Sasa aina gani ya gari, kwa ajili ya shughuli gani na la kiwango gani cha thamani inabaki kuwa jambo linalotenganisha kundi moja na lingine la wamiliki wa magari.
Wasanii, wanamichezo na watu wengine maarufu dunaini mara nyingi hutumia magari ya kifahari zaidi na yenye thamani kubwa kwa sababu ya shughuli zao na namna wanavyojiweka kwenye macho ya watu wanaowafuatilia.
Hata barani Afrika, inaonekana sasa kama kitu cha kawaida kwa watu maarufu wakiwemo wasanii, wafanyabiashara na wanamichezo kumiliki magari makali, ya kisasa na ya bei ya juu.
Mtandao wa Car mart Nigeria unamtaja David 'Davido' Adeleke kumiliki karibu magari 10 ya kifahari yakiwemo Rolls-Royce Cullinan 2019, Bentley Bentayga na Range Rover Sport.
Ayodeji 'Wizkid' Balogun pamoja na magari mengine anamiliki Lamborghini Uru na Porsche Panamera na msanii Diamond Platnumz wa Tanzania wiki hii ameonyesha gari yake mpya ya The 2021 Rolls-Royce Cullinan, kama moja ya magari yake ya kifahari likiwemo Cadillac Escalade.
Sasa yapo magari mengi tu ya kisasa, kifahari na ya thamani ya juu kama McLaren Speedtail, Pininfarina Battista, Mercedes-AMG Project One, Koenigsegg Jesko, Aston Martin Valkyrie, W Motors Lykan Hypersport, Pagani Huayra BC Roadster, Bugatti Chiron Pur Sport na Lamborghini Sian FKP 37.
Kwa mujibu wa mitandao mikubwa duniani kama Luxe.digital, motor 1 na wealthygorilla, magari yafuatayo yanatajwa kuwa ya gharama kubwa zaidi kwenye soko la sasa na kuyamiliki ni kasheshe.
Moja ya magari ya kifahari yenye gharama kubwa kuyamiliki kutoka Maybach. Gari moja la Maybach Exelero linagharimu dola milioni 8 na linaweza kwenda kwa mwenda wa kasi wa juu zaidi wa kilometa 351 kwa saa.
Kama umetazama video ya wimbo wa Lost One ya mwanamuziki maarufu duniani Jay-Z mwaka 2006 basi gari unaloliona la kisasa zaidi linaitwa Maybach Exelero.
Matairi ya gari hii yana ukubwa wa inchi 21 yakitajwa kuwa ya kipekee katika aina ya magari yanayofanana na haya ya 'sports cars'. Lina uwezo wa kubeba uzito wa mpaka kilo 2721.
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.