Tafiti zimeonesha kwamba ulezi na mtama viliweza kuboresha afya ya moyo na mishipa ya damu kwa kupunguza mafuta mabaya ‘triglycerides’ kwa panya waliotumika kwenye majaribio. Mmh! Vipi kama haitokei kwa binadamu?
Kuna utafiti mwingine ulifanyika China, ulionesha kwamba kadri watu walivyokula jamii ya mtama hatari ya kufa kwa saratani ya koo ilipungua kadri mtu alivyokula zaidi. Hii ilifanyika kwa kulinganisha na watu ambao wanakula mahindi na ngano.
Wanasayansi wengine walieleza kuwa, shida ya mahindi na ngano huenda ni kwa sababu ya fangasi wanaoitwa fusaria C, ambao wanaweza kusababisha saratani, huwa wanapatikana kwenye mahindi yaliyotunzwa nyumbani kwa mazingira ya China (chang et al, 1985) na South Afrika (Marasasi et al, 1979) hatujui hapa kwetu haijafanyiwa utafiti.
Tafiti zimeonesha kemikali phenolic, kemikali mmea zilizopo kwenye ngano zinauwezo wa kupambana na saratani. Inazuia seli za saratani zisiendelee kuzaliana.
Pamoja na kwamba mtama unazuia seli za saratani zisiendelee kuzaliana haiathiri hata seli moja ambayo iko na afya njema. Yaani seli za kawaida inaziacha ziendelee na maisha yake.
Mara nyingi kinachomuua mgonjwa wa saratani ni kwa sababu seli za saratani zimehama sehemu yake ya mwanzo zimeenda sehemu nyingine ya mwili kufanya uharibifu.
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.