Hawa viumbe wanatesa kweli kweli, kuna mmoja hapa amechemsha kichwa changu haswa. Kuna kazi naifanya sehemu, nikiimaliza inatakiwa nitafute sehemu tulivu nikake na kujitafakari upya, huu ni ujinga kwa kweli. Unahangaika na kazi kuanzia asubuhi mpaka jioni, unakosa hata muda wa kwenda kula. Kuna mwehu mmoja anakwambia "kwanini hijanipigia simu" ukimueleza ulikuwa wapi na kwa mazingira yapi anakasirika na kukata simu, yeye akili yake muda wote anaamini unatembea unatafuta wanawake, akipiga simu hataki asikie sauti ya kike, ila wewe ukisikia sauti ya kiume kawaida.
Kama haya ndio mapenzi bora wale tunaoita, Hit and run kuliko kuonesha upendo kwa kiumbe chenye wivu uliopitiliza.
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.