Viganja Mashavuni Mwangu

Viganja Mashavuni Mwangu

SEHEMU YA 44

Hakutaka kubaki kimya, alichokifanya ni kumpigia simu Cassian. Mwanaume huyo aliyekuwa ofisini alipoona simu ya mlinzi wa getini ikiingia, akaanza kuogopa, haikuwa kawaida, akili yake ilimwambia kwamba inawezekana kulikuwa na tatizo limetokea nyumbani.

Kabla ya kuipokea akaanza kujiuliza maswali mengi yasiyokuwa na majibu kwamba kabla ya kuondoka nyumbani kulikuwa na jambo baya gani lililokuwa limetokea nyumbani?

Hakuna! Sasa kwa nini mlinzi huyo alikuwa akimpigia simu? Kulikuwa na nini? Akapiga moyo konde na kupokea simu.

“Hamisi! Kuna nini?”
“Eti ulimwambia Sikujua awapeleke hospitalini watoto?” lilikuwa swali la kwanza kabisa, swali ambalo lilimshtua mno Cassian.

“Unasemaje?”
“Sikujua kawapeleka watoto hospitalini. Kachukua gari na kuondoka nalo huku watoto wakiwa humo,” alisema Hamisi maneno ambayo yalimfanya Cassian kuinuka kwenye kiti huku akionekana kuchanganyikiwa.

“Unasemaje?” aliuliza, akasimama, mwili ulikuwa ukimtetemeka na kijasho chembamba kumtoka.

**** Cassian hakuamini alichokuwa amekisikia kutoka kwa mlinzi, alimuuliza tena na tena na jibu lilikuwa lilelile kwamba dada wa kazi za ndani, Sikujua aliyekuwa akimwamini sana aliondoka na watoto nyumbani kwake, na alipokuwa ameelekea, hakukuwa na aliyepafahamu.

Alichanganyikiwa, haraka sana akakata simu na kuwapigia polisi, alipowapa taarifa, wakamwambia kwamba wangefika nyumbani kwake kwa ajili ya kuzungumza, ilikuwa ni lazima wajue ni kitu gani kilitokea mpaka mfanyakazi huyo kuondoka na watoto.

Yeye mwenye akaondoka ofisini, hakutaka kumpigia simu mke wake kwa kuona kwamba angemchanganya, ilikuwa ni lazima apambane yeye kama yeye kuona ingekuwaje ndipo amwambie mkewe kilichokuwa kimetokea.

Njiani, alionekana kuwa na mawazo mengi, alishindwa kabisa kuyazuia machozi kumtoka, moyo wake uliuma na kuchoma, kile kilichokuwa kimetokea kilikuwa kama ndoto kwake, hakuamini kama Sikujua angeweza kufanya kitu kama hicho.

Hakuchukua muda mrefu akafika nyumbani kwake, hakuliingiza gari, akateremka na kumfuata mlinzi, hata kabla hajamfikia tayari polisi wakafika mahali hapo na wote kumfuata mlinzi ambaye alianza kuhadithia kila kitu kilichokuwa kimetokea.
 
SEHEMU YA 45

Ulionekana kuwa uzembe mkubwa, ilikuwaje nyumbani kwa bilionea mkubwa kama Cassian kutokee na mfanyakazi kufanya jambo kama hilo, utekaji uliokuwa umefanyika ulikuwa ni wa kizembe sana ambao hawakuamini kama ungeweza kutokea sehemu yoyote ile.

“Inawezekana vipi?” aliuliza polisi mmoja, maelezo ya mlinzi yalionyesha tukio hilo lilikuwa la kizembe.

Kila mmoja alishangaa, walihisi kulikuwa na kitu kilichokuwa kimetokea. Walianza na mlinzi, walihisi kwamba alikuwa akijua mambo mengi kuhusu tukio hilo lililokuwa limetokea.

Alijitetea kwa upande wake kwamba hakuwa akifahamu kitu chochote kile na kwa sababu Cassian na Naseku walikuwa wakimwamini sana Sikujua, hakuwa na la kuuliza lolote lile kwa kuamini kwamba kwa kila kitu alichokuwa akikifanya kilikuwa sahihi.

“Nitamwambia nini mke wangu? Huu ni mtihani mkubwa sana kwangu!” alisema Cassian huku akionekana kuumia mno.

Simu zikapigwa, polisi wa kila kituo wakapewa taarifa juu ya kilichokuwa kimetokea. Kitu cha kwanza kabisa ambacho kwao kilionekana kuwa na uhakika wa kujua mahali watoto walipokuwa kilikuwa ni kulitafuta gari lake.

Polisi walikimbizana, kutekwa kwa watoto wa Cassian, bilionea mkubwa ilikuwa ni sawa na kutekwa kwa watoto wa rais. Polisi wakaondoka katika vituo vyao na kuingia mitaani, wakasaidiana na trafki kulitafuta gari hilo.

Hawakutaka watu wengine wafahamu kilichokuwa kimetokea, ulikuwa ni msako wa kimyakimya ambao waliamini kwamba usingeweza kuwashtua watu wengi.

Ilipofika saa 10:15 jioni, gari la Naseku likaanza kuingia mahali hapo. Kwanza hali aliyokutana nayo nyumbani ilimshtua, hakukuwa na mlinzi, geti alifunguliwa na mume wake, alibaki akijiuliza maswali mengi pasipo majibu yoyote yale.

Alimfahamu Cassian, alikuwa mwanaume mwenye furaha tele lakini kwa siku hiyo alivyokuwa akimwangalia alionekana kabisa kuwa na kitu kilichokuwa kikimtatiza moyoni mwake kwani hata tabasamu ambalo alijitahidi kumuonyeshea lilionekana kutokutoka moyoni mwake.

“Mume wangu! Kuna nini?” aliuliza Naseku huku akionekana kuwa na hofu kubwa.
“Hakuna kitu!” alijibu Cassian
 
Duh
SEHEMU YA 45

Ulionekana kuwa uzembe mkubwa, ilikuwaje nyumbani kwa bilionea mkubwa kama Cassian kutokee na mfanyakazi kufanya jambo kama hilo, utekaji uliokuwa umefanyika ulikuwa ni wa kizembe sana ambao hawakuamini kama ungeweza kutokea sehemu yoyote ile.

“Inawezekana vipi?” aliuliza polisi mmoja, maelezo ya mlinzi yalionyesha tukio hilo lilikuwa la kizembe.

Kila mmoja alishangaa, walihisi kulikuwa na kitu kilichokuwa kimetokea. Walianza na mlinzi, walihisi kwamba alikuwa akijua mambo mengi kuhusu tukio hilo lililokuwa limetokea.

Alijitetea kwa upande wake kwamba hakuwa akifahamu kitu chochote kile na kwa sababu Cassian na Naseku walikuwa wakimwamini sana Sikujua, hakuwa na la kuuliza lolote lile kwa kuamini kwamba kwa kila kitu alichokuwa akikifanya kilikuwa sahihi.

“Nitamwambia nini mke wangu? Huu ni mtihani mkubwa sana kwangu!” alisema Cassian huku akionekana kuumia mno.

Simu zikapigwa, polisi wa kila kituo wakapewa taarifa juu ya kilichokuwa kimetokea. Kitu cha kwanza kabisa ambacho kwao kilionekana kuwa na uhakika wa kujua mahali watoto walipokuwa kilikuwa ni kulitafuta gari lake.

Polisi walikimbizana, kutekwa kwa watoto wa Cassian, bilionea mkubwa ilikuwa ni sawa na kutekwa kwa watoto wa rais. Polisi wakaondoka katika vituo vyao na kuingia mitaani, wakasaidiana na trafki kulitafuta gari hilo.

Hawakutaka watu wengine wafahamu kilichokuwa kimetokea, ulikuwa ni msako wa kimyakimya ambao waliamini kwamba usingeweza kuwashtua watu wengi.

Ilipofika saa 10:15 jioni, gari la Naseku likaanza kuingia mahali hapo. Kwanza hali aliyokutana nayo nyumbani ilimshtua, hakukuwa na mlinzi, geti alifunguliwa na mume wake, alibaki akijiuliza maswali mengi pasipo majibu yoyote yale.

Alimfahamu Cassian, alikuwa mwanaume mwenye furaha tele lakini kwa siku hiyo alivyokuwa akimwangalia alionekana kabisa kuwa na kitu kilichokuwa kikimtatiza moyoni mwake kwani hata tabasamu ambalo alijitahidi kumuonyeshea lilionekana kutokutoka moyoni mwake.

“Mume wangu! Kuna nini?” aliuliza Naseku huku akionekana kuwa na hofu kubwa.
“Hakuna kitu!” alijibu Cassian
Duh Yajayo.....!!!!

Watoto wawe salama tu!
 
SEHEMU YA 46

“Unajua ni kwa jinsi gani sipendi kudanganywa mpenzi. Niambie kuna nini! Hata kama kuna kitu kinachouma mno, wewe niambie tu kwanza,” alisema Naseku huku akimwangalia mume wake huyo ambaye bado hakuonyesha furaha yoyote ile.

“Tuingie ndani kwanza!”
“Hakuna tatizo?”
“Hakuna!”
“Na mlinzi yupo wapi?”
“Tuingie ndani, tutaongea.”

Cassian akamshika mkono Naseku na kuingia naye ndani ya nyumba hiyo, walipofika sebuleni, macho ya mwanamke huyo yakatua kwa polisi wanne waliokuwa sebuleni.

Hilo lilimuogopesha zaidi, akahisi kulikuwa na tatizo kwani haikuwa kawaida kwa polisi kufika nyumbani kwake hapo.

Alitaka kujua, alihisi mapigo yake ya moyo yakiongezeka kudunda, aliogopa, aliyafumba macho yake kwa sekunde kadhaa, akamuomba Mungu amtie nguvu kwa lolote ambalo angelisikia mahali hapo.

“Mke wangu...” aliita Cassian huku akimwangalia Naseku ambaye hakujua kilichokuwa kimetokea lakini cha ajabu kabisa akaanza kulia.

Hakuweza kumwambia mke wake, moyo wake ulimuuma, alijiona yeye kuwa chanzo kwa kile kilichotokea, polisi mmoja aliyekuwa mahali hapo ndiye aliyemwambia Naseku kila kitu kilichokuwa kimetokea.

Mwanamke huyo hakuamini alichokisikia, yaani watoto wake aliowapenda kwa moyo mmoja wawe wametekwa, tena na mfanyakazi wa ndani ambaye walimwamini kupita kawaida?

“Haiwezekani!” alisema Naseku huku akilia.
Ilikuwa kazi kubwa kumbembeleza mwanamke huyo, alilia kwa uchungu mno na ni Cassian ndiye aliyekuwa mfariji wake kwa ajili ya kumbembeleza katika kipindi kigumu kama hicho alichokuwa akipitia.

“Nyamaza mke wangu! Nyamaza bebi,” alisema Cassian huku akiwa amemkumbatia Naseku aliyekuwa akilia kama mtoto mdogo.

“Watoto wangu! Watoto wangu wao wapi?” aliuliza Naseku huku akiendelea kulia m,no.

Wakati wakiwa hapo, polisi wakapigiwa simu na kuambiwa kwamba gari aina ya Range SUV lililokuwa na namba za usajili T768NYC lilikutwa katika Ufukwe wa Coco huku likiwa limetekelzwa, walihisi kwamba kama wangeanzia huko wangejua mahali watoto walipokuwa.
 
SEHEMU YA 47

“Tunakuja hukohuko” alisema polisi mmoja. Wakawaambia kilichokuwa kimetokea na hivyo wote kuondoka ndani ya nyumba hiyo. Naseku naye hakutaka kubaki, alitaka kujua kilichokuwa kikiendelea hivyo naye kuungana nao na kuelekea huko.

Njiani, hakuwa amenyamaza, bado aliendelea kulia tu. Hakukuwa na kitu alichokuwa akikipenda moyoni mwake kama watoto wake, alikuwa tayari kupoteza kila kitu lakini si kuwapoteza watoto wake aliokuwa akiwapenda mno.

Hawakuchukua muda mrefu wakawa wamefika katika ufukwe huo ambapo moja kwa moja wakaanza kulifuata gari hilo lililozungukwa na watu wengi ufukweni hapo.

Walipolifikia, wakalisogelea na kuufungua mlango wa mbele huku wakiwa na glovusi mikononi mwao, macho yao yalipotua ndani ya gari hilo hawakuweza kuamini, kulikuwa na damu nyingi katika kiti cha pembeni na nyuma picha ambayo ilionyesha kulikuwa na mauaji yaliyokuwa yamefanyika ndani ya gari hilo.

“Wamewaua watoto wangu...” alisema Naseku na kuanza kulia upya, kilio kikubwa kilichowashtua watu wote waliokuwa mahali hapo.

“Damu! Wamewaua hawa watoto,” alisema polisi mmoja, kama ilivyo kwa Naseku na Cassian, hata na yeye moyo ukaanza kuuma, ulikuwa ni ukatili mkubwa ambao hawakutakiw akufanyiwa watoto wadogo kama hao.

Je, nini kitaendelea?
 
SEHEMU YA 48

Evelyne alikuwa chumbani kwake, kichwa chake kilikuwa kikimfikiria Cassian ambaye bado aliendelea kuumiza moyo wake kupita kawaida.

Maumivu aliyokuwa nayo moyoni mwake hayakuisha na ndiyo maana kitu pekee alichokuwa akikihitaji kwa kipindi hicho ni kuwaua watoto wa mwanaume huyo.

Aliwatuma watu ambao walimwambia kwamba iwe isiwe ilikuwa ni lazima kufanikisha kile alichokuwa kikihitaji. Hilo halikuwa tatizo kwani baada ya siku kadhaa, akapewa taarifa kwamba tayari watoto walikuwa waekwishatekwa.

Moyo wake ukawa na furaha tele, akamwambia Mwajuma kwamba tayari kazi aliyokuwa akitaka kwa kipindi kirefu ilikuwa imekamilika, watoto aliokuwa akiwataka walikuwa mikononi mwake.

Mwajuma akafurahia, akaona kwamba mtihani mgumu waliokuwa nao kipindi chote ukawa umekamilika na kwa kuwa alihitaji rafiki yake awe na furaha tele siku zote, akamwambia kwamba kwamba bado alikuwa naye bega kwa bega.

“Wapo wapi tukawaue?” aliuliza Mwajuma huku akionekana kuwa na hasira kali hata zaidi ya alizokuwa nazo Evelyn.
“Subiri! Wanasema wapo njiani!” alisema Evelyne.

Alichukua simu yake na kuwapigia watu wake kwa lengo la kuwaambia kwamba hawakutakiwa kuwaua watoto hao wao bali walitakiwa kumsubiria kwani yeye ndiye aliyekuwa na jukumu la kuwamaliza kwa mkono wake.

Kila alipokuwa akipiga simu, haikuwa ikipokelewa, moyo wake ulikuwa na presha kubwa, alikuwa na kimuemue ambacho hakuwa nacho kabla. Hakuacha, muda wote alikuwa akiwapigia simu lakini majibu yalikuwa yaleyale kwamba simu haikuwa ikipatikana.

Akahisi kulikuwa na tatizo, akahisi kwamba inawezekana watu hao walikuwa wamemgeuka na ndiyo maana walizima simu zao na hawakutaka kuziwasha kwa ajili yake.

Alihuzunika, ilipofika majira ya saa sita mchana akawapigia tena, wakati huo simu ilikuwa ikiita kuonyesha kwamba iliwasha, alisubiri, haikupokelewa kwa wakakati, alikuwa na hamu kubwa, baada ya sekunde kadhaa, simu ikapokelewa na sauti ya upande wa pili kusikika.

“Samahani simu iliisha chaji,” alisema mwanaume aliyesikika upande wa pili.
“Usijali! Imekuwaje huko?” aliuliza Evelyne.
 
Mbona
SEHEMU YA 48

Evelyne alikuwa chumbani kwake, kichwa chake kilikuwa kikimfikiria Cassian ambaye bado aliendelea kuumiza moyo wake kupita kawaida.

Maumivu aliyokuwa nayo moyoni mwake hayakuisha na ndiyo maana kitu pekee alichokuwa akikihitaji kwa kipindi hicho ni kuwaua watoto wa mwanaume huyo.

Aliwatuma watu ambao walimwambia kwamba iwe isiwe ilikuwa ni lazima kufanikisha kile alichokuwa kikihitaji. Hilo halikuwa tatizo kwani baada ya siku kadhaa, akapewa taarifa kwamba tayari watoto walikuwa waekwishatekwa.

Moyo wake ukawa na furaha tele, akamwambia Mwajuma kwamba tayari kazi aliyokuwa akitaka kwa kipindi kirefu ilikuwa imekamilika, watoto aliokuwa akiwataka walikuwa mikononi mwake.

Mwajuma akafurahia, akaona kwamba mtihani mgumu waliokuwa nao kipindi chote ukawa umekamilika na kwa kuwa alihitaji rafiki yake awe na furaha tele siku zote, akamwambia kwamba kwamba bado alikuwa naye bega kwa bega.

“Wapo wapi tukawaue?” aliuliza Mwajuma huku akionekana kuwa na hasira kali hata zaidi ya alizokuwa nazo Evelyn.
“Subiri! Wanasema wapo njiani!” alisema Evelyne.

Alichukua simu yake na kuwapigia watu wake kwa lengo la kuwaambia kwamba hawakutakiwa kuwaua watoto hao wao bali walitakiwa kumsubiria kwani yeye ndiye aliyekuwa na jukumu la kuwamaliza kwa mkono wake.

Kila alipokuwa akipiga simu, haikuwa ikipokelewa, moyo wake ulikuwa na presha kubwa, alikuwa na kimuemue ambacho hakuwa nacho kabla. Hakuacha, muda wote alikuwa akiwapigia simu lakini majibu yalikuwa yaleyale kwamba simu haikuwa ikipatikana.

Akahisi kulikuwa na tatizo, akahisi kwamba inawezekana watu hao walikuwa wamemgeuka na ndiyo maana walizima simu zao na hawakutaka kuziwasha kwa ajili yake.

Alihuzunika, ilipofika majira ya saa sita mchana akawapigia tena, wakati huo simu ilikuwa ikiita kuonyesha kwamba iliwasha, alisubiri, haikupokelewa kwa wakakati, alikuwa na hamu kubwa, baada ya sekunde kadhaa, simu ikapokelewa na sauti ya upande wa pili kusikika.

“Samahani simu iliisha chaji,” alisema mwanaume aliyesikika upande wa pili.
“Usijali! Imekuwaje huko?” aliuliza Evelyne.
Mbona hatare hii sasa!!
 
SEHEMU YA 49

“Sikujua aliwateka watoto, akaondoka na gari lao kisha kwenda kuwamaliza huko, kisha akaitupa miili yao baharini,” alisema mwanaume huyo.

“Mbona hamkuniambia nije kuwaua mimi mwenyewe?” aliuliza Evelyne huku akionekana kuumia sana.

“Alihisi kwamba alikuwa akifuatiliwa, si unajua yule ni bilionea alikuwa na mkono mrefu! Aliogopa na ndiyo maana aliwamaliza.

Ngoja nikutumie picha,” alisema mwanaume huyo na kilichofuata ni kumtumia picha kadhaa zilizoonyesha wingi wa damu na kisu ndani ya gari hilo.

Kwa damu zilizoonekana tu, ilionyesha kwamba ni picha za kusikitisha, hazikuishia picha hizo bali kulikuwa na picha nyingine zilizoonyesha mfuko mkubwa wa nailoni huku ukiwa na damu nyingi kiasi kwamba hata yeye mwenyewe alisisimka.

Kilichokuwa ndani ya mfuko ule aliambiwa kwamba ni watoto, badala ya moyo wake kufurahi, akaanza kulia, picha ilimsisimua na hakuamini kwamba yeye ndiye aliyekuwa nyuma ya tukio lile.

Walikuwa watoto wadogo ambao aliamini kwamba Mungu alikuwa akiwalinda, kwa wivu wake, hasira zake akaagiza watoto hao wauawe, kweli wakauawa na kuwekwa kwenye mfuk wa nailoni.

Alishindwa kuyazuia machozi yake, akaanza kulia kwa maumivu makali kiasi kwamba hata Mwajuma akabaki akimshangaa, ilikuwaje alie na wakati yeye ndiye aliyeagiza watoto hao wauawe kama ilivyokuwa?

“Mbona unalia sasa?” aliuliza Mwajuma huku akimwangalia rafiki yake huyo.
“Inauma sana! Sikustahili kuwafanyia hivi watoto hawa.

Hivi Mungu atanisamehe kweli?” aliuliza Evelyne huku akiendelea kulia kama mtoto.

**** Aliyekuwa akisubiriwa alikuwa ni Sikujua tu, aliwapa taarifa kwamba tayari tukio la utekaji lilikuwa limefanikiwa kwa asilimia mia moja hivyo kitu pekee walichokuwa wakitaka kukiona kwa wakati huo ni watoto kuletwa na kisha wampigie simu Evelyne na kwenda kuwaua kwa mikono yake.

Muda ulikwenda lakini Sikujua hakuwa amefika, walimpigia simu mara kwa mara lakini hakuwa akipokea, walikasirika sana lakini baada ya saa moja, akawapigia yeye na kuwaambia kwamba alikuwa kwenye hatua za mwanzo za kuwaua.
“Unawaua?” aliuliza jamaa mmoja.
 
SEHEMU YA 50

“Ndiyo! Nimeanza kuwachinja kama kuku. Mtaona kwenye taarifa ya habari usiku jinsi damu zilivyotapakaa,” alisema Sikujua.

“Mmh! Sawa.”
“Nazileta maiti tu huko!” “Hapana! Hutakiwi kuzileta, kama vipi nenda nazo baharini, zitupe huko, telekeza gari halafu njoo,” alisema jamaa kwa kutoa maelekezo.

“Haina shida!” alisema Sikujua na kufanya kile alichoambiwa.
Dakika arobaini na tano baada ya kuzungumza naye na kuwaambia kwamba alikuwa kwenye hatua za kwanza za kuwaua watoto hao, Sikujua akafika nyumbani hapo, kwa jinsi alivyoonekana, hakuonekana kuwa kawaida hata kidogo.

Mikono yake ilijaa damu, macho yake yalikuwa mekundu kama mtu aliyekuwa amelia sana, hiyo iliwaonyesha kwamba wakati Sikujua akifanya mauaji hayo, alikuwa akilia kupita kawaida.

“Pole sana! Ndiyo ukubwa huo,” alisema jamaa mmoja na kumkumbatia Sikujua.
“Ila picha inatisha sana.

Ninaiona kichwani mwangu jinsi nilivyokuwa nikiwachinja, hakika picha hii haitotoka ubongoni mwangu!

Kwa nini nimewaua kinyama hivi?” aliuliza Sikujua huku akilia kama mtoto kiasi kwamba kila mmoja alikuwa akimuonea huruma.

Walichokifanya ni kuwaruhusu watoto wa Mzee Marcus kuondoka mahali hapo kwani tayari walichokuwa wamekitaka kwa muda mrefu tayari walikippata.

“Wapelekeni hao watoto wa yule mzee kwake. Tayari mchakato umekamilika,” alisema jamaa huyo na hivyo watoto hao kuchukuliwa na kurudishwa kwa mzee huyo.
****

Cassian na mkewe, Naseku hawakuacha kulia, mioyo yao ilichoma kupita kawaida na hawakuamini kama walikuwa wakipitia maisha waliyokuwa wakipitia.

Walilia mno, picha ya gari iliyokuwa ikionekana mbele yao iliwaumiza mno. Polisi wakawatoa katika eneo la tukio na kuondoka nao.

Kila mmoja alikuwa akihuzunika kwani Walter na Walker walikuwa watoto wazuri mno ambao hawakutakiwa kuuawa kikatili kama ilivyokuwa imetokea.

Wakiwa ndani ya gari ndipo kichwa cha Cassian kikakumbuka kuhusu Mzee Marcus, huyo ndiye mtu aliyekuwa amewaambia kuhusu huyo mfanyakazi na kumchukua.

Waliambiwa kwamba alikuwa msichana mwema, aliyejua kukaa na watoto, sasa ilikuwaje msichana huyohuyo aondoke na watoto wao na kwenda kuwaua kikatili.
 
SEHEMU YA 51

Hakutaka kupoteza muda, alichokifanya ni kuwasiliana na mzee huyo na kumwambia kila kitu kilichokuwa kimetokea na hivyo kutaka kuonana naye.
“Haina shida,” alisema mzee Marcus huku tayari akiwa amekwishapewa watoto wake.

Majira ya alasiri, mzee huyo akafika nyumbani kwa Cassian na kuanza kuongea naye, taarifa aliyokuwa akipewa ni kama hakuwa akiifahamu, alihuzunika mpaka machozi kumlenga, alimuonyesha Cassian kwamba kama kuchomwa kwa tukio hilo hata na yeye alikuwa amechomwa hivyohivyo.

“Yaani Sikujua ndiye amefanya haya?” aliuliza Mzee Marcus huku akionekana kutokuamini.
“Ndiyo!”
“Sikujua huyuhuyu ninayemjua?”
“Ndiyo!”

Akaanza kutokwa na machozi, maigizo aliyokuwa akiyafanya mahali hapo ilikuwa vigumu sana kugundua kwamba alijua mchongo mzima juu ya kile kilichokuwa kimetokea.

Yeye ndiye aliyetakiwa kutoa maelezo polisi juu ya msichana huyo ili polisi wajue ni kwa jinsi gani alikuwa amempata msichana huyo mpaka kumuamini na kumpelekea Cassian.

Hilo halikuwa tatizo, wakaelekea kituo cha polisi na kueleza kila kitu kuhusu msichana huyo. Kwake, alionekana kuwa mwema kwani aliwahi kuishi naye kwa miaka mingi na hakukuwa na kitu chochote kilichotokea.

“Inawezekana kuna mtu alimtuma kufanya hivi,” alisema Cassian.
“Sijui kwa kweli, ila cha muhimu ni kwamba moyo wa binadamu unaweza kubadilika muda wowote ule,” alisema Mzee Marcus.

Alikuwa akimheshimu sana, hakutaka kuwaambia polisi wamshikilie bali aliamua kuwaambia kwamba wafanye kila linalowezekana mpaka maiti za watoto wake zinapatikana ili kama kwenda kuzizika, basi azizike kwa mkono wake.

Wakaondoka, nyumbani, bado maombolezo yalikuwa yakiendelea, kila mmoja alikuwa akilia sana, walihitaji kuziona maiti hizo, walijua kwamba wangeumia sana lakini hawakuwa na jinsi, siku ya kwanza ikakatika, ya pili mpaka ya tatu bado maiti hizo hazikuwa zimeonekana.

Je, nini kitaendelea?
 
SEHEMU YA 52

Sikujua alikuwa ndani ya gari, watoto walikuwa pembeni yake, alikuwa akiwaangalia huku moyo wake ukimwambia kwamba siku hiyo alitakiwa kufanya kila liwezekanalo kuhakikisha watoto hao wanauawa mikononi mwake.
Moyo wake ulidhamiria kuua kwa asilimia mia moja, kutoka hapo Mbezi Beach mpaka Mwenge hakukuwa mbali sana kwa kuwa tu hakukuwa na foleni kubwa, aliendesha huku akili yake ikijifikiria ni kwa namna gani alitakiwa kuwamaliza watoto hao ambao wala hawakuwa wakilia, ndiyo kwanza walikuwa wakicheka pale walipokuwa kana kwamba walikuwa wakienda kununuliwa nguo za sikukuu.
Gari lilipofika Makongo, likasimamishwa na msafara wa rais uliokuwa ukipita maeneo ya Mwenge. Alikasirika, alitaka kuwahi kuwamaliza watoto hao kwani iwe isiwe ilikuwa ni lazima kuwamaliza siku hiyohiyo.
Aliangalia huku na kule, magari mbalimbali yaliyokuwa katika msafara wa rais yalikuwa yakiendelea na safari ya kuvuka katika mataa ya Mwenge. Alitulia garini lakini alipoyarudisha macho yake kwa mapacha wale waliokuwa katika kiti cha mbele, kitu cha ajabu kabisa kikaukumba moyo wake, kitu ambacho hakuwahi kukifikiria kama kingemjia moyoni mwake hasa katika kipindi kama hicho.
Moyo wake wa kikatili, ukaingiwa na huruma nzito kiasi cha kumfanya kukosa amani kabisa. Kila alipokuwa akiwaangalia watoto wale, akahisi moyo wake ukisinyaa kabisa.
Akaanza kujuta kwa uamuzi aliochukua wa kukubali kuwateka watoto wale, akabaki akilengwa na machozi, mbele yake akawaona watu wengi wakiwa wamesimama wakimwangalia, wote hao walikuwa wakimlaumu kwa uamuzi aliotaka kuuchukua kipindi hicho.
Alijishangaa, hakuwa hivyo, hakuwa na hali hiyo tangu azaliwe, ni kitu gani kilichokuwa kikimfanya kuingiwa na huruma ya ghafla hivyo. Mbali na huruma hiyo akaanza kuisikia sauti moyoni mwake ikimlaumu kwa kile alichotaka kukifanya kwamba kwa nini aliuruhusu moyo wake kutaka kuwaua watoto wale, malaika wa Mungu ambao hawakuwa na hatia yoyote ile.
 
Back
Top Bottom