Tumosa
JF-Expert Member
- Jul 21, 2016
- 16,527
- 52,623
SEHEMU YA 53
Alisakamwa moyoni mwake mpaka akahisi maumivu mazito, akabaki akisikitika kwa kile alichotaka kukifanya.
Nguvu ya kutaka kufanya mauaji ikaanza kuondoka moyoni mwake na akajikuta akiingiwa na upendo wa hali ya juu kwa watoto wale.
“Siwezi kuwaua! Siwezi kuuawa watoto wasio na hatia,” alisema Sikujua.
Aliendelea kusubiri mpaka msafara uishe ndipo waliporuhusiwa akaliondoa gari lake mahali hapo na kuondoka.
Aliambiwa kwamba ni lazima aende akawaue watoto hao, hakutaka kufanya hivyo hata kidogo hivyo alichokifanya ni kuondoka mpaka katika soko la Mwananyamala ambapo akanunua kuku wawili na kisu kisha kuingia ndani ya gari.
Kwanza hakutaka kuondoka kuelekea baharini, alichokitaka ni kwenda kwa rafiki yake aliyekuwa akiishi Magomeni, alipofika, akamuachia watoto hao kwa lengo la kuwafuata baadaye.
“Wewe! Ndiyo watoto gani hawa?” aliuliza rafiki yake huyo huku akishangaa.
Sikujua hakuwa na jinsi, akamwambia rafiki yake huyo kila kitu kilichotokea kwamba hakutaka kuwamaliza watoto hao, alikuwa kwenye harakati kubwa ya kuokoa maisha yao hivyo ilikuwa ni lazima amsaidie kwa ajili ya kuwa nayo kwa muda wakati yeye akielekea Coco Beach kufanya kile alichotaka kufanya.
“Usichelewe,” alisema rafiki yake huyo na kuondoka.
Kidogo moyo wake ukajisikia amani, akafurahi, akawaangalia kuku wale, walikuwa wakilia, aliondoka nao mpaka alipofika Coco Beach ambapo kwa muda huo hakukuwa na watu wengi, akawachukua wale kuku, akawachinja kisha kunyunyizia damu zile ndani ya gari lile, hakuishia hapo, akawaweka katika mfuko mweupe wa nailoni ambao ulionyesha jinsi ulivyolowa damu huku ndani kukiwa na kitu, akaupiga picha, akaliacha na yeye kuondoka zake kutoa taarifa kwamba mauaji aliyokuwa ameambiwa, yalikuwa yamefanyika.
Alisakamwa moyoni mwake mpaka akahisi maumivu mazito, akabaki akisikitika kwa kile alichotaka kukifanya.
Nguvu ya kutaka kufanya mauaji ikaanza kuondoka moyoni mwake na akajikuta akiingiwa na upendo wa hali ya juu kwa watoto wale.
“Siwezi kuwaua! Siwezi kuuawa watoto wasio na hatia,” alisema Sikujua.
Aliendelea kusubiri mpaka msafara uishe ndipo waliporuhusiwa akaliondoa gari lake mahali hapo na kuondoka.
Aliambiwa kwamba ni lazima aende akawaue watoto hao, hakutaka kufanya hivyo hata kidogo hivyo alichokifanya ni kuondoka mpaka katika soko la Mwananyamala ambapo akanunua kuku wawili na kisu kisha kuingia ndani ya gari.
Kwanza hakutaka kuondoka kuelekea baharini, alichokitaka ni kwenda kwa rafiki yake aliyekuwa akiishi Magomeni, alipofika, akamuachia watoto hao kwa lengo la kuwafuata baadaye.
“Wewe! Ndiyo watoto gani hawa?” aliuliza rafiki yake huyo huku akishangaa.
Sikujua hakuwa na jinsi, akamwambia rafiki yake huyo kila kitu kilichotokea kwamba hakutaka kuwamaliza watoto hao, alikuwa kwenye harakati kubwa ya kuokoa maisha yao hivyo ilikuwa ni lazima amsaidie kwa ajili ya kuwa nayo kwa muda wakati yeye akielekea Coco Beach kufanya kile alichotaka kufanya.
“Usichelewe,” alisema rafiki yake huyo na kuondoka.
Kidogo moyo wake ukajisikia amani, akafurahi, akawaangalia kuku wale, walikuwa wakilia, aliondoka nao mpaka alipofika Coco Beach ambapo kwa muda huo hakukuwa na watu wengi, akawachukua wale kuku, akawachinja kisha kunyunyizia damu zile ndani ya gari lile, hakuishia hapo, akawaweka katika mfuko mweupe wa nailoni ambao ulionyesha jinsi ulivyolowa damu huku ndani kukiwa na kitu, akaupiga picha, akaliacha na yeye kuondoka zake kutoa taarifa kwamba mauaji aliyokuwa ameambiwa, yalikuwa yamefanyika.