Vilevile wanaume wenye zaidi ya umri wa miaka 40 ni asilimia 40 ya wale wasioweza kuwatosheleza wake zao kindoa kutokana na tatizo linaloathiri sehemu zao za siri. (uume kushindwa).
Mwanaume au mwanamke aliye katika hali hiyo pia anaweza kukejeliwa au kupokea shutuma chungu nzima kutoka kwa jamii iwapo siri yake itajulikana nyumbani ama mahala popote pale.
Kutokana na hilo wanaume ambao hujipata katika hali hiyo ya kiafya hupendelea sana kutoshiriki katika mjadala kuhusu suala hilo kwasababu hujihisi kukatishwa tamaa.
Kunapotokea hali kama hiyo , magonjwa mengine pia huanza kumwathiri mwanaume kama huyo na mara nyingi huogopa kushiriki na wake zao katika tendo la ndoa.
Na iwapo mwanaume anashindwa kutekeleza wajibu wake nyumbani, humfanya mke wake kuanza kumshuku na hivyobasi kusababisha kuzuka kwa ugomvi wa mara kwa mara bila sababu.
Hali ya maumbile nyeti kushindwa kuwa tayari, kwa kitaalamu Erectile dysfunction (ED) ni wakati ambapo mwanamume hawezi kushiriki katika tendo la ndoa kwa dakika 15 mfululizo.
Utafiti umeonesha kwamba iwapo mwanaume ana uwezo wa kushiriki katika tendo la ndoa, sehemu yake ya siri huonesha mihemko nyakati za alfajiri anapoamka.
Uwezo mkubwa wa kufikiri unahusiana na kiasi cha ndoto mtu anazoota
Inaaminika kuwa watu wenye uwezo mkubwa wa kufikiri (Intelligent Quotient – IQ) huota ndoto nyingi zaidi kuliko watu wenye IQ ndogo. Hili kwako likoje? Naamini utatupa maoni yako hapo chini.
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.