Chona
JF-Expert Member
- Mar 8, 2010
- 523
- 365
Nadhani tunafanya makosa kuhusisha siasa kwenye kila kitu.
Haiwezekani Machinga wajengewe jengo la kufanyia biashara kisha wao walikache na kujijengea vibanda ili wasilipe kodi. Kama tatizo ni bei juu basi wangeunda timu ya kukutana na mamlaka husika kulalamikia hilo lakini si kujiamlia kujenga wakati vyumba bado vipo.
Tabia ya watu kujiamlia kufanya wanayotaka hata wasiporuhusiwa imeshamiri. Ukichunguza kwenye vituo vya daladala, daladala nyingi hazipendi kusimama na kupark kwenye vituo. Nyingi zinavizia pembeni kabla ya kutuo na wakati mwingine zinapiga foreni barabara kila mmoja akitaka kuwa nyuma ya mwingine huku sehemu za vituo zikiwa wazi. Inashangaza kweli. Ukienda kwenye vituo ambavyo vimejengwa mahususi kwa ajili ya abiria, tayari vimevamiwa na wafanyabiashara ndogo. Utakuta wamepanga bidhaa zao na wengine wameweka meza na mianvuli huku sehemu za abiria zikiwa ndo seat za kukaa au meza.
Nadhani ifike mahali watu waheshimu taratibu bila itikadi. Mji lazima uonekane ni mji kwa mpangilio na taratibu.
Haiwezekani Machinga wajengewe jengo la kufanyia biashara kisha wao walikache na kujijengea vibanda ili wasilipe kodi. Kama tatizo ni bei juu basi wangeunda timu ya kukutana na mamlaka husika kulalamikia hilo lakini si kujiamlia kujenga wakati vyumba bado vipo.
Tabia ya watu kujiamlia kufanya wanayotaka hata wasiporuhusiwa imeshamiri. Ukichunguza kwenye vituo vya daladala, daladala nyingi hazipendi kusimama na kupark kwenye vituo. Nyingi zinavizia pembeni kabla ya kutuo na wakati mwingine zinapiga foreni barabara kila mmoja akitaka kuwa nyuma ya mwingine huku sehemu za vituo zikiwa wazi. Inashangaza kweli. Ukienda kwenye vituo ambavyo vimejengwa mahususi kwa ajili ya abiria, tayari vimevamiwa na wafanyabiashara ndogo. Utakuta wamepanga bidhaa zao na wengine wameweka meza na mianvuli huku sehemu za abiria zikiwa ndo seat za kukaa au meza.
Nadhani ifike mahali watu waheshimu taratibu bila itikadi. Mji lazima uonekane ni mji kwa mpangilio na taratibu.
