Shunie
JF-Expert Member
- Aug 14, 2016
- 153,008
- 453,976
- Thread starter
- #141
SEHEMU YA 29
Bila Naseku kuingilia kati basi hali ya Cassian ingekuwa mbaya mahali hapo. Oscar alionekana kukasirika, ilikuwa ni afadhali kucheza na maisha yake lakini si kucheza na dada yake huyo aliyeonekana kuwa kila kitu.
Watu waliokuwa pembeni baada ya kuona Naseku amemzuia mwanaume huyo nao ndiyo wakaingilia na kumzuia.
Oscar alikuwa akiongea peke yake huku akiwataka watu hao wamuachie ili amuonyeshee mwanaume huyo kwamba alikuwa mtu hatari aliyekuwa akiheshima katika mtaa huo.
Muda wote huyo Cassian hakuongea kitu, alibaki akiashangaa tu, mambo aliyokuwa akiyafanya mwanaume huyo yalimshangaza lakini akazuia hasira zake kwani kama angeamua kumpoteza kijana huyo, ilikuwa ni kuongea mara moja tu na wasingemuona tena katika dunia hii.
“Mbona mnanishika! Mbona mnagombelezea bhana?” aliuliza Oscar huku akiwa ameshikwa huku na kule.
“Tulia kwanza! Utaua!”
“Mimi nataka niue sasa! Hawa mbung’o ni kuwaua tu! Kwenda kwao kuwapigia misele dada zao hawataki! Jamani si mniache! Mbona mnanishika kama mtoto wenu,” alisema Oscar huku akionekana kuwa na hasira sana.
Naseku ndiye aliyemtuliza zaidi kaka yake na kumwambia kwamba mwanaume huyo hakuwa mtu mbaya, alikuwa mtu mzuri ambaye alifika mahali hapo si kwa lengo la kumtongoza kama walivyokuwa wanaume wengine bali alikuwa hapo kwa ajili ya kumsaidia mama yao.
Kidogo hilo likamfanya Oscar kutulia. Mama yao alikuwa mgonjwa ndani, alikuwa akisumbuliwa na mgonjwa wa miguu kuvimba, alikuwa kitandani mwaka wa pili, kipindi cha nyuma walikuwa wamesumbuka kumpeleka hospitalini lakini kikafika kipindi wakatulia kwani hawakuwa na msaada wowote wa kifedha.
Kidogo Naseku ndiye aliyeonekana kuwa msaada, yeye ndiye aliyekuwa akitafuta pesa kwa ajili ya kumsaidia mama yake na hata kununua chakula cha humo ndani.
Oscar hakuwa akijali, alichokuwa akikiangalia kilikuwa ni ulevi tu. Alikuwa mvuta bhangi na mtafunaji mirungi maarufu hapo Tandale. Maisha yake yaliishia hapo, alijua kabisa kwamba mwisho wa kila kitu ilikuwa ni lazima kufa.
Bila Naseku kuingilia kati basi hali ya Cassian ingekuwa mbaya mahali hapo. Oscar alionekana kukasirika, ilikuwa ni afadhali kucheza na maisha yake lakini si kucheza na dada yake huyo aliyeonekana kuwa kila kitu.
Watu waliokuwa pembeni baada ya kuona Naseku amemzuia mwanaume huyo nao ndiyo wakaingilia na kumzuia.
Oscar alikuwa akiongea peke yake huku akiwataka watu hao wamuachie ili amuonyeshee mwanaume huyo kwamba alikuwa mtu hatari aliyekuwa akiheshima katika mtaa huo.
Muda wote huyo Cassian hakuongea kitu, alibaki akiashangaa tu, mambo aliyokuwa akiyafanya mwanaume huyo yalimshangaza lakini akazuia hasira zake kwani kama angeamua kumpoteza kijana huyo, ilikuwa ni kuongea mara moja tu na wasingemuona tena katika dunia hii.
“Mbona mnanishika! Mbona mnagombelezea bhana?” aliuliza Oscar huku akiwa ameshikwa huku na kule.
“Tulia kwanza! Utaua!”
“Mimi nataka niue sasa! Hawa mbung’o ni kuwaua tu! Kwenda kwao kuwapigia misele dada zao hawataki! Jamani si mniache! Mbona mnanishika kama mtoto wenu,” alisema Oscar huku akionekana kuwa na hasira sana.
Naseku ndiye aliyemtuliza zaidi kaka yake na kumwambia kwamba mwanaume huyo hakuwa mtu mbaya, alikuwa mtu mzuri ambaye alifika mahali hapo si kwa lengo la kumtongoza kama walivyokuwa wanaume wengine bali alikuwa hapo kwa ajili ya kumsaidia mama yao.
Kidogo hilo likamfanya Oscar kutulia. Mama yao alikuwa mgonjwa ndani, alikuwa akisumbuliwa na mgonjwa wa miguu kuvimba, alikuwa kitandani mwaka wa pili, kipindi cha nyuma walikuwa wamesumbuka kumpeleka hospitalini lakini kikafika kipindi wakatulia kwani hawakuwa na msaada wowote wa kifedha.
Kidogo Naseku ndiye aliyeonekana kuwa msaada, yeye ndiye aliyekuwa akitafuta pesa kwa ajili ya kumsaidia mama yake na hata kununua chakula cha humo ndani.
Oscar hakuwa akijali, alichokuwa akikiangalia kilikuwa ni ulevi tu. Alikuwa mvuta bhangi na mtafunaji mirungi maarufu hapo Tandale. Maisha yake yaliishia hapo, alijua kabisa kwamba mwisho wa kila kitu ilikuwa ni lazima kufa.