Sina muda wa Salamu.
Nina hasira kichizi.
Wadau kuna hawa vijana wanaoingia na kutoka VETA huku mtaani wanafungua showroom zao za aluminium kufanya ufundi majumbani kufunga vioo kwenye madirisha.
Vijana mnapopewa kazi fanyeni kazi msilete utoto utoto na ujanja ujanja kwenye kazi ukipewa kazi hakikisha kazi imenyooka usiache kipengele chochote kwenye kazi, usipige konakona nyingi hio ni kazi kijana hio kazi inakujengea profile yako na usimfanye tajiri km fala mbumbumbu hajui kitu huyo tajiri ana wakaguzi wake wataikagua hio kazi.
Madogo wamepewa kazi wamelipwa full package yaani pesa yote mpaka na ya chakula njooni mfunge vioo kwenye madirisha. Vijana wakafika site wakaanza kufunga upande wa kwanza wa nyumba wamefanya vizuri marks 95% nikawapa.
Vijana walipohamia upande wa pili wakalipua kazi upande wote kioo ukisukuma mpaka utumie nguvu nusu kujichana mikono nusu kukipasua marks 0% kabisa.
Sasa Vijana km hawa wanapewa kazi wanalipua kazi wanataka kazi kweli? Unawapa kazi wafanye kazi vijana wanalipualipua tu kazi wanaondoka wakidhani kwamba tajiri hatokagua kazi.
Mbaya zaidi tajiri unawafuata kwa upole kabisa unawaambia vijana mmeharibu kazi kule emu njooni mrekebishe wanajibu sawa tajiri tunakuja kurekebisha sababu ya upole wa tajiri na mizunguko mingi aliyonayo vijana hawaji kurekebisha, anarudi kuuliza vijana walikuja anaambiwa vijana hawakuja kurekebisha zinapita siku 2 vijana hawataki kurekebisha kazi na pesa wamekula, vijana mnachezea kazi?
Hivi vijana hamjui kwamba unapofanya kazi nzuri kwa viwango kitaalamu yaan professional inakutengenezea uaminifu wa kazi zingine, wigo mpana wa kazi na inakujengea mtandao mzuri wa kupata kazi nyingine zaidi?
Kwanini mnachezea kazi vijana? Mnapewa kazi mnachezea kazi vijana kwanini? Kwanini mkipewa kazi mnacheza na kazi mnalipua kazi hamfanyi kazi kwa viwango vinavyotakiwa kwanini vijana mnachezea kazi?
Jirekebisheni vijana usicheze na kazi, ukipewa kazi fanya kazi tena nyoosha kazi iwe na viwango sio unalipualipua tu kisha unaondoka.