Vidonda vidogo mdomoni (Aphthous Mouth Ulcers)

vidonda mdomoni.jpg

VIDONDA vya Kinywa ni michubuko inayotokea kwenye mdomo na ulimi. Vidonda hivi katika kinywa husababisha mhusika kupata maumivu kwa maana kinywa ni moja ya sehemu ya mwili yenye mishipa mingi ya fahamu na wakati mwingine vidonda katika kinywa husababisha kushindwa kuongea vizuri.

Ingawa vidonda hukufanya ujisikie vibaya, huwa vinapona vyenyewe ndani ya wiki moja au mbili. Vidonda vya Kinywa hutokea kwenye au ndani ya mashavu, midomo (lips), ulimi, kingo na kuta za meno pia huweza kusambaa mpaka kwenye koromeo ikiwa havitatibiwa kwa wakati.

Aina za Vidonda vya Kinywa

Vidonda vya mdomo huwa vya duara na hutokea ndani ya kinywa, kwenye ulimi na midomo. Vinaweza kuvimba na kuwa vyeupe, vyekundu au vya kijivu. Inawezekana kuwa na kidonda kimoja au zaidi wakati mmoja na kusambaa ndani ya kinywa.

Soma zaidi hapa=> Chanzo na Jinsi ya Kuzuia Vidonda vya Kinywa! | Fikra Pevu
 
Wakuu poleni kwa majukumu!

Nimekua nikipata hili tatizo tangu nikiwa shule hasa wakati wa mitihani
na kipindi hiki limenitokea tena

ni vidonda vidogo kama vipele vinavyonitokea wakati nina axienty au stress-msongo wa mawazo na hupotea vyenyewe baada ya siku 4 mpaka 5
je kuna mtu anayepatwa pia na hali kama hii?

je nini chanzo cha hili tatizo?

nini matibabu yake?

ni tatizo la kawaida au inanipasa kumuona daktari?
 
Ushauri kapime uwingi wa damu(hb) and if u dont mind pima damu kubwa...matibabu yake Nysation oral suspension il kapme kwanza ivo vipimo..poole
 
Inaumiza kidogo Boss!

huweza kunitokea mpaka
mara 3 mpaka 4 kwa mwaka

nimeona nitafute namna ya kuimaliza

Mbona mara tatu au nne kwa mwaka si mbaya kivile.

Hivyo huwa ni vidonda vya homa inayoweza kusababishwa na msongo wa mawazo au mazonge.

Ni hali ya kawaida sana maishani.

Na sidhani kama unaweza kuimaliza kwa sababu kwenye maisha hali za msongo wa mawazo na mazonge ni za kawaida sana kwa watu wengi.

Na hata ukienda spitali kumwona tabibu sanasana atakachokuambia ufanye ni kuongeza ulaji wa matunda yenye vitamini C ingawa hiyo nayo si tiba.

Pengine unachoweza kujitahidi kufanya ni kuangalia nini maishani mwako ambacho hukuletea hizo hali na kujaribu kufanya mabadiliko kidogo.

Zaidi ya hapo, hivyo vidonda ni kama mafua. Havina tiba. Huja na kutoweka vyenyewe tu.
 
Ushauri kapime uwingi wa damu(hb) and if u dont mind pima damu kubwa...matibabu yake Nysation oral suspension il kapme kwanza ivo vipimo..poole

Shukrani Mkuu
hapo kwenye damu kubwa
ni pa muhimu sana
 
Mbona mara tatu au nne kwa mwaka si mbaya kivile.

Hivyo huwa ni vidonda vya homa inayoweza kusababishwa na msongo wa mawazo au mazonge.

Ni hali ya kawaida sana maishani.

Na sidhani kama unaweza kuimaliza kwa sababu kwenye maisha hali za msongo wa mawazo na mazonge ni za kawaida sana kwa watu wengi.

Na hata ukienda spitali kumwona tabibu sanasana atakachokuambia ufanye ni kuongeza ulazi wa matunda yenye vitamini C ingawa hiyo nayo si tiba.

Pengine unachoweza kujitahidi kufanya ni kuangalia nini maishani mwako ambacho hukuletea hizo hali na kujaribu kufanya mabadiliko kidogo.

Zaidi ya hapo, hivyo vidonda ni kama mafua. Havina tiba. Huja na kutoweka vyenyewe tu.
Shukrani sana
umenipa nguvu kubwa ya kua ni hali ya kawaida Mkuu...haya maisha siku hazifanani

mipango isipotimia mtu unanyongonyea sana na kuhisi kila kitu kitakwama mwisho wake ni haya maradhi

Ahsante-It's means a lot!
 
Wadau habarini za jioni.

Jamani naombeni msaada kwani ninasumbuliwa na tatizo la vidonda vya mdomoni nimekwenda sana hospitali huwa wananipa dawa zilezile mara vitamin B mara dawa za droppers kiufupi vinanisumbua kuna kipindi nilikuwa natumia kula machungwa pamoja na leya yake ya ndani ile nyeupe angalau ilinisaidia lakini sasa machungwa hayapatikani vimenirudia tena vinanisumbua mno, naombeni msaada wa mbadala wa dawa nilizozizoea.

Ahsanteni sana!
 
mdomo upi??? maana hata uke some time una mdomo hadi mashavu!

kama ni mdomo wa chakula hivo vidonda vipo ndani ya mdomo kwa juu kwenye fiz au ulimi au nnje kwenye lips
 
mdomo upi??? maana hata uke some time una mdomo hadi mashavu!

kama ni mdomo wa chakula hivo vidonda vipo ndani ya mdomo kwa juu kwenye fiz au ulimi au nnje kwenye lips

OK mkuu ni mdomo wa chakula na vidonda vipo ndani ya mashavu , kwenye lips kwa ndani kidogo kabla ya kutoka nje. Kiufupi kwenye ngozi laini ya ndani ya kinywa.
 
Wadau habarini za jioni...!!!
Jamani naombeni msaada kwani ninasumbuliwa na tatizo la vidonda vya mdomoni nimekwenda sana hospitali huwa wananipa dawa zilezile mara vitamin B mara dawa za droppers kiufupi vinanisumbua kuna kipindi nilikuwa natumia kula machungwa pamoja na leya yake ya ndani ile nyeupe angalau ilinisaidia lakini sasa machungwa hayapatikani vimenirudia tena vinanisumbua mno, naombeni msaada wa mbadala wa dawa nilizozizoea.
Asanteni sana....!!!!
Nitafute mimi kwa wakati wako nipate kukutibia upate kupona.
Ukiwa na Shida yoyote ile
Unaweza kunitafuta kwa Mawasiliano MziziMkavu Email barua ya pepe. fewgoodman@hotmail.com What's App na Viber +90534450816
 
Wakuu habarini,,jbo hili limekuwa linanikera sana maana kila inapotokea nimepata homa,iwe malaria au taifod bas nikinywa dawa nikianza kupata nafuu bas lazima nitoke kidonda kwenye lips za mdomo je hii inatokana na nn,,na nifanyaje ili kuiepuka maana zaman sikuwa hivyo
 
Salama mkuu hilo tatizo husababishwa na herpes simples virus Type 1 ni kirusi ambacho hujificha kipindi mfumo wako wa ulinzi unapokua vizuri ila unaposhuka àidha kwa kupata stress au homa Kali na kadhaalika hao jamaa wana amka na kuleta hivyo vijidonda hapo.
 
tunkamanin! sasa nn tiba ya iyo kitu jamaa aliyouliza? maana hata mm nimekuwa victim sana wa ilo tatizo ivyo tufanyeje ili tuweze kudhibit hali iyo? mm vinanitoka kwenye ulim mpaka nashindwa kula
 
Mara nyingi magonjwa ya virus ni auto limited yanapona yenyewe. Ila itakubidi uwe na subira tu kama dawa waweza tumia kina acyclovir na jamii yake sinasaidi kupunguza kasi na inazuia usiwaambukize wengine, kwa maelezo zaidi muone daktari.
 
huu ugonjwa umekuwa nami kwa miaka tangu nikiwa mdogo unakuja na kuisha, mara ya mwanza kabisa ilinitokea kipindi nikiwa mdogo nilikuwa nimeweka waya mdomoni mdogo wangu pasipokujua akachomeka kwenye socket ya umeme, nilipigwa soti vikawa vinakuja na kuisha. ila kwa sasa kimekuja kimoja kikubwa kwenye ukingo wa shavu kwa ndani (kwenye meno ya mwisho) yani nikifumba mdomo kama nataka kutafuna nang'ata hcho kipele kikubwa. kinauma sana sana hadi nakosa amani. naombeni msaada wa sababu pamoja na tiba plz japo jana nimenunua medioral pamoja na vitamin B complex natumia.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom