Mmawia
JF-Expert Member
- Aug 20, 2013
- 123,237
- 98,199
Ni kweli kitendo cha kuwatia kizuizini miaka na miaka bila mashitaka mashehe wa Zanzibar wasiotaka Muungano ni kitendo cha kionevu na kifashisti. Wengine tunakubaliana kabisa na Edward Lowassa, tunalaani na kukemea uwepo wa political prisoners ambao walishatoka magerezani toka JKN anatoka madarakani miaka ya 80.
Lakini katika kutetea mashehe hao, Lowassa amevuka mipaka kwa kiasi cha kutisha. Lowassa ameongelea vurugu na taharuki za siasa za kidini zilizokuwepo enzi za Ally Hassan Mwinyi na Benjamin Mkapa, mpaka ikafikia kulazimika kudhibiti hali ile kwa kutumia watu wa usalama na askari wenye mbwa kuingia misikitini kusikiliza mawaidha na kukamata watu. Lowassa anataka misikiti na mashehe radical and firebrand wa enzi zile warudi kwa sababu misikiti siku hizi imekuwa baridi.
Lakini uchochezi wa kijahili na mbaya kuliko wote ambao usingeutegemea kutoka kwa Edward Lowassa ni pale aliposema WAISLAMU SASA WAANZE KUONGEA LUGHA AMBAYO SERIKALI INAIELEWA.
Lugha ya Waislamu ambayo serikali itailewa ni ipi, kujilipua? Muhimu tukumbuke hapa pakiwaka hapa kwa milipuko ya kidini sio wewe wala mimi wala Lowassa wala Magufuli wala polisi wala majeshi yeyote atakaekuwa na hakika ya kubaki salama.
Hiyo lugha ndiyo ipi haswaaa hadi unashadadia kiasi hicho ambayo waislam hawaijui?