Video ya ng'ombe, Pundamilia na Binadamu Ngorongoro itufundishe Maasai wana haki ya kuishi

Beatrice Kamugisha

JF-Expert Member
May 18, 2019
762
6,980
Maulid Kitenge na Mzee wa Kaliua mmefanya Kubwa sana kutetea uhai wa watoto wa Kimasai. Natambua Binadamu wabinafsi awatawaelewa na Binadamu wanafiki watawaambia na kuwadanganya kwamba Masai anatakiwa kuishi na wanyama Ngorongoro kama kivutio Cha utalii na kwamba Masai ni Moja ya factor iliyochangia Ngorongoro kuingia kwenye maajabu ya Dunia.

Naomba wanaowashambulia na kuwatisha watuambie ni nani Kati Yao anaweza akamwacha mwanaye anachunga ng'ombe ndani ya eneo lenye wanyama wakali kisa anawafurahisha watalii? Ni nani Kati Yao yupo tayari japo kushuka Ngorongoro nakutembea kwenye hifadhi akipishana na wanyama kama tunavyotaka maasai wafanye? Nani baina Yetu angependa kuishi nyumba za tembe ambazo jua na baridi ni Yako?

Mlichokifanya ndicho kilipaswa kufanywa na activists wengi wa nchi na Dunia. Walipaswa kutambua na kueleza Dunia kwamba mambo mawili lazima yafanyike. Moja kumtaftia Masai eneo la ufugaji au kuwawekea mazingira wanyama wasikutane na Maasai Kwa kuongeza eneo la ufugaji na kupunguza eneo la mbuga.

Kwanini nawapongeza Wanahabari hawa?
1. Kwanza wamesimamia kutetea haki ya kuishi ya wanadamu waliopo mbugani. Hii ni haki ya msingi inayotambulika Duniani. Hakuna mwandamu Wala serikali inapaswa kudhulumu haki ya kuishi. Je, Kwa miaka yote ambayo Ngorongoro imekuwepo wamekufa Watu wangapi Kwa kuvamiwa na wanyama?

2. Kitenge na Mzee wa Kaliua wamesimama kuieleza Dunia kwamba watoto Wana haki yakupata elimu. Hii ni haki ya msingi Kwa watoto. Kama serikali n wadau wengine wanathamini haki za Binadamu haki ya elimu Kwa watoto wanaozaliwa mbugani Nani anailinda?

3. Kitenge na Osca wameieleza na kuikumbisha Dunia kwamba iache kutumia ujinga wa fikra na kukosa elimu kwa wamasai kama kigezo Cha kuwasubject kwenye hatari ya wanyama wakali. Leo mchukue masai wa DSM au aliyesafiri kwenda nje then mpeleke akafuge ng'ombe kule mbugani kama atakubali. Lazima tukubali kwamba kinachowasukuma Masai kutoogopa wanyama SIYO Jambo jingine Bali ni ujinga. Hata Sisi wengine mababu zetu walizaliwa maporini Lakini kadri walivyopata uelewa walijitenga na wanyama.

4. Wameikumbusha serikali kuacha siasa na maisha ya Wamasai , waje na Suluhu. Walichukilie suala la loliondo na Longido kwa uzito wake. Wawekeze kulinda uhai wa Masai, wawekeze fedha za utalii kujenga Shule. Inatia simanzi eneo ambalo nikivutio cha utalii linakuwa maskini wakati fedha zinazozalishwa ni nyingi mno. Hakuna Masai anaweza akaondokana na umaskini kwa aiana ya ufugaji wanaofanya Ngorongoro. Hakuna mkulima atatoboa. Serikali ichukue fedha ajenge miundombinu ya kuwakwamua Hawa Binadamu kwenye vifo vinavyoepukika. Tuache kuwafanya wanadamu wenzenu vivutio vya utalii Kwa umaskini na ujinga wao.

Hongera Osca na Kitenge, mtapigwa Mawe Lakini wanaowapiga mawe wakumbuke uhai wa Binadamu ni zaidi ya historia.

Wanaowapiga mawe watambie Masai wana haki ya kuishi salama na kupata elimu pamoja na huduma za afya. Tuache siasa na maisha ya ndugu zetu WASIO na elimu.
 
Na waganda wanaoishi na wanyama kwenye Queen Elizabeth National Park huko Uganda nao ni wajinga kama wamasai ?Acha tutafuta easy solutions kwa a delicate na difficult situation ya wanyama na binadamu ku co-exist kwenye hifadhi mbalimbali.Human Wildlife Conflicts (HWC) ni tatizo la kidunia. Cheap popularity isitubebe. Eti wamasai wamevamia?
 
Usichojua ni kwamba hao wamasai hawajaanza kuishi hapo jana na muingiliano wao na wanyama hujaanza juzi.

Na kingine ni kwamba ngorongoro ni conservation area.

Usichojua ni kwamba wamasai wameishi hapo hata kabla ya hao wanyama hawajaja kuweka makazi hapo.
 
Afadhali kidogo documentary ya Dar24media ilijaribu kujadili tatizo hili kisomi.

Hawa makanjanja wawili wametafuta cheap popularity huku hawajafanya homework ya kujua tatizo haswa la Hifadhi ya Ngorongoro ni nini?

Nawashauri wajipange upya na kama walienda kama watalii wa ndani, basi waendelee na utalii wao wa ndani.

Tatizo hilo ni complex halihitaji majibu rahisi wala hoja nyepesi.
 
Tatizo ni siasa za kivyama zinazowanifaisha wachache na kuwaumiza wengi.

Sidhani kama Mbunge wa Ngorongoro anaishi hapo na familia yake au anaweza kuishi hapo na watoto wake wakafanya hizo shughuli za kuchunga ngombe ili kuwafurahisha Mabeberu wanaokuja kufurahisha nafsi zao Kwa kuwaona wanyama na binadamu walionyimwa Elimu wakiishi pamoja .

Binadamu yeyote ukimnyima Elimu na mawasiliano kama kusafiri na kuona maendeleo na kujifunza Dunia inakoelekea basi unamfanya awe sawa na mnyama.


Miaka 50 ijayo hapo patakua na kundi la watu watakaokuwa wanakalamika kuwa Babu zao walitengwa na kunyimwa Elimu. Kama ilivyokua Kwa wafugaji wengine na wavuvi ambao mkoloni alipokuja wakikata kupeleka watoto shule na kuwapeleka kuchunga ngombe. Matokeo yake walipozidi kuzaana bila mpangilio wakajiona hawana ardhi ya kutosha kufuga na hawawezi kuendelea kukaa Eneo moja. Wakienda maeneo ya wengine wanaanzisha vita ili kuendelea na Mila zao za kujichanganya na wanyama matokeo yake wanajichanganya na wakulima .

Utasikia kule bungeni mnafiki akisema kwa sauti kubwa kabisa ,"Wale ni Wapiga kura wangu wasisumbuliwe".Wakati mnafiki hakai hapo Wala watoto wake Wala wajukuu zake na kizazi chake kamwe hakitakuja kukaa pale. Anapata kura za kitalii.

Kwanza
Ningekuwa Mkuu wa machifu ningefanya yafuatayo: -
Ningempiga chini Mbunge yeyote wa chama ambaye angeleta siasa kwenye uchumi wa nchi na maendeleo ya watu katika Karne hii.

Pili.
Ningeweka mpango mkakati wa miaka 20 ambapo ingekua ni lazima kila Familia ya kimaasai isomeshe mtoto mmoja kwenye fani ya mifugo mpaka level ya Chuo kikuu.
Watoto wote wa kimaasai ingekua ni lazima wasome vyuo vya jamii vinavyotoa fani ya mifugo kwa ngazi ya cheti hata kama ameishia darasa la Saba.
Baada ya hapo kila Mwaka pangekua na safari za Wamasai na familia zao kwenda Denmark kujifunza na kuona jinsi Mabeberu wanavyofuga kisasa na wanavyoishi maisha ya kitajiri Kwa kutumia mifugo michache yenye tija.

Hakuna Mmaasai atakayetoka ulaya kutembea atarudi na kufurahi kukaa kwenye nyumba ya tembe. Hakuna Mmaasai atarudi kutoka kwenye ziara ulaya na kufurahi kusubiri watalii wakizungu watupe chipa za maji ili waokote kwenda kuwekea mafuta ya taa.
Hakuna Mmaasai atatoka ziarani Denmark halafu aendelee kufurahia mifugo inayotoa nusu Lita ya maziwa. Hakuna Mzazi atakayetaka kukosa fursa ya mtoto wake kwenda kutembelea Denmark kujifunza ufugaji.
Miaka 30 ijayo mbele tungekua tumebadili fikra za kijinga za kuwaacha binadamu wenzetu waishi maisha ya kijima Kwa sababu TU ya kukosa Elimu na exposure ya Dunia yenye maendeleo makubwa ya kiuchumi na kijamii.
Chifu wa kimaasai aende Denmark ashukie hoteli nzuri na mama yoyo wa kimaasai.
Kesho mama yoyo akirudi hawezi kukubali kuendelea na maisha ya kulala na ngombe kwenye ngosi ya punda na nyasi badala ya godoro.

Tatu .
Ningeweka mkakati wa Kupiga marufuku ufugaji wa kuhamahama ndani ya hifadhi.
Mifugo ingetakiwa ibaki michache kwenye Eneo dogo.
Pawe na shule ya kisasa inayofundisha mitaala ya kimataifa. Inadhaminiwa na mamlaka ya hifadhi ya ngorongoro. Wakifaulu wanapekekwa shule za kimataifa na kupata scholarship kusoma nchi za ulaya,china na Canada.

Huu ujinga wa kuwatumia Watu waliokosa fursa ya Elimu Kwa manufaa ya kisiasa na kujipatia pesa kupitia NGOs za kujifanya zinatetea haki za wafugaji zingekwesha na Wamasai wangekua ni watu wanaozakisha maziwa na nyama na kuuza nje ya nchi kisasa mana ni asili yao kufuga na wangekua wanafuga kisasa kabisa na wangeishi maisha Bora sana.

Nne.
Ningehakikisha kuwa maeneo ya wafugaji yanatengwa nchi nzima na kupeleka magreda yasawazishe maeneo ya kupanda majani ya mifugo na kujenga majosho na mabwawa ya maji ya kuhifadhi maji wakati wa mvua kuabiliana na ukame.

Uzalendo wa kweli kwa kila mtanzania ni jukumu la kila mmoja.Sio uzalendo wa kujipatia kura kitapeli na kinafiki.
Usilotaka kufanyiwa usimganyie mwenzako.
Kama hupendi mtoto wako Aishi na pundamilia badala ya kwenda shule basi na wa mwenzako pia asiwe kama mnyama ili kufurahisha Watalii.
 
Kuna watu humu na wengine nawaona tweeter wanatokwa povu na hii issue ila sasa najaribu kuwauliza "Wakurya na waikoma walikuwa wakiishi ndani ya hifadhi ya Serengeti but waliondolewa" leo masai ndiye anaonekana anaonewa.

Na kuna jamaa msomi wa sheria huko twitter anaandika kama siyo msomi, but mdau hapo juu 1000 digits asante umenena jambo kubwa.
 
Jamii nyingi za kifugaji kwa kawaida yao huwa hawapendi kusoma wala kusomea watoto wao
Wao dili zao ni kuozesha watoto wa kike tena wakiwa wadogo kwenye ndoa za mitala ili wapate ng'ombe
Na kuoa wake wengi ili wapate watoto wengi (man power) ya kuchunga mifugo yao
Wewe kama hujui basi tembea uone
 
Ningeweka mpango mkakati wa miaka 20 ambapo ingekua ni lazima kila Familia ya kimaasai isomeshe mtoto mmoja kwenye fani ya mifugo mpaka level ya Chuo kikuu.
Nani kakwamnia familia nyingi za kimasai hazijasomesha watoto mpaka chuo kikuu.? Mnaishi wapi ninyi? Lubega zivaliwazo zisikuchanganye, kuna kujielewa huku kusikomithilika.
 
Yani una akili mpaka zinamwajika. Akili kubwa Sana wewe
emoji106.png
emoji106.png
 
Kuishi na wanyama wakali hatari. wafugaji wakubali tu kutoka mbugani
Hilo swala linahitaji umakini mkubwa. Ile ni "conservation area". Wananchi hapo hawaelewi nini maana yake, Kisha hao wamasai wapewe Elimu, itafutwe muafaka ambao utaleta faida Kwa serikali na hiyo jamii ya wamasai. Amani na mshikamano ndo liwe lengo kuu.

Ni wazi kwamba hata kama Ile ni conservation area Kuna kasoro na dosari nyingi Sana zimejitokeza. Mfano hilonla watoto kuwa wachungaji, mara kadhaa watoto wa kimasai wameliwa ama kujeruhiwa na wanyama wakali.
Wapo watu wanawatumia kupata fedha, mfano kwenye zile boma za wamasai wanaendaga wazungu, je zile fedha zinawanufaishaje Hawa wamasai?? Na hizo NGO zilizoanzishwa kwa utitiri zinanufaisha hii jamii ya wamasai?

JMABO LIFANYIKE, KIKUBWA ELIMU NA ELIMU IWE YA MTAA NA YA DARASANI
 
Usichojua ni kwamba hao wamasai hawajaanza kuishi hapo jana na muingiliano wao na wanyama hujaanza juzi.

Na kingine ni kwamba ngorongoro ni conservation area.
Usichojua ni kwamba wamasai wameishi hapo hata kabla ya hao wanyama hawajaja kuweka makazi hapo.
Tatizo sio kuishi, population yao inaongezeka day to day na wanyama wa kufugwa the same.
More population inaongezeka, watahitaji makazi zaid, means ongezeko la nyumba.
Wanyama pori watazidi kusogezwa nje na hifadhi kuwa ndogo in the name of ongezeko la makazi.

Ongezeko la makazi means watazidi ku expand na ku cover more space, mwishowe kutakuwa na mji katikati ya mbuga which not a good idea.
 
Tatizo sio kuishi, population yao inaongezeka day to day na wanyama wa kufugwa the same.
More population inaongezeka, watahitaji makazi zaid, means ongezeko la nyumba.
Wanyama pori watazidi kusogezwa nje na hifadhi kuwa ndogo in the name of ongezeko la makazi.

Ongezeko la makazi means watazidi ku expand na ku cover more space, mwishowe kutakuwa na mji katikati ya mbuga which not a good idea.
jaribu siku moja uje Arusha utembelee ngorongoro
 
Back
Top Bottom