Péter Magyar kipo kwenye mwelekeo wa kupata ushindi wa kishindo (landslide victory). Kinatarajiwa kujizolea viti 137 na kupata theluthi mbili ya wingi wa wabunge (supermajority) bungeni.

Waliojitokeza Kupiga Kura: Uchaguzi huu umeweka rekodi ya kihistoria kwa kuwa na asilimia 77% hadi 78% ya watu waliojitokeza kupiga kura. Hiki ndicho kiwango cha juu zaidi katika historia ya Hungary tangu nchi hiyo ilipoondokana na mfumo wa Kikomunisti.

Vipaumbele vya Kampeni: Kampeni ya Magyar ilijikita katika mapambano dhidi ya rushwa, mageuzi ya kiuchumi, na kuboresha sekta za afya na elimu. Pia aliahidi kurejesha uhusiano mzuri kati ya Hungary na Umoja wa Ulaya (EU).

Athari Kimataifa: Kushindwa kwa Orbán kunatazamwa na wengi kama pigo kubwa kwa washirika wake wa karibu, wakiwemo Rais wa Urusi Vladimir Putin na Donald Trump wa Marekani. Kwa upande mwingine, viongozi wa Ulaya kama Ursula von der Leyen wamepongeza matokeo haya na kuyaita "wakati wa kihistoria kwa demokrasia ya Ulaya".
Pigo kwa Trump na Putin
 
Somo kwetu kutokana na uchaguzi huu ni kuwa:
1. Hauwezi kulazumisha upendezwe siku zote. Iko siku utatoka. Huyu jamaa alibadili Katiba ili iwe vigumu chama chake kushindwa. Ametawala kibabe lakini wananchi walipomchoka wakamtema.
2. Hauwezi kuung'oa utawala uliokuwepo kwa amani kwa kususia uchaguzi. Hapa kwetu ACT wanalijua hilo lakini Chadema waliamini inawezekana. Wapinzani Hungary waliingia katika uchaguzi huku wakijua thika kwamba mazingira ya uchaguzi si rafiki. Na kuwa mpinzani wao anapendwa anapendwa na watawala wa Marekani na Urusi. Yote hayo hayakusaidia kitu. Tuliona hilo pia Zambia.
3. Lilikuwa kosa kubwa kwa Chadema kutoshiriki uchaguzi. Wangeshiriki wangekuwa katika nafasi nzuri sana kwa ajili ya chaguzi za 2029 na 2030. Wote tunajua kuwa wabunge wachache wa Chadema wanatosha sana kuwapeleka puta wabunge wa chama tawala.
4. Utawala mpya wa Hungary sasa unaweza kurekebisha uchafu wote wa utawala uliopita kwa sababu wameshika mpini. Hapa kwetu hiyo nafasi haipo.

Amandla...
Kuna kitu huelewei,

Hungary na Zambia zina tume huru ya uchaguzi kwa muda mrefu tu.

Hata Zimbabwe ya Mugabe ilikuwa na tume huru ya uchaguzi, wapinzani wanashinda na matokeo yanatangazwa vizuri kabisa na tume ila Mugabe anakataa kuondoka madarakani anawaambia raia hawezi kukabidhi nchi kwa makaratasi wakati yeye aliipata kwa mtutu wa bunduki, aliposhindwa kucheza na tume baadaye ndio akaanza michezo ya kuwafanyia vurugu kubwa wapinzani mpaka wakawa hawawezi tena kushiriki uchaguzi kwa hofu ya usalama wao.

Tanzania haijawahi kuwa na tume huru ya uchaguzi.
 
Kuna kitu huelewei,

Hungary na Zambia zina tume huru ya uchaguzi kwa muda mrefu tu.

Hata Zimbabwe ya Mugabe ilikuwa na tume huru ya uchaguzi, wapinzani wanashinda na matokeo yanatangazwa vizuri kabisa na tume ila Mugabe anakataa kuondoka madarakani anawaambia raia hawezi kukabidhi nchi kwa makaratasi wakati yeye aliipata kwa mtutu wa bunduki, aliposhindwa kucheza na tume baadaye ndio akaanza michezo ya kuwafanyia vurugu kubwa wapinzani mpaka wakawa hawawezi tena kushiriki uchaguzi kwa hofu ya usalama wao.

Tanzania haijawahi kuwa na tume huru ya uchaguzi.
Voting was extended for another day after a lack of ballot papers disrupted voting,[18][19] with some voters being forced to queue overnight to cast their ballots.[20] There were reportedly delays of up to 10 hours in opposition stronghold areas.[21] The Zimbabwe Electoral Commission acknowledged the late distribution of ballot papers at some polling stations and blamed it on printing delays "arising from numerous court challenges".[22] Forty-one poll monitors were arrested during the election, being accused of illegally attempting to announce results before the state elections body.[23] Accusations of vote rigging were made by the opposition.

Hii ndio hali ilivyo sasa hivi Zimbabwe.

Nadhani hauelewi maana ya "independence". Independence sio tu kumtangaza mpinzani kuwa mshindi bali namna uchaguzi mzima ulivyoendesha. Hata Tanzania kuna wakati wapinzani walitangazwa kuwa washindi. Na hiyo ndio argument ya watetezi wa hali ilivyo Tanzania. Kuwa mbona wakina Lissu, Mbowe, Lema, Sugu, Ruge n.k. wote waliwahi kuwashinda wagombea wa chama tawala na kutangazwa washindi. Wengi tunasema kuwa kutangazwa baadhi kushinda sio uthibitisho wa uhuru wa tume ya uchaguzi.

Mara nyingi kinachotokea katika hizo nchi ulizodai kuwa zina Tume Huru za Uchaguzi ni kuwa wananchi wanalazimisha matokeo sahihi kutangazwa kutokana na wingi wao na kuonyesha kuwa hawatakubali usanii wa aina yeyote kufanyika. Imekuwa hivyo Hungary, ilikuwa hivyo Zambia, ilikuwa hivyo Malawi.

Amandla...
 
View attachment 3571650

Uchaguzi wa Hungary umekwisha na aliyekuwa Waziri Mkuu kwa miaka 16, Viktor Orban, kipenzi cha Trump na Putin, na mwiba mkali kwa European Union na Ukraine amepigwa chini vibaya sana.

Kwenye bunge lenye viti 199, chama cha mpinzani wake, Péter Magyar, kimejizolea zaidi ya viti 135 ambayo ni zaidi ya theluthi mbili itakayowapa mandate ya kufanya mabadiliko ya katiba bila kuzuiliwa.

Kwenye uchaguzi wa mwaka 2010, chama cha Viktor Orban kilipata hiyo super majority na kubadili katiba iliyofanya awe anashinda viti hata kama anapata kura chache ikiwamo pamoja na kupunguza viti kwenye miji mikubwa ambako alikuwa na ushindani na kuongeza viti kwenye maeneo ya vijijini ambako alikuwa anawarubuni kirahisi ingawa majimbo hayo yana watu wachache kulinganisha na mjini.

Kufuatia mabadiliko hayo aliendelea kushinda mara tatu zaidi na hivyo kukaa madarakani miaka 16.

Utawala wake ulijaa rushwa na upendeleo sana huku hali ya uchumi wa nchi ikiwa inazidi kuwa mbaya siku hadi siku.

Sijui kama hilo linaweza kufanyika Tanzania.

======

Waziri Mkuu wa Hungary, Viktor Orbán, amekubali kushindwa katika uchaguzi uliofanyika Jumapili, Aprili 12, 2026, na hivyo kuhitimisha utawala wake wa miaka 16. Orbán amekiri kuwa matokeo hayo yana "maumivu" lakini yako wazi, na amesema yeye pamoja na chama chake cha Fidesz sasa watalitumikia taifa wakiwa upande wa upinzani.

Uchaguzi huo umeshindwa na chama cha Tisza, kinachoongozwa na Péter Magyar. Kwa wasiomfahamu, Magyar alikuwa mshirika wa karibu wa zamani wa Orbán kabla ya kugeuka na kuwa mkosoaji wake namba moja.

Dondoo Muhimu za Uchaguzi Huu:

Mshindi: Chama cha Tisza cha Péter Magyar kipo kwenye mwelekeo wa kupata ushindi wa kishindo (landslide victory). Kinatarajiwa kujizolea viti 137 na kupata theluthi mbili ya wingi wa wabunge (supermajority) bungeni.

Waliojitokeza Kupiga Kura: Uchaguzi huu umeweka rekodi ya kihistoria kwa kuwa na asilimia 77% hadi 78% ya watu waliojitokeza kupiga kura. Hiki ndicho kiwango cha juu zaidi katika historia ya Hungary tangu nchi hiyo ilipoondokana na mfumo wa Kikomunisti.

Vipaumbele vya Kampeni: Kampeni ya Magyar ilijikita katika mapambano dhidi ya rushwa, mageuzi ya kiuchumi, na kuboresha sekta za afya na elimu. Pia aliahidi kurejesha uhusiano mzuri kati ya Hungary na Umoja wa Ulaya (EU).

Athari Kimataifa: Kushindwa kwa Orbán kunatazamwa na wengi kama pigo kubwa kwa washirika wake wa karibu, wakiwemo Rais wa Urusi Vladimir Putin na Donald Trump wa Marekani. Kwa upande mwingine, viongozi wa Ulaya kama Ursula von der Leyen wamepongeza matokeo haya na kuyaita "wakati wa kihistoria kwa demokrasia ya Ulaya".
Hiyo landslide ya Magyar (75% sijui 78%) kwa mama Dr. Samia Sululu ni cha mtoto-mama alikomba kura zote- 98.99%.
Yaani mama unaweza kusema hakuwa na mpinzani
 
Kwa hapa Tanzania mkileta nywi nywi nywi mtaliwa vichwa fasta.
Voting was extended for another day after a lack of ballot papers disrupted voting,[18][19] with some voters being forced to queue overnight to cast their ballots.[20] There were reportedly delays of up to 10 hours in opposition stronghold areas.[21] The Zimbabwe Electoral Commission acknowledged the late distribution of ballot papers at some polling stations and blamed it on printing delays "arising from numerous court challenges".[22] Forty-one poll monitors were arrested during the election, being accused of illegally attempting to announce results before the state elections body.[23] Accusations of vote rigging were made by the opposition.

Hii ndio hali ilivyo sasa hivi Zimbabwe.

Nadhani hauelewi maana ya "independence". Independence sio tu kumtangaza mpinzani kuwa mshindi bali namna uchaguzi mzima ulivyoendesha. Hata Tanzania kuna wakati wapinzani walitangazwa kuwa washindi. Na hiyo ndio argument ya watetezi wa hali ilivyo Tanzania. Kuwa mbona wakina Lissu, Mbowe, Lema, Sugu, Ruge n.k. wote waliwahi kuwashinda wagombea wa chama tawala na kutangazwa washindi. Wengi tunasema kuwa kutangazwa baadhi kushinda sio uthibitisho wa uhuru wa tume ya uchaguzi.

Mara nyingi kinachotokea katika hizo nchi ulizodai kuwa zina Tume Huru za Uchaguzi ni kuwa wananchi wanalazimisha matokeo sahihi kutangazwa kutokana na wingi wao na kuonyesha kuwa hawatakubali usanii wa aina yeyote kufanyika. Imekuwa hivyo Hungary, ilikuwa hivyo Zambia, ilikuwa hivyo Malawi.

Amandla...
 
Back
Top Bottom