Video: Ubishani ni Zanzibar ni nchi au siyo? Wenzenu upande wa Zanzibar ni Wazanzibari au Watanzania? Wasira, Rais Samia vs Tundu Lissu: Nani mkweli?

Uzima Tele

JF-Expert Member
Jan 20, 2023
1,198
2,618

Ndugu wana JF - Jukwaa la Siasa;

Mjadala wa muungano tata wa Tanganyika na Zanzibar (1964) unaendelea tena leo....

Na kwa kweli mjadala huu haupaswi kuishia njiani isipokuwa tu wote tumeelewana na kukubali kuwa lipo tatizo ktk muungano huu linalostahili kutatuliwa sasa na sio kesho kama tunataka kuendelea nao...

Leo katika video hiyo☝🏻☝🏻 ni makala ya uchambuzi toka kwa mchambuzi nguli wa maswala ya kisiasa, kijamii na kiuchumi ndugu Ansbert Ngurumo kupitia YouTube channel yake [SK Media Online TV] anayeishi uhamishoni Uingereza

Katika uchambuzi huu, Ansbert Ngurumo anazimulika kauli za watu watatu juu muungano wa Tanganyika na Zanzibar (1964) ambao ni;

1. Mzee Steven Wassira a.k.a Tyson (CCM)
2. Rais Samia Suluhu Hassan (CCM)

3. Tundu Antipasy Lissu (CHADEMA)

Hawa wote wanajibu maswali mawili muhimu yafuatayo ambayo ndiyo msingi mkuu wa ubishani unaoendelea sasa ktk muungano huu;

1. KWAMBA, Zanzibar ni nchi au sio nchi?

2. KWAMBA, Watu au wananchi wa nchi ya Zanzibar ni Watanzania au Wazanzibari?

Nani mkweli kati ya hawa watu watatu kuhusu muungano wetu? Nini maoni yako? Tatizo liko wapi? Ni kitu gani kinafichwa kupitia muungano huu?

Tazama na sikiliza video hiyo ya dakika 14 tu hadi mwisho kisha tumia akili yako kupima mwenyewe halafu sema kitu.

Na bila shaka kasi ya internet imeboreka kiasi chake na hivyo kila mtu ataifungua video hii bila kuhangaika sana..
==========================================
 
Mkuu zanzibar Ni nchi kulingana na Katiba ya Zanzibar ya mwaka 1984 yenye marekebisho yakr mwaka 2010..

na ni Miongoni mwa Nchi zinazounda Tanzania..
Screenshot_20240515_220213_Adobe Acrobat.jpg


Hata hivyo kwa Mujibu Wa Katiba ya zanzibar Ikisomwa pamoja na sheria namba 5 ya mwaka 1985 au Maarufu Sheria ya Uzanzibar ya mwaka 1985..
Inasema hivi Mzanzibar Ni Mtanzania mwenye Ukazi wa Zanzibar
Screenshot_20240515_220841_Adobe Acrobat.jpg


Na sheria namba 5 ya mwaka 1985 au Maarufu Sheria ya Uzanzibar ya mwaka 1985..
Screenshot_20240501_173439_Adobe Acrobat.jpg

Screenshot_20240501_173507_Adobe Acrobat.jpg

Screenshot_20240501_185307_Adobe Acrobat.jpg

Screenshot_20240501_185404_Adobe Acrobat.jpg
 

1. Tanzania ni nchi moja ya JMT yenye uraia mmoja tuu wa JMT. Zanzibar sio nchi, ni sehemu ya JMT.
2. Wananchi wa Zanzibar ni Watanzania ila pia ni wakaazi wa Zanzibar. Ukaazi sio uraia.
P
Boss, for this context wakaazi wa Mwanza tunaweza kuwaita wamwanza? If not. Kwanini? Wakati wao ni wakaazi wa Mwanza? Kwanini kwa Zanzibar inawezekana?
 
1. Tanzania ni nchi moja ya JMT yenye uraia mmoja tuu wa JMT. Zanzibar sio nchi, ni sehemu ya JMT.
2. Wananchi wa Zanzibar ni Watanzania ila pia ni wakaazi wa Zanzibar. Ukaazi sio uraia.
P
But Pascal najua umeshafika Unguja a.k.a Zanzibar na umejionea mfumo wa maisha yao, kweli ni shm ya JMT lakoni mfumo wao wa maisha ni unaeleza tofauti kubwa iliyopo kati yetu Watanganyika na wao Wazanzibari.

Wao wanajivunia uzanzibari wao lkn wewe hujivunii utanganyika wako why?.

Utanganyika ni haupo (achana na JMT ila nje ya muungano) tunapiga tu mitkasi ya keyboard ila huyo mbunge wa kutoka nchini Zanzibari ana jambo linapaswa kujadiliwa.
 
Mkuu zanzibar Ni nchi kulingana na Katiba ya Zanzibar ya mwaka 1984 yenye marekebisho yakr mwaka 2010..

na ni Miongoni mwa Nchi zinazounda Tanzania..
View attachment 2991069

Hata hivyo kwa Mujibu Wa Katiba ya zanzibar Ikisomwa pamoja na sheria namba 5 ya mwaka 1985 au Maarufu Sheria ya Uzanzibar ya mwaka 1985..
Inasema hivi Mzanzibar Ni Mtanzania mwenye Ukazi wa Zanzibar
View attachment 2991070

Na sheria namba 5 ya mwaka 1985 au Maarufu Sheria ya Uzanzibar ya mwaka 1985..View attachment 2991074
View attachment 2991075

View attachment 2991076
View attachment 2991080
Kwa hiyo shida ya "kutojitambua" iko upande wetu wa pili yaani Tanganyika..

Tanganyika na Watanganyika wako wapi?

Jina halisi la nchi hii kumbe linapaswa kuwa ni

"Jamhuri ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar"

na siyo


"Jamhuri ya Muungano wa Tanzania"

Hili jina la "Tanzania" ilitoka wapi? Shida iko kweye jina hili. Uchawi uko humu ndani ya jina hili. Inawezekana vipi kiongozi mmoja anayeitwa "Julius Kambarage Nyerere" abadili jina la nchi na uraia wetu bila ya ridhaa ya wananchi wenyewe??

Huu ni wakati wa kuhoji maamuzi ya huyu aitwaye baba wa taifa hili Mwl Julius K. Nyerere..

Kuna maamuzi yake mengine mengi yalikuwa very fatal na ya hovyo sana na yanahitaji kurekebishwa sasa au kuachana nayo kabisa maana ni mitego ya mauti na kikwazo cha ustawi wetu kama taifa na nchi..
 
1. Tanzania ni nchi moja ya JMT yenye uraia mmoja tuu wa JMT. Zanzibar sio nchi, ni sehemu ya JMT.
Basically, hili pengine halina ubishi wowote kwa sababu katiba hii inayoitwa ya "Jamhuri ya muungano wa Tanzania ya mwaka 1977" inasema hivyo.

Lakini upande wa pili katiba ya Zanzibar ya 1984 inai over-rule katiba ya JMT ya 1977 kwa kusema kuwa "Zanzibar ni nchi yenye mipaka yake" na mipaka hiyo kutajwa na katiba yao kwa kupingana kabisa na katiba ya JMT ya 1977..!!

Kwa hiyo tusemeje ndugu Pascal Mayalla? Kwamba Wazanzibar wamevunja katiba ya JMT na kwa hiyo kutenda kosa la uhaini? What's your opinion on this?
2. Wananchi wa Zanzibar ni Watanzania ila pia ni wakaazi wa Zanzibar. Ukaazi sio uraia.
P
Hili ndilo linalowakera Wazenj. Ndio maana wanataka mamlaka kamili. Wanataka kutoka ktk kongwa la Muungano.

Nadhani ni wakati wa susi Watanganyika kuitafuta kwa nguvu zote Tanganyika ilikofichwa baada ya kuibiwa..

Ni lazima tuwe na "wakaazi wa Tanganyika" lakini tukiwa na uraia wa Tanzania kama walivyo wazenj🤔!

Tunataka katiba ya Tanganyika itakayofafanua namna Watanganyika watakavyofaidi haki za Utanganyika wao kama walivyo Wazenj..

All in all, Tanganyika tunatawaliwa na raia wa kigeni toka nchi inayoitwa Zanzibar kwa kigezo feki cha Muungano!!
 
Boss, for this context wakaazi wa Mwanza tunaweza kuwaita wamwanza? If not. Kwanini? Wakati wao ni wakaazi wa Mwanza? Kwanini kwa Zanzibar inawezekana?
Kwa Zanzibar inawezekana kwasababu Zanzibar ina autonomy yake ya mambo yake ya ndani, wakati mambo ya Tanzania ni ya wote wakiwemo Wanzanzibari.

Elimu kuhusu katiba, sheria na haki ni muhimu ili watu wajue kuhusu autonomy ya Zanzibar na kuacha hizi kelele za ubaguzi, kutaka kuwabagua, tena afadhali ya sasa, mimi nimeingia Zanzibar kwa passport enzi hizo!.

P
 
But Pascal najua umeshafika Unguja a.k.a Zanzibar na umejionea mfumo wa maisha yao, kweli ni shm ya JMT lakoni mfumo wao wa maisha ni unaeleza tofauti kubwa iliyopo kati yetu Watanganyika na wao Wazanzibari.

Wao wanajivunia uzanzibari wao lkn wewe hujivunii utanganyika wako why?.

Utanganyika ni haupo (achana na JMT ila nje ya muungano) tunapiga tu mitkasi ya keyboard ila huyo mbunge wa kutoka nchini Zanzibari ana jambo linapaswa kujadiliwa.
Mimi nimezaliwa Tanzania, na wengi wetu tumezaliwa Tanzania, waliozaliwa Tanganyika wote by now ni wastaafu, wako over 60 years, na walipopata akili, walikuwa tayari Tanzania, ni Watanganyika gani hao wa kuililia Tanganyika na kujivunia Tanganyika?.

Muungano ni kama ndoa, Zanzibar ni kama mwenza, sasa wewe kama mwenza wako anajipodoa, na wewe utataka kujipodoa ili mlingane?. Hebu acheni hizi kitu!.
P
 
Kwa hiyo shida ya "kutojitambua" iko upande wetu wa pili yaani Tanganyika..

Tanganyika na Watanganyika wako wapi?

Jina halisi la nchi hii kumbe linapaswa kuwa ni

"Jamhuri ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar"

na siyo


"Jamhuri ya Muungano wa Tanzania"

Hili jina la "Tanzania" ilitoka wapi? Shida iko kweye jina hili. Uchawi uko humu ndani ya jina hili. Inawezekana vipi kiongozi mmoja anayeitwa "Julius Kambarage Nyerere" abadili jina la nchi na uraia wetu bila ya ridhaa ya wananchi wenyewe??

Huu ni wakati wa kuhoji maamuzi ya huyu aitwaye baba wa taifa hili Mwl Julius K. Nyerere..

Kuna maamuzi yake mengine mengi yalikuwa very fatal na ya hovyo sana na yanahitaji kurekebishwa sasa au kuachana nayo kabisa maana ni mitego ya mauti na kikwazo cha ustawi wetu kama taifa na nchi..
Tanzania ni nchi inayotambulikana kimataifa. kama huijui basi ni wewe peke yako
 
Mimi nimezaliwa Tanzania, na wengi wetu tumezaliwa Tanzania, waliozaliwa Tanganyika wote by now ni wastaafu, wako over 60 years, na walipopata akili, walikuwa tayari Tanzania, ni Watanganyika gani hao wa kuililia Tanganyika na kujivunia Tanganyika?.

Muungano ni kama ndoa, Zanzibar ni kama mwenza, sasa wewe kama mwenza wako anajipodoa, na wewe utataka kujipodoa ili mlingane?. Hebu acheni hizi kitu!.
P
HUo mfano wa muungano ni kama ndoa uishie humuhumu Jf,wazanzibari huwa hawapendi kuusikia kabisa,wanahisi hapo mwanamke ni zanzibar na mwanaume ni Tanganyika,kwa hiyo wanahisi tumewaowa
 
Basically, hili pengine halina ubishi wowote kwa sababu katiba hii inayoitwa ya "Jamhuri ya muungano wa Tanzania ya mwaka 1977" inasema hivyo.

Lakini upande wa pili katiba ya Zanzibar ya 1984 inai over-rule katiba ya JMT ya 1977 kwa kusema kuwa "Zanzibar ni nchi yenye mipaka yake" na mipaka hiyo kutajwa na katiba yao kwa kupingana kabisa na katiba ya JMT ya 1977..!!

Kwa hiyo tusemeje ndugu Pascal Mayalla? Kwamba Wazanzibar wamevunja katiba ya JMT na kwa hiyo kutenda kosa la uhaini? What's your opinion on this?

Hili ndilo linalowakera Wazenj. Ndio maana wanataka mamlaka kamili. Wanataka kutoka ktk kongwa la Muungano.

Nadhani ni wakati wa susi Watanganyika kuitafuta kwa nguvu zote Tanganyika ilikofichwa baada ya kuibiwa..

Ni lazima tuwe na "wakaazi wa Tanganyika" lakini tukiwa na uraia wa Tanzania kama walivyo wazenj🤔!

Tunataka katiba ya Tanganyika itakayofafanua namna Watanganyika watakavyofaidi haki za Utanganyika wao kama walivyo Wazenj..

All in all, Tanganyika tunatawaliwa na raia wa kigeni toka nchi inayoitwa Zanzibar kwa kigezo feki cha Muungano!!
It's true katiba ya Zanzibar imefanya uhaini kujiinua na kujiita nchi na kutaja mipaka yake, ila katiba ya JMT haiitambui katiba ya Zanzibar!, kwasababu haituhusu!. Huwezi kufanya uhaini kwa sehemu ambayo sio nchi!. Katiba ya Zanzibar kujiita nchi ni kujifurahisha tuu, mwisho Chumbe!. Nchi ni moja tuu, JMT!.

Hata wewe na mkeo, anabeba pochi lake au mkoba wake, wewe huwa unachunguza anabeba nini kwenye mkoba wake?. Kwa nini huchunguzi?, ni kwasababu, hayakuhusu!.

Zanzibar ina utawala wake wa ndani, ni mambo yasiyotuhusu, hata akijiita nchi ya Zanzibar, taifa la Zanzibar, ufalme wa Zanzibar. etc, as long as kimataifa Tanzania ni nchi moja ya JMT, mambo ya Zanzibar ni yao, hayatuhusu, kuna tatizo gani?.

Tanzania ni nchi moja, yenye uraia mmoja tuu wa JMT, Zanzibar sio nchi, bali ni sehemu ya JMT, huwezi kufanya uhaini kwa eneo ambalo sio nchi!.

P
 
HUo mfano wa muungano ni kama ndoa uishie humuhumu Jf,wazanzibari huwa hawapendi kuusikia kabisa,wanahisi hapo mwanamke ni zanzibar na mwanaume ni Tanganyika,kwa hiyo wanahisi tumewaowa
Huu ndio ukweli wa mambo, tena sio wanahisi tumewaoa, bali huyo mwanamke ndie alijitongozesha, akajibebisha, Mzee Tanganyika akachukua ngoma, akaoa, akatia ndani, analisha, anatunza, anagharimia kila kitu, mke kazi kupendeza tuu, kila kitu bure!.

Niliwahi kuuliza humu Tangu lini Mke Ndani Ya Ndoa Akaomba Uhuru ili Kutoka Nje Ya Ndoa? Aruhusiwe?

Tanzania itakuwa na wanaume wa ajabu wanao ona wivu na wake zao kwa kutamani wawe sawa kwa sawa!.
Mwacheni mkeo apendeze. Mpe kila anachokitaka!.

P
 
It's true katiba ya Zanzibar imefanya uhaini kujiinua na kujiita nchi na kutaja mipaka yake, ila katiba ya JMT haiitambui katiba ya Zanzibar!, kwasababu haituhusu!. Huwezi kufanya uhaini kwa sehemu ambayo sio nchi!. Katiba ya Zanzibar kujiita nchi ni kujifurahisha tuu, mwisho Chumbe!. Nchi ni moja tuu, JMT!.

Hata wewe na mkeo, anabeba pochi lake au mkoba wake, wewe huwa unachunguza anabeba nini kwenye mkoba wake?. Kwa nini huchunguzi?, ni kwasababu, hayakuhusu!.

Zanzibar ina utawala wake wa ndani, ni mambo yasiyotuhusu, hata akijiita nchi ya Zanzibar, taifa la Zanzibar, ufalme wa Zanzibar. etc, as long as kimataifa Tanzania ni nchi moja ya JMT, mambo ya Zanzibar ni yao, hayatuhusu, kuna tatizo gani?.

Tanzania ni nchi moja, yenye uraia mmoja tuu wa JMT, Zanzibar sio nchi, bali ni sehemu ya JMT, huwezi kufanya uhaini kwa eneo ambalo sio nchi!.

P
Wana Rais,wimbo wa Taifa,bendera,bunge,baraza la mawaziri,mipaka,ni vile tu hawana kiti UN ila ni nchi kamili
 
Back
Top Bottom