M Z A N Z I B A R I
JF-Expert Member
- Dec 15, 2015
- 21,739
- 117,399
Mikutano yetu ya kampeni katika hiyo mikoa ya Mtwara na Lindi ilifana sana. Watu wengi walihamasika na hoja zangu za kujenga uchumi shirikishi.
Nilifafanua kauli mbiu ya ‘Haki Sawa kwa Wote’ kuwa ni pamoja na haki za kiuchumi, haki za kisiasa na haki za kijamii.
Vijana wa Profesa Malima walihangaika kuhakikisha tunazunguka nchi nzima kufanya kampeni. Juma Kilaghai alikuwa Katibu wangu wakati wa Kampeni, japo kutokana na hali halisi tulikubaliana abakie Dar es Salaam kusukuma mambo pale ambapo kungekuwa na mkwamo wowote.
Nilifafanua kauli mbiu ya ‘Haki Sawa kwa Wote’ kuwa ni pamoja na haki za kiuchumi, haki za kisiasa na haki za kijamii.
Vijana wa Profesa Malima walihangaika kuhakikisha tunazunguka nchi nzima kufanya kampeni. Juma Kilaghai alikuwa Katibu wangu wakati wa Kampeni, japo kutokana na hali halisi tulikubaliana abakie Dar es Salaam kusukuma mambo pale ambapo kungekuwa na mkwamo wowote.