Mwishowe nmewafikiaSEHEMU YA 38
“Nashukuru sana! Naomba uniitie huyo msichana, nitamlipa kiasi chochote kile,” alisema Cassian.
“Hakuna shida.”
*** Ilikuwa ni rahisi kwa Evelyne kusahau kila kitu kilichotokea katika maisha yake, kusahau tarehe ya siku yake ya kuzaliwa, kuwasahau watu waliomtendea mabaya kuliko kumsahau Cassia na mambo yote aliyokuwa ameyafanya.
Ilikuwa ni aibu kubwa, hakutoka ndani, kila alipokuwa chumbani kwake alikuwa mtu wa kulia tu, alihuzunika, aliumia moyoni mwake na wakati mwingine alihisi kwamba ilikuwa ni afadhali kujiua kuliko kuendelea kuishi.
Rafiki yake, Mwajuma ndiye aliyekuwa karibu naye, yeye ndiye aliyekuwa akimbembeleza usiku na mchana na hata msichana huyo alipotaka kufanya maamuzi magumu ya kutaka kujiua, Mwajuma alikuwa akimuokoa, alifanya hivyo mara tatu kwa nyakati tofauti.
Alimchukuia Cassian, aliilaani siku aliyokutana na mwanaume huyo, aliwachukia wanaume wote duniani hata kama wengine hawakumfanya kile alichofanyiwa na Cassian.
Alilia sana, alihuzunika mno na moyo wake kuchomwa na kitu cha moto kilichokuwa na ncha kali.
Siku zikakatika, alijiapiza kwamba ilikuwa ni lazima kulipiza kiasi kwa Cassian, kama alikuwa amemuumiza kwa staili ile na yeye ilikuwa ni lazima kumuumiza kwa pigo lenye maumivu kama lile.
Kwa mwaka mzima alikuwa chumbani, ni mara chache tu ndizo alizokuwa akitoka ndani, tena usiku, kila alipokuwa akipita kwenye mitandao ya kijamii, watu walimcheka, walimdhihaki kwa kile kilichokuwa kimetokea na hivyo moyo wake kubaki na kidonda kikubwa ambacho hakudhani kama kuna siku kingekuja kupona.
Mwajuma ndiye aliyekuwa akifuatilia kila kitu kilichokuwa kikiendelea, yeye ndiye aliyemwambia Cassian kwamba alikuwa amepata mwanamke mwingine, wa uswahilini, asiyejua hata thamani ya dola ya Kimarekani kwa pesa ya Kitanzania.
Shukrani!!!!Karibu tena mpenzi
Ebu shangaa jamani
Evelyne ni mpumbavu,eti Mungu analipia machozi yake,hovyo kabisaRoho mbaya ya Evelyine inataka kuteketeza watoto wasio na hatia!
hawa watoto wasiuliwe tu!
Yaan hapo anajua Mungu kamlipia
SEHEMU YA 42
Wakamwambia kwamba watoto wake walikuwa wazima kabisa na ili kumridhisha wakamuonyeshea picha za watoto hao ambao walikuwa wamefungwa vitambaa.
“Naomba msiwaue,” alisema mzee huyo huku akitetemeka.
“Hilo si tatizo! Unachotakiwa ni kufanya tunachotaka ukifanye,” alisema mwanaume mmoja.
Wakaanza kumwambia kile walichokuwa wakikihitaji. Alihitajika kumwambia Cassian kwamba atafute dada wa kufanya kazi za ndani ambaye huyo ndiye angekaa na watoto aliokuwa amewapata na msichana huyo hakuwa na sababu ya kumtafuta kwani walitaka kumpa wao wenyewe.
“Jamaniiii!”
“Kama hutaki basi tuwaue!”
“Naomba msiwaue!”
“Basi fanya tulichokwambia!”
Wakamwambia zaidi jinsi hali ilivyotakiwa kufanywa. Hakutakiwa kubisha, ili watoto wake wawe salama ilikuwa ni lazima kufanya kile ambacho watu hao walimtaka kukifanya. Wakakubaliana na kuondoka huku akiacha namba ya simu.
Siku iliyofuata, akapata ugeni, alikuwa msichana mwenye sura mbaya ambaye ndiye huyo aliyetakiwa kutumwa kwa Cassian kwa ajili ya kufanya kazi za ndani kumbe lengo kubwa likiwa ni kuwateka watoto hao na kwenda kuwaua.
Akampigia simu Cassian, aliongea naye kwa kirefu, akamsifia msichana huyo kwamba alikuwa mtu safi, aliyewalea watoto wake mpaka kukua.
Cassian hakuwa na hofu, alimwamini Mzee Marcus na hivyo kuhitaji kuonana na msichana huyo.
Alipomuona tu, kwa jinsi alivyokuwa, akahisi kwamba kweli huyo alikuwa mfanyakazi wa ndani na hivyo kumkaribisha kwa mikono miwili. “Unaitwa nani?”
“Sikujua!”
“Ooh! Sawa. Karibu sana mama!” alimkaribisha Cassian.
Hakukuwa na mtu aliyegundua kwamba mwanamke huyo alikuwa mbaya, wakatokea kumwamini, kila siku ilikuwa ni lazima wampe majukumu yote ya kuwalea watoto hao kitendo kilichomfanya kuwa karibu na watoto hao.
Kila siku asubuhi walikuwa wakiondoka kuelekea katika majukumu yao, nyumbani alikuwa akibaki msichana huyo na watoto hao tu pamoja na walinzi waliokuwa wakilinda mahali hapo.
Siku zilikatika, watoto wao walikuwa furaha yao kubwa, waliendelea kuwapenda, na kila siku walipokuwa wakirudi, kitu cha kwanza kilikuwa ni kuwajulia hali.