Beberu-mpya
JF-Expert Member
- Feb 14, 2017
- 216
- 106
Kweli kabisa, pia vilivyokuw vinagaiw walijipa wenyew wakubwa kwanza pia kod ni miezi 6 na mwaka. Kwa mmachinga inamuiwa vigum kumuduGharama za pango zipo juu,machinga hawaimudu na ndiyo sababu ya kujenga vibanda nje..
Tuko Dodoma kwa sasa.Hilo jengo limeshindikana kwa biashara ya machinga, serikali ingegeuza tu ofisi za idara mbalimbali
Sasa mbona hawataki wenzao wakodishwe?jingo lina masharti makubwa na ni gharama ukilinganisha na uhalisia wa biashara. wale jamaaa wamekua mkombozi kwa mtanzania mwenye kipato cha chini. nimefikiria zaidi ya kile ninachokijua
Sasa uliza humo ndani nafasi ipo basi, ni majanga tukwa hiyo walikataa kukaa ndani wakaweka vibanda nnje ya jengo la biashara ili watu wasiingie ndani wakija waishie hapo nnje, wao hawalipi kodi huku wanauza, walio ndani wanalipakodi lakini hawauzi.
Kwa hiyo km hakuna nafasi watandaze biashara popote?Sasa uliza humo ndani nafasi ipo basi, ni majanga tu
Hili suala la daladala kuegesha nyuma ya kituo ni kero sana halafu anaacha mkia barabarani,tatizo waswahili kila kitu ni siasa.Nadhani tunafanya makosa kuhusisha siasa kwenye kila kitu.
Haiwezekani Machinga wajengewe jengo la kufanyia biashara kisha wao walikache na kujijengea vibanda ili wasilipe kodi. Kama tatizo ni bei juu basi wangeunda timu ya kukutana na mamlaka husika kulalamikia hilo lakini si kujiamlia kujenga wakati vyumba bado vipo.
Tabia ya watu kujiamlia kufanya wanayotaka hata wasiporuhusiwa imeshamiri. Ukichunguza kwenye vituo vya daladala, daladala nyingi hazipendi kusimama na kupark kwenye vituo. Nyingi zinavizia pembeni kabla ya kutuo na wakati mwingine zinapiga foreni barabara kila mmoja akitaka kuwa nyuma ya mwingine huku sehemu za vituo zikiwa wazi. Inashangaza kweli. Ukienda kwenye vituo ambavyo vimejengwa mahususi kwa ajili ya abiria, tayari vimevamiwa na wafanyabiashara ndogo. Utakuta wamepanga bidhaa zao na wengine wameweka meza na mianvuli huku sehemu za abiria zikiwa ndo seat za kukaa au meza.
Nadhani ifike mahali watu waheshimu taratibu bila itikadi. Mji lazima uonekane ni mji kwa mpangilio na taratibu.