Hakuwahi kukasirika hata kama tunapoteza mfululizo. Alibaki kuwa upande wa watoto wake, hata kama anashinikizwa kiasi gani. Hii ni imani ya hali ya juu. Nadhani ndio uliokuwa udhaifu wake mkubwa.
Majukwaani mashabiki walikuwa wakimtusi wakitaka atumie pesa kusajili kwenye mechi za vipigo, lakini Wenger siku zote aliendelea kuwaamini wachezaji aliokuwa nao. Binafsi sijawahi kukutana na kocha mwingine kama huyo aliyekuwa na imani kubwa kwa wachezaji wake."
SUPASTAA Cristiano Ronaldo mshahara wake wa Pauni 28 milioni anaovuna kwa mwaka huko Juventus ni mara tatu ya wachezaji wengine wanaomfuatia kwa kulipwa huko kwenye Serie A, huku akizifunika klabu zaidi ya nne kwenye bili yao ya mishahara kwa mwaka.
Ni hivi, staa huyo wa Juventus mwenye umri wa miaka 34 kwa msimu mmoja analipwa pesa nyingi kushinda klabu kadhaa kwenye Serie A mishahara yao yote inayowalipa wachezaji wao ndani ya mwaka.
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.