Ndahani
Platinum Member
- Jun 3, 2008
- 18,158
- 9,181
Ni kweli kitendo cha kuwatia kizuizini miaka na miaka bila mashitaka mashehe wa Zanzibar wasiotaka Muungano ni kitendo cha kionevu na kifashisti. Wengine tunakubaliana kabisa na Edward Lowassa, tunakemea na kulaani kurudi kwa political prisoners ambao walishatoka magerezani toka JKN anatoka madarakani miaka ya 80.
Lakini katika kutetea mashehe hao, Lowassa amevuka mipaka kwa kiasi cha kutisha. Lowassa ameombea zirudi siku zile za taharuki za siasa za kidini zilizokuwepo enzi za Ally Hassan Mwinyi na Benjamin Mkapa, mpaka ikafikia kudhibiti hali ile kwa kutumia watu wa usalama na askari wenye mbwa kuingia misikitini kusikiliza mawaidha na kukamata watu. Lowassa anataka misikiti na mashehe radical and firebrand wa enzi zile warudi kwa sababu misikiti siku hizi imekuwa baridi.
Lakini uchochezi wa kijahili na mbaya kuliko wote ambao usingeutegemea kutoka kwa Edward Lowassa ni pale aliposema WAISLAMU SASA WAANZE KUONGEA LUGHA AMBAYO SERIKALI INAIELEWA.
Lugha ya Waislamu ambayo serikali itailewa ni ipi, kujilipua? Muhimu tukumbuke hapa pakiwaka hapa sio wewe wala mimi wala Lowassa wala Magufuli wala Shehe wala Kadinari wala polisi wala majeshi yeyote atakaekuwa na hakika ya kubaki salama.
Lugha gani unapoteza muda wako bure. Tanzania ni kubwa kuliko individuals wachache wenye agenda za kutisha