Uzi maalum wa kupeana Likes: Comment chochote upate "Like"

Real Madrid hii haina kuleta sababu za VAR. Wala sababu za kulaumu mfumo. Sijui kulaumu uchovu na mambo mengine. Kwa maneno machache tu yenye usahihi. Real Madrid hali ni mbaya na wachezaji ndio shida.
 
Kocha Solari anajaribu kurahisisha mambo akidai shida ni kufunga. Nahodha Sergio Ramos analiondoa tatizo kwa wachezaji na kuwalaumu marefa. Kila mmoja anajaribu kusema analoona linafaa.
 
Lakini jambo moja tu, kipigo cha kutoka kwa Real Sociedad kinafichua shida nyingi kwenye kikosi hicho cha Los Blancos. Kwa sasa imeshuka zaidi kwenye msimamo hadi nafasi ya tano na imeachwa pointi 10 na mahasimu wao, Barcelona. Utashangaa, Real Madrid imezidiwa hadi na Alaves. Nani alaumiwe? Wenye hoja dhaifu, watakwambia kisa Cristianno Ronaldo.
 
Kweli sababu za Madrid kufanya vibaya ni Ronaldo? Sitaki kuamini hilo. Shida wachezaji wengi wa Madrid wamevimbiwa mafanikio. Mataji matatu mfululizo ya Ligi ya Mabingwa Ulaya, michuano yenye hadhi kubwa kabisa kwa ngazi ya klabu huko Ulaya, inatosha kuwafanya wachezaji hao wajiona hawana sababu tena kupigania kitu cha zaidi.
 
Wachezaji wana vipaji vikubwa tu, lakini shida hakuna tena kupambana. Julen Lopetegui alionekana hafai, lakini Solari naye hafai pia. Wachezaji wamepoteza ile njaa. Ramos hana kitu kingine cha kutafuta na sasa anacheza tu kusubiria mafao yake. Nini sababu, Zinedine Zidane? La, haiwezi kuwa shida. Kwa ilipofikia Real Madrid, Zidane asingekuwa na kitu cha ajabu kufanya kwenye timu hiyo tena.
 
Jambo ambalo Madrid inapaswa kulifanya kwa sasa. Kitu ambacho Florentina Perez anapaswa kufanya kwa wakati huu ni kufungua milango ya kundi kubwa la wachezaji waliopo waondoke. Anahitaji kubaki na watoto kama Vinicius Junior, Dani Ceballos na wengine. Anahitaji kuleta mastaa wengine wapya wasiopungua wanne, ili kuja na dhana tofauti katika kuhakikisha timu inarudisha njaa yake ya mafanikio. Anahitaji kuwa na beki wa kati mpya wa kiwango cha dunia. Viungo wawili wa maana na washambuliaji wawili matata. Anamhitaji Eden Hazard, anamhitaji Kylian Mbappe, anamhitaji Neymar. Anamhitaji Paul Pogba, anamhitaji John Stones.
 
Back
Top Bottom