Video: Ubishani ni Zanzibar ni nchi au siyo? Wenzenu upande wa Zanzibar ni Wazanzibari au Watanzania? Wasira, Rais Samia vs Tundu Lissu: Nani mkweli?

Kwa hiyo shida ya "kutojitambua" iko upande wetu wa pili yaani Tanganyika..

Tanganyika na Watanganyika wako wapi?

Jina halisi la nchi hii kumbe linapaswa kuwa ni

"Jamhuri ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar"

na siyo


"Jamhuri ya Muungano wa Tanzania"

Hili jina la "Tanzania" ilitoka wapi? Shida iko kweye jina hili. Uchawi uko humu ndani ya jina hili. Inawezekana vipi kiongozi mmoja anayeitwa "Julius Kambarage Nyerere" abadili jina la nchi na uraia wetu bila ya ridhaa ya wananchi wenyewe??

Huu ni wakati wa kuhoji maamuzi ya huyu aitwaye baba wa taifa hili Mwl Julius K. Nyerere..

Kuna maamuzi yake mengine mengi yalikuwa very fatal na ya hovyo sana na yanahitaji kurekebishwa sasa au kuachana nayo kabisa maana ni mitego ya mauti na kikwazo cha ustawi wetu kama taifa na nchi..
Aliyebuni jina sio Julius Kambarage Burito Nyerere au Abeid Aman Karume bali ni huyu hapa chini:
Jina la Tanzania lilibuniwa na mmoja wa wananchi walioshiriki mchakato wa kutafuta jina la nchi hii, baadaya muungano wa Tanganyika na Zanzibar mwaka 1964.Mohammed Iqbal Dar ndiye aliyebuni jina la Tanzania, wakati huo akiwa na umri wa miaka 18 akiwa mwanafunzi wa Shule ya Sekondari Mzumbe.Mwandishi huyo baada ya kuonana na Mohammed Iqbal Dar akamuuliza:MWANDISHI: Uliingiaje katika shindano la kubuni jina la nchi?IQBAR DAR: Siku moja nilikuwa maktaba nikijisoma Gazeti la Tanganyika Standard ambalo siku hizi linaitwa Daily News, mikaona tangazo lililosema: "Muungano wa Tanganyika na Zanzibar unafahamika kama Republic of Tanganyika and Zanzibar jina likaonekana refu sana. Kwa hiyo wananchi wote mnaombwa kushiriki kwenye shindano la kupendekeza jina moja litakalozitaja nchi zote mbili yaani Tanganyika na Zanzibar."

IQBAR DAR: Nilichukua karatasi nikaandika kwanza Bismillah Raahman Rahimu hii ni kutokana na imani ya dini yangu. Baada ya hapo nikaandika jina la Tanganyika kisha nikaandika Zanzibar halafu nikaandika jina langu la Iqbal halafu nikaandika jina la Jumuiya yangu ya kidini ya Ahmadiya. Baada ya hapo nikamrudia tena MwenyeziMungu, nikamuomba anisaidie ili nipate jina zuri kutoka katika majina hayo niliyokuwa nimeandika. Baada ya hapo nilichukua herufi tatu kutoka jina la nchi ya Tanganyika yaani TAN na kwa upande wa Zanzibar nikachukua herufi tatu za mwanzo ZAN, kisha anikaunganisha nikapata jina TANZAN.

IQBAR DAR: Kabla ya kulipeleka kunakohusika serikalini nilifanya utafiti mdogo na kugundua kuwa nchi nyingi za Afrika majina yao yanaishIA na IA kwa mfano EthiopIA, ZambIA, NigerIA, TunisIA, SomalIA, GambIA, NamibIA, LiberIA, MauritanIA.
Baada ya utafiti huo nikapendekeza na kuamua kwamba jina TANZANIA ndilo litumike kuwakilisha nchi hizi mbili yaani Tanganyika na Zanzibar. Kwa maana hiyo jina TANZANIA limezaliwa kutoka katika majina manne ambayo ni Tanganyika, Zanzibar, Iqbal na Ahmadiyya.

TAN-Tanganyika
ZAN-Zanzibar
IA-IQBAR AHMADIYYA
TAN-ZAN-IA
 
Katiba ya Zanzibar ni kwa ajili ya mambo ya ndani ya Zanzibar, Katiba ya JMT haitambui katiba ya Zanzibar. Tanzania ni nchi moja ya JMT, Zanzibar sio nchi ni sehemu ya JMT. Hivyo haijalishi katiba ya Zanzibar inasema nini kuhusu Zanzibar, hayo ni mambo yao, hayatuhusu!.
P
Mkuu P
Yanawahusu sana Watanganyika usikwepe kwa kuwa una utambulisho halisi, sema ukweli na utakuweka huru daima. Kwanini mtu wa Zanzibar anateuliwa uongozi Tanganyika lakini wa bara hawezi kuteuliwa wala kugombea uongozi Zanzibar?
This is ridiculous to argue with the intellectuals
 
Mkuu P
Yanawahusu sana Watanganyika usikwepe kwa kuwa una utambulisho halisi, sema ukweli na utakuweka huru daima. Kwanini mtu wa Zanzibar anateuliwa uongozi Tanganyika lakini wa bara hawezi kuteuliwa wala kugombea uongozi Zanzibar?
This is ridiculous to argue with the intellectuals
Unahitaji elimu ya uraia kuhusu haki za Mtanzania, kila Mzanzibari kwanza ni Mtanzania ndipo kisha ni Mzanzibari. Lakini sio kila Mtanzania ni Mzanzibari!. Haki za Zanzibar ni kwa Wanzanzibari wakaazi pekee!.

Ukioa mke, anakuja kwako, na anakuja kwenu, kwako kunakuwa kwake, na kwenu ni kwake, lakini kwao ni ukweni ni kwao tuu, ukweni kwa mkeo sio kwako!. Zanzibar ni ukweni!. Tangu lini Mke Ndani Ya Ndoa Akaomba Uhuru ili Kutoka Nje Ya Ndoa? Aruhusiwe?
P
 
Unahitaji elimu ya uraia kuhusu haki za Mtanzania, kila Mzanzibari kwanza ni Mtanzania ndipo kisha ni Mzanzibari. Lakini sio kila Mtanzania ni Mzanzibari!. Haki za Zanzibar ni kwa Wanzanzibari wakaazi pekee!.

Ukioa mke, anakuja kwako, na anakuja kwenu, kwako kunakuwa kwake, na kwenu ni kwake, lakini kwao ni ukweni ni kwao tuu, ukweni kwa mkeo sio kwako!. Zanzibar ni ukweni!. Tangu lini Mke Ndani Ya Ndoa Akaomba Uhuru ili Kutoka Nje Ya Ndoa? Aruhusiwe?
P
Sihitaji elimu yako gushi ya uraia wakati nina akili timamu, nimesoma na ni uwezo wa kuchanganua mambo 'empirically' halafu unaniletea nadharia za siasa uchwara bila uhalisia (Utopian) hapa.

1. Mme ni nani kati ya Tanganyika na Zanzibar?

2. Mke ni yupi kati ya Tanganyika na Zanzibar?

Je, wajua kwamba

1. Tanganyika inawakilishwa na mnyama Simba na wala sio Twiga?

2. Je wajua Zanzibar inawakilishwa mnyama Mbuzi na chui na sio Pweza na Mwani?
 
Sihitaji elimu yako gushi ya uraia wakati nina akili timamu, nimesoma na ni uwezo wa kuchanganua mambo 'empirically' halafu unaniletea nadharia za siasa uchwara bila uhalisia (Utopian) hapa.

1. Mme ni nani kati ya Tanganyika na Zanzibar?

2. Mke ni yupi kati ya Tanganyika na Zanzibar?

Je, wajua kwamba

1. Tanganyika inawakilishwa na mnyama Simba na wala sio Twiga?

2. Je wajua Zanzibar inawakilishwa mnyama Mbuzi na chui na sio Pweza na Mwani?
Ndoa ya muungano sio ndoa za jinsia, ni ndoa ya two equal partners wenye haki sawa and equal status.
P
 
Aliyebuni jina sio Julius Kambarage Burito Nyerere au Abeid Aman Karume bali ni huyu hapa chini:
Jina la Tanzania lilibuniwa na mmoja wa wananchi walioshiriki mchakato wa kutafuta jina la nchi hii, baadaya muungano wa Tanganyika na Zanzibar mwaka 1964.Mohammed Iqbal Dar ndiye aliyebuni jina la Tanzania, wakati huo akiwa na umri wa miaka 18 akiwa mwanafunzi wa Shule ya Sekondari Mzumbe.Mwandishi huyo baada ya kuonana na Mohammed Iqbal Dar akamuuliza:MWANDISHI: Uliingiaje katika shindano la kubuni jina la nchi?IQBAR DAR: Siku moja nilikuwa maktaba nikijisoma Gazeti la Tanganyika Standard ambalo siku hizi linaitwa Daily News, mikaona tangazo lililosema: "Muungano wa Tanganyika na Zanzibar unafahamika kama Republic of Tanganyika and Zanzibar jina likaonekana refu sana. Kwa hiyo wananchi wote mnaombwa kushiriki kwenye shindano la kupendekeza jina moja litakalozitaja nchi zote mbili yaani Tanganyika na Zanzibar."

IQBAR DAR: Nilichukua karatasi nikaandika kwanza Bismillah Raahman Rahimu hii ni kutokana na imani ya dini yangu. Baada ya hapo nikaandika jina la Tanganyika kisha nikaandika Zanzibar halafu nikaandika jina langu la Iqbal halafu nikaandika jina la Jumuiya yangu ya kidini ya Ahmadiya. Baada ya hapo nikamrudia tena MwenyeziMungu, nikamuomba anisaidie ili nipate jina zuri kutoka katika majina hayo niliyokuwa nimeandika. Baada ya hapo nilichukua herufi tatu kutoka jina la nchi ya Tanganyika yaani TAN na kwa upande wa Zanzibar nikachukua herufi tatu za mwanzo ZAN, kisha anikaunganisha nikapata jina TANZAN.

IQBAR DAR: Kabla ya kulipeleka kunakohusika serikalini nilifanya utafiti mdogo na kugundua kuwa nchi nyingi za Afrika majina yao yanaishIA na IA kwa mfano EthiopIA, ZambIA, NigerIA, TunisIA, SomalIA, GambIA, NamibIA, LiberIA, MauritanIA.
Baada ya utafiti huo nikapendekeza na kuamua kwamba jina TANZANIA ndilo litumike kuwakilisha nchi hizi mbili yaani Tanganyika na Zanzibar. Kwa maana hiyo jina TANZANIA limezaliwa kutoka katika majina manne ambayo ni Tanganyika, Zanzibar, Iqbal na Ahmadiyya.

TAN-Tanganyika
ZAN-Zanzibar
IA-IQBAR AHMADIYYA
TAN-ZAN-IA
🤔🤔🤔⁉⁉⁉
 
Ndoa ya muungano sio ndoa za jinsia, ni ndoa ya two equal partners wenye haki sawa and equal status.
P
P, umechokonoa kitu usichojua madhara yake

Taja hapa ni nani mme au mke kati ya Tanganyika na Zanzibar kwa mwenziwe?

Usizunguke kama nguchiro kwa kuwianisha hadhi za mamlaka ya usawa usiokuwepo. Tusiwe na mawazo tegemezi yaliyotekwa na kikundi fulani (elites) dhidi ya watu wasiojitambua (lumpen)
 
Katiba ya Zanzibar ni kwa ajili ya mambo ya ndani ya Zanzibar, Katiba ya JMT haitambui katiba ya Zanzibar. Tanzania ni nchi moja ya JMT, Zanzibar sio nchi ni sehemu ya JMT. Hivyo haijalishi katiba ya Zanzibar inasema nini kuhusu Zanzibar, hayo ni mambo yao, hayatuhusu!.
P

Mwanasheria Pascal Mayalla naona umeamua kupambana kwa kupiga mayowe badala ya kuyatazama mambo ktk jicho pevu la kisheria..

Kama umefikia hatua ya kutamka "tutaulinda muungano huu kwa gharama zozote", ila ujue kuwa tupo tutakaosema "huu muungano tutaufutilia mbali kwa gharama zozote".

Kukiwa na confrontation ya dizaini hii kati ya wawili katika ndoa, unadhani kutatokea nini kwa kusigana huku badala ya kupatana kwa kutatua kasoro za ndoa yetu?

Umeulinganisha muungano kama ndoa ya mume na mke, na kwamba, kusisitiza kuwa wanandoa huwa hawaachani. Lakini hii ina ukweli wowote?kweli?

Mr Pascal Mayalla ndoa huvunjika. Hata hii inaweza kuvunjika na kama hao wenzako huko wana mawazo kama yako, basi itavunjika haraka sana..
 
View attachment 2991056
Ndugu wana JF - Jukwaa la Siasa;

Mjadala wa muungano tata wa Tanganyika na Zanzibar (1964) unaendelea tena leo....

Na kwa kweli mjadala huu haupaswi kuishia njiani isipokuwa tu wote tumeelewana na kukubali kuwa lipo tatizo ktk muungano huu linalostahili kutatuliwa sasa na sio kesho kama tunataka kuendelea nao...

Leo katika video hiyo☝🏻☝🏻 ni makala ya uchambuzi toka kwa mchambuzi nguli wa maswala ya kisiasa, kijamii na kiuchumi ndugu Ansbert Ngurumo kupitia YouTube channel yake [SK Media Online TV] anayeishi uhamishoni Uingereza

Katika uchambuzi huu, Ansbert Ngurumo anazimulika kauli za watu watatu juu muungano wa Tanganyika na Zanzibar (1964) ambao ni;

1. Mzee Steven Wassira a.k.a Tyson (CCM)
2. Rais Samia Suluhu Hassan (CCM)

3. Tundu Antipasy Lissu (CHADEMA)

Hawa wote wanajibu maswali mawili muhimu yafuatayo ambayo ndiyo msingi mkuu wa ubishani unaoendelea sasa ktk muungano huu;

1. KWAMBA, Zanzibar ni nchi au sio nchi?

2. KWAMBA, Watu au wananchi wa nchi ya Zanzibar ni Watanzania au Wazanzibari?

Nani mkweli kati ya hawa watu watatu kuhusu muungano wetu? Nini maoni yako? Tatizo liko wapi? Ni kitu gani kinafichwa kupitia muungano huu?

Tazama na sikiliza video hiyo ya dakika 14 tu hadi mwisho kisha tumia akili yako kupima mwenyewe halafu sema kitu.

Na bila shaka kasi ya internet imeboreka kiasi chake na hivyo kila mtu ataifungua video hii bila kuhangaika sana..
==========================================
Unataka maneno ya wanasiasa au unataka Katiba ambazo ndio miongozo?
Katiba ya Zanzibar kwenye Preamble inasemaje?
Katiba ya Tanganyika inasemaje?
 
Paschal leo umeandika hisia au halisia? Kwa hiyo unamaanisha Mzanzibar ni uraia batili?
Sio ubatili, hakuna raia wa Zanzibar kwasababu Zanzibar sio nchi, haina raia, nchi ni Tanzania na uraia ni mmoja tuu, uraia wa Tanzania.

Ila Zanzibar ni eneo halali lenye utawala wake wa ndani na eneo hilo lina wakaazi, hivyo kile kitambulisho cha ukaazi wa Zanzibar ni kitambulisho cha ukaazi wa eneo la Zanzibar na sio kitambulisho cha uraia wa Zanzibar, hakuna raia wa Zanzibar, raia wote ni raia wa Tanzania na wana haki zote za uraia sawa sawa ikiwemo kumiliki ardhi na ajira ndani ya JMT!.
P
 
Ziko ndoa nyingi tuu, wanandoa wanasigana, lakini performance inaendelea na ndoa inaendelea. Usisikilize kelele za vitimbakwiri vya wapinga muungano, muungano wetu ni imara, na tutaulinda kwa gharama yoyote, hata kama baadhi ya gharama hizo ni machozi, jasho na damu!.
P
Muungano ni imara kwa sababu inatumika nguvu ya dola . Upinzani ulikuwa Zanzibar tu ,lakini kidogo kidogo wa Tanganyika mnaanza kujitambua ingawa wenye njaa na walafi mko wengi mnaojipendekeza kwa wenye Muungano
 
Sio ubatili, hakuna raia wa Zanzibar kwasababu Zanzibar sio nchi, haina raia, nchi ni Tanzania na uraia ni mmoja tuu, uraia wa Tanzania.

Ila Zanzibar ni eneo halali lenye utawala wake wa ndani na eneo hilo lina wakaazi, hivyo kile kitambulisho cha ukaazi wa Zanzibar ni kitambulisho cha ukaazi wa eneo la Zanzibar na sio kitambulisho cha uraia wa Zanzibar, hakuna raia wa Zanzibar, raia wote ni raia wa Tanzania na wana haki zote za uraia sawa sawa ikiwemo kumiliki ardhi na ajira ndani ya JMT!.
P
Wakati wa Karume Sr. Ukifika 18yrs. Ilikuwa lazima uchukuwe id inaitwa Kadi ya Uraia
Hiyo ilithibitisha Uraia wako. Na ilikuwa hupati hata kununua nguo dukani Kama huna hiyo Kadi . Hizi Kadi ziliondoka baada kuuliwa Karume. Lakini bila Kadi Wazanzibari tunajuana.
 
Wengi wanaunga mkono Tanganyika kwa sababu ya chuki kwa Samia na haswa uislamu wake. Kuhoji juu ya Tanganyiko ni kificho tu cha chuki zao dhidi ya uislam wa Rais.

Magufuli angekuwa hai mpaka leo usingesikia hoja hizi zikijadiliwa, ni hawa hawa waliomtazama Samia kama mtu anayeleta waarabu pale bandarini wakishindwa kuona kuwa ni suala lililo ndani ya ilani ya uchaguzi ya CCM, Chuki zinawapofusha.
Sasa wewe huu ni muungano gani?. Zanzibar si wana rais wao. Vile vile Tanganyika wapate rais wao. Harafu kuwe na rais wa muungano wa nchi zote mbili
 
Back
Top Bottom