Uzi maalum wa kupeana Likes: Comment chochote upate "Like"

Mfano Bugatti La Voiture Noire, ni tafsiri ya gari binafsi la Jean Bugatti aina ya 57 SC Atlantic ambalo lilitoweka baada ya vita kuu ya pili ya dunia. Lilitengenezwa mwaka 1934 na Jean Bugatti, mtoto mkubwa wa mwanzilishi wa kampuni hiyo, Ettore Bugatti, sasa limerejea lakini kwa namna ya kipekee kwa kuongezwa ubunifu wa kuvutia na kuwa moja ya magari ya bei ya juu kabisa kuwahi kuuzwa. Limeuzwa kwa dola $19 million.
 
Kwa kukadiria tu thamani ya gari moja la Bugatti La Voiture Noire unaweza kujenga karibu nyumba 400 za kiwango cha kati zenye vyumba vinne na kila kitu ndani. Ukithaminisha nyumba hiyo kwa thamani ya dola 45,000 mpaka 55,000 kwa moja.
 
Lina horsepower 1500 na mwendo kasi wa kilometa 420 kwa saa. Tangu kununuliwa kwa bei hiyo mwaka 2019 mpaka sasa hakuna toleo lingine la gari ya kifahari lililotolewa na kuipiku La Voiture Noire kwa gharama na kuongoza kwa mara ya pili mfululizo kama gari lenye thamani zaidi duniani. Kuzinduliwa kwa Rolls-Royce Boat Tail Mwezi May mwaka huu kutaiondosha Bugatti La Voiture Noire kwenye chati ya kuwa juu gari lenye thamani ya juu duniani.
 
Wengi wanaweza kuishia kwenye Bugatti La Voiture Noire kama gari lenye thamani zaidi, lakini lipo gari jipya linaloingia sokoni sasa kutoka Rolls-Royce linaitwa Rolls-Royce Boat Tail. Ni toleo la kipekee ambalo kwa miaka minne limekuwa likitengenezwa muondo na muonekano wake. Ukilitaka gari hili lenye friji mbili ndani litatengenezwa kwa mahitaji yako yakiwemo ya rangi.
 
Injini na chesesi yake ni kama toleo la Rolls-Royce Phantom. Ingawa haijathibitishwa, inaelezwa kuwa Jay Z na mkewe Beyonce ndio walioweka oda ya kutengenezewa gari hili. Lakini taarifa rasmi ni kwamba yatatengenezwa magari matatu tu ya Rolls-Royce Boat Tail 2021 na moja litauzwa kwa dola $28.0 Million.
 
Lakini kama wanadamu tunatofautiana katika matumizi.
Jarida la Business Insider liliwahi kuangazia vile bilionea wa kawaida anavyoweza kutumia dola milioni 80 kwa mwaka, huku Wamarekani wengi wakiwa na kipato cha nchini ya dola 60,000.
 
Na miongoni mwa mabilionea wakubwa duniani, Jeff Bezos akiwa mmoja wao, akiweza kutumia dola 88,000 kiwango hicho kikiwa sawa na matumizi ya wastani ya Marekani yaani dola 1.
 
Kulingana na utafiti uliofanywa na jarida la business insider, asilimia 60 ya mamilionea duniani walisema kwamba kwanza kabisa wanapopata pesa wanachokipa kipaumbele ni kusafiri.
 
Back
Top Bottom